Smart boy Shewedy
JF-Expert Member
- Jan 17, 2017
- 3,691
- 3,426
Kupambana wanaweza wakapambana sana lakini unadhani wanaweza kumshinda Marekani kule Amerika Kusini ?? Ni sawa na leo hii useme kwamba Marekani anaweza akashindana na Urusi kule Ulaya Mashariki halafu akashinda kirahisi.
Kuna kitu mkuu Elungata alikisema juzi na watu wakapuuza. Marekani akivamia Venezuela kimabavu basi Urusi naye atapata kisingizio cha kuvamia Ukraine kimabavu na hata Uchina naye atapata kisingizio cha kufanya vurugu kwenye the South China Sea.
Marekani atakuwa ametengeneza precedent mbaya sana na kufungua Pandora Box ambapo kutakuwa na fujo duniani kote.
Huyo anajiandalia mazingira ya kuwa mkimbizi wa kisiasa!! Sitashangaa akiibukia kwenye ubalozi wa Taifa lolote la Magharibi linalomuunga mkono akiomba ukimbizi! Huyu ni msaliti sijapata kuona!! Yuko Tayari kukaribisha Taifa lenye lengo la kupora mafuta yao!Given the current situation; that is easier said than done.
Wamarekani ninaowajua...kama hawaoni hatari yoyote ya kuvamia...hawasubiri cha sababu. Kuna uwezekano mipini iliyowekwa na Russia na China kidiplomasia na kiusalama..bado inamtatiza. Ebu fikiria, US aingie kichwa kichwa pale Caracas...halafu atolewe nishai kama pale Damascus aibu wataiweka wapi...na hapo ndiyo itakuwa fursa ya nchi hizo za Amerika ya Kusini zitamgeuka US mara moja na kujitangazia uhuru kamili!!!(Nawaza)Siyo mpole, anajua akifanya ujinga tu kule Washington watapata kisingizio kizuri cha kumvamia. Tena watamtwanga hataamini, maana sidhani kama kuna nchi inaweza ikashindana na Marekani kule Amerika Kusini halafu ikabaki salama.
Mkuu si umesema kule Amerika ya kusini(AK) US anawashirika wengi...sas wasi wasi wake nini ukanda kuchafuka wakati yeye ana wafuasi wengi!?Mwisho kabisa Marekani anacheza vizuri kwasababu anajua kama Venezuela itachafuka basi ule ukanda wote utachafuka kama ilivyo mashariki ya kati.
Wamarekani ninaowajua...kama hawaoni hatari yoyote ya kuvamia...hawasubiri cha sababu. Kuna uwezekano mipini iliyowekwa na Russia na China kidiplomasia na kiusalama..bado inamtatiza. Ebu fikiria, US aingie kichwa kichwa pale Caracas...halafu atolewe nishai kama pale Damascus aibu wataiweka wapi...na hapo ndiyo itakuwa fursa ya nchi hizo za Amerika ya Kusini zitamgeuka US mara moja na kujitangazia uhuru kamili!!!(Nawaza)
Nadhani kuna vitu vya muhimu sana ambavyo lazima tuviweke sawa hapa. Mosi, International Order is interconnected and affected by great power politics. Hakuna kitu kitakochofanywa na taifa kubwa halafu kisiwe na madhara kwa jumuiya ya kimataifa, iwe kisheria, iwe kiuchumi au kisiasa: Venezuela ni dhahiri kabisa hawezi kupigana na Marekani hata kama Urusi na Uchina wako pale.Mkuu si umesema kule Amerika ya kusini(AK) US anawashirika wengi...sas wasi wasi wake nini ukanda kuchafuka wakati yeye ana wafuasi wengi!?
Ngoja niseme tu kuwa Malcom Lumumba upo juu sana siasa za kimaifa, yaani navutiwa kusoma michango yako, ila za huku kwa jiwe vepeee!?Nadhani kuna kitu cha muhimu sana ambavyo lazima tuviweke sawa hapa. Mosi, International Order is interconnected and affected by great power politics. Hakuna kitu kitakochofanywa na taifa kubwa halafu kisiwe na madhara kwa jumuiya ya kimataifa, iwe kisheria, iwe kiuchumi au kisiasa: Venezuela ni dhahiri kabisa hawezi kupigana na Marekani hata kama Urusi na Uchina wako pale.
