Jumatatu ogofya kwa January Makamba

Jumatatu ogofya kwa January Makamba

Kama kuna siku mbaya katika historia ya dini ya kikristo ni siku ya Ijumaa kuu, Petro hakuamini kama Yesu anaweza kukamatwa na akateswa, tena akauawa bila muujiza wowote wa kujiokoa kutokea. Lakini hayo yote yaliendelea mbele ya macho yake.

Siku ya leo kwa January itakuwa masaa 12 kama miaka 12, kutumbuliwa kwa Sefue kumemfanya apoteze confidence kabisa, hakuamini kama imetokea, Jana kama amelala sina uhakika lakini taarifa za kiintelijensia zimenasa ushahidi kuwa alikuwa akihaha kujipanga namna ya kujinasua kwa kufanya vikao mbalimbali na confidant wake usiku kucha.

Kanusho la muitaliano limeonekana kuchafua hali ya hewa zaidi, hasa ukizingatia jamaa alishajichanganya na kukubali kuchangiwa mipesa na huyo bwana. Sasa leo ndo Ijumaa kuu yake, usiulize kwanini, nachokuahidi kaa mkao wa kushtuka kwa taarifa ya kurugenzi ya habari magogoni.

Jumatatu hii ni ogofya kwa kijana wenu huyu, muitaliano katika hali ya kushangaza jana kaanza kulipa madeni yake pale hotelini, Pesa katoa wapi, mimi sijui.

Habari ya asubuhi,leo kulikoni umeamkia Bumbuli??
 
Ngoma Inogile, ninadhani JM kakosea kumlipa Muitliano, alichofanya sasa ni kumnyamazisha asimwage ushahidi zaidi, jamaa angejiuliza kwanza ushahidi mwingine atakaoleta muitaliano utaibua kashfa mpya au ile ile, bila shaka jibu lingekuwa Kashfa ile ile. Kwa vile hii kashfa tayari ni well known hakukuwa na sababu ya kujaribu kuizima kwa kumlipa Muitaliano pesa zake. Ninaona ni kosa kumlipa yule Jamaa kwa sababu hii Kashfa imeshafika Mbali JM hana namna atachomoa sasa kama unapoteza kazi kwanini ulipe tena mapesa? Si bora angekomaa tu, liwalo na Liwe, apoteze kazi abaki na hayo Madola.
1. Kumbe pesa alikuwa nayo kwanini hakumrudishia jamaa pesa yake muda mrefu (KOSA)
2. Aliposikia anatuhumiwa kwanini alikimbilia kujibu angekauka mpaka saa hizi kusingekuwa na uthibitisho wa ushiriki wake (KOSA)
3. Mfuko wa Ushirika Bumbuli unakaguliwa mahesabu yake? Ni nani wanauchangia kwa interest gani walizo nazo na Bumbuli. Kama hakuna statement inayoweza kumclear kuwa hajapitisha pesa chafu huko mfuko utakuwa sehemu ya kumuangamiza
4. Mambo ya Dada Mwamy yalipaswa yaongelewe na Mwammy na mambo ya Kaka Jan yaongelewe na Kaka Jan, kila mtu kujaribu kuongea mambo ya wote wawili wamejikuta wanajichanganya na kuleta hisia zaidi (KOSA)
5. Maandishi ya Muitaliano yameacha mashaka mengi kuliko majibu, bor asingejibu kwa maandishi angejibu kwa mdomo mbele ya watu kadhaa committed alafu hao watu wasimame kumtetea makamba.

Tunaangalia saa zetu, wiki itaisha kweli kwa mshikaji???

Cha mtu MAVI,Usichopenda kutendewa wewe....Golden rule.............Bye tuonane Bumbuli mchana huu
 
Nadhani kanuni izingatiwe Pythagoras Kama mwanza na kwingineko.... makamba na mwamvita wakalale stakishari uchunguzi uendelee
 
Hakuna hoja hapo mkuu yule muitaliano kaongea vizuri sijaona shida ya makamba ilipo ila aliingizwa tu kwasababu ya dada yake.
we utakubari kuingizwaa tu kwa sababu ya dadako; rafiki yako?? Kwa taarifa yako deal zote za hao wakuu huwa zinaenda kimtindo huo ili ikitokea soo basi kuwepo na namna ya kujitetea kama unavyofanya sasa. hakuna kupokea pesa directly lazima ipitie kwa mtu wa karibu tena anayehaminika. Ukimpa directly hawapokeagi. Ndio mana utaona mkuu alietoka mwanae kawa tajiri enzi zake mara anamiliki ...... stail ndo hiyo!
 
Hakuna hoja hapo mkuu yule muitaliano kaongea vizuri sijaona shida ya makamba ilipo ila aliingizwa tu kwasababu ya dada yake.

