MWAISEMBA CR
Member
- Apr 21, 2014
- 86
- 78
✳UHUSIANO WA JUBILEE YA MIAKA 70 YA ISRAEL NA KURUDI KWA YESU KULINYAKUA KANISA✳
*Na: Shujaa Charles Mwaisemba*
_▶SHEREHE YA MIAKA 70(JUBEILEE) YA TAIFA LA ISRAEL_
_▶UFUNGUZI WA UBALOZI WA MAREKANI HUKO JERUSALEM_
_▶MAANDAMANO YA WAPALESTINA DHIDI YA ISRAELI_
✍Ili kuweza kuelewa Msingi wa Somo letu,Ni muhimu kuelewa Matukio makuu matatu yaliyotabiriwa na Manabii na Yesu mwenyewe kuwa yatatokea Siku za mwisho kama dalili kuu za kuja kwa Bwana Yesu kulinyakua kanisa lake
*TUKIO LA 1⃣ : _WAYAHUDI WATARUDI KATIKA NCHI YA ISRAEL { YEREMIA 30:3}_*
Wayahudi walikuwa wametawanywa dunia nzima katika mwaka 70B.K,tokea wakati huo,kwa karibu miaka 2000 hawakuwa na nchi iliyokuwa yao wenyewe, ni kwasababu walimfanya Mungu dhambi .
Mara baada ya vita vya pili vya dunia,Mwaka 1945 kuisha Wayahudi kutoka pande zote walianza kujikusanya mmoja mmoja kwa namna kama wanaambia kuwa warudi kwenye nchi yao. Kulianza kufanyika mipango mingi kwenye mabunge na Nchi za Ulaya na marekani kuhusu Israel ndipo kwa ghafla ikiwa kama sauti ya kuambiana imewajia kwa wakati mmoja kuanza kurudi mmoja baada ya wengine na kuwakuta Wenyeji wao Wapalestina katika maeneo hayo
Waingereza pamoja na wamarekani waliwasaidia sana kuwafukuza Wapalestina maeneo Haya ya sasa Ya Israel ili kuwaruhusu Wanaisrael kufika maeneo hayo.Na kwa pamoja ndani ya Muda mfupi wanayahudi walikusanyika na kuwa wengi sana hata kupelekea kuanza kutaka tena Israel litambulike kama Taifa.
*TUKIO LA 2⃣: _ISRAEL LITAKUWA TAIFA TENA_*
Tukio hili litimia katika Mwezi *May 14, 1948* ambapo Israel ikaanza tena kutambulika kama Taifa huru baada ya kupotea katika Uso wa dunia kwa miaka mingi ya nyuma iliyopita .Na Eneo hilo kumilikiwa na Hawa Wapalestina kwa muda wote hivyo tangu wakati huo Wapalestina kufukuzwa kwa nguvu kuwapisha wayahudi sehemu yao ndipo kulipoanza uhasama wa muda mrefu baina ya mataifa haya mawili ambayo wote wanadai Ardhi hiyo ni milki yake.
Hivyo kumekuwepo na mapigano ya Muda mrefu dhidi ya Wayahudi(Wana Israel) na Wapalestina ambapo Israel wanazidi kujitanua kuchukua maeneo na mipaka yao ya zamani iliyokuwepo hadi kwenye maandiko hasa Mpaka kwenye Mji wa Yerusalem ambapo ndipo Ngome pia ya Wapalestina na Waislamu kote ulimwenguni maana ndipo kulipokuwepo Msikiti wao mkubwa unaoheshimika unaoitwa *AL-AQSA* Na huku Israel nao wakidai eneo hilo ni lao kwakuwa ndipo kulipokuwepo na Hekalu la Suleiman
*TUKIO LA 3⃣ : _JIJI LA YERUSALEM LITAKUWA HURU KUTOKA KWA MAADUI ZAKE_*
Kwa tukio hili ndio moyo halisi wa somo letu hili,Na hili ndio tukio pekee ambalo lilikuwa limebaki ambalo halijatimizwa kwa Muda mrefu, na hii ni kutokana na Sababu kwanza mpaka sasa Wapalestina bado wanaamini jiji la Yerusalemu lipo chini yao, maana ndipo Pia upo ule msikiti wa kiislamu
Hapa kuna mambo makuu mawili ya kujifunza na kuyaelewa kama Kanisa au Mtu yeyote anayesoma ujumbe huu na ujue jinsi yalivyo na uhusiano mkubwa na kuja kwa Bwana Wetu Yesu
*1⃣ JUBILEE YA MIAKA 70 YA TAIFA LA ISRAEL NA UFUNGUZI WA UBALOZI WA MAREKANI KATIKA JIJI LA YERUSALEM*