Historia inatufundisha hivyo, na tunafahamu kwamba tukiitoa CUBA, Marekani amefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuwashinda wakomunisti walipojaribu kupeleka ushawishi wao kule Amerika Kusini. CUBA alipona kwasababu ya makubaliano baina ya Krushchev na Kennedy kwamba isitishiwe tena kijeshi na uhuru wake uheshimike.
Sasa Marekani hata kama ana uwezo wa kuvamia kijeshi na kumwondoa Maduro lazima ifikirie mbele kwamba nini kitatokea Venezuela baada ya Maduro, na madhara yake kwenye siasa za kimataifa. Vivyo hivyo nikasema leo hata Urusi ana uwezo mkubwa sana wa kumtwanga Ukraine, Poland, Latvia na Lithuania ndani ya masaa tu, lakini unadhani kutakuwa hakuna madhara yoyote yale kwenye siasa za dunia ??
Pili, kuna jambo moja muhimu sana analolisemaga Prof John Mearshimer kwamba "History is never linear". Kuna mambo mengi yanaweza kutokea hapo katikati ambayo hata mataifa makubwa hayakutarajia kuyaona. Marekani amejifunza Afghanistani, Iraq, Libya na Syria kwamba kuvamia nchi na kupindua uongozi ni kitu kingine na kutengeneza mfumo mpya ni kitu kingine kabisa (Tena hichi cha pili ndicho kigumu kuliko vyote).
Tatu, anachokifanya Vladmir Putin pale Venezuela ni kilekile ambacho alikifanya Krushchev miaka ya 50 baada ya Marekani kuweka makombora ya Jupiter na Thor kule Uturuki kwenye mpaka wa Urusi ya Kisovieti. Nikita Kruschev alisema hivi "I will show Americans how it feels to have weapons of mass destruction placed on your door step" akapeleka makombora kule CUBA. Lakini ukweli ambao ni mchungu ni huu, Urusi mbali na CUBA na Bolivia unadhani anaweza kupambana na Marekani kirahisi rahisi tu ?
Mfano wako wa Syria ni dhahiri kabisa, lakini kuna kitu cha muhimu umekisahau kabisa: Umoja ambao ulikuwa unapingana na Assad na Urusi ulikuwa umevunjika wenyewe tokea mwanzo.
Waandishi wakubwa wa siasa za Mashariki ya Kati kama Sharmine Narwani wanasema hivi: Washikrika wakuu wanaompinga Assad walikuwa hawazungumzi lugha moja. Qatar alikuwa anazungumza lugha moja na Uturuki, lakini amegombana na Saudi Arabia na Marekani. Uturuki anampinga Assad lakini Marekani anawaunga mkono Wakurdi ambao ni adui wa Uturuki. Saudi Arabia na Qatar walikuwa hawaelewani kabisa, huku Marekani akitaka kumuua Raisi wa Uturuki" Leo hii Marekani amesema anaunda kikosi kipya chenye wapiganaji kama 30000 ili kumpiga Assad lakini Uturuki kasema atawatandika kwasababu ni magaidi. Upande mwingine Qatar na Iran wanaanza kuzungumza lugha moja.
Maswali:
Hebu tujadili.....
- Hivi unadhani Uturuki angekuwa upande wa Marekani tokea mwanzo unahisi Urusi angefurukuta kirahisi ?? Kwanza kupita pale kwenye The Bosphorous kuelekea Meditteranean ingekuwa ni rahisi ??
- Kupamba na waasi ilikuwa ni lazima ndege za Urusi zitumie anga la Uturuki. Uturuki alivyotungua ndege ya Urusi mambo yalikuwa siyo mambo na Putin alichukia sana. Lakini unadhani kwanini Putin aliamua kumuokoa Erdogan asife wakati CIA walipotaka kumfanyizia ??(Putin alitumia huu mwanya kuendelea kuwagawanya)
- Unadhani kwanini Marekani ilifika mbali sana na kuamua kumpindua Erdogan ?? Unadhani utawala ambao ungewekwa baada ya Erdogan ungekuwa ni rafiki kwa Urusi, Iran na Syria ?? Unadhani Urusi angeendelea kutumia anga la Urusi ??
