Jua haya kuhusu Vatican

Jua haya kuhusu Vatican

Kanisa Katoliki na Vatican, kama taasisi ya kidini, ina sera zake za kidiplomasia na uhusiano wa kimataifa zinazotokana na mambo ya kihistoria, kisheria, na kikanuni. Sababu za Vatican kutokuwa na uhusiano wa kidiplomasia na baadhi ya mataifa kama China na Korea Kaskazini zinaweza kujumuisha mambo kadhaa:

Mgogoro wa Kisiasa: Mataifa mengi yana uhusiano wa kidiplomasia na Vatican kulingana na maslahi yao ya kisiasa, kiuchumi, na kijamii. Migogoro ya kisiasa, ideolojia tofauti, na sera za serikali husika zinaweza kusababisha kutokuwepo kwa uhusiano wa kidiplomasia.

Sera za Kidini: Nchi kama China na Korea Kaskazini zina sera za kidini zinazotofautiana na mafundisho ya Kanisa Katoliki. Kwa mfano, China ina sera kali za kudhibiti shughuli za kidini na Kanisa Katoliki. Hii inaweza kusababisha mgogoro au kutokubaliana katika masuala ya kidini na kisiasa.
Mambo ya Kihistoria: Historia ya uhusiano kati ya Vatican na mataifa hayo inaweza kuathiri hali ya sasa. Kwa mfano, historia ya uhusiano kati ya Vatican na China imekuwa na changamoto, ikiwa ni pamoja na suala la uteuzi wa maaskofu.

Haki za Binadamu: Baadhi ya mataifa huwa na rekodi mbaya ya haki za binadamu, ambayo inaweza kuwa kizuizi kwa Vatican kutambua uhusiano wa kidiplomasia au kushirikiana kikamilifu.

Misingi ya Kidiplomasia: Vatican inazingatia pia misingi ya kidiplomasia ambayo inaweza kuhusisha masuala kama uhuru wa kidini, haki za binadamu, na masuala ya kisiasa.
Hivyo, kutokuwepo kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Vatican na nchi kama China na Korea Kaskazini ni matokeo ya mambo mengi yanayochangia, ikiwa ni pamoja na masuala ya kisiasa, kidini, na kihistoria.
 
Mkuu tujifunze tu tukiwa na akili huru "open minded" kama ni dhambi Biblia inasema katika Warumi 3:23 "..Wote wametenda dhambi nankupungukiwa na utukufu wa Mungu".
nimekuelewa mkuu uko sahihi ila mwakilishi wa MUNGU duniani hadhaniwi kutenda madhambi ya kutisha.Mimi binafsi sioni mahali YESU alipotenda dhambi.
Kimsingi silipingi kanisa katoliki ila ukisoma vituko vya mapapa waliopita utaona vituko mno.Yuko papa mmoja alimuhukumu Galileo Galilei kisa tu kasema dunia ndio inalizunguka Jua na dunia ni mviringo aliwekwa kifungo cha ndani hadi Galileo wa watu akafa papa Yohane hivi karibuni alikiri na kuomba radhi.Je anajua vita vya msalaba vilipiganwa na dhehebu gani kukandamiza madhebebu mengine.
Kanisa katoliki lingekuwa sahihi sana kusingetokea protestants
Yuko papa mmoja alivyoshika madaraka alimchukia sana papa aliyemtangulia akaamuru afukuliwe maiti yake ikawekwa kizimbani kushitakiwa maiti ikaonekana ina hatia akaamua mifupa yake ichomwe kisha itupwe baharini.
Mimi ningemuunga mkono jamaa angesema kuwa Papa ni mtumishi wa mungu duniani akiongoza kanisa la katoliki sio kusema ni mwakilishi wa Mungu duniani.
Akisema hivyo waislam wao watasemaji,je wahindu wasiomuabudu mungu wetu huyu wao watasemaje,je ma baniani watasemaje?,je wa jain watasemaje je washinto wa japani watasemaje,je wa tao wa Japani watasemaje,je ma budha watasemaje,je ma rasta watasemaje?,je zoroaster watasemaje?
Aelewe wote hawa ni binadamu wana nyama na damu kama sisi.
 