Tukio hili na la Muhimu sana na ni la kinabii kabisa ambalo kila mmoja hapaswi kulichukulia kisiasa na kuona kama ni la kawaida Kwani ndio Kutimia kwa tukio hili la Kuutambua Mji wa Yerusalem kama ndio makao Makuu ya Israel ndio tukio pekee lililokuwa limebaki kama Ishara kubwa ya Kurudi kwa Bwana Yesu kulinyakua kanisa
Jambo hili,la ajabu na la kushangaza,Cha ajabu yake limetokea wakati huu huu ambapo Taifa hili la Israel linatimiza miaka 70 tangu kuwapo kwake (1948-1918).Na cha ajabu leo 14/5/2018 ndio Israel inatimiza miaka 70 kamili ya Kuwepo kwake tangu Tarehe 14/5/1948.Kumbuka wakati nafundisha Somo la dhiki kuu!nilishafundisha maana ya 70 katika unabii jinsi ilivyo na maana kubwa kibiblia(Ikiwa hujajifunza kuhusu hilo wasiliana nami kwa namba hizo chini,nitakupatia masomo hayo niliyofundisha kwa urefu kuhusu miaka 70 hiyo na maana yake)
Sambamba na hili Rais wa Marekani, *Donald Trump* alizungumza maneno mazito ambayo yaliushangaza ulimwengu kwa kutamka Hadharani kuwa anautambua *JIJI LA YERUSALEM KAMA NDIO MAKAO MAKUU MAPYA KWA TAIFA LA ISRAEL BADALA YA TELHAVIV* . Na zaidi siku hii hii ya Leo (14/5/2018) ndio amefungua Ubalozi wake wa Marekani katika jiji hilo hilo la *YERUSALEM KAMA ISHARA YA KUUTAMBULISHA KWA DUNIA KUWA NDIO MAKAO MAKUU PA ISRAEL*
Kumbuka nilikuambia,Hapa Yerusalem ndipo pia Eneo linalomilikiwa na wapalestina kwa Muda mrefu na kudai ni eneo lao kwasababu ya kuwepo na msikiti mkubwa wa kislamu duniani *(Sehemu pa pili panaheshimika kwenye nguzo za kiislam)*
Hivyo Kama watakatifu tunapoyaona haya kuwa ndani ya Miaka 70 ya Israel ndipo jiji la Yerusalem kunaanza kutambulika kama Jiji la Israel badala ya Palestina,Basi ni wakati ambapo kama Kanisa tunapaswa kujua mwisho upo karibu sana na Yesu yupo karibu sana kurudi kuja kulinyakuwa Kanisa lake
Sipo kukwambia kwamba Yesu anarudi mwaka huu wa 70 wa Taifa la Israel (Hakuna anayejua Saa wala siku atakayorudi mwana wa adamu) ila nipo kukujulisha juu ya majira na dalili za kurudi kwake alizotuachia Yesu ambaye nae hakutaka tukose kuzijua ili Asije akarudi akatukuta hatujajiandaa Kwa kumlaki Bwana Yesu mawinguni
✍Ila ninachoweza kukwambia wewe unaesoma ujumbe kuwa Yesu yupo karibu kurudi wakati wowote kuanzia sasa maana tukio hili la mwisho limeanza kutimizwa leo hii tarehe 14/5/2018 ,hivyo ikiwa umerudi Nyuma huu ni wakati wa kumrudia upya Bwana,Ikiwa bado hujaojoka huu ni wakati wa kuokoka na Ikiwa umechoka huu na wakati wa kuinuka tena na kuanza upya,Ukiwa ni mtakatifu basi zidi kujitakasa zaidi maana siku tusiyodhani ndipo atakapokuja Mwana wa Adamu
✍Jambo lingine nililotaka kukumbusha,Kumbuka ikiwa Israel leo wameshalimiliki Jiji la Yerusalem kama jiji lao basi ujue linalofuata hapo ni kutaka kuubomoa huo *msikiti wa AL-AQSA* na kutaka kujenga tena Hekalu 3 la Suleiman ambapo ndipo litakaposimamishwa Chukizo la Uharibifu mahali patakatifu ambapo Mpinga Kristo atakuwa ameshadhihirishwa tayari.Hivyo unapata kuelewa ni jinsi gani tulivyokuwa tumeshamaliza muda wetu hapa duniani.Kumbuka matukio hayo ya kubomolewa kwa Msikiti na Kuja kwa mpinga Kristo hakutakuwa na Nguvu kabla kanisa Kunyakuliwa Hivyo kumbe kabla ya haya kutokea lazima sisi watakatifu tuwe tumeshanyakuliwa.
