Juan Guaido wa Venezuela kufungwa miaka 30 jela

Moscow siku hizi hapigani vita za kiitakadi kama umoja wa kisovieti. Hapa ni maslahi tu ya kiuchumi na mzani wa nguvu, ujamaa dhidi ya ubepari hakuna siku hizi. Kule Syria Urusi hakwenda kulinda ujamaa bali maslahi yake ya kiuchumi. Kule Ukraine Marekani ameenda kwasababu za maslahi ya kiuchumi na siyo vita dhidi ya wajamaa.

Ujamaa umekufa na hauna nguvu tena kwenye dunia hii ya sasa, kule Venezuela Uchina na Urusi wanapiga kelele kwasababu wana maslahi mapana ya kiuchumi. Wameikopesha sana serikali ya maduro kipindi kile imekutwa na majanga ya kiuchumi. Juzi hapa ameenda Uchina kuomba mkopo na kukubaliana kwamba watalipa mkopo kwa kutumia mafuta. Hii ni neema kwa Uchina.

Mbali na hilo imegundulika kwamba Venezuela ndiyo nchi yenye mafuta mengi hapa duniani, Uchina atayataka na Marekani anayataka.

Upande wa pili wa shilingi kama Marekani atafanikiwa kukamata utajiri wa mafuta wa Venezuela unategemea Urusi atapona kwenye soko la dunia la mafuta ?? Marekani atakuwa anacheza na bei za mafuta kama anavyofanya kule Saudi Arabia ili kuwaumiza warusi ambao asilimia zaidi ya 50% ya pato la taifa hutegemea mafuta.

Kuna mambo ya kuyaangalia sana, Urusi kupambana na Marekani kule Venezuela ni ngumu sana kwasababu mbali na Cuba sidhani kama ana washirika wenye nguvu. Kule Syria ilikuwa ni rahisi kwasababu alikuwa na washirika vyuma kama Iran, Lebanon na Hezbollah. Venezuela ni tofauti kidogo kwasababu Marekani ndiyo ana washirika wengi sana ambao wameizunguka Venezuela. Colombia na Venezuela wanashare mpaka wa kilomita zaidi ya 2000. Vikosi vya Marekani viko Columbia mpaka sasa.

Mwisho kabisa Marekani anacheza vizuri kwasababu anajua kama Venezuela itachafuka basi ule ukanda wote utachafuka kama ilivyo mashariki ya kati. Colombia hatapona. Serikali ya maduro ikianguka kutakuwa na ombwe la madaraka ambalo litapelekea makundi madogo madogo kuzaliwa, biashara haramu kutoka colombia na wimbi la wakimbizi ambalo kama likienda Colombia basi lazima kitanuka tu....
Safi saana umeeleza vizuri sana

Sasa kama ni maslahi yao basi watamsaidia maduro kufa kupona na kwa bahati nzuri China this time now lazima aingie mazima ili kurinda maslahi yake sasa tayari urusi ana mshirika mwenye nguvu

All in all hii Venezuela ni muhimu saana kwa urusi na China kuliko USA alafu hawa Colombia nchini kwao si kuna kundi la waasi wanaotaka kuangusha utawala?

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Safi saana umeeleza vizuri sana

Sasa kama ni maslahi yao basi watamsaidia maduro kufa kupona na kwa bahati nzuri China this time now lazima aingie mazima ili kurinda maslahi yake sasa tayari urusi ana mshirika mwenye nguvu

All in all hii Venezuela ni muhimu saana kwa urusi na China kuliko USA alafu hawa Colombia nchini kwao si kuna kundi la waasi wanaotaka kuangusha utawala?

Sent using my iPhone using jamiiforum app
Venezuela ni muhimu sana kwa Marekani tokea kitambo na wana historia ndefu sana. Hivi unajua kipindi chote cha vita ya pili ya dunia Marekani alikuwa ananunua mafuta ya Venezuela ? Mpaka leo hii na vikwazo bado Marekani ananunua mafuta ya Venezuela.