nimekuelewa mkuu uko sahihi ila mwakilishi wa MUNGU duniani hadhaniwi kutenda madhambi ya kutisha.Mimi binafsi sioni mahali YESU alipotenda dhambi.
Kimsingi silipingi kanisa katoliki ila ukisoma vituko vya mapapa waliopita utaona vituko mno.Yuko papa mmoja alimuhukumu Galileo Galilei kisa tu kasema dunia ndio inalizunguka Jua na dunia ni mviringo aliwekwa kifungo cha ndani hadi Galileo wa watu akafa papa Yohane hivi karibuni alikiri na kuomba radhi.Je anajua vita vya msalaba vilipiganwa na dhehebu gani kukandamiza madhebebu mengine.
Kanisa katoliki lingekuwa sahihi sana kusingetokea protestants
Yuko papa mmoja alivyoshika madaraka alimchukia sana papa aliyemtangulia akaamuru afukuliwe maiti yake ikawekwa kizimbani kushitakiwa maiti ikaonekana ina hatia akaamua mifupa yake ichomwe kisha itupwe baharini.
Mimi ningemuunga mkono jamaa angesema kuwa Papa ni mtumishi wa mungu duniani akiongoza kanisa la katoliki sio kusema ni mwakilishi wa Mungu duniani.
Akisema hivyo waislam wao watasemaji,je wahindu wasiomuabudu mungu wetu huyu wao watasemaje,je ma baniani watasemaje?,je wa jain watasemaje je washinto wa japani watasemaje,je wa tao wa Japani watasemaje,je ma budha watasemaje,je ma rasta watasemaje?,je zoroaster watasemaje?
Aelewe wote hawa ni binadamu wana nyama na damu kama sisi.
Unafahamu hata wewe ni sura na mfano wa Mungu, Kwa kifupi unamuwakilisha Mungu Duniani?...
 
Kuna kitu wengi wetu hatukifahamu vizuri nadhani ni kutokana na kutopitia kwa kina misingi saba ya Kihemetikia "hermetic principles" ambayo kiuhalisia ni zao la Afrika (Misri)misingi hiyo imesaidia Imani za mataifa mengi sana ya Asia na Ulaya zikiwemo jamii zinazohifadhi Siri zake sana kama Freemasons n.k

Ukweli ni kuwa katika misingi hiyo saba upo msingi unaosema kila kitu kina uwili kinzani unaokamilishana "bipolarity" mfano wema na uovu ni kitu kilekile katika uelekeo tofauti " evil and good are two ends of the same continuum" .Kuna uelekeo wema unakuwa uovu lakini wema huohuo Kuna uelekeo unabaki kuwa wema.

Tatizo letu ni kuwa tunapokiona kitu kilekile katika uelekeo tofauti tunafikiru ni vitu viwili tofauti ila kwa kweli vitu huwa ni vilevile na tofauti ni uelekeo tu. Unapoelekea upande mwingine wa wema wema huohuo huonekana kama uovu.
 
Kuna kitu wengi wetu hatukifahamu vizuri nadhani ni kutokana na kutopitia kwa kina misingi saba ya Kihemetikia "hermetic principles" ambayo kiuhalisia ni zao la Afrika (Misri)misingi hiyo imesaidia Imani za mataifa mengi sana ya Asia na Ulaya zikiwemo jamii zinazohifadhi Siri zake sana kama Freemasons n.k

Ukweli ni kuwa katika misingi hiyo saba upo msingi unaosema kila kitu kina uwili kinzani unaokamilishana "bipolarity" mfano wema na uovu ni kitu kilekile katika uelekeo tofauti " evil and good are two ends of the same continuum" .Kuna uelekeo wema unakuwa uovu lakini wema huohuo Kuna uelekeo unabaki kuwa wema.

Tatizo letu ni kuwa tunapokiona kitu kilekile katika uelekeo tofauti tunafikiru ni vitu viwili tofauti ila kwa kweli vitu huwa ni vilevile na tofauti ni uelekeo tu. Unapoelekea upande mwingine wa wema wema huohuo huonekana kama uovu.
uko sawa hapa umeongea kisayansi na kifalsafa zaidi
kwenye fizikia tunasema to every action there is equal and opposite reaction hiyo ni Newton third law of motion
kwenye falsafa Karl Max alipata kusema the law of unit and opposite of struggle
kila ktu kina kinyume chake mfano kinyume cha shibe ni njaa.Tungekuwa tuna shibe tu kusingekuwa na haja ya kufanya kazi kwa ajili ya kutafuta chakula
Kinyume cha baridi ni joto
kinyume cha MUNGU ni shetani
kuna wakati nilikuwa najiuliza kama MUNGU alikuwa anatupenda kwanini akatuletea shetani wa kutudanganya lazima alikuwa na sababu yake maalam kutuwekea kitu cha kujaribu imani zetu
 
