Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,926
- 31,169
Leo kwenye uwanja wa Azimio la Arusha kulikuwa na zoezi la kumsimika Bwana Godluck Ole Medeye ukamanda wa vijana Arumeru magharibi.Bwana G Medeye tayari katangaza atagombea ubunge katika jimbo la Arumeru magharibi linaloshikiliwa na Mheshimiwa Elisa Mollel.
Sherehe zilianza na maandamano makubwa ya wafuasi wa Bwana Godluck ole Medeye waliokuwa wamevalia fulana zenye picha zake.
Bwana Medeye ni mkurugenzi wa rasilimali watu Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) ana shahada ya uzamili MBA.Bwana Medeye ni mfuasi mwaminifu wa Edward Ngoyai Elowassa.
Siasa za chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha na Manyara zimegawanyika katika makundi mawili makubwa.
Kundi la kwanza ni lile la wabunge/wanasiasa wanaomuunga mkono Mheshimiwa E Lowassa.Kundi la pili ni lile la wabunge/wanasiasa wanampinga Lowassa likiongozwa na Mheshimiwa sendeka,Lekule Laiser,Elissa Mollel ambao wameunda mtandao wa kuwakinga dhidi ya mashambulizi ya Mheshimiwa Lowassa & Company.
Naomba kuwasilisha.
Sherehe zilianza na maandamano makubwa ya wafuasi wa Bwana Godluck ole Medeye waliokuwa wamevalia fulana zenye picha zake.
Bwana Medeye ni mkurugenzi wa rasilimali watu Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) ana shahada ya uzamili MBA.Bwana Medeye ni mfuasi mwaminifu wa Edward Ngoyai Elowassa.
Siasa za chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha na Manyara zimegawanyika katika makundi mawili makubwa.
Kundi la kwanza ni lile la wabunge/wanasiasa wanaomuunga mkono Mheshimiwa E Lowassa.Kundi la pili ni lile la wabunge/wanasiasa wanampinga Lowassa likiongozwa na Mheshimiwa sendeka,Lekule Laiser,Elissa Mollel ambao wameunda mtandao wa kuwakinga dhidi ya mashambulizi ya Mheshimiwa Lowassa & Company.
Naomba kuwasilisha.