Jordan imeshapeleka jeshi lake mpakani tayari kwa vita na Israel

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,186
10,922
Baada ya muda mrefu wa ukimya jana Jumanne serikali ya Jordan imeongeza idadi ya askari na vifaa vya kivita mpakani na Israel tayari kwa mapigano iwapo Israel itaendelea kuhatarisha usalama wao na kuvunja mkataba baina yao.

Hayo yamebainishwa na waziri mkuu wa Jordan,Bisher Khasawneh akielezea mwenendo usio kuwa mzuri wa Israel kwa wapalestina wanaoishi ukingo wa mashariki kuvuka mto Jordan

Katika maelezo hayo ya utayari wa kivita waziri mkuu huyo amesema kumekuwa na shinikizo kwa baadhi ya wabunge wa Israel wakisema suluhisho la wapalestina walio maeneo hayo ni kuingia Jordan.

Kivitendo walowezi wa kiyahudi wamekuwa wakiongeza mashambulizi kwa wapalestina kwa kuwatoa kwenye majumba yoo na mashamba kwa nguvu ili waondoke na kuingia Jordan.

Waziri mkuu huyo amesema vitendo hivyo ni aina ya ukiukwaji wa mkataba baina yao wa mwaka 1994.

Akaongeza kwa kusema aina yoyote ya kuwahamisha kwa nguvu na matendo yanayopelekea hilo ni ukiukwaji wa mkataba huo.

Hali hiyo itapelekea na wao kuuona mkataba huo kama ni kipande cha karatasi kilichojaa mavumbi basi.

Vitendo hivyo vya Israel mbali ya kukiukwa kwa mkataba amesema vile vile vinahatarisha usalama wa Jordan jambo ambalo hawataweza kulivumilia.

Watu upande wa Jordan wametoa ushahidi wa kuoona idadi kubwa ya magari ya kivita na vifaru vikielekea kwenye bonde la Jordan mpakani na Israel.

Jordan says it beefs up army presence along borders with Israel

 
Waziri mkuu wa Jordan

1700628068587.png
 
Acheni ushabiki, marekani amekaa miaka 20 Afghanistan wanakadiriwa kuuawa watu elfu 70, Israel ndani ya mwezi mmoja wameua watu elfu 20, aisee vita sio vya kushabikia usiombe yatokee sehemu ulipo na familia yako
Sio kushabikia lakini akitokea mtu akaamua hataki kufa kikondoo huyo ndiye tunayemuona ni binadamu wa kweli.
 
Hiyo ni mikwara tu ya kujihami, hakuna vita yoyote itayotokea...

Linapokuja suala la mgogoro wa Wayahudi na Wapalestina, mataifa rafiki huwa yanasikilizia hao ndugu wawili wapatane wenyewe...

Hivyo tarajia kuona Hamas na Israel watadundana weeee, mwisho watafikia muafaka wao kwa wao na maisha yataendelea...

Ingeweza kuwa ni vita kali endapo tu Israel lingekuwa ni taifa lenye himaya ya kikristo...
 
Baada ya muda mrefu wa ukimya jana Jumanne serikali ya Jordan imeongeza idadi ya askari na vifaa vya kivita mpakani na Israel tayari kwa mapigano iwapo Israel itaendelea kuhatarisha usalama wao na kuvunja mkataba baina yao.

Hayo yamebainishwa na waziri mkuu wa Jordan,Bisher Khasawneh akielezea mwenendo usio kuwa mzuri wa Israel kwa wapalestina wanaoishi ukingo wa mashariki kuvuka mto Jordan

Katika maelezo hayo ya utayari wa kivita waziri mkuu huyo amesema kumekuwa na shinikizo kwa baadhi ya wabunge wa Israel wakisema suluhisho la wapalestina walio maeneo hayo ni kuingia Jordan.

Kivitendo walowezi wa kiyahudi wamekuwa wakiongeza mashambulizi kwa wapalestina kwa kuwatoa kwenye majumba yoo na mashamba kwa nguvu ili waondoke na kuingia Jordan.

Waziri mkuu huyo amesema vitendo hivyo ni aina ya ukiukwaji wa mkataba baina yao wa mwaka 1994.

Akaongeza kwa kusema aina yoyote ya kuwahamisha kwa nguvu na matendo yanayopelekea hilo ni ukiukwaji wa mkataba huo.

