Julius Nyerere, Julius Caesar, Sahib na vitabu vya Sheikh Ponda

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,908
30,253
JULIUS NYERERE, JULIUS CAESAR, SAHIB NA VITABU VIJAVYO VYA SHEIKH PONDA

Kuna rafiki yangu kaniambia kuwa wakati alipokuwa anafanyakazi katika shirika moja kubwa la kimataifa linaloshughulika na Afrika ndipo alipomjua Mwalimu Nyerere vizuri sana.

Anasema hakuna kilichokuwa kinampita kilichoandikwa na Mwalimu au kuhusu yeye.

Huyu sahib yangu si Mtanzania lakini ana mapenzi makubwa na Tanzania na anasema vitu viwili ndivyo vilivyomfanya aipende Tanzania.

Kitu cha kwanza ni Julius Nyerere na cha pili ni mchezo wa William Shakespeare, "Julius Caesar," mchezo kitabu chake alichotafsiri Mwalimu kwa Kiswahili mwaka wa 1963.

Haya ndiyo yalikuwa mazungumzo yetu siku ya kwanza tulipokutana na akanialika chakula cha jioni nyumbani kwake.

Nimeshangaa kwa yeye kumpenda Shakespeare kwa sababu nilipojulishwa kwake haraka baada ya kuachana nikamtafuta Google.

Naam sahib yangu ni msomi mkubwa na kasoma elimu nzito na kaandika mambo makubwa kuhusu Afrika.

"Mohamed nimesoma kitabu chako na nilikipata Marekani kanipa Mtanzania mmoja tukifanya kazi shirika moja.''

Aliponiambia tu kuwa kasoma kitabu changu kimoyomoyo nikasema, "Bismillah..." kwani nilijua nini kitafuata.

Sahib akasema, ''Huyu jamaa aliniambia kuwa maswali yangu yote ninayomuuuliza kuhusu Tanzania nitapata majibu yake katika kitabu chako.''
Nilichokitegemea kuja hakikuja kama vile nlivyotegemea.

Kikaja kitu kingine kabisa hata hivyo si mbali na yale niliyotegemea.

Sahib ananisomea kipande cha Shakespeare, "There is a tide in the affairs of men which taken at the flood leads on to fortune omitted all the voyage of their life is bound in shallows and miseries?''

Brutus huyo anatafakari alifanye sasa au asubuhi na ana hofu akisubiri huenda nafasi ikampita.

Nikajiambia kumbe ile Bismillah yangu haikwenda patupu.
Maneno haya aliyosema Brutus mazito.

Wanasiasa huyatumia wanapojuta kwa kutochukua hatua stahiki na pili hutumia kwa kuchukua hatua wakafanikiwa au wasifanikiwe.

Nikamwambia umenikumbusha mzee wangu marehemu Aboud Jumbe alipata siku moja kunisomea kipande hicho alipokuwa ananieleza maisha yake na vipi alikuja kuondoshwa madarakani mwaka wa 1984.

"Ukifahamiana na Mzee Aboud Jumbe?"
''Ni baba yangu kwani yeye alinichukua mimi kama mwanae.''

''Aboud Jumbe alikuwa mtu wa aina gani nimesoma kitabu cha Dr. Harith Ghassany...''

Wamarekani wanamsemo, ''There is no free lunch in America.''
Maana yake ni kuwa mtu akikualika chakula cha mchana basi jua ana lake jambo analotaka kwako.

Mimi sitaki kuwa mwizi wa fadhila siwezi kusema kuwa kwa kualikwa chakula cha usiku sahib alikuwa anataka kitu kwangu la hasha.

Mazungumzo yale yote yalikuja kwa kuwa naamini hakupata kukutana na mtu wa aina yangu kwani alinieleza kuwa katika mambo ambayo alikuwa yanamshangaza sana na kumsikitisha ni kuwa katika ofisi za ubalozi wa Tanzania huko nje hakupata kukutana na Muislam hata mmoja ila yule aliyempa kitabu changu UN, New York na yeye lau ni Mtanzania lakini anatoka Zanzibar na huko kila utakayemgusa ndiye.

Basi nikamjibu kuwa wapo lakini ni wachache mno.

Chakula kinakuwa na ladha zaidi kwa muziki mororo na mzungumzo matamu.

Ana vitu si mchezo lakini ndege kaitia katika dhoruba ya upepo mkali.
Nikahisi kama vile wale kamba ladha yake inanibadilikia.

Mimi nimepata kuwa ndani ya ndege iliyopigwa na dhoruba.
Mtu yeyote aliyepitia hali hii atanielewa.

Hili linafaa sana kumuombea adui wako limfike.