Venezuela ni moja ya wanufaika wakubwa wa Lend-Lease Programme ya Raisi Franklin Roosevelt na wao walikuwa kati ya nchi 10 zilizopewa msaada na Marekani ili waweze kuzalisha mafuta kwa wingi.

Marekani akipata visima vya mafuta vya Venezuela basi atapunguza utegemezi kula Saudi Arabia na atakuwa ni tajiri sana. International Energy Agency wanasema kwamba hadi kufika mwaka 2030 mafuta yatakuwa yanauzika sana na soko kubwa litakuwa kule Asia likiongozwa na India na Uchina.

Matumizi makubwa ya mafuta kwenye miaka 50 ijayo yatakuwa ni kwenye Petro-Chemicals kuliko Gasoline. Petro-Chemicals ndizo zinatumika kutengenezea madawa yako unayokunywa ili usiumwe, Plastiki na Mbolea.

Asilimia zaidi y 12% ya mafuta ya duniani leo hii ni kwenye matumizi ya Petro-Chemicals na hiyo inayobaki ndiyo hutumika kuendeshea mitambo. Sasa miaka ijayo ongezeko la watu litafanya mafuta yazalishwe kwa wingi. Uchina na India watahitaji sana mafuta kwa ajili ya Petro-Chemicals ambazo huzalisha madawa, plastiki na mbolea.

Hivyo kama Marekani ndiyo atakuwa anamiliki vyanzo vingi vya mafuta hapa duniani pamoja na kuwa ndiye muuzaji mkuu akiwauzia mataifa makubwa kama India na Uchina basi atakuwa ndiyo anacheza na siasa ya dunia.

Wenzetu hawa wamepewa akili na Mungu ya kuangalia miaka 50 mbele. Hivyo kule Venezuela Marekani is there to stay.....

CC: Wick
 
Venezuela ni muhimu sana kwa Marekani tokea kitambo na wana historia ndefu sana. Hivi unajua kipindi chote cha vita ya pili ya dunia Marekani alikuwa ananunua mafuta ya Venezuela ? Mpaka leo hii na vikwazo bado Marekani ananunua mafuta ya Venezuela.

Venezuela ni moja ya wanufaika wakubwa wa Lend-Lease Programme ya Raisi Franklin Roosevelt na wao walikuwa kati ya nchi 10 zilizopewa msaada na Marekani ili waweze kuzalisha mafuta kwa wingi.

Marekani akipata visima vya mafuta vya Venezuela basi atapunguza utegemezi kula Saudi Arabia na atakuwa ni tajiri sana. International Energy Agency wanasema kwamba hadi kufika mwaka 2030 mafuta yatakuwa yanauzika sana na soko kubwa litakuwa kule Asia likiongozwa na India na Uchina.

Matumizi makubwa ya mafuta kwenye miaka 50 ijayo yatakuwa ni kwenye Petro-Chemicals kuliko Gasoline. Petro-Chemicals ndizo zinatumika kutengenezea madawa yako unayokunywa ili usiumwe, Plastiki na Mbolea.

Asilimia zaidi y 12% ya mafuta ya duniani leo hii ni kwenye matumizi ya Petro-Chemicals na hiyo inayobaki ndiyo hutumika kuendeshea mitambo. Sasa miaka ijayo ongezeko la watu litafanya mafuta yazalishwe kwa wingi. Uchina na India watahitaji sana mafuta kwa ajili ya Petro-Chemicals ambazo huzalisha madawa, plastiki na mbolea.

Hivyo kama Marekani ndiyo atakuwa anamiliki vyanzo vingi vya mafuta hapa duniani pamoja na kuwa ndiye muuzaji mkuu akiwauzia mataifa makubwa kama India na Uchina basi atakuwa ndiyo anacheza na siasa ya dunia.

