Mwanzoni tulijua kuwa wewe ni mtu makini kume tumekosea. Nadhani hata wanaokutumikisha wanajua kuwa wewe si makini na ndio maana wanakuwekea spidi gavana na kukuambia uache ubabe. Mwanzoni nilidhani wamekuonea kumbe walikuwa sahihi. Upo kama roboti. Nimegundua hili kutokana na matamshi na kauli zako. Barabara zote nchini unazijua wewe. Vifungu vyote vya sheria umevikariri wewe. Hizo sheria ni kwa ajili ya binadamu lakini wao/sisi sio programmed kama wewe.
Juzi hapa mkizindua barabara pale Dodoma, Pinda alikupiga dongo kuwa Rais alikupeleka uvuvi, na kule unajua idadi ya samaki nchini. Rais akaona bora akurudishe ujenzi. Tatizo lako mkuu unamtumikia kafiri kupitiliza, hadi unampa kero.
Wewe ni mchapakazi sawa, lakini yawezekana huna maadili ya kazi. Hakuna mtanzania anayekuwazia urais. Wanakuwazia uwaziri tu kwa kuwa watanzania wanajua unajua kutumika.
Achana kabisa na siasa zako za maji taka. Sio kila unapotoa neno hadharani usifie chama chako na kuponda upinzani. Kwa taarifa yako, unaowahutubia ni wapinzani. Sasa unapoponda viongozi wao na harakati za upinzani, wanakuchukia kweli. Wanakuoanisha na majina yako.
Tatizo lako mkuu unatupa mawe hovyo kiasi cha kuwatwanga na wazazi wako pia. Nakufananisha na Abunuwasi kukata tawi ulilokalia. Hilo tawi ni wananchi. Mpita njia akikuambia kuwa unafanya kosa kwani utaanguka, unamkejeli. Utakapoanguka utamkimbilia aliyekuambia ukweli kumwomba utabiri zaidi, angalia asijekwambia utakufa lini.
Achana na upinzani kwani ni jeshi kubwa kwa sasa. Una kashfa nyingi tu tunazozifahamu na nyingine zitafahamika. Una kashfa ya kuuza nyumba za serikali. Una kashfa za kumpa kimada wako nyumba ya serikali. Una kashfa ya kunyanyasa staff wako kwa kuletewa majungu na wapambe wako. Una kashfa ya ubabe, n.k, n.k. Fanya kazi, kiongozi kwani huijui kesho. Kazi ya kubwabwaja mwachue nape. Kaajiriwa kwa kazi hiyo. We kazi yako miundombinu. Usiwe kama mzazi anayewapa wanae mahitaji kwa masimango. Wenzako umeshwasikia wanabwabwaja hovyo? Time will tell