- Turudi kule Amerika Kusini: Unadhani kuna nchi ya Amerika Kusini ambayo inaweza kumsumbua au kumpinga Marekani akisema chochote dhidi ya Venezuela ukiwatoa CUBA na Bolivia ?? Unadhani Urusi atakuwa na nguvu ile ile aliyonayo kule Ulaya Mashariki na Mashariki ya Kati ??
Nikitoka villa park nitakuja kubishaNadhani kuna vitu vya muhimu sana ambavyo lazima tuviweke sawa hapa. Mosi, International Order is interconnected and affected by great power politics. Hakuna kitu kitakochofanywa na taifa kubwa halafu kisiwe na madhara kwa jumuiya ya kimataifa, iwe kisheria, iwe kiuchumi au kisiasa: Venezuela ni dhahiri kabisa hawezi kupigana na Marekani hata kama Urusi na Uchina wako pale.
Historia inatufundisha hivyo, na tunafahamu kwamba tukiitoa CUBA, Marekani amefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuwashinda wakomunisti walipojaribu kupeleka ushawishi wao kule Amerika Kusini. CUBA alipona kwasababu ya makubaliano baina ya Krushchev na Kennedy kwamba isitishiwe tena kijeshi na uhuru wake uheshimike.
Sasa Marekani hata kama ana uwezo wa kuvamia kijeshi na kumwondoa Maduro lazima ifikirie mbele kwamba nini kitatokea Venezuela baada ya Maduro, na madhara yake kwenye siasa za kimataifa. Vivyo hivyo nikasema leo hata Urusi ana uwezo mkubwa sana wa kumtwanga Ukraine, Poland, Latvia na Lithuania ndani ya masaa tu, lakini unadhani kutakuwa hakuna madhara yoyote yale kwenye siasa za dunia ??
Pili, kuna jambo moja muhimu sana analolisemaga Prof John Mearshimer kwamba "History is never linear". Kuna mambo mengi yanaweza kutokea hapo katikati ambayo hata mataifa makubwa hayakutarajia kuyaona. Marekani amejifunza Afghanistani, Iraq, Libya na Syria kwamba kuvamia nchi na kupindua uongozi ni kitu kingine na kutengeneza mfumo mpya ni kitu kingine kabisa (Tena hichi cha pili ndicho kigumu kuliko vyote).
Tatu, anachokifanya Vladmir Putin pale Venezuela ni kilekile ambacho alikifanya Krushchev miaka ya 50 baada ya Marekani kuweka makombora ya Jupiter na Thor kule Uturuki kwenye mpaka wa Urusi ya Kisovieti. Nikita Kruschev alisema hivi "I will show Americans how it feels to have weapons of mass destruction placed on your door step" akapeleka makombora kule CUBA. Lakini ukweli ambao ni mchungu ni huu, Urusi mbali na CUBA na Bolivia unadhani anaweza kupambana na Marekani kirahisi rahisi tu ?
Mfano wako wa Syria ni dhahiri kabisa, lakini kuna kitu cha muhimu umekisahau kabisa: Umoja ambao ulikuwa unapingana na Assad na Urusi ulikuwa umevunjika wenyewe tokea mwanzo.
Waandishi wakubwa wa siasa za Mashariki ya Kati kama Sharmine Narwani wanasema hivi: Washikrika wakuu wanaompinga Assad walikuwa hawazungumzi lugha moja. Qatar alikuwa anazungumza lugha moja na Uturuki, lakini amegombana na Saudi Arabia na Marekani. Uturuki anampinga Assad lakini Marekani anawaunga mkono Wakurdi ambao ni adui wa Uturuki. Saudi Arabia na Qatar walikuwa hawaelewani kabisa, huku Marekani akitaka kumuua Raisi wa Uturuki" Leo hii Marekani amesema anaunda kikosi kipya chenye wapiganaji kama 30000 ili kumpiga Assad lakini Uturuki kasema atawatandika kwasababu ni magaidi. Upande mwingine Qatar na Iran wanaanza kuzungumza lugha moja.
Maswali:
Hebu tujadili.....