Wenzetu hawa wamepewa akili na Mungu ya kuangalia miaka 50 mbele. Hivyo kule Venezuela Marekani is there to stay.....
Fact

Sasa huoni kuwa urusi na China watapambana ili USA asifanikiwe hapo maana akitusua tu wameisha

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Fact

Sasa huoni kuwa urusi na China watapambana ili USA asifanikiwe hapo maana akitusua tu wameisha

Sent using my iPhone using jamiiforum app
Kupambana wanaweza wakapambana sana lakini unadhani wanaweza kumshinda Marekani kule Amerika Kusini ?? Ni sawa na leo hii useme kwamba Marekani anaweza akashindana na Urusi kule Ulaya Mashariki halafu akashinda kirahisi.

Kuna kitu mkuu Elungata alikisema juzi na watu wakapuuza. Marekani akivamia Venezuela kimabavu basi Urusi naye atapata kisingizio cha kuvamia Ukraine kimabavu na hata Uchina naye atapata kisingizio cha kufanya vurugu kwenye the South China Sea.

Marekani atakuwa ametengeneza precedent mbaya sana na kufungua Pandora Box ambapo kutakuwa na fujo duniani kote.
 
Kupambana wanaweza wakapambana sana lakini unadhani wanaweza kumshinda Marekani kule Amerika Kusini ?? Ni sawa na leo hii useme kwamba Marekani anaweza akashindana na Urusi kule Ulaya Mashariki halafu akashinda kirahisi.

Kuna kitu mkuu Elungata alikisema juzi na watu wakapuuza. Marekani akivamia Venezuela kimabavu basi Urusi naye atapata kisingizio cha kuvamia Ukraine kimabavu na hata Uchina naye atapata kisingizio cha kufanya vurugu kwenye the South China Sea.

Marekani atakuwa ametengeneza precedent mbaya sana na kufungua Pandora Box ambapo kutakuwa na fujo duniani kote.
Dah pia rwanda wataivamia burundi

Sasa kwanini urusi wavamie Ukraine na why China wafanye vurugu ukanda wake

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Moscow ana nguvu na ushawishi lakini sidhani kama na nguvu kiasi hicho kule Amerika Kusini kama ambavyo ana nguvu kule Syria. Sema Marekani anaogopa kwamba akiivamia Venezuela basi anaweza hatarisha hata usalama wake mwenyewe hivyo anacheza kwa akili sana. Kushindana na Marekani kule Amerika Kusini ni sawa na kushindana na Urusi kule Ulaya Mashariki au Uchina kule bahari ya Uchina Kusini.

Ngumu sana kushindana na Marekani kwenye The Western Hemishphere ndiyo maana Lex Tillerson alisema kwamba hata biashara za Uchina zinahatarisha usalama na maslahi yake. Kiufupi The Munroe Doctrine bado inaendelea kufanya kazi, Urusi ya Kisovieti ilijaribu kupeleka ukomunisti kule Amerika Kusini lakini Marekani akatengeza makundi ya wauza unga, waasi na madikteta ili kuwavuruga kabisa wakomunisti.

Unakumbuka Nicaragua miaka ya 1980's ilivyosimbuliwa na magaidi ?? Au tusiende mbali, unakumbuka walivyovamia Panama na kumtoa Manuel Noriega ?? Hatari sana...
Plan ya kupeleka magenge wa dawa za kulevya mwisho wa siku imewarudi wamarekani kwa kujaza vijana mateja ktk fukwe za Florida na kuongeza tatizo la utoroshaji fedha yao ya dola kienyeji.

Sasa wanaishia kuwekeza pesa nyingi kuzuia utakatishaji fedha na kuzuia madawa ya kulevya kwenye ardhi yao.

Gharama za kuokoa mateja wenye uraibu na kuzuia ngada ni kubwa mno hasa kiuchumi.
 
Plan ya kupeleka magenge wa dawa za kulevya mwisho wa siku imewarudi wamarekani kwa kujaza vijana mateja ktk fukwe za Florida na kuongeza tatizo la utoroshaji fedha yao ya dola kienyeji.

Sasa wanaishia kuwekeza pesa nyingi kuzuia utakatishaji fedha na kuzuia madawa ya kulevya kwenye ardhi yao.

