Josephat Isango, Mhariri wa Habari Tanzania Daima akamatwa na Polisi

isango ni mchumia tumbo,namjua vizuri halafu ni mlevi balaa.naona alitaka auze stori ili apate za kunywea kiroba
 
Hii ni taarifa njema hawa waandishi na wahariri wanahatarisha AMANI ya taifa. na apewe adhabu kali ili iwe fundisho pia kama ikithibitika na kagazeti haka kafungiwe kabisa
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni,kuwakamata wana habari kama hawa ni kuminya uhuru wa habari. Kama taarifa imepotoshwa ni kazi ya wasemaji wa serkali kutuambia ukweli ni upi,
 
Haya wafuasi wa CHADEMA gazeti lenu la udaku.
Usiwe chizi kama sura yako!! Gazeti la Tz Daima si la udaku, lile ni gazeti linaloandaliwa na wasomi na linasomwa na wasomi wenye kuelewa maana ya habari.
 
Hivi kati ya Isango na Radio Iman wanaotangaza uchochezi kila siku yupi wa kukamatwa kwanza? Gazeti limeshaomba radhi sasa mahojiano ya nini kama si kutishana tu?

Wachochezi wanaachwa lakini wale wenye harufu ya Chadema tu maadui wa jeshi la polisi!!!
mkuu hii serikali yaani inatakiwa tuachane nayo 2015 maana inatia aibu sana
 
Kwa nini akamatwe? Kufukuzwa sehemu sio uchochezi, isitoshe gazeti liliomba msamaha katika toleo la jana. Polisi wafanye kazi ya kutafuta wahalifu na sio kupoteza muda kwa mambo ambayo hayana msingi.
Kwa mfano kwa nini Radio Imani bado inaruhusiwa kurusha matangazo? Upi ni uchochezi kusingiziwa kuwa umefukuzwa kutoka sehemu fulani au kukashifu imani za watu wengine?
 
Hivi ndio shemeji mtu na baba rizi walipofikia hapa?nchimbi wanaoua viongozi wa dini ushawakamata?kazi mnayo mwaka huu...
 
Wanajamvi salaam; kwa taarifa za hivi punde ni kuwa Josephat Isango ambaye ni Mhariri wa habari wa Tz Daima amekamatwa na Polisi na anapelekwa ofisi ya DCI kwa mahojiano zaidi.

Ni kutokana na stori aliyoandika juzi kuwa IGP na Nchimbi walifukuzwa Geita kwenye mgogoro wa kuchinja.

Source: Mimi mwenyewe.

Update: Baada ya kumhoji wameenda pia kupekua anakoishi maeneo ya Sinza
Wanaua raia, bado tu, wanamwagia tindikali mashehe, bado tu, wanafunga mashehe, bado tu, wanaua mapadre, bado tu, sasa wanakamata wanahabari nakufifisha habari za uovu wao,

Sisi tayari tumeshaasi kuanzia mwili hadi moyo, hatutishwi na madhila watupayo.
 
Polisi wenyewe mbona upelelezi hawaujui hadi JK amewatosa na kuamua kukodi FBI, hawa hadhi yao ni kesi za kuku tu.!!
 
Hii ni taarifa njema hawa waandishi na wahariri wanahatarisha AMANI ya taifa. na apewe adhabu kali ili iwe fundisho pia kama ikithibitika na kagazeti haka kafungiwe kabisa
Ukishayaona hay ni dalilili za utawala ulioshindwa kufikia ukomo wa kutawala, unachoshabikia ni anguko la hao unaowashabikia.
 
Si walifungie tu kama walivyolifungia Mwanahalisi?...Hata Raiamwema nalo lifungieni...Bakizeni Uhuru, Mzalendo, Uwazi, Ijumaa, Dar Leo na KIU kwakuwa zinaelimisha jamii na hazina uchochezi!!!... Grrrrrrrr!!!
 
Hivi kati ya Isango na Radio Iman wanaotangaza uchochezi kila siku yupi wa kukamatwa kwanza? Gazeti limeshaomba radhi sasa mahojiano ya nini kama si kutishana tu?

Wachochezi wanaachwa lakini wale wenye harufu ya Chadema tu maadui wa jeshi la polisi!!!

Nawashauri mngeandaa maandamano ya amani ama mkusanye sahihi 100 ( za wakristo )kanisani kuishinikiza serikali iifungie Radio Imaan ili tusikilize Wapo Radio na Radio Maria tuburudike na mapambio tuachane na habari za kiuchunguzi za Radio Imaan ama mi nadhani muwaburuze mahakamani ili wakithibitika hawaongei UONGO na UZUSHI basi haya mambo yawe yameisha kwani kila siku kuitaja Radio Imaan sio kuwa mnachuki nayo tu bali pia hao wenye hio dini yao hamuwapendi kabisaaa...
 
Back
Top Bottom