Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 898
- 2,206
Wadau zipo taarifa kuwa Uongozi wa Chadema unafanya mazungumzo na mwanasiasa machachari John Shibuda apeperushe bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 nafasi ya Urais.
Hesabu zinazopigwa ni namna ya kupata kura nyingi kutoka Sukuma Land (Kanda ya Ziwa) kutokana na takwimu za Sensa 2022 kuonesha wenye sifa za kupiga kura kutoka Kanda hiyo kuwa 8.6milioni. Hizi kura ni nyingi na mtu pekee mwenye ushawishi Kanda hiyo ni John Shibuda.
Taarifa hizi zimevujishwa na Shibuda mwenyewe akiongea na viongozi wa chama chake Ada-Tadea jijini Dodoma kikao cha ndani akisema, "tujiandae kisaikolojia kujiunga na Chadema na mimi nigombee Urais 2025 kupambana na Rais Samia, maongezi yanaendelea".
Nawatakia kila lakheri.
Hesabu zinazopigwa ni namna ya kupata kura nyingi kutoka Sukuma Land (Kanda ya Ziwa) kutokana na takwimu za Sensa 2022 kuonesha wenye sifa za kupiga kura kutoka Kanda hiyo kuwa 8.6milioni. Hizi kura ni nyingi na mtu pekee mwenye ushawishi Kanda hiyo ni John Shibuda.
Taarifa hizi zimevujishwa na Shibuda mwenyewe akiongea na viongozi wa chama chake Ada-Tadea jijini Dodoma kikao cha ndani akisema, "tujiandae kisaikolojia kujiunga na Chadema na mimi nigombee Urais 2025 kupambana na Rais Samia, maongezi yanaendelea".
Nawatakia kila lakheri.