Gharama za kuokoa mateja wenye uraibu na kuzuia ngada ni kubwa mno hasa kiuchumi.
Agreed na hata Venezuela ikichafuka Marekani ajiandae na wimbi la wakimbizi. Lakini yote tisa faida za kiuchumi ambazo Marekani atazipata kutokana na kuvamia Venezuela ni kubwa kuliko hasara.

Kibaya zaidi ni kwamba linapokuja suala la maslahi Marekani huweka utu pembeni kwasababu sera za Washington haziendeshwi na Wamarekani tena bali makampuni makubwa kama Raytheon, Boeing, Halliburton, Exxon Mobil, Monsanto etc. Haya hayajali sana raia mnaishije.

Kule Iraq vita umeuwa wamarekani wengi sana na kuleta hasara lakini kampuni la Halliburton lilipata faida mara tano zaidi ya ilivyo kawaida. Vita ikianza huko Venezuela makampuni ya Silaha na mafuta stocks zao lazima ziende juu sana. Bila vita na vurugu uchumi wa Marekani hauwezi kwenda
 
Agreed na hata Venezuela ikichafuka Marekani ajiandae na wimbi la wakimbizi. Lakini yote tisa faida za kiuchumi ambazo Marekani atazipata kutokana na kuvamia Venezuela ni kubwa kuliko hasara.

Kibaya zaidi ni kwamba linapokuja suala la maslahi Marekani huweka utu pembeni kwasababu sera za Washington haziendeshwi na Wamarekani tena bali makampuni makubwa kama Raytheon, Boeing, Halliburton, Exxon Mobil, Monsanto etc. Haya hayajali sana raia mnaishije.

Kule Iraq vita umeuwa wamarekani wengi sana na kuleta hasara lakini kampuni la Halliburton lilipata faida mara tano zaidi ya ilivyo kawaida. Vita ikianza huko Venezuela makampuni ya Silaha na mafuta stocks zao lazima ziende juu sana. Bila vita na vurugu uchumi wa Marekani hauwezi kwenda
Sina cha kuongeza kwenye comment yako.
Upo sahihi 100/100.
 
Dah pia rwanda wataivamia burundi

Sasa kwanini urusi wavamie Ukraine na why China wafanye vurugu ukanda wake

Sent using my iPhone using jamiiforum app
Rwanda and Burundi are specks of dusts and too insignificant to shake an entire fabric of international order. And i fail to understand why you even brought them into this geopolitical landscape.

China and Russia will reciprocate violence in order to maintain the global balance of power, consolidate powers within their spheres of influence and further their economic interests. Adui yako akiwa anajiongeza na wewe unatakiwa ujiongeze ili asikuache sana, hii ndiyo falsafa ya siasa za dunia tokea karne ya 20.
 
Agreed na hata Venezuela ikichafuka Marekani ajiandae na wimbi la wakimbizi. Lakini yote tisa faida za kiuchumi ambazo Marekani atazipata kutokana na kuvamia Venezuela ni kubwa kuliko hasara.

Kibaya zaidi ni kwamba linapokuja suala la maslahi Marekani huweka utu pembeni kwasababu sera za Washington haziendeshwi na Wamarekani tena bali makampuni makubwa kama Raytheon, Boeing, Halliburton, Exxon Mobil, Monsanto etc. Haya hayajali sana raia mnaishije.

Kule Iraq vita umeuwa wamarekani wengi sana na kuleta hasara lakini kampuni la Halliburton lilipata faida mara tano zaidi ya ilivyo kawaida. Vita ikianza huko Venezuela makampuni ya Silaha na mafuta stocks zao lazima ziende juu sana. Bila vita na vurugu uchumi wa Marekani hauwezi kwenda
Tatizo la Venezuela ni karibu sana na USA kufanya vita pale ni kama kufanya ugomvi kwenye home backyard.

Kama ulivyosema marekani na nchi jirani kama Canada watapokea wakimbizi wengi sana.

Pia baaadhi ya silaha watakazo uza kule wamarekani au warusi zitakazo tekwa toka kwa majeshi ya serikali au wapinzani zitarudi marekani kwa wingi kwa njia ya panya (contrabands of ilegal firearms) kama silaha haramu na kuongeza uhalifu utokanao na silaha haramu.
 
