[h=3]Mwanasiasa wa upinzani nchini Afrika Kusini, Julius Malema ameshindwa katika juhudi zake za kutaka kesi ya ufisadi dhidi yake itupiliwe mbali huku akikabiliwa na tisho la kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo mwaka ujao.[/h]
Kiongozi huyo wa zamani wa tawi la vijana la chama tawala ANC ameshitakiwa kwa makosa ya kutengeza pesa kwa njia haramu , udanganyifu na kujihusisha na mitandao ya uhalifu.
Jaji Ephraim Makgoba alisema kuwa kesi itaanza kusikilizwa tarehe 30 mwezi Septemba mwaka 2014.
Anadaiwa kupokea dola za kimarekani, 392,000 kutokana na mikataba na maafisa wa serikali , madai anayoyakanusha.
Chanzo cha habari
Kiongozi huyo wa zamani wa tawi la vijana la chama tawala ANC ameshitakiwa kwa makosa ya kutengeza pesa kwa njia haramu , udanganyifu na kujihusisha na mitandao ya uhalifu.
Jaji Ephraim Makgoba alisema kuwa kesi itaanza kusikilizwa tarehe 30 mwezi Septemba mwaka 2014.
Anadaiwa kupokea dola za kimarekani, 392,000 kutokana na mikataba na maafisa wa serikali , madai anayoyakanusha.
Chanzo cha habari