*2⃣ MAANDAMANO MAKUBWA YA WAPALESTINA DHIDI YA ISRAEL KUCHUKUA JIJI LAO LA YERUSALEM*
Kama mtu wa rohoni ni Muhimu kuelewa Pamoja matukio haya kwetu yanatupa kujiandaa na kunyakuliwa kanisa ua Kuja kwa Bwana Yesu kulinyakuwa Kanisa lakini upande wa Pili,utakuwa ni mwanzo mkubwa na endelevu wa kuzifungulia kazi za Mpinga Kristo kuanza kufanya kazi kwa nguvu kubwa kuliko wakati wowote *2THETHALONIKE 2:7*
Na moja ya Kazi za Mpinga Kristo zinazotenda kazi baada ya haya yote kutokea siku ya leo 14/5/2018 *(Ufunguzi wa ubalozi wa marekani &Jubilee ya miaka 70 ya Taifa la Israel)* ni hili la Maandamano ya nchi nzima ya wapalestina dhidi ya Israel Kupinga vikali Israel kuchukua jiji lao la Yerusalem
✍Maandamano haya yalianza muda mrefu(15/4/1948) tangu Mwanzoni kabisa mwa Taifa la Israel mara baada ya kutangwa ambapo Wapalestina walifukuzwa kutoka eneo lilikaliwa na israel yaliyopelekea kuketa janga kubwa la kupoteza watu zaidi ya 700,000.Lakini mwaka 1998 ndipo *Rais Yesser arafat* ndipo siku hiyo ikapewa jina la *Catastophe disaster au Siku ya Nakba(Kiarabu) au siku ya janga* ambapo imekuwa ikitumika kuhamashana ili kurudi tena nchini pao( Yaani Eneo wanalokaa Israel Sasa)
✍Ila Maandamano ya Mwaka huu ambayo yanaanza Rasmi leo (15/5/2018) ingawa tangu jana(14/5/2018) tayari walikuwa wameshayaanza ili kuzuia Haya matukio mawili yasitokee ya kusherekea Miaka 70 ya Taifa la Israel na kuzinduliwa kwa Ubalozi wa marekani palaYerusalemu ambapo ndipo pametangazwa kuwa ni Mjii kuu wa Israel ambapo mpaka sasa Wapalestina Maelfu kwa maelfu ya watu wamekusanyika Kuuzunguka Israel na kuta zote za Yerusalem ili kupinga maamuzi haya ya *Rais wa marekani Donald Trump* Kuufanya Yerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Na mpaka sasa watu zaidi ya 50 wamekufa kwenye maandamano hayo na watu zaidi ya 1400 wameumizwa vibaya na kujeruhiwa
Na Vuguvugu hili la maandamano linaloendelea mpaka sasa litakuwa ni Endelevu maana Sasa umekuwa si tu Ugomvi kati ya Israel na Palestina bali Mgogoro kati ya Mataifa yote ya Kiislam yaliyo chini OIC Kuisaidia Palestina katika Vita hivyo na Upande wa pili,Israel kusaidiwa na Marekani pamoja na Mataifa mengi ya kikristo ambayo yanataka kumuunga mkono mmarekani Kwa kufungua balozi zao hapo hapo Yerusalem
Hapa ndipo Mahali pa Msingi kufahamu kama Kanisa au kama watu wa Rohoni tusio vipofu,Kuacha kushabikia haya mambo kisiasa na Kushindana na *DONALD TRUMP* Na kumlaani kwa kitendo anachofanya cha Kuisaidia Israel kuupata mji mkuu wao wa Yerusalem.Kwa hili *Donald Trump(Rais wa Marekani)* anatumiwa na Mungu kwa viwango vya juu kutimiza unabii ule tuliouona Kuhakikisha *YERUSALEM UNAWEKWA HURU KUTOKA KWA MAADUI ZAKE(WAPALESTINA)*
Hivyo kama Kanisa tuyaonapo haya hatunabudi *KUIOMBEA AMANI ISRAEL*,Kumuombea Mmarekani na wote wanaoisadia Israel katika Vita hii na maandamano haya yaliyokusudiwa kufanyika kwa muda mrefu na wakati endelevu kupingana na Israel.Huu ni wakati kila aliye Upande wa Mungu kuitakia heri Israel,Kuiombea Amani na ndipo tutakapofanikiwa kama Maandiko yasemavyo