Labda mleta mada awe na taarifa zaidi ya tulizo nazo kuwa Mtaliano alimsafisha Makamba January toka jana na kumwomba radhi mzee Yusuph Makamba kwa kadhia hii kwa familia yake. Mtaliano alisema wazi kuwa ugomvi ni wake na mpenzi wake Mwavita ila anasema alimlaumu kaka mtu(January) pale alipoombwa na Mtaliano kuingilia kati mgogoro huo kufikia suluu nae kukataa kwa madai hayo ni masuala ya mapenzi kati yao hayamhusu. Sasa mshusha uzi unasubiri saa nane Mtaliano akamchane live January utasubiri sana na huenda huo mkutano usiwepo. Raisi anayo majukumu ya kikatiba kwa wananchi wake na sio masuala ya mapenzi nenda kazini na uwe na tabia ya kujisomea yanayojiri nchini na yenye mashiko zaidi.
 
Hakuna hoja hapo mkuu yule muitaliano kaongea vizuri sijaona shida ya makamba ilipo ila aliingizwa tu kwasababu ya dada yake.
Dada ya nani? ya January! kwa JPJM January hayuko salama kwa sababu dada yake ametumia nafasi ya kaka kujinufaisha na kuna likelihood kuwa january pia kanufaika! La msingi ni kuwa muitaliano pia achukuliwe hatua!
 
Dada ya nani? ya January! kwa JPJM January hayuko salama kwa sababu dada yake ametumia nafasi ya kaka kujinufaisha na kuna likelihood kuwa january pia kanufaika! La msingi ni kuwa muitaliano pia achukuliwe hatua!
Muitaliano achukuliwe hatua? kwa kutuiburia fisadi! hapana hasingejitokeza lazima alishinikizwa kutoa mlungula na hapo ndio pona yake. kaka kakili kupokea utamu . kiongozi unapokea mapesa hiv hiv.
Mie nikichangajya na zangu napata jibu UFISADI. Muitaliano kaamua kuweka wazi baada ya jamaa kupotezea akijua hizi ni zama hatari za Magu mtumbuaji. zingekuwa zama zile sijui kama ingejulikana mana jamaa angepata ingine kama ile ya Bagamoyo imedunda. TUSUBIRI SAA8
 
Hakuna hoja hapo mkuu yule muitaliano kaongea vizuri sijaona shida ya makamba ilipo ila aliingizwa tu kwasababu ya dada yake.
big issue upendeleo wa uwekezaj bagamoyo harbour shida ipohapo
 
Yetu Macho na Masikio kusikia na kuangalia yatakayojiri..... Its too early kuhukumu. Ngoja niweke Akiba ya Maneno
 
muhongo mmemchafua lakini wapi...serikali haiendeshwi kwa upuuzi wa mitandaoni
Mkuu mimi nashindwa kabisa Watz wenzangu, mtu anafurahia na kupanga leo fulani anafukuzwa kwa ushahidi eti wa dada mmoja kaandika instagram! Tanzania bado inasafari ndefu sana, hata sisi Wananchi ni tatizo ila hatujajua tu. Mimi naomba mipaka ya Afrika Mashariki ifunguliwe katika nyanja zote ili tuamshwe. Usishangae wanaofanya upuuzi ukakuta ni Bachelor holder yupo mtaani analaumu hakuna ajira. Kwa uwezo huo wa kufikiri lazima kila kitu uone ni giza tu.
 
Nilichogundua mtoa mada una roho mbaya au unamwonea wivu makamba au kwa alikil yko fupi unadhan kufukuza tu ndo utendaji bora

Mtoa hoja amefanya tu uchambuzi na kuunganisha dots na taarifa, kusema mtoa hoja ana roho mbaya ni kukosa hoja
 
Kama kuna siku mbaya katika historia ya dini ya kikristo ni siku ya Ijumaa kuu, Petro hakuamini kama Yesu anaweza kukamatwa na akateswa, tena akauawa bila muujiza wowote wa kujiokoa kutokea. Lakini hayo yote yaliendelea mbele ya macho yake.

Siku ya leo kwa January itakuwa masaa 12 kama miaka 12, kutumbuliwa kwa Sefue kumemfanya apoteze confidence kabisa, hakuamini kama imetokea, Jana kama amelala sina uhakika lakini taarifa za kiintelijensia zimenasa ushahidi kuwa alikuwa akihaha kujipanga namna ya kujinasua kwa kufanya vikao mbalimbali na confidant wake usiku kucha.

Kanusho la muitaliano limeonekana kuchafua hali ya hewa zaidi, hasa ukizingatia jamaa alishajichanganya na kukubali kuchangiwa mipesa na huyo bwana. Sasa leo ndo Ijumaa kuu yake, usiulize kwanini, nachokuahidi kaa mkao wa kushtuka kwa taarifa ya kurugenzi ya habari magogoni.

Jumatatu hii ni ogofya kwa kijana wenu huyu, muitaliano katika hali ya kushangaza jana kaanza kulipa madeni yake pale hotelini, Pesa katoa wapi, mimi sijui.
Mkuu Yesu angeweza kujiokoa pale msalabani ila aliuvaa ubinadamu ili unabii utimie
 
Back
Top Bottom