mwehu ndama
JF-Expert Member
- Nov 12, 2019
- 556
- 1,947
Katika soka neno tapeli sio tusi, bali hutumika kumbainisha mtu anaejipatia sifa na umaarufu chanya pasipo juhudi na uwezo wake binafsi kama ilivyo kwa kocha juma mgunda gadiola mnene.
Kibonge huyu toka Tanga, ni kocha mzuri ila sio kocha wa kiwango wanachokitaka mbumbumbu fc, achilia mbali kwa mabingwa wa nchi Yanga afrika ambako mnene huyu, hana uwezo wakukaaa walau katika benchi la ufundi kutoa ushauri.
Mgunda ni wale makocha wa timu za madaraja ya kati, makocha ambao mara nyingi ni uwezo binafsi wa wachezaji ndio uwarahisishia kazi na sio mbinu zao.
Gadiola mnene hana mbinu za kisasa za kimpira bali ni muhamasishaji tu kama Ahmed ally, mara kadhaa anategemea kuwajaza sumu wachezaji katika mechi kubwa na mambo yanapokuwa magumu hugeuka sangoma kwa kujivika vibwaya, kupasua nazi na kufanya ulozi kwa niaba ya timu.
Kwa wafwatiliaji wazuri wa soka, nadhani mtakuwa mnajua athari za timu kubwa kufukuza makocha,. "Mara nyingi mara tu baada ya kocha kufukuzwa katika timu kubwa, kocha anaekaimu nafasi hunufaika kwa sababu kwa wakati huo kila mchezaji kikosini huanza kuhisi nafasi yake ya kucheza iko mashakani na kila mtu anakuwa na nafasi sawa chini ya kucha mpya, hivyo wachezaji hujituma kwa ajili ya kupigania nafasi ya kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza, lakini pia hujituma sana kutaka kuwaaminisha mashabiki wa timu yao kuwa tatizo sio wao bali ni kocha alieondoka.Na nikatika nyakati kama hizi ndipo makocha matapeli kama Juma mgunda au julio kiwelu hujizolea umaarufu wa uwongo na kuonekana wao ni makocha wazuri lakini mara kadhaa wameumbuliwa na muda. Kwani kadiri muda unavyosonga ndipo wachezaji urudi katika default settings na kuanza kucheza kama walivyozoea.
Ushauri wangu kwenu mbumbumbu fc, ni kuachana na mpiga ramli juma mgunda kabla hajawarudisha shimoni kwa mara nyingine. Huyo ni kocha wa timu ndogo na timu za wanawake, Tff ilijichanganya kumpa timu ya taifa yaliyotupata ni aibu.
Viva Yanga afrika
Kibonge huyu toka Tanga, ni kocha mzuri ila sio kocha wa kiwango wanachokitaka mbumbumbu fc, achilia mbali kwa mabingwa wa nchi Yanga afrika ambako mnene huyu, hana uwezo wakukaaa walau katika benchi la ufundi kutoa ushauri.
Mgunda ni wale makocha wa timu za madaraja ya kati, makocha ambao mara nyingi ni uwezo binafsi wa wachezaji ndio uwarahisishia kazi na sio mbinu zao.
Gadiola mnene hana mbinu za kisasa za kimpira bali ni muhamasishaji tu kama Ahmed ally, mara kadhaa anategemea kuwajaza sumu wachezaji katika mechi kubwa na mambo yanapokuwa magumu hugeuka sangoma kwa kujivika vibwaya, kupasua nazi na kufanya ulozi kwa niaba ya timu.
Kwa wafwatiliaji wazuri wa soka, nadhani mtakuwa mnajua athari za timu kubwa kufukuza makocha,. "Mara nyingi mara tu baada ya kocha kufukuzwa katika timu kubwa, kocha anaekaimu nafasi hunufaika kwa sababu kwa wakati huo kila mchezaji kikosini huanza kuhisi nafasi yake ya kucheza iko mashakani na kila mtu anakuwa na nafasi sawa chini ya kucha mpya, hivyo wachezaji hujituma kwa ajili ya kupigania nafasi ya kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza, lakini pia hujituma sana kutaka kuwaaminisha mashabiki wa timu yao kuwa tatizo sio wao bali ni kocha alieondoka.Na nikatika nyakati kama hizi ndipo makocha matapeli kama Juma mgunda au julio kiwelu hujizolea umaarufu wa uwongo na kuonekana wao ni makocha wazuri lakini mara kadhaa wameumbuliwa na muda. Kwani kadiri muda unavyosonga ndipo wachezaji urudi katika default settings na kuanza kucheza kama walivyozoea.
Ushauri wangu kwenu mbumbumbu fc, ni kuachana na mpiga ramli juma mgunda kabla hajawarudisha shimoni kwa mara nyingine. Huyo ni kocha wa timu ndogo na timu za wanawake, Tff ilijichanganya kumpa timu ya taifa yaliyotupata ni aibu.
Viva Yanga afrika