*♨{ ZABURI 122:6}*
*_" Utakieni Yerusalem Amani(Pray for Peace for Jerusalem) na wote wanaipenda watafanikiwa"_*
✍Ndugu zangu kuna baraka tele tutazipata kama tukiombea sana Israel wakati huu kuliko wakati wowote ndipo tutakapofanikiwa,Vinginevyo tutakaribisha Laana juu ya Laana juu yetu au juu ya nchi zetu.Hivyo tuendelee kukemea kazi za Mpinga Kristo zinazoaanza kufanya kazi nyakati hizi kabla Kanisa halijanyakuliwa,Tuombe na tukemee kuwa mipango yote inayopangwa juu ya Israel isipate kufanikiwa bali tukaone kweli wakiumiliki Mji wao kama ilivyotabiriwa
♂Je umejifunza nini Mpaka hapo? *IKIWA UMEBARIKIWA NA SOMO HILI* basi usiache kushare kwa wengine nao wayafahamu haya kama ulivyofahamu wewe.Share facebook,Share Whatsap group na kwa marafiki zako wote au ndugu zako wote,Ili nae apokee maonyo haya ili yamkini asije akaingia katika mtego wa kuilaani Israel na zaidi asije akaishi tu bila kufanya maandalizi ya maisha na Yesu akarudi bila kumnyakua
Ikiwa hujaokolewa ila baada ya somo hili unahitaji kuokoka basi wasiliana nami kwa namba hapo chini nami nitakuombea upewe Uwezo wa kushinda dhambi na kuokoka ila ikiwa pia umebarikiwa au una swali au unahitaji ushauri pia usisite kuwasiliana nami kwa namba hzio hapo chini. *MUNGU AKUBARIKI*
* Na: Shujaa Charles Mwaisemba*
*0712-054498/0759-420202*
_stmwaisembac@gmail.com_
*Na: Shujaa Charles Mwaisemba*
_▶SHEREHE YA MIAKA 70(JUBEILEE) YA TAIFA LA ISRAEL_
_▶UFUNGUZI WA UBALOZI WA MAREKANI HUKO JERUSALEM_
_▶MAANDAMANO YA WAPALESTINA DHIDI YA ISRAELI_
✍Ili kuweza kuelewa Msingi wa Somo letu,Ni muhimu kuelewa Matukio makuu matatu yaliyotabiriwa na Manabii na Yesu mwenyewe kuwa yatatokea Siku za mwisho kama dalili kuu za kuja kwa Bwana Yesu kulinyakua kanisa lake
*TUKIO LA 1⃣ : _WAYAHUDI WATARUDI KATIKA NCHI YA ISRAEL { YEREMIA 30:3}_*
Wayahudi walikuwa wametawanywa dunia nzima katika mwaka 70B.K,tokea wakati huo,kwa karibu miaka 2000 hawakuwa na nchi iliyokuwa yao wenyewe, ni kwasababu walimfanya Mungu dhambi .
Mara baada ya vita vya pili vya dunia,Mwaka 1945 kuisha Wayahudi kutoka pande zote walianza kujikusanya mmoja mmoja kwa namna kama wanaambia kuwa warudi kwenye nchi yao. Kulianza kufanyika mipango mingi kwenye mabunge na Nchi za Ulaya na marekani kuhusu Israel ndipo kwa ghafla ikiwa kama sauti ya kuambiana imewajia kwa wakati mmoja kuanza kurudi mmoja baada ya wengine na kuwakuta Wenyeji wao Wapalestina katika maeneo hayo
Waingereza pamoja na wamarekani waliwasaidia sana kuwafukuza Wapalestina maeneo Haya ya sasa Ya Israel ili kuwaruhusu Wanaisrael kufika maeneo hayo.Na kwa pamoja ndani ya Muda mfupi wanayahudi walikusanyika na kuwa wengi sana hata kupelekea kuanza kutaka tena Israel litambulike kama Taifa.