Kama ulikua huijui nchi ndogo kuliko zote dunia ni ipi wacha nikufahamishe;-
Nchi ndogo kuliko zote duniani ni VATICAN,
VATICAN ni nchi iliopo ndani nchi ya ITALIA katika jiji la ROMA,
Nchi ya VATICAN lugha yake ya taifa ni ni KILATINI,
Fedha ya nchi hiyo ya VATICAN inaitwa YURO,
Nchi ya VATICAN ina ukubwa wa hekta 44 sawa na kilometa 0.44,
Nchi ya VATICAN ilipata uhuru wake 11/2/1929,
Unaweza kushangaa kusikia kuwa VATICAN pia imepata uhuru si ndio,
Sasa nikwambie tu kuwa awali hapakua na nchi iitwayo VATICAN,
VATICAN asili yake ilikua ni jina la mtaa uliopo ndani jijini la ROMA,
Baadae mtaa huo wakaamua kuupa hadhi ya nchi kamili,
Ili kutenganisha utawala utawala wa kidini nawa kidunia,
Ilikua huru kutoka kwa nchi ya ITALIA kupitia mkataba maalumu,
Mkataba huo ulisainiwa na dikteta BENITO MUSOLIN,
Kwaniaba ya mfalme wa ITALIA wa wakati huo na PIETRO GASPAM kwaniaba ya PAPA,
Kiongozi wa nchi ya VATICAN huitwa PAPA,
Kiongozi wa nchi hiyo hupatikana baada ya PAPA aliepo KUFA au kuacha kazi kutokana na matatizo ya KIAFYA,
Nafasi ya PAPA huombwa na makadinali kutoka duniani kote,
Na baadae jopo la uchaguzi wa PAPA hukaa nchini humo na kumchagua mmoja,
Huwezi kuwa PAPA kabla hujawa kardinali,
Kardinali ndio cheo cha juu kabisa kabla ya PAPA katika kanisa katoliki,
Kikawaida kila nchi ina kardinali mmoja tu,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo kiongozi wake wa nchi,
Huwa si raia wa kuzaliwa wa nchi hiyo kabisa kabisa,
VATICAN ndio makao makuu ya kanisa katoliki duniani,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake wote,
Sio raia wa kuzaliwa na uraia wao unakikomo kulingana na pasport zao,
VATICAN ndio nchi inayoongoza kwa kuwa na mabalozi wengi duniani,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo ukienda kuwakilisha nchi yako,
Unatakiwa uishi nchi nyengine na sio vatican,
Nadhani hujanielewa wacha nifafanue yaani iko hivi,
Ukichaguliwa na rais wako uende kuiwakilisha nchi yako nchini VATICAN,
Unaenda kuripoti VATICAN halafu unatakiwa kwenda kuishi ROMA nchini ITALIA na sio nchini VATICAN,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake karibu nusu huishi nje ya nchi hiyo katika balozi zake,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake wote ni dini moja na dhehebu moja tu,
Raia wa VATICAN uraia wao ukiisha huwa raia wa ITALIA moja kwa moja,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo zaidi ya nusu ya nchi hiyo ni bustani tu,
Nchi ya VATICAN watu wake jumla ni 791,
Hiyo idadi haitakiwi kuongezeka wala kupungua,
Nchi ya VATICAN ina mabalozi zaidi ya 180 duniani kote,
Walinzi wa nchi hiyo hutoka nchi moja tu duniani,
Nayo sio nchi nyengine ni nchi ua USWISI na walinzi hao huitwa walinzi wa PAPA,
Idadi ya walinzi wa nchi ya VATICAN ni 100 tu hawapungui wala kuongezeka,
Nchi ya VATICAN raia wake hawalipi kodi,
Nchi ya VATICAN hupata kipato chake kupitia utalii, stempu,
Pamoja na michango kutoka kwa wanachama au waumini wa dini hiyo duniani kote,
Nchi ya VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo ukitaka kwenda huko,
Unatakiwa ukate pasport ya nchi nyengine ndio ufike,
Nadhani hujanielewa wacha nifafanue yaani iko hivi,
Nchi ya VATICAN yenyewe haina pasport wala VISA,
Kwahiyo ukitaka kwenda VATICAN unatakiwa ukate VISA ya ITALIA,
Ambayo hiyo ndio itakayo kuwezesha kuingia moja kwa moja VATICAN,
Raia wa ITALIA huingia bure nchini VATICAN bila kuulizwa,
VATICAN ndio nchi pekee duniani ambayo wanawake wote wa nchi hiyo ni masista,
Makao makuu ya nchi ya VATICAN yapo katika kanisa kuu la nchi hiyo,
Ambalo pia ndio kanisa kuu la wakristo wa dhehebu la ROMA duniani,
Kanisa kuu la wakristo wa dhehebu la ROMA duniani linaitwa St.Peter,
Kanisa hilo la St.Peter lipo nchini humo VATICAN,
Katika nchi ya VATICAN kuna kanisa moja tu liitwa St.Peter,
Ni marufuku kuoa au kuolewa ukiwa VATICAN.

Makala hii imeletwa kwenu na na Dhulkad Madara kutoka morogoro
 
Hujasema na idadi ya mashoga nchini Vatican ni ngapi, rais wao ni punga pia?
 
Back
Top Bottom