Hali hiyo itapelekea na wao kuuona mkataba huo kama ni kipande cha karatasi kilichojaa mavumbi basi.

Vitendo hivyo vya Israel mbali ya kukiukwa kwa mkataba amesema vile vile vinahatarisha usalama wa Jordan jambo ambalo hawataweza kulivumilia.

Watu upande wa Jordan wametoa ushahidi wa kuoona idadi kubwa ya magari ya kivita na vifaru vikielekea kwenye bonde la Jordan mpakani na Israel.

Jordan says it beefs up army presence along borders with Israel

Mikwara tu hiyo,
 
Baada ya muda mrefu wa ukimya jana Jumanne serikali ya Jordan imeongeza idadi ya askari na vifaa vya kivita mpakani na Israel tayari kwa mapigano iwapo Israel itaendelea kuhatarisha usalama wao na kuvunja mkataba baina yao.
Hayo yamebainishwa na waziri mkuu wa Jordan,Bisher Khasawneh akielezea mwenendo usio kuwa mzuri wa Israel kwa wapalestina wanaoishi ukingo wa mashariki kuvuka mto Jordan
Katika maelezo hayo ya utayari wa kivita waziri mkuu huyo amesema kumekuwa na shinikizo kwa baadhi ya wabunge wa Israel wakisema suluhisho la wapalestina walio maeneo hayo ni kuingia Jordan.Kivitendo walowezi wa kiyahudi wamekuwa wakiongeza mashambulizi kwa wapalestina kwa kuwatoa kwenye majumba yoo na mashamba kwa nguvu ili waondoke na kuingia Jordan.
Waziri mkuu huyo amesema vitendo hivyo ni aina ya ukiukwaji wa mkataba baina yao wa mwaka 1994.Akaongeza kwa kusema aina yoyote ya kuwahamisha kwa nguvu na matendo yanayopelekea hilo ni ukiukwaji wa mkataba huo.Hali hiyo itapelekea na wao kuuona mkataba huo kama ni kipande cha karatasi kilichojaa mavumbi basi.
Vitendo hivyo vya Israel mbali ya kukiukwa kwa mkataba amesema vile vile vinahatarisha usalama wa Jordan jambo ambalo hawataweza kulivumilia.
Watu upande wa Jordan wametoa ushahidi wa kuoona idadi kubwa ya magari ya kivita na vifaru vikielekea kwenye bonde la Jordan mpakani na Israel.

Jordan says it beefs up army presence along borders with Israel

haiwezekani.
Jordan ni muungwana sana anaweza kuweka majeshi yake kwenye mipaka yake na Israel Lakini hawezi thubutu kuichokoza wala kuingia vitani na Israel.

Kumbuka dinari ya Jordan na shekeli ya Israel ndizo hutumika kununua bidhaa, huduma na biashara huko Israel, West Bank na Jordan yenyewe.
Ni ndugu hawa wamejazana pande zote mbili, hadi kiwango cha kushindwa kuwatofautisha huyu ni nani wa upande gani, ispokua kwa stakabadhi tu..
 
Hamas tu wameshindwa wataweza Jordan yenye vifaru na ndege za kivita.
Tusubiri na Misri wapate akili kama hiyo.
Wewe utakuwa wa juzi au kama ni wa zamani umeamua kupuuzia historia ya vita baina ya Taifa la Israel na Waarabu. Wamisri wenyewe waligundua kuwa hawawezi kamwe kuja kuishinda Israel kwenye uwanja wa vita, wakaamua kuwekeana mkataba wa amani.
 
haiwezekani.
Jordan ni muungwana sana anaweza kuweka majeshi yake kwenye mipaka yake na Israel Lakini hawezi thubutu kuichokoza wala kuingia vitani na Israel.

Kumbuka dinari ya Jordan na shekeli ya Israel ndizo hutumika kununua bidhaa, huduma na biashara huko Israel, West Bank na Jordan yenyewe.
Ni ndugu hawa wamejazana pande zote mbili, hadi kiwango cha kushindwa kuwatofautisha huyu ni nani wa upande gani, ispokua kwa stakabadhi tu..
Udugu wa namna hiyo wala Israel haiuthamni.Wanataka wawabamize wawe tabaka la chini yao.
 
Back
Top Bottom