*TUKIO LA 2⃣: _ISRAEL LITAKUWA TAIFA TENA_*
Tukio hili litimia katika Mwezi *May 14, 1948* ambapo Israel ikaanza tena kutambulika kama Taifa huru baada ya kupotea katika Uso wa dunia kwa miaka mingi ya nyuma iliyopita .Na Eneo hilo kumilikiwa na Hawa Wapalestina kwa muda wote hivyo tangu wakati huo Wapalestina kufukuzwa kwa nguvu kuwapisha wayahudi sehemu yao ndipo kulipoanza uhasama wa muda mrefu baina ya mataifa haya mawili ambayo wote wanadai Ardhi hiyo ni milki yake.
Hivyo kumekuwepo na mapigano ya Muda mrefu dhidi ya Wayahudi(Wana Israel) na Wapalestina ambapo Israel wanazidi kujitanua kuchukua maeneo na mipaka yao ya zamani iliyokuwepo hadi kwenye maandiko hasa Mpaka kwenye Mji wa Yerusalem ambapo ndipo Ngome pia ya Wapalestina na Waislamu kote ulimwenguni maana ndipo kulipokuwepo Msikiti wao mkubwa unaoheshimika unaoitwa *AL-AQSA* Na huku Israel nao wakidai eneo hilo ni lao kwakuwa ndipo kulipokuwepo na Hekalu la Suleiman
*TUKIO LA 3⃣ : _JIJI LA YERUSALEM LITAKUWA HURU KUTOKA KWA MAADUI ZAKE_*
Kwa tukio hili ndio moyo halisi wa somo letu hili,Na hili ndio tukio pekee ambalo lilikuwa limebaki ambalo halijatimizwa kwa Muda mrefu, na hii ni kutokana na Sababu kwanza mpaka sasa Wapalestina bado wanaamini jiji la Yerusalemu lipo chini yao, maana ndipo Pia upo ule msikiti wa kiislamu
Hapa kuna mambo makuu mawili ya kujifunza na kuyaelewa kama Kanisa au Mtu yeyote anayesoma ujumbe huu na ujue jinsi yalivyo na uhusiano mkubwa na kuja kwa Bwana Wetu Yesu
*1⃣ JUBILEE YA MIAKA 70 YA TAIFA LA ISRAEL NA UFUNGUZI WA UBALOZI WA MAREKANI KATIKA JIJI LA YERUSALEM*
Tukio hili na la Muhimu sana na ni la kinabii kabisa ambalo kila mmoja hapaswi kulichukulia kisiasa na kuona kama ni la kawaida Kwani ndio Kutimia kwa tukio hili la Kuutambua Mji wa Yerusalem kama ndio makao Makuu ya Israel ndio tukio pekee lililokuwa limebaki kama Ishara kubwa ya Kurudi kwa Bwana Yesu kulinyakua kanisa
Jambo hili,la ajabu na la kushangaza,Cha ajabu yake limetokea wakati huu huu ambapo Taifa hili la Israel linatimiza miaka 70 tangu kuwapo kwake (1948-1918).Na cha ajabu leo 14/5/2018 ndio Israel inatimiza miaka 70 kamili ya Kuwepo kwake tangu Tarehe 14/5/1948.Kumbuka wakati nafundisha Somo la dhiki kuu!nilishafundisha maana ya 70 katika unabii jinsi ilivyo na maana kubwa kibiblia(Ikiwa hujajifunza kuhusu hilo wasiliana nami kwa namba hizo chini,nitakupatia masomo hayo niliyofundisha kwa urefu kuhusu miaka 70 hiyo na maana yake)
Sambamba na hili Rais wa Marekani, *Donald Trump* alizungumza maneno mazito ambayo yaliushangaza ulimwengu kwa kutamka Hadharani kuwa anautambua *JIJI LA YERUSALEM KAMA NDIO MAKAO MAKUU MAPYA KWA TAIFA LA ISRAEL BADALA YA TELHAVIV* . Na zaidi siku hii hii ya Leo (14/5/2018) ndio amefungua Ubalozi wake wa Marekani katika jiji hilo hilo la *YERUSALEM KAMA ISHARA YA KUUTAMBULISHA KWA DUNIA KUWA NDIO MAKAO MAKUU PA ISRAEL*
Kumbuka nilikuambia,Hapa Yerusalem ndipo pia Eneo linalomilikiwa na wapalestina kwa Muda mrefu na kudai ni eneo lao kwasababu ya kuwepo na msikiti mkubwa wa kislamu duniani *(Sehemu pa pili panaheshimika kwenye nguzo za kiislam)*
