Kitu bob mikwara, ndondi kati ya Mike Tyson dhidi ya Evander Holifid (sijui kama nimepatia majina), bob mazishi, zena na betina, profesa ndumilakuwili, dokta love pimbi, chepe, nk.
Hao ni miongoni mwa wahusika ndani ya Sani au Bongo.
Pamoja na J.M. Kaduma kuna mchoraji mwingine aliitwa Fortunatus Ndila sijui yuko wapi?
umemsahau lodilofa,bush stars & born town,mayuku,zuma,linda na obi ndani ya kisiwa cha kitintale kwa mzee ole.dah wengine mtaongezea wakuu.
umemsahau lodilofa,bush stars & born town,mayuku,zuma,linda na obi ndani ya kisiwa cha kitintale kwa mzee ole.dah wengine mtaongezea wakuu.
Wachoraji magwiji ambao sitawasahu ni hawa
1. Ndilla
2. Kaduma
3. Atakalo Soko
4. Prince Magic
Na story ambayo naikumbuka ya Ndila ni Anga za Wenyewe na story ya Aah mamdogo ya Prince Magic
Msako wa hayawani kama sijakosea.Baada ya Kaduma kutoka Sani alikwenda Bonkgo ambapo nakumbuka hadithi ya maneno ilikuwa imetungwa na Eddie Ganzel, siikumbuki jina ila ilikuwa inahusu upelelezi juu ya kifo cha bosi mmoja aliyegongwa na gari. Dah!!
Nadhani huyu ndo mchoraji wa ile hadithi ya "anga za wenyewe", mtanisaidia mnaokumbuka vizuri.
Hapana!!! usipotoshe mkuu, hiyo hadithi imechorwa na 4tunatus Ndilla.
magembe R.Malima juhudi zako ni za kuungwa mkono!!
John Kaduma ni Gwiji wa kukumbukwa.
Masoud Kipanya najua upo humu jaribuni kuandaa siku japo mara moja kwa mwaka kuwakumbuka hawa magwiji ili na nyie mkumbukwe na vizazi vya mbele.
APEPE John Kaduma
Magembe nakumbuka michoro yako ile kipindi kile tuko kwa Mrisho, nadhani utakuwa unakamilisha mambo Fulani Fulani tu ili uanze ila kwa uwezo wa kuchora nakuaminia.
Na kwa katuni enzi hizo Sanifu ndio funga kazi. Walichora wataalam wa katuni wote unaowajua. Lilimilikiwa na wamiliki wa Majira, DarLeo na Business Times. Wanaitwa Business Times Ltd
Daaah!!! mmenikumbusha mbali sana khs WIMBI la KITINTALE! mambo ya Tajiri wakidosi MAYUKU kipindi hicho KJJN kupata hela ishu! waliokuwa wanaishi DAR wakija kjjn wanakuja na copy hata km imechanika mi nilikuwa naitunza mara nyingi nilikuwa napenda Stori ya OBY alivyokuwa mPambanaji dah kuna mambo mengi ya zamani yalikuwa matam sana acheni2! Kwa cc tunaoyatamani hata cjui tutayapata wapi! BIG UP kwaalieanzisha hii mada nimefurahi sn ndg yenu!
Usimwache Mapung'o alipewa mke kwa sababu ya soka. Nilikuwa napenda shati lake linavopepea akichomoka na mpira
Tulikuwa tunakaa class wengiiii then mmoja anakaa katikati anasoma mechi za watani wa jadi
Nadhani hadithi ilikua inaitwa Wimbi la Kitintale huenda ndani ya 'kisiwa cha kitintale' sikumbuki vizuri.
Kuna mtu mwingine wa riwaya akiitwa george mwakingili na hadithi ya kinywa cha mauti gazeti motomoto.
Mkuu,
Hiyo project isiwe ndoto, manake nna hamu sana ya ku travel back in time and down memory lane! By the way, unaweza kuwa na contact details za Hussein Tuwa? Yule jamaa alinikosha sana na riwaya yake ya Mtuhumiwa. Natamani sana niipate
ili niisome tena.