John Heche mwenyekiti mpya BAVICHA taifa

Hatimaye CHADEMA tumevuka tanuru jingine la uchaguzi huu.Namshukuru MUNGU sana.Ndugu zangu CHADEMA hivi sasa imekua na kuwa na maadui wengi sana.Tunapigwa na vyama vyote vya siasa iwe chama kilichopo maradarakani au vya upinzani.Uchaguzi huu ulikuwa ni mtihani mwingine kwa chama.Wagombea wengi sana walijitokeza katika nafasi mbalimbali zilizotangazwa.Mwanzoni tulifurahi sana tukijua kuwa chama kimekuwa sana lakini humo humo wagombea ambao hawakuwa na nia njema na CHADEMA walijitokeza.Katika kila nafasii kulikuwa na wagombea ambao hawakuwaserious na lengo la kuitaka nafasi hiyo,wengine walikuwa wapo kwaajili ya kugawa kura,wengine waliomba kwaajili ya kuuza sura na wengine waliomba kwaajili ya maslahi binafsi/maslahi ya watu binafsi na kuna wengine walikuwa wanadhamira njema kabisa ya kutaka kuwatumikia vijana na kukijenga chama kwa maslahi ya chama.Pamoja na kwamba CHADEMA hatuna Kitengo thabiti cha Intelejensia(Kwa maana ya watu wenye Taaluma hii ).lakini kwakuwa chama hiki kina mkono wa MUNGU,MUNGU alitumia njia zake za asili kuwang'amua waliokuwa na nia mbaya.Baadhi yao wakaenguliwa kwa mujibu wa Kanuni na Taratibu za chama na baadhi walishindwa kwenye sanduku la kura. Binafsi nilikuwa naziangalia nafasi nyeti ili zipate viongozi wazuri wenye nia nzuri ya kujenga chama na waliogombea kwa ridhaa zao sio kwa kuwekwa au kushawishiwa na watu fulani.
Nafasi ya Uenyekiti nimefurahi ameshinda John Heche na ndio alikuwa chaguo langu tangu mwanzo 2009.Heche ana misimamo anaweza kusimamia misimamo yake na anamalengo mazuri na BAVICHA.Amegombea kwa ridhaa yake. HONGERA chalii Heche.
Nasubiri kuona tunapata Katibu Mkuu , Mwekahazina na Mratibu wa Uhamasishaji wazuri kwa maslahi ya chama.

Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.
Hapo kwenye red,sasa mlijuaje kama hamna intelligence ya kutosha...siasa bwana
 
Hapo kwenye red,sasa mlijuaje kama hamna intelligence ya kutosha...siasa bwana

Mjomba/Shangazi soma vizuri ili uelewe,usikimbilie kujibu kabla hujasoma mpaka mwisho.Nimejieleza vizuri kwamba pamoja na kwamba kitengo hicho sio thabiti lakini MUNGU ametumia njia zake za asili.

Pole kwa kutoelewa.Nimeandika kwa Kiswahili chepesi tu
 
Mjomba/Shangazi soma vizuri ili uelewe,usikimbilie kujibu kabla hujasoma mpaka mwisho.Nimejieleza vizuri kwamba pamoja na kwamba kitengo hicho sio thabiti lakini MUNGU ametumia njia zake za asili.

Pole kwa kutoelewa.Nimeandika kwa Kiswahili chepesi tu

Mungu yupi?....sorry!
 
Heche ni mzuri, moyo wake wote uko CDM matatizo madogo madogo ambayo aliwahi kutajwa kuwa nayo atabadilika naamini. kuna vijitabia mtu/binadamu anafanya but kadiri umri unavoenda anaimarika na kubadilika. hakuna binadamu aliye kamili. tumtakie heri na kumpa ushirikiano

Hapo ndo Watanzania tupoppotea tena sana pamoja na kwamba amechaguliwa katika uongozi wa vijana wa CDM lakini anatakiwa kuiwaza Tanzania na namna ya kuimarisha misingi ya nchi yetu kwa manufaa ya umma wa watanzania na sio kuwaza na kuota chama.
 
Hapo kwenye red,sasa mlijuaje kama hamna intelligence ya kutosha...siasa bwana

Knowing your area of weakness is a desired strength!! You are deadly weak if you don't recognize your weakness.

This is what CDM did and they had to be keen on it without fightinh but winning it with common sense .i.e (.....MUNGU alitumia njia zake za asili...) , and I believe this what Regia Mtema is putting forward. We need leadership that can identify areas of improvement on both short and long terms. What is wrong with Regia's comment in this perspective.
 
Okay!!....duh hii kali.

Imeandikwa .......mshukuruni Mungu kwa kila jambo..... mkaribieni Mungu na shetani atawakimbia........mpeni Mungu utukufu kwa matendo yake makuu (ikiwemo na kukupa uongozi uliokuwa ukiuota na kuuhitaji, na hii ni sehemu ngumu sana kwa Binadamu kuifanikisha salama hakika inahitaji mkono wa Mungu). Au hupendi wewe kumhusisha Mungu katika hili?
 
