Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia Makamu Mwenyekiti wake Taifa, Mheshimiwa John Heche, kimezungumza na waandishi wa habari pamoja na wanachama wa chama hicho, na kueleza masikitiko makubwa kufuatia kifo cha Hayati Edwin Mtei, Mwasisi wa CHADEMA.
Akizungumza katika mkutano huo, Heche amesema chama kimeguswa kwa kiasi kikubwa na msiba huo mzito, na kueleza kuwa Hayati Mtei alikuwa nguzo muhimu katika harakati za demokrasia nchini.
Katika kumuenzi na kudumisha kumbukumbu ya mchango wa Hayati Mtei, Heche ameeleza kuwa CHADEMA kimepitisha azimio la kujenga chuo maalum kitakachotumika kama kumbukumbu na heshima ya kudumu kwa Mwasisi huyo wa chama.
Akizungumza katika mkutano huo, Heche amesema chama kimeguswa kwa kiasi kikubwa na msiba huo mzito, na kueleza kuwa Hayati Mtei alikuwa nguzo muhimu katika harakati za demokrasia nchini.
Katika kumuenzi na kudumisha kumbukumbu ya mchango wa Hayati Mtei, Heche ameeleza kuwa CHADEMA kimepitisha azimio la kujenga chuo maalum kitakachotumika kama kumbukumbu na heshima ya kudumu kwa Mwasisi huyo wa chama.