The Tomorrow People
JF-Expert Member
- Jul 11, 2013
- 2,690
- 2,855
Toka ajiite mwamba wa kaskazini, toka aseme hayupo next level Bali level yake mwenyewe....Joh Makini amekuwa akipanda siku baada ya Siku. Na siri kubwa ninayo iona Kwa Hawa weusi ni kwamba wanaubunifu wa hali ya Juu...pili wamefanikiwa sana kutengenezw Hiphop yenye ladha ya kitanzania... wamepunguza sana zile Swaga za kimagharibi. Tatu weusi ni watu poa sana hawanati wala hawajivuni... Ni watu ambao wako kazini na wanajua wanachokifanya. Nne wanaheshima ya kazi ( work ethic) Tano Joh na weusi sio watu wa mabiff na maskendo ya kipuuzi. Wao wako busy na note tuu.
A'city in the house.
A'city in the house.