Juma Nkamia ni mnafiki

Juma Nkamia ni mnafiki

Anaongea bungeni sasa hivi anasema alipokua BBC alikua kwenye kitengo cha propaganda na aliwaaminisha waingereza mambo ya UONGO ambayo ETI leo anayajutia.

Anasema alifanya hivyo ili KUGANGA NJAA watoto wake wasome. UNAFIKI MKUBWA SANA HUU. kujifanya upo hivi kumbe upo vile.

Biblia na Quran ZIMEKEMEA WANAFIKI.

Mtu anayetubu, ni mtu mzuri, Msameheni.
 
Kama umekili kuwa ulikua kwy kitengo cha propaganda wakati unafanya kazi BBC ya kuhalalisha kuwa Iraq ilikua Ina silaha za sumu ambazo ni propaganda za wamerikani, ikiwa unajua si kweli ni uongo na umekilia umefanya hivyo kwa ajili ya kulinda chakula cha watoto wako, je huoni hata sasa unachochotetea ni kwa ajili ya kulinda chakula cha watoto wako, na si kwa ajili ya mustkabali wa Taifa?


Hili swali hawezi kujibu
 
Nilikuwa napenda sana kumsikiliza Juma Nkamia kwenye kipindi cha michezo enzi za RTD kisha VOA kila jumatatu kwenye ulimwengu wa michezo. Alipogombea ubunge kupitia CCM ndio ulikuwa mwisho wangu wa kumsikiliza juma,
Jamaa ni mnafiki sana na nimtu anaependa fitina japo alishindwa pale msimbazi enzi za katibu mwenezi na kuamua kujiuzuru, Kwanini asimuige mwenzake Swedi bin Mwinyi kwani jamaa anazeeka na heshima yake ya kutosha, au Salim Mbonde
 
Huyu mbumbumbu sijui nimuite kwa jina gani.

Mkuu Ben usijisumbue kutafuta Nomino ya Mtu huyu..hii hapa KAA- HABA MGANGA NJAA.
ILA SIYO WA KUMSUTA SANA KWANI HII NI SERA YA CHAMA CHAO.FITINA NA MAJUNGU KWAO DAIMA UKWELI NA UWAZI MWIKO!
 
Hakuna kipya alichosema Juma. Waandishi wa kibongo ni shida tupu! Hamwoni hata Pasco anavyoshabikia na kuunga mkono vibahasha ili watoto wapishane maliwatoni?
Mkuu Mzito K, ni kweli naunga mkono bahasha kwa asilimia 100% ila siungi mkono "bahasha"!.

Kwa vile kuna bahasha na "bahasha", ili kuijua tofauti, nisome HAPA!.
Pasco wa jf ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea!, nikimaanisha naifanya kazi ya uandishi "just for the love of it!" not for returns or rewards!. Ninashughuli nyingine "inayolipa!" na ndiyo hiyo inayo "wapishanisha" wale watoto wangu 6!.
Pasco.
 
Kondoa sijui walikosa mtu wakumtuma mjengoni?? Bora jimbo lingebaki wazi kuliko huyu kilaza.
 
Mkuu Mzito K, ni kweli naunga mkono bahasha kwa asilimia 100% ila siungi mkono "bahasha"!.

Kwa vile kuna bahasha na "bahasha", ili kuijua tofauti, nisome HAPA!.
Pasco wa jf ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea!, nikimaanisha naifanya kazi ya uandishi "just for the love of it!" not for returns or rewards!. Ninashughuli nyingine "inayolipa!" na ndiyo hiyo inayo "wapishanisha" wale watoto wangu 6!.
Pasco.
Mkuu Pasco, tofauti ya bahasha na 'bahasha' ni hizo Apostrophes tu
 
Last edited by a moderator:
Anaongea bungeni sasa hivi anasema alipokua BBC alikua kwenye kitengo cha propaganda na aliwaaminisha waingereza mambo ya UONGO ambayo ETI leo anayajutia.

Anasema alifanya hivyo ili KUGANGA NJAA watoto wake wasome. UNAFIKI MKUBWA SANA HUU. kujifanya upo hivi kumbe upo vile.

Biblia na Quran ZIMEKEMEA WANAFIKI.
Aliacha lini unafiki wake? Alikwenda kutubua wapi? Huyu siye aliyesema haongei na mbwa anaongea na mwenye mbwa? Huyu ni wq kupuuzwa tu hana lo lote. Halafu inasemekana hata huko chuoni anaandikiwa assignments. Aibu iliyoje!


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Mara kadhaa Mbunge wa Kondoa kupitia CCM JUMA NKAMIA amekuwa akiwaponda sana waandishi wa habari na vyombo vyao pamoja na kwamba naye alitokea kwenye utangazaji. Sijafahamu vema kinachomsumbua kwa sababu mara zote hoja zake za kuwachafua wenzie hao hazina mashiko. Jana ( 04/09/2013 ) kaja na jipya la kuhuzunisha eti akiwa mtangazaji wa BBC anasema aliweza kuwa mmoja wa watangazaji ambao waliwaaminisha walimwengu kuwa IRAQ ilikuwa na silaha za sumu wakati haikuwa kweli. Anadai alikuwa anadanganya vile ili kuganga njaa na watoto wake waishi.

Matokeo ya propaganda zile za NKAMIA ilipelekea UN chini ya Marekani kuivamia IRAQ na kuua raia wengi wasio na hatia na hadi kiongozi wa Iraq naye kuuawa. Mbunge gani huyu wa ovyo namna hii anajisifia kushiriki kuua aafu wabunge wenzia wa CCM na kibaraka MREMA chini ya Naibu Spika NDUGAI wanamshangilia, huu ni upumbavu.

Chanzo cha kusema hayo ni pale wabunge wa CDM na CUF walipoamua kutoka nje kupinga kuburuzwa na Naibu Spika na waandishi wengi wakawafuata wabunge hao kule nje, eti wanafuata nini nje wakati habari ziko kwa wabunge waliobaki ndani.

Kwa hakika anastahili kuomba radhi kwa kuropoka maneno hayo, wangekufa wananchi wa Kondoa angechekelea ? Ndo kwanza nmeingia kikamilifu katika JF hebu nambieni hawa wabunge wa eneo la katikati ya nchi kupitia CCM WAKOJE ? yuko MM,yuko BAJAJI, yuko JN, yuko Naibu S. MBONA MAJANGA ! :A S 2152:
 
mchawi akiwa anakufa hujikuta anaropoka siri ya maovu yake yote aliyoyafanya .

Huyu Nkamia ni S.I Unit ya wauaji wengine wengi ndani ya CCM na serikali hii kwa ujumla.
 
Anastahili kupelekwa the Hague kwa kusababisha vita ambavyo vilileta maafa makubwa na ambavyo madhara yake yanaathiri watu hadi leo. Yaani hii nchi ingekuwa na polisi weledi mpaka sasa wangeshamtia pingu. Kinyume chake wanamchekea. Hii nchi kweli inapita kipindi kigumu. Na bado tutasikia mengi.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
kwa hiyo sasa yupo ktk mission nyingine za kuganga njaa bungeni...?mwehu huyu kwani alikuwa na nini ch akujua kuwa taarifa aliyokuwa kaitoa ni uongo wakati hakuwahi fika field na habaro zote walikuw awkaichukua ktk idhaa ya kiingereza na vyombo vingine?
 
Hapo katikati ya nchi kuna matatizo! karibu wabunge wao wote ni uharu! Hivi yule Lusinde yupo wapi cku hizi na ile elimu yake ya standard seven...
 
Back
Top Bottom