Imeandikwa .......mshukuruni Mungu kwa kila jambo..... mkaribieni Mungu na shetani atawakimbia........mpeni Mungu utukufu kwa matendo yake makuu (ikiwemo na kukupa uongozi uliokuwa ukiuota na kuuhitaji, na hii ni sehemu ngumu sana kwa Binadamu kuifanikisha salama hakika inahitaji mkono wa Mungu). Au hupendi wewe kumhusisha Mungu katika hili?
Sipendi kabisa ,haimake sense hata kidogo.
Mungu wangu anaweza kuwa shetani kwako,
Si unajua wazungu na waarabu walivyotupumbaza?
 
hongera dada. lkn anatokea mkoa gani huyo? na sisi wa\pwani pwani tutakumbukwa lini cdm? au tuhamie huko sote?

It was by voting, (I mean election and not selection) so wapi anatoka is senseless and does not make any count in my view.
 
"To ceaser what is His and to God what is His"........God has nothing to do with ur politics games,leave God out of this..haa
 
Sipendi kabisa ,haimake sense hata kidogo.
Si unajua wazungu na waarabu walivyotupumbaza?

Kwa hiyo angalia kama mungu wako anaweza kuwa shetani, basi mkono wa Mungu asiyeweza kuwa shetani utakuondoa na mungu wako pia. Hapo ndipo utajua kwa hakika kuwa mungu wako ni shetani na utamwaacha. Bila shaka Mungu wa wote hawi shetani anabaki Mungu kwa wote.
 
Kwa hiyo angalia kama mungu wako anaweza kuwa shetani, basi mkono wa Mungu asiyeweza kuwa shetani utakuondoa na mungu wako pia. Hapo ndipo utajua kwa hakika kuwa mungu wako ni shetani na utamwaacha. Bila shaka Mungu wa wote hawi shetani anabaki Mungu kwa wote.
Babuu!!..yaishe,umeshinda!!
 
hongera dada. lkn anatokea mkoa gani huyo? na sisi wa\pwani pwani tutakumbukwa lini cdm? au tuhamie huko sote?

Malaria Sugu.Mimi siziwezi siasa zako za udini na Ukabila.Hizo peleka Kanisani na Misikitini na Ukabila peleka huko Kenya sio hapa Tanzania.Hapa kwetu Tanzania kuna Makabila 120 Ukabila hautawezekana. Kama nyie mnachagua watu kwasababu ya Kabila zao au dini zao basi kwetu hakuna uchaguzi wa dini kwakuwa hapa sio kanisani wala msikitini na wala hakuna uchaguzi wa kabila kwakuwa hatuchagui machifu wala mamwinyi. Tunachgua watu kulingana na merits zao bila kujali dini,kabila wala uwezo kifedha.

Jumapili njema
 
Hongera sana JOHN HECHE kwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Bavicha,kazi yako kubwa ni kuleta mshikamano kwa vijana wote wa Chadema nchi nzima,pia kuhakikisha kuwa jimbo la Tarime uchaguzi ujao linarudi Chadema.Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Chadema,Mungu ibariki Bavicha.

Hongera Heche. Tunataka uongozi wenye vision kuhusu Tanzania ya leo na miaka 50 ijayo.
 
"To ceaser what is His and to God what is His"........God has nothing to do with ur politics games,leave God out of this..haa

Imeandikwa.......Mamlaka zote ziko chini yake huziweka yeye na kuziondoa........ndiye Mungu wa miungu, Bwana wa Mabwana, Mfalme wa Wafalme, mwanzo na mwisho..........yeye ndiye Kiongozi wa kweli..........

Please, Please, you tell God to "leave". I can not for sure!!!
 
Malaria Sugu.Mimi siziwezi siasa zako za udini na Ukabila.Hizo peleka Kanisani na Misikitini na Ukabila peleka huko Kenya sio hapa Tanzania.Hapa kwetu Tanzania kuna Makabila 120 Ukabila hautawezekana. Kama nyie mnachagua watu kwasababu ya Kabila zao au dini zao basi kwetu hakuna uchaguzi wa dini kwakuwa hapa sio kanisani wala msikitini na wala hakuna uchaguzi wa kabila kwakuwa hatuchagui machifu wala mamwinyi. Tunachgua watu kulingana na merits zao bila kujali dini,kabila wala uwezo kifedha.

Jumapili njema

THANK YOU!!!

Very cute, I hope it has been well understood otherwise Dada USISUMBUKE NAO SANA WATU WENYE FIKRA ZA HIVI, Wewe waangalie tu hawawazi kingine ni uozo huu tu ndo humo kwenye fikra basi.
 
Imeandikwa.......Mamlaka zote ziko chini yake huziweka yeye na kuziondoa........ndiye Mungu wa miungu, Bwana wa Mabwana, Mfalme wa Wafalme, mwanzo na mwisho..........yeye ndiye Kiongozi wa kweli..........

Please, Please, you tell God to "leave". I can not for sure!!!
Duh!..basi kamweka ghadafi,mubarak,assad,kim jong il....kwanini awaweke hawa kuwatawala viumbe vyake?....wamemkosea nini?
 
"To ceaser what is His and to God what is His"........God has nothing to do with ur politics games,leave God out of this..haa

ivi wewe unajua Biblia au umeropoka tu? Huo mstari Yesu alikuwa anaongelea nini? Mara ngapi Mungu ameweka Wafalme Israel na nchi nyingine nyingi? wacha kuweka mistari michache kwa kusudi la kupotoza watu...
 
Back
Top Bottom