Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, amekanusha vikali tuhuma zinazomhusisha na mauaji ya aliyekuwa mjumbe wa Sekretarieti ya chama hicho, Ali Mohamed Kibao, akitaja majaribio hayo kama mkakati wa kisiasa wa "kubambika kesi" na kuhamisha lawama kutoka kwa wahusika halisi.
Akizungumza leo, Januari 17, 2026 mbele ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), Mnyika amehoji uwezekano wa yeye kusimamisha basi mchana kweupe maeneo ya Kibo na kumteka kiongozi huyo bila vyombo vya dola kuchukua hatua.
Katibu Mkuu huyo ameibua upya maswali kwa Jeshi la Polisi kuhusu hatua zilizochukuliwa tangu mwaka 2024. Amehoji kama polisi waliwahoji mashuhuda muhimu waliokuwemo ndani ya basi wakati Kibao anatekwa, akiwemo dereva wa basi lililokuwa limembeba marehemu, kondakta wa basi husika na askari mstaafu aliyekuwa abiria na ambaye alishuhudia watekaji wakiwa na bunduki na kuwaonya abiria wasiingilie kati.
Ali Mohamed Kibao alitekwa Septemba 6, 2024, na mwili wake kupatikana Ununio siku iliyofuata ukiwa umeharibiwa vibaya, tukio ambalo lilizua mshtuko mkubwa nchini na kimataifa.
Akizungumza leo, Januari 17, 2026 mbele ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), Mnyika amehoji uwezekano wa yeye kusimamisha basi mchana kweupe maeneo ya Kibo na kumteka kiongozi huyo bila vyombo vya dola kuchukua hatua.
Katibu Mkuu huyo ameibua upya maswali kwa Jeshi la Polisi kuhusu hatua zilizochukuliwa tangu mwaka 2024. Amehoji kama polisi waliwahoji mashuhuda muhimu waliokuwemo ndani ya basi wakati Kibao anatekwa, akiwemo dereva wa basi lililokuwa limembeba marehemu, kondakta wa basi husika na askari mstaafu aliyekuwa abiria na ambaye alishuhudia watekaji wakiwa na bunduki na kuwaonya abiria wasiingilie kati.
Ali Mohamed Kibao alitekwa Septemba 6, 2024, na mwili wake kupatikana Ununio siku iliyofuata ukiwa umeharibiwa vibaya, tukio ambalo lilizua mshtuko mkubwa nchini na kimataifa.
