John Mnyika: Too Soon to Lose you!

John Mnyika: Too Soon to Lose you!

Boreless

Member
Joined
Aug 25, 2009
Posts
67
Reaction score
45
Nahisi unaumia na kushikwa katika mtanziko kutokana na kinachoendelea katika chama chenu. Hali yako inakuwa mbaya sana pale unapohisi katika baadhi ya mambo nafsi haikubaliani na hukumu wala mikakati inayofanywa na waliokujengea mazingira wewe kuwa upande wao dhidi ya pande hasimu. Unatamani uwe impartial lakini katika vita hivi hakuna nafasi hiyo. Wakati mwingine unatamani uvuke zuria ujiunge na upande wa pili lakini nalo hili linakuwea gumu. Umefungwa katika kifungo cha kulipa fadhila kiasi kwamba kuna mahali unadhulumika kuafikiana na unaopingana nao kimawazo na kimkakati. Katika mtanziko huu naamini unaweza kuwa unapita katika wakati mgumu zaidi hata kuliko MM, M1, M2 na M3.

Naweza kukutabiria kwa hakika kuwa uamuzi mgumu na wa busara utakaoufanya katika sakata hili utakuwa na ubashiri wa mafanikio yako ya kisiasa kuanzia ubunge 2015 na vyeo vikubwa katika chama na nchi katika kipindi cha 2015-2025 Mungu akikupa uzima. Lakini iwapo utashindwa kupiga hesabu vizuri matokeo yatakuwa kinyume chake. siombei, ila utapotea katika siasa za uwakilishi na za vyama. Katika kadhia hii, kulingana na hitimisho la saga zima wako wanasiasa wengi e.g Mch Msigwa, Mh. Halima, etc watapotea na wengine watapotezwa katika ulingo wa siasa. Wewe Mnyika siombei na sitopenda upotee wala nyota yako izamishwe. Napenda niendelee kukuona ukishiriki kutoa mchango katika uwakilishi na siasa za vyama vya nchi ijayo baada ya 2015.

Katika suala hili kujiweka kwako sawa siyo lazima uhame kambi. Unaweza ku-play determined role ya ku-initiate upatanishi wa kambi hasimu na record itakupa heshima ya pekee. Na utabaki salama ukikwea juu katika siasa za nchi hii.

Ninakuombea tafakuri yakinifu itakayofuatiwa na maamuzi makini.

Lakini katika yote kumbuka kuwa mpole kama ua maana MM ni mjanja kama nyoka!
 
ZeMarcopolo acha ushabiki...hivi kwa nini katika msiba huu wanaopiga ndulu sana ni walio maadui?!
Kitu kimoja wengi hawajui juu ya Waraka ulio mtandaoni ni kuwa umefanyiwa uhariri. Kama ungewekwa kama ulivyokamatwa Zitto asingekuwa na guts za kuitisha press conference jana na wala wapigandulu wa Lumumba wasingkuwa na upenyo wa kupiga mayowe
 
Last edited by a moderator:
Baba na mama wako timu moja, wee unamshawishi ashabikie sijui mitimu gani, ugali wenyewe wa shikamoo. Unamtakia mma kweli? Heshimuni watu wanaliowaaribisha mjini na kuwaonesha njia.

Maskio ya binadamu hayazidi kichwa.
 
ZeMarcopolo acha ushabiki...hivi kwa nini katika msiba huu wanaopiga ndulu sana ni walio maadui?!
Kitu kimoja wengi hawajui juu ya Waraka ulio mtandaoni ni kuwa umefanyiwa uhariri. Kama ungewekwa kama ulivyokamatwa Zitto asingekuwa na guts za kuitisha press conference jana na wala wapigandulu wa Lumumba wasingkuwa na upenyo wa kupiga mayowe

kwa nini ufanyiwe uhariri? kinafichwa nini?
 
anachotakiwa kukifuata ni maamuzi ya chama tu na si vinginevyo .
 
Nenda chooni ukajisaidie ukishamaliza pupu urudi tena hapa na thread ya maana!!!! Aisee, mnatumika vibaya. Sasa tumeshamwondoa Saliti wenu mnaanza kumsakama Mnyika!!! Take it easy. Mission failed!!! totally!!
 
Mdee ndiye ana hali ngumu zaidi! Anaheshimu na kukubali falsafa za ZITTO lakini hana ujasiri wa kutupa tonge! Unakumbuka ile issue ya kule Kigoma jinsi alivyojikanyaga?
 
kwa nini ufanyiwe uhariri? kinafichwa nini?
Ni suala la Kimkakati na kutoa nafasi ya watuhumiwa kuonyesha kitubio. Lakini kwa bahati mbaya matamshi ya Zitto na Kitila Mkumbo jana hayakuzingatia nafasi na fursa walizopewa. Hivyo CHADEMA makao makuu inaweza kutaka kufunua baadhi ya mambo ya hatari na ya ndani zaidi yaliyohaririwa au kuachwa katika waraka uliowekwa mitandaoni. Hili hata Mama Zitto analijua kuwa waraka halisi ni wa moto, unapilipili na unawasha au unachoma kabisa
 
Last edited by a moderator:
Ni suala la Kimkakati na kutoa nafasi ya watuhumiwa kuonyesha kitubio. Lakini kwa bahati mbaya matamshi ya Zitto na Kitila Mkumbo jana hayakuzingatia nafasi na fursa walizopewa. Hivyo CHADEMA makao makuu inaweza kutaka kufunua baadhi ya mambo ya hatari na ya ndani zaidi yaliyohaririwa au kuachwa katika waraka uliowekwa mitandaoni. Hili hata Mama Zitto analijua kuwa waraka halisi ni wa moto, unapilipili na unawasha au unachoma kabisa

Ndugu tunaweza kukubaliana na wewe kwa uliyoyaandika kuhusiana na waraka kueditiwa blah blah lakini uwache uongo wako kuhusu Mnyika
 
Last edited by a moderator:
Ndugu tunaweza kukubaliana na wewe kwa uliyoyaandika kuhusiana na waraka kueditiwa blah blah lakini uwache uongo wako kuhusu Mnyika
Unaweza kunipa sababu ya msingi ya Mnyika kuzima simu zake zinazojulikana kwa umma na kukatika kimawasiliano toka wiki ya tarehe 10? Pili, Je, ni kweli Mnyika alikuwa miongoni mwa delegation ya wabunge wa Kamati ya Maliasili iliyokwenda nje? Wadhani kwa nini aliamua kulazimisha safari ya ghafla kukacha kikao cha Kamati Kuu?
 
Nimeamini kweli ukimya wa Uongozi wa Chadema unawapa shida sana .Nawaomba Chadema wao waongee tu pale penye ulazima hawa wanaofanya siasa JF ni wachache tu na wachumia tumbo wengi wao .Naona sasa wana anza kushambulia personalities .Unataka Mnyika afanyeje eti ? Kila muosha maiti naye ataoshwa so kila tu na mzigo wake acheni upuuzi mitandaoni .
 
Nyie endeleeni kutaka madaraka si tunakomboa nchi vijijini.
 
ivi ashamaliza ile on-line masters alokuwa anasoma?
 
Back
Top Bottom