Rubani katoa tangazo abiria wote wafunge mikanda pamoja na wahudumu.
Ulikuwa usiku mkubwa Emirates inakata mawingu kati ya Dubai na Tehran.

Mbawa za ndege unasisikia zinalalamika mfano wa mlango wenye bawaba mbovu zilizoshika kutu.

Nikamrejesha sahib kwa ''Julius Caesar,'' ili kumtoa kwenye ile dhoruba nikamwambia kuwa baada ya kutafsiriwa kitabu kile na Mwalimu Nyerere, Shule ya Pugu waliucheza mchezo mzima mbele yake.

Nikamfahamisha kuwa mchezo ule ulirushwa mubashara radioni na mimi niliusikiliza wote bila kusinzia.

Ilikuwa mwaka wa 1964 na nilikuwa na umri wa miaka 12.

Nikimpenda Mwalimu na ule mchezo naweza kusema ndiyo ulinifanya nimpende William Shakespeare.

Sahib akanipokea na vipi ''The Merchant of Venice?''
Taib.

Chombo kimeshatoka kwenye mawimbi makubwa yanayochafua tumbo kinaelea buheri wa hamsa ishirini.

Nikacheka nikampa kipande kimoja kutoka, ''The Merchant of Venice:''

''Signor Antonio, many a time and oft
In the Rialto you have rated me
About my moneys and my usances.
Still have I borne it with a patient shrug,
For sufferance is the badge of all our tribe.''

Huyu Yahudi Shylock, mla riba.
''Mohamed umemsoma sana Shakespeare.''

Kisha akanipokea kutoka pale akanitupia jiwe akaendelea pale nilikoishia:

''You call me misbeliever, cutthroat dog,
And spet upon my Jewish gaberdine—''
Nilitabasamu nikampa mkono kama ishara ya kumwambia, ''Hakika wewe ni bingwa.''

Allah kawajaalia baadhi ya waja wake nema kubwa ya elimu.
Namtazama sahib wangu nimepwelewa.

Huyu mtu kasoma vyema na uwezo wake wa kuhifadhi ni hatari.
Lakini huyu mtu hakusoma Fasihi.

''Sasa ukitaka kuingia ndani ya ubongo wa Nyerere soma vitabu hivi alivyotafsiri utamuelewa vyema,'' anaieleza huku akikung'uta mkono wangu.

''Why Julius Caesar,'' ''Why Merchant of Venice,'' and for that matter why not ''Wafanyabiashara wa Venice'' it has to be, ''Mabepari wa Venice.''

''Hawa akina Sykes wakifanya biashara hawa, au sivyo?''
Sahib ananiuliza.

Haya ndiyo niliyokuwa nikiyasubiri toka asubuhi mwanzo alipokitaja kitabu changu.

''Rafiki zake wote wa karibu walikuwa wafanyabiashara,'' najibu.
''Hawa ndiyo walikuwa wafadhili wakubwa wa TANU.

Mzee Rupia, Dossa Aziz, Abdul na Ally Sykes wote walikuwa wafanyabishara.''

''Nyerere alikuwa kiongozi jasiri sana.''
Sahib wangu alimaliza na kuongeza, ''Mabepari wa Dar es Salaam.''

Hapa sote tukaangua kicheko.
Kalamu ina nguvu kushinda kitabu.

Siku Sheikh Ponda aliponiletea kitabu chake, ''Juhudi na Changamoto,'' nilimwambia, ''Ndugu yangu sasa umeingia katika dunia nyingine mpya kwako maisha yako hayatakuwa kama yale uliyozoea unatia mguu katika nchi hujapatapo kufika wala kuifikiria akilini kwako.''

Nimaeyasema haya wakati sikuwa najua kuwa Sheikh Ponda tayari kaandika vitabu 16.

Vitabu 16.

Vitabu 16 na vingine unakiogopa kitabu kwa kusikia jina lake tu ukaanza kujitisha mwenyewe.

Nani shujaa na jasiri kiasi akitajiwa Dr. John Sivalon asishtuke hata kidogo akitajiwa kuwa kuna kitabu kimeandikwa na Sheikh ponda kuhusu Dr. Sivalon.
Au akitajiwa kitabu cha ''Masheikh Gerezani,'' ''Waislam na Mkono wa Dola,'' ''Pitio la Zanzibar.''

Sheikh Ponda katufanyia kazi kubwa sana.
Kalamu ya Sheikh Ponda imetufungulia ukweli.

Sahib yangu na wengine mfano wake ambao hawakuwa wanaijua Tanzania vitabu hivi vitawasaidia kuijua nchi yetu na siasa zake.