- Hivi unadhani Uturuki angekuwa upande wa Marekani tokea mwanzo unahisi Urusi angefurukuta kirahisi ?? Kwanza kupita pale kwenye The Bosphorous kuelekea Meditteranean ingekuwa ni rahisi ?? Hii ni moja ya sababu mpaka leo Uturuki amekataa kusaini ule mkataba uitwao The United Nations Convention on the law of the Sea of 1982.
- Kupambana na waasi ilikuwa ni lazima ndege za Urusi zitumie anga la Uturuki. Uturuki alivyotungua ndege ya Urusi mambo yalikuwa siyo mambo na Putin alichukia sana. Lakini unadhani kwanini Putin aliamua kumuokoa Erdogan asife wakati CIA walipotaka kumfanyizia ??(Putin alitumia huu mwanya kuendelea kuwagawanya)
- Unadhani kwanini Marekani ilifika mbali sana na kuamua kumpindua Erdogan ?? Unadhani utawala ambao ungewekwa baada ya Erdogan ungekuwa ni rafiki kwa Urusi, Iran na Syria ?? Unadhani Urusi angeendelea kutumia anga la Urusi ??
- Turudi kule Amerika Kusini: Unadhani kuna nchi ya Amerika Kusini ambayo inaweza kumsumbua au kumpinga Marekani akisema chochote dhidi ya Venezuela ukiwatoa CUBA na Bolivia ?? Unadhani Urusi atakuwa na nguvu ile ile aliyonayo kule Ulaya Mashariki na Mashariki ya Kati ??
Kama unataka kubishana nenda kwenye vijiwe vya kahawa, lakini kama unataka mjadala nakukaribisha kwa mikono miwili.Nikitoka villa park nitakuja kubisha
Sent using my iPhone using jamiiforum app
Kama unataka kubishana nenda kwenye vijiwe vya kahawa, lakini kama unataka mjadala nakukaribisha kwa mikono miwili.
SawaSasa mjadala utoke wap tena aliyakuwa umeeleza vizuri na kwa fact lkn pale kwa China siwezi kukubari aise japo najua atashinda lakini kwa mbinde saana
Sent using my iPhone using jamiiforum app
Asante sana mkuu kwa bandiko lako hili. Niwie radhi kwa kuchelewa kujibu hoja zako kimjadala kama ulivyozianisha kwenye bandiko. Hoja zako nimekubaliana nazo; zile ambazo nimezitazama kiutofauti nimezipa herufi kuanzia (a) mpaka (f) kwenye nukuu na utofauti huo nimeueleza hapa chini. Pia maswali yako nimeyajibu kwa mtirirko ule ule ulioutoa.(a) ..... Venezuela ni dhahiri kabisa hawezi kupigana na Marekani hata kama Urusi na Uchina wako pale....
(b) ....CUBA alipona kwasababu ya makubaliano baina ya Krushchev na Kennedy kwamba isitishiwe tena kijeshi na uhuru wake uheshimike...
(c)..... Pili, kuna jambo moja muhimu sana analolisemaga Prof John Mearshimer kwamba "History is never linear". Kuna mambo mengi yanaweza kutokea hapo katikati ambayo hata mataifa makubwa hayakutarajia kuyaona.
(d) .... Marekani amejifunza Afghanistani, Iraq, Libya na Syria kwamba kuvamia nchi na kupindua uongozi ni kitu kingine na kutengeneza mfumo mpya ni kitu kingine kabisa (Tena hichi cha pili ndicho kigumu kuliko vyote).
(e).... Lakini ukweli ambao ni mchungu ni huu, Urusi mbali na CUBA na Bolivia unadhani anaweza kupambana na Marekani kirahisi rahisi tu ?
(f)... Mfano wako wa Syria ni dhahiri kabisa, lakini kuna kitu cha muhimu umekisahau kabisa: Umoja ambao ulikuwa unapingana na Assad na Urusi ulikuwa umevunjika wenyewe tokea mwanzo. ...