Hivyo Kama watakatifu tunapoyaona haya kuwa ndani ya Miaka 70 ya Israel ndipo jiji la Yerusalem kunaanza kutambulika kama Jiji la Israel badala ya Palestina,Basi ni wakati ambapo kama Kanisa tunapaswa kujua mwisho upo karibu sana na Yesu yupo karibu sana kurudi kuja kulinyakuwa Kanisa lake
Sipo kukwambia kwamba Yesu anarudi mwaka huu wa 70 wa Taifa la Israel (Hakuna anayejua Saa wala siku atakayorudi mwana wa adamu) ila nipo kukujulisha juu ya majira na dalili za kurudi kwake alizotuachia Yesu ambaye nae hakutaka tukose kuzijua ili Asije akarudi akatukuta hatujajiandaa Kwa kumlaki Bwana Yesu mawinguni
✍Ila ninachoweza kukwambia wewe unaesoma ujumbe kuwa Yesu yupo karibu kurudi wakati wowote kuanzia sasa maana tukio hili la mwisho limeanza kutimizwa leo hii tarehe 14/5/2018 ,hivyo ikiwa umerudi Nyuma huu ni wakati wa kumrudia upya Bwana,Ikiwa bado hujaojoka huu ni wakati wa kuokoka na Ikiwa umechoka huu na wakati wa kuinuka tena na kuanza upya,Ukiwa ni mtakatifu basi zidi kujitakasa zaidi maana siku tusiyodhani ndipo atakapokuja Mwana wa Adamu
✍Jambo lingine nililotaka kukumbusha,Kumbuka ikiwa Israel leo wameshalimiliki Jiji la Yerusalem kama jiji lao basi ujue linalofuata hapo ni kutaka kuubomoa huo *msikiti wa AL-AQSA* na kutaka kujenga tena Hekalu 3 la Suleiman ambapo ndipo litakaposimamishwa Chukizo la Uharibifu mahali patakatifu ambapo Mpinga Kristo atakuwa ameshadhihirishwa tayari.Hivyo unapata kuelewa ni jinsi gani tulivyokuwa tumeshamaliza muda wetu hapa duniani.Kumbuka matukio hayo ya kubomolewa kwa Msikiti na Kuja kwa mpinga Kristo hakutakuwa na Nguvu kabla kanisa Kunyakuliwa Hivyo kumbe kabla ya haya kutokea lazima sisi watakatifu tuwe tumeshanyakuliwa.
*2⃣ MAANDAMANO MAKUBWA YA WAPALESTINA DHIDI YA ISRAEL KUCHUKUA JIJI LAO LA YERUSALEM*
Kama mtu wa rohoni ni Muhimu kuelewa Pamoja matukio haya kwetu yanatupa kujiandaa na kunyakuliwa kanisa ua Kuja kwa Bwana Yesu kulinyakuwa Kanisa lakini upande wa Pili,utakuwa ni mwanzo mkubwa na endelevu wa kuzifungulia kazi za Mpinga Kristo kuanza kufanya kazi kwa nguvu kubwa kuliko wakati wowote *2THETHALONIKE 2:7*
Na moja ya Kazi za Mpinga Kristo zinazotenda kazi baada ya haya yote kutokea siku ya leo 14/5/2018 *(Ufunguzi wa ubalozi wa marekani &Jubilee ya miaka 70 ya Taifa la Israel)* ni hili la Maandamano ya nchi nzima ya wapalestina dhidi ya Israel Kupinga vikali Israel kuchukua jiji lao la Yerusalem
✍Maandamano haya yalianza muda mrefu(15/4/1948) tangu Mwanzoni kabisa mwa Taifa la Israel mara baada ya kutangwa ambapo Wapalestina walifukuzwa kutoka eneo lilikaliwa na israel yaliyopelekea kuketa janga kubwa la kupoteza watu zaidi ya 700,000.Lakini mwaka 1998 ndipo *Rais Yesser arafat* ndipo siku hiyo ikapewa jina la *Catastophe disaster au Siku ya Nakba(Kiarabu) au siku ya janga* ambapo imekuwa ikitumika kuhamashana ili kurudi tena nchini pao( Yaani Eneo wanalokaa Israel Sasa)