Kweli Tanzania ni kisiwa cha amani?
Amani inaweza kuwapo vipi penye ubaguzi?

1662521046044.png
1662521123132.png
1662521157861.png
 
Shikamoo Mzee

Nimekuwa nafatilia maandiko yako kwa muda mrefu sana.

Ukweli nikwambie mzee waangu nilikuwa nayaona kama yana mrengo wa kidini na undugu sana. Kuna hoja zako mbili zimenifanya nijiunge na JF ili nikuulize mwenyewe nisikie maoni yako mzee wangu kama hutojali. Na pia nitangulize samahani kama kwa namna yoyote nitakuwa nimekukwaza.

1. Kuhusu kitabu cha "The Merchant of Venice'' kilichotafsiriwa na Mwl. Baba wa taifa letu la Tanzania. Na wewe kusema marafiki na wapigania uhuru wote waliofutwa kwenye historia ya Uhuru wa Tanganyika walikuwa ni wafanyabiashara na Waislamu.

Unadhani kwa sera za mwalimu za ujamaa tatizo hapo ilikuwa ni udini au ni huo ufanyabiashara wao? Ungekuwa ni wewe ndo Mwl. Unahubiri ujamaa ilhali unaendelea kushikamana na mabepari ambao nia yao kubwa ilikuwa ni kujilimbikizia mali?

2. Kwenye andiko lako la kuhusu kitabu cha mzee wetu Shekh I. Ponda
Umesema waislamu wanakandamizwa na wananyimwa haki zao za msingi na mwanajamvi akakuuliza haki gani ingawa lugha iliyotumika haikuwa ya staha ila majibu uliyotoa ni kuhusu wasifu wako.

Nikukumbushe tu mzee wangu muungwana akivuliwa nguo huchutama. Kama mzee ulipaswa kumpuuza na kumjibu kwa staha siku nyingine hatorudia. Binasfi nilikuwa nasubiria kusikia majibu kutoka kwako wa hizo haki tulozonyimwa na wenzetu wakazipewa ni haki gani hizo?

Nitashukuru sana kama utabisaidia majibu.
 
Shikamoo Mzee

Nimekuwa nafatilia maandiko yako kwa muda mrefu sana.

Ukweli nikwambie mzee waangu nilikuwa nayaona kama yana mrengo wa kidini na undugu sana. Kuna hoja zako mbili zimenifanya nijiunge na JF ili nikuulize mwenyewe nisikie maoni yako mzee wangu kama hutojali. Na pia nitangulize samahani kama kwa namna yoyote nitakuwa nimekukwaza.

1. Kuhusu kitabu cha "The Merchant of Venice'' kilichotafsiriwa na Mwl. Baba wa taifa letu la Tanzania.
Na wewe kusema marafiki na wapigania uhuru wote waliofutwa kwenye historia ya Uhuru wa Tanganyika walikuwa ni wafanyabiashara na Waislamu.

Unadhani kwa sera za mwalimu za ujamaa tatizo hapo ilikuwa ni udini au ni huo ufanyabiashara wao?
Ungekuwa ni wewe ndo Mwl. Unahubiri ujamaa ilhali unaendelea kushikamana na mabepari ambao nia yao kubwa ilikuwa ni kujilimbikizia mali?

2. Kwenye andiko lako la kuhusu kitabu cha mzee wetu Shekh I. Ponda
Umesema waislamu wanakandamizwa na wananyimwa haki zao za msingi na mwanajamvi akakuuliza haki gani ingawa lugha iliyotumika haikuwa ya staha ila majibu uliyotoa ni kuhusu wasifu wako.

Nikukumbushe tu mzee wangu muungwana akivuliwa nguo huchutama. Kama mzee ulipaswa kumpuuza na kumjibu kwa staha siku nyingine hatorudia. Binasfi nilikuwa nasubiria kusikia majibu kutoka kwako wa hizo haki tulozonyimwa na wenzetu wakazipewa ni haki gani hizo?

Nitashukuru sana kama utabisaidia majibu
Silver...
Mrengo wa kidini.

Waislam wakifutiwa historia yao na wakaiandika upya historia ya uhuru huo kwako ni udini?

Vipi kuhusu wafutaji wa historia hiyo wao si wadini?

Waislam wakibaguliwa katika elimu na fursa za kazi nk.
Wakaeleza kuwa wanabaguliwa huo ni udini?

Vipi hao wanaotumia madaraka yao kuwabagua Waislam hao si wadini?
Sasa mtu ananiuliza mimi haki gani yeye anauliza kama nani?

Mbona wanaoshutumiwa kwa udini wako kimya?

Kwa nini hawaulizi wanaoshutumiwa mnashutumiwa kwa kitu gani na kwa nini hamtoi majibu?
 