Waandishi wakubwa wa siasa za Mashariki ya Kati kama Sharmine Narwani wanasema hivi: Washikrika wakuu wanaompinga Assad walikuwa hawazungumzi lugha moja. Qatar alikuwa anazungumza lugha moja na Uturuki, lakini amegombana na Saudi Arabia na Marekani. Uturuki anampinga Assad lakini Marekani anawaunga mkono Wakurdi ambao ni adui wa Uturuki. Saudi Arabia na Qatar walikuwa hawaelewani kabisa, huku Marekani akitaka kumuua Raisi wa Uturuki" Leo hii Marekani amesema anaunda kikosi kipya chenye wapiganaji kama 30000 ili kumpiga Assad lakini Uturuki kasema atawatandika kwasababu ni magaidi. Upande mwingine Qatar na Iran wanaanza kuzungumza lugha moja.
======
Maswali:
Hebu tujadili.....
- Hivi unadhani Uturuki angekuwa upande wa Marekani tokea mwanzo unahisi Urusi angefurukuta kirahisi ?? Kwanza kupita pale kwenye The Bosphorous kuelekea Meditteranean ingekuwa ni rahisi ?? Hii ni moja ya sababu mpaka leo Uturuki amekataa kusaini ule mkataba uitwao The United Nations Convention on the law of the Sea of 1982.
- Kupambana na waasi ilikuwa ni lazima ndege za Urusi zitumie anga la Uturuki. Uturuki alivyotungua ndege ya Urusi mambo yalikuwa siyo mambo na Putin alichukia sana. Lakini unadhani kwanini Putin aliamua kumuokoa Erdogan asife wakati CIA walipotaka kumfanyizia ??(Putin alitumia huu mwanya kuendelea kuwagawanya)
- Unadhani kwanini Marekani ilifika mbali sana na kuamua kumpindua Erdogan ?? Unadhani utawala ambao ungewekwa baada ya Erdogan ungekuwa ni rafiki kwa Urusi, Iran na Syria ?? Unadhani Urusi angeendelea kutumia anga la Uturuki ??
- Turudi kule Amerika Kusini: Unadhani kuna nchi ya Amerika Kusini ambayo inaweza kumsumbua au kumpinga Marekani akisema chochote dhidi ya Venezuela ukiwatoa CUBA na Bolivia ?? Unadhani Urusi atakuwa na nguvu ile ile aliyonayo kule Ulaya Mashariki na Mashariki ya Kati ??
Mufti umejificha wapi yakheee!
Kashafungwa😆😆😆😆😆😆Kiongozi wa upinzani Venezuela anakabiliwa na kifungo cha miaka 30 jela
Feb 27, 2019 08:04 UTC
Juan Guaidó, kiongozi wa upinzani aliyejitangaza kuwa rais wa mpito wa Venezuela anaandamwa na kifungo cha miaka 30 jela.
Hayo yamesemwa na Juan Carlos Valdez, Naibu Jaji wa Jopo la Haki la Mahakama ya Juu nchini humo katika mahojiano na shirika la habari la Sputnik la Russia na kuongeza kuwa, hatua ya Guaido ya kwenda Colombia mnamo Februari 22 ilikiuka agizo la kumtaka asitoke nje ya nchi, lililotolewa na Mahakama ya Juu nchini humo, na hivyo amejiweka katika hatari ya kufungwa miaka 30 jela.
Amefafanua kuwa, "Guiado ni mtu anayekwepa sheria. Kitendo cha kutoroka nchini kinyume cha sheria na kisha kurejea hukumu yake ni kifungo cha hadi miaka 30 jela."
Venezuela ilitumbukia katika mzozo wa kisiasa mwishoni mwa mwezi jana baada ya Juan Guaidó, kiongozi wa upinzani kujitangaza kuwa rais wa muda wa nchi hiyo.
Hatua hiyo iliyotekelezwa tarehe 23 Januari 2019, iliungwa mkono na Marekani na nchi za Ulaya, huku serikali ya Caracas ikiitaja kuwa ni sawa na tangazo la mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Rais Nicolás Maduro.
Licha ya uungaji mkono wa hali na mali wa Marekani na kambi ya Magharibi kwa Juan Guaidó, lakini raia na jeshi la Venezuela pamoja na mataifa kama vile Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Russia, China, Mexico, Uturuki, Afrika Kusini na Italia wameendelea kumuunga mkono Rais Nicolás Maduro anayetambulika kisheria.
Tags
VENEZUELA