Maduro ameshazalisha wakimbizi zaidi ya milioni tatu na kusababisha anguko la kishindo la uchumi. Uhalali wa kutawala upo wapi?
 
Rwanda and Burundi are specks of dusts and too insignificant to shake an entire fabric of international order. And i fail to understand why you even brought their into this geopolitical landscape.

China and Russia will reciprocate violence in order to maintain the global balance of power, consolidate powers within their spheres of influence and further their economic interests. Adui yako akiwa anajiongeza na wewe unatakiwa ujiongeze ili asikuache sana, hii ndiyo falsafa ya siasa za dunia tokea karne ya 20.
Kweli kabisa lkn urusi kupigana na Ukraine nadhan Russia atashinda lkn atayumba saana kiuchumi so sidhani kama ni vyepesi Russia kufanya hivyo

China nae majirani zake sio wa kitoto kama hawa wawili wanaotaka kutwangana

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Kweli kabisa lkn urusi kupigana na Ukraine nadhan Russia atashinda lkn atayumba saana kiuchumi so sidhani kama ni vyepesi Russia kufanya hivyo

China nae majirani zake sio wa kitoto kama hawa wawili wanaotaka kutwangana

Sent using my iPhone using jamiiforum app
Hata Wamarekani na Umoja wa Ulaya walifikiri hivihivi mwanzo, walivyompindua Viktor Yanukovich Warusi wakavamia Crimea ndani ya siku moja tu na hakuna aliyeamini. Ukraine ikijaribu kupigana na Urusi ni suala la masaa tu Kiev yote inaanguka.

Kule Uchina nako Japani, Vietnamu, Taiwani, Ufilipino na Korea hawawezi kabisa kupigana na Uchina. Kiufupi bara zima la Asia ukiwatoa Warusi hakuna anayeweza kupigana na Uchina katika kipindi hiki. Ashajenga kambi za jeshi kwenye visiwa na anaendelea kusema asilimia 80% ya bahari ile ni yake.

Rodrigo Duterte alijisemea hivi "they want me to confront China, but that would be suicide" kila siku iendayo kwa Mungu Uchina atakuwa anafanya Salami Slicing Tactic na watakuja kushangaa Pacific yote ile imetawaliwa na manowari za Uchina.
 
Kwa urusi na Ukraine naweza kukubari kweli Kiev itaangukia kwa warusi kama wakipigana

Lkn collaboration ya JAPAN ,Korea na wengineo sioni kama China atatoka salama alafu pia kumbuka hawaelewani na India
Hata Wamarekani na Umoja wa Ulaya walifikiri hivihivi mwanzo, walivyompindua Viktor Yanukovich Warusi wakavamia Crimea ndani ya siku moja tu na hakuna aliyeamini. Ukraine ikijaribu kupigana na Urusi ni suala la masaa tu Kiev yote inaanguka.

Kule Uchina nako Japani, Vietnamu, Taiwani, Ufilipino na Korea hawawezi kabisa kupigana na Uchina. Kiufupi bara zima la Asia ukiwatoa Warusi hakuna anayeweza kupigana na Uchina katika kipindi hiki. Ashajenga kambi za jeshi kwenye visiwa na anaendelea kusema asilimia 80% ya bahari ile ni yake.

Rodrigo Duterte alijisemea hivi "they want me to confront China, but that would be suicide" kila siku iendayo kwa Mungu Uchina atakuwa anafanya Salami Slicing Tactic na watakuja kushangaa Pacific yote ile imetawaliwa na manowari za Uchina.

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Kwa urusi na Ukraine naweza kukubari kweli Kiev itaangukia kwa warusi kama wakipigana

Lkn collaboration ya JAPAN ,Korea na wengineo sioni kama China atatoka salama alafu pia kumbuka hawaelewani na India

Sent using my iPhone using jamiiforum app
Uwe na siku njema mkuu.
 
Back
Top Bottom