After all these years, no one is interested in your BS anymore. Everybody just got sick & tired of you. Just go away Mzee.
 
After all these years, no one is interested in your BS anymore. Everybody just got sick & tired of you. Just go away Mzee.
Njabu...
Tuchukulie ni kweli kuwa hakuna mtu anapenda kunisoma.
Lakini hapa anafukuzwa mtu?

Mtu kama hapendezewi na kalamu yako si anaacha tu kukusoma?
Sick and tired hufungui post yangu uumwe na uchoke.

Lakini si kweli wengi wanapendezewa na uandishi wangu.
Napendwa sana.

Nadhani unajua kuwa hapa JF nimepewa nishani kwa uandishi wangu.

1662576453294.jpeg
 
Njabu...
Tuchukulie ni kweli kuwa hakuna mtu anapenda kunisoma.
Lakini hapa anafukuzwa mtu?

Mtu kama hapendezewi na kalamu yako si anaacha tu kukusoma?
Sick and tired hufungui post yangu uumwe na uchoke.

Lakini si kweli wengi wanapendezewa na uandishi wangu.
Napendwa sana.

Nadhani unajua kuwa hapa JF nimepewa nishani kwa uandishi wangu.

View attachment 2349327
msamehee tu balehe nayo ikizingira sio mchezo kujinasua baadhi ya Mambo
 
Stick to authoring story books for kids with all-Muslim characters. You may even want to introduce djinns in your next Big Adventure Book for Muslim Kids.
 
Njabu...
Tuchukulie ni kweli kuwa hakuna mtu anapenda kunisoma.
Lakini hapa anafukuzwa mtu?

Mtu kama hapendezewi na kalamu yako si anaacha tu kukusoma?
Sick and tired hufungui post yangu uumwe na uchoke.

Lakini si kweli wengi wanapendezewa na uandishi wangu.
Napendwa sana.

Nadhani unajua kuwa hapa JF nimepewa nishani kwa uandishi wangu.

View attachment 2349327
Mungu Akulinde kakayetu
 
Silver...
Mrengo wa kidini.

Waislam wakifutiwa historia yao na wakaiandika upya historia ya uhuru huo kwako ni udini?

Vipi kuhusu wafutaji wa historia hiyo wao si wadini?

Waislam wakibaguliwa katika elimu na fursa za kazi nk.
Wakaeleza kuwa wanabaguliwa huo ni udini?

Vipi hao wanaotumia madaraka yao kuwabagua Waislam hao si wadini?
Sasa mtu ananiuliza mimi haki gani yeye anauliza kama nani?

Mbona wanaoshutumiwa kwa udini wako kimya?

Kwa nini hawaulizi wanaoshutumiwa mnashutumiwa kwa kitu gani na kwa nini hamtoi majibu?
80-20

Hehehehe
 
Njabu...
Tuchukulie ni kweli kuwa hakuna mtu anapenda kunisoma.
Lakini hapa anafukuzwa mtu?

Mtu kama hapendezewi na kalamu yako si anaacha tu kukusoma?
Sick and tired hufungui post yangu uumwe na uchoke.

Lakini si kweli wengi wanapendezewa na uandishi wangu.
Napendwa sana.

Nadhani unajua kuwa hapa JF nimepewa nishani kwa uandishi wangu.

View attachment 2349327
Jamii za Kiislamu huwa hawakupi recognition and appreciation for being such an outstanding and upstanding Muslim Personality by way of petty awards kama hizi? Najua hizi tuzo zitakuwa mia na zaidi. Hebu tuwekee picha.
 
Silver...
Mrengo wa kidini.

Waislam wakifutiwa historia yao na wakaiandika upya historia ya uhuru huo kwako ni udini?

Vipi kuhusu wafutaji wa historia hiyo wao si wadini?

Waislam wakibaguliwa katika elimu na fursa za kazi nk.
Wakaeleza kuwa wanabaguliwa huo ni udini?

Vipi hao wanaotumia madaraka yao kuwabagua Waislam hao si wadini?
Sasa mtu ananiuliza mimi haki gani yeye anauliza kama nani?

Mbona wanaoshutumiwa kwa udini wako kimya?

Kwa nini hawaulizi wanaoshutumiwa mnashutumiwa kwa kitu gani na kwa nini hamtoi majibu?
utakufa mdomo wazi kwa dhambi ya udini.Pepo haitafutwi kwa urongo!

Samia anawalambisha asali umeufyata kimya!
 
sio kisikiwa cha amani ni kisiwa cha ccm .kikiwa na familia chache ndio zinashika nchi hii
 
Back
Top Bottom