✍Ila Maandamano ya Mwaka huu ambayo yanaanza Rasmi leo (15/5/2018) ingawa tangu jana(14/5/2018) tayari walikuwa wameshayaanza ili kuzuia Haya matukio mawili yasitokee ya kusherekea Miaka 70 ya Taifa la Israel na kuzinduliwa kwa Ubalozi wa marekani palaYerusalemu ambapo ndipo pametangazwa kuwa ni Mjii kuu wa Israel ambapo mpaka sasa Wapalestina Maelfu kwa maelfu ya watu wamekusanyika Kuuzunguka Israel na kuta zote za Yerusalem ili kupinga maamuzi haya ya *Rais wa marekani Donald Trump* Kuufanya Yerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Na mpaka sasa watu zaidi ya 50 wamekufa kwenye maandamano hayo na watu zaidi ya 1400 wameumizwa vibaya na kujeruhiwa
Na Vuguvugu hili la maandamano linaloendelea mpaka sasa litakuwa ni Endelevu maana Sasa umekuwa si tu Ugomvi kati ya Israel na Palestina bali Mgogoro kati ya Mataifa yote ya Kiislam yaliyo chini OIC Kuisaidia Palestina katika Vita hivyo na Upande wa pili,Israel kusaidiwa na Marekani pamoja na Mataifa mengi ya kikristo ambayo yanataka kumuunga mkono mmarekani Kwa kufungua balozi zao hapo hapo Yerusalem
Hapa ndipo Mahali pa Msingi kufahamu kama Kanisa au kama watu wa Rohoni tusio vipofu,Kuacha kushabikia haya mambo kisiasa na Kushindana na *DONALD TRUMP* Na kumlaani kwa kitendo anachofanya cha Kuisaidia Israel kuupata mji mkuu wao wa Yerusalem.Kwa hili *Donald Trump(Rais wa Marekani)* anatumiwa na Mungu kwa viwango vya juu kutimiza unabii ule tuliouona Kuhakikisha *YERUSALEM UNAWEKWA HURU KUTOKA KWA MAADUI ZAKE(WAPALESTINA)*
Hivyo kama Kanisa tuyaonapo haya hatunabudi *KUIOMBEA AMANI ISRAEL*,Kumuombea Mmarekani na wote wanaoisadia Israel katika Vita hii na maandamano haya yaliyokusudiwa kufanyika kwa muda mrefu na wakati endelevu kupingana na Israel.Huu ni wakati kila aliye Upande wa Mungu kuitakia heri Israel,Kuiombea Amani na ndipo tutakapofanikiwa kama Maandiko yasemavyo
*♨{ ZABURI 122:6}*
*_" Utakieni Yerusalem Amani(Pray for Peace for Jerusalem) na wote wanaipenda watafanikiwa"_*
✍Ndugu zangu kuna baraka tele tutazipata kama tukiombea sana Israel wakati huu kuliko wakati wowote ndipo tutakapofanikiwa,Vinginevyo tutakaribisha Laana juu ya Laana juu yetu au juu ya nchi zetu.Hivyo tuendelee kukemea kazi za Mpinga Kristo zinazoaanza kufanya kazi nyakati hizi kabla Kanisa halijanyakuliwa,Tuombe na tukemee kuwa mipango yote inayopangwa juu ya Israel isipate kufanikiwa bali tukaone kweli wakiumiliki Mji wao kama ilivyotabiriwa
♂Je umejifunza nini Mpaka hapo? *IKIWA UMEBARIKIWA NA SOMO HILI* basi usiache kushare kwa wengine nao wayafahamu haya kama ulivyofahamu wewe.Share facebook,Share Whatsap group na kwa marafiki zako wote au ndugu zako wote,Ili nae apokee maonyo haya ili yamkini asije akaingia katika mtego wa kuilaani Israel na zaidi asije akaishi tu bila kufanya maandalizi ya maisha na Yesu akarudi bila kumnyakua
Ikiwa hujaokolewa ila baada ya somo hili unahitaji kuokoka basi wasiliana nami kwa namba hapo chini nami nitakuombea upewe Uwezo wa kushinda dhambi na kuokoka ila ikiwa pia umebarikiwa au una swali au unahitaji ushauri pia usisite kuwasiliana nami kwa namba hzio hapo chini. *MUNGU AKUBARIKI*
* Na: Shujaa Charles Mwaisemba*
*0712-054498/0759-420202*
_stmwaisembac@gmail.com_