Job Ndugai Umetukatisha Tamaa

Aisee Ndugai ni kituko cha mwaka, hivi angesikiliza hoja ya Mbowe hata kwa dakika mbili tu, kisha akai crush angepumgukiwa nini? nchi imepoteza muelekeo. eti huyu ndiyo naibu spika... yaani mpka unasikia kichefuchefu
 
Ndugai ulichaguliwa na wabunge wenzako ili kuliongoza bungle kwa uadilifu na bila upendeleo kwa chama chako lakini unazidi kuonyesha jinsi unavyopemdelea chama Hebu badlika mh

Yule ni vuvuzela ati!!!.....Ni sawa na kimpigia mbuzi gitaa...Angallia kwanza ile kichwa yake sometimes huwa naona kama inatoa moshi...
 
Udhaifu wa Ndugai ni chachu ya Mabadiriko, Udhaifu wake ni kielezo kuwa chama chake siyo makini, hawana watu makini wa kusimamia mambo muhimu ya nchi. Chama cha Ndugai kina ogopa kuwapa majukumu watu wenye uwezo na weledi kama Sita na kuweka vilaza, matokeo yake ndiyo haya.
 
Ndugao ni kiongozi dhaifu na pia na hisi nafasi aliyo nayo alibebwa ila hana hata chembe ya talanta ya uongozi

Ugonjwa wa Ndugai alirithi kwa Makinda! hizi taka tunazoziona ni muendelezo wa midudu alowahi kuiperfom alipokuwa deputy wa Sitta coz alishafanya ubabe huu kwa Zitto miaka kadhaa ilopita. Usipoteze kadi yako maana ndo silaha ya kumalizia udhalimu huu.
Nawasilisha.
 
Anafanya haya kwa sababu anajua kuwa taifa limeupokea wakati wa mabadiliko. Ikumbukwe kuwa punda mkata roho mateke yake hujidhihirisha. Ahsante kwa Ndugai kwa mchango wa kuinywesha sumu CCMagamba na kuionesha muda wa maziko 2015.
 
Ndugai ulichaguliwa na wabunge wenzako ili kuliongoza bungle kwa uadilifu na bila upendeleo kwa chama chako lakini unazidi kuonyesha jinsi unavyopemdelea chama Hebu badlika mh

ukiona yule jamaa anakalia kiti hujue kuna jambo la kustahajabisha anataka kulifanya.
 
Mi kudhani nilielewa vibaya kwamba ndugai hamnazo upstairs. Mbowe nilimsikia na kumwona akisema anayo hoja, tena kwa unyenyekevu sana. Nilishindwa kuelewa wapi amekosea kiasi cha kutolewa nje kwa maguvu. CCM imezoea kutumia maguvu ikiambiwa ukweli kwani daima ukweli unauma. Baadae wabunge wa ccm na Lyatonga (CCM Damu) walianza kuongelea tukio na sikumwona yeyote aliyeangelea issues. Walishangiliana kwa upuzi walioelezana kuhusu wapinzani na sio kuengelea mswada. Walijikomba sana kwa JK ati ni mvumilivu, ati wananchi wameona kwamba wapinzani hawafai, blablablaaaa. Hivi mie nawauliza wapunge wa ccm waliochoka kichwani, mnadhani Tanzania ya leo ni ileile ya 1947? Mnakosea, sisi sio wapumbavu kiasi hicho. Kibao kimegeukia ccm na wataendelea kujimaliza kwa ujinga wao wenyewe. Ni aibu kumfanyia upumbavu ule kiongozi mkuu wa upinzani bungeni ambaye kama angeruhusiwa kusema tungejua kama anaongelea takataka au tunu. Sasa CCM mnachokifanya ni kuwapa nafasi ya umaarufu wapinzani wenu maana huku nje tunachambua kila neno lisemwalo bungeni na kujua nani ni pumba na nani ni mchele. Kuweni macho ccm, ya Arusha inaelekea hayajawafunza maana sikio la kufa halisikii dawa. Mnaruhusu polisi kufanya yale mliyozoea kuwaruhusu mitaani kwa kuburuza waheshimiwa LIVE wakati dunia yote inaona, sasa mtatudanganyia wapi? Angalia baada ya wapinzani kutoka, pumba tu ziliongelewa na kulialia tu kwa mfa maji. Wapinzani ni chachu ya hioja bungeni. Nilimsikia yule bwana mdogo wa Sikonge sijui akidai CCM wanatumia hoja ya nguvu. Hakujua kwamba hata kiswahili kilimwendea kombo akashindwa kutofautisha na nguvu ya hoja na ndo matokeo ya jana.

Tanzania, CCM inatumia hila zote kuhakikisha hoja yao ya nguvu ishinde kuendeleza serikali mbili maana uhai wao umo katika serikali mbili bila Tanganyika kuwapo. Wazanzibari wenyewe wamewashitukia siku nyingi na ndo maana ccm ikaona iwakwepe kutoa maoni yake kuhusu mswada huu, maana wanaelewa kwamba Zanzibar inataka kuiona Tanganyika inakuwapo.
 
Yeye nikiongozi ila anashindwa kufuata zile kanuni za uongozi hapaswi kufanya maamuzi kama yale ambayo anajua kabisa yatakuw na negative feedback kama yale hakupaswa kutoa amri kama ile na kitu cha kujiuliza kwanin akiwa yeye tu ndo vurugu zinatimuka?
 
Habar wanajamii, hakika naibu spika ameudhihirishia uma na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla kwa jinsi alivyokosa busara, hekima na weledi katika kutimiza majukumu yake kama kiongozi muhmu kabisa wa chombo cha kutunga sheria badala yake ameendekeza ubabe, na utashi wa kisiasa, naibu spika anapaswa kutambua bunge ni taasisi ya uma na si mali yake binafsi au ya chama chake cha siasa, anapaswa kuheshimu utu na maoni ya binadamu wengne, kwa nguvu aliyoitumia jana imemshushia heshma na ataondoka katika kiti cha unaibu spika akiwa na sifa mbaya ambayo itamchukua muda kuisafisha sifa hyo, mh ndugai anapaswa asome alama za nyakati na aache kuongoza bunge kwa hisia, mbona mh makinda au muhagama wanaepuka vurugu hzi? Hakika ndugai ndo mwanzilish wa vurugu hz kwa tabia yake ya udikteta na kutoheshmu mawazo ya wenzake!
 
Mtu -------- akili yake ndio ikoh hivyo. Hana akili timamu ndio maana anafanya haya.
Kwa wajinga wachache wanaweza kufikiri kama anakisaidia chama cha ccm lakini ukweli ni kwamba anakiharibia tu. Sura ya ccm mbele ya jamii inazidi kuchafuliwa na watu kama hawa.
 
Yan ndugai ameonyesha ni kwa jinsi gana amekosa busara na hekima katika kufanya maamuzi, alitakiwa kusoma mood ya wabunge wa upinzani kabla ya kutoa maamuzi ya kibabe na kutojali hadhi za wabunge wenzake kwa hli ndugai ametenda dhambi kubwa kwani kuamuru viongozi wenzake kuburuzwa nje kama ci binadamu kwa hli inabidi ajitazame kwa kina
 
sorry kama nitawagusa na wengine ila ukweli ni kwamba watu wafupi huwa wanajistukia kuona kama vile hawaheshimiki, kwa hiyo mara nyingi hujaribu kujitutumua ili na wao waonekane, so sio kosa lake kimo nacho kinachangia
 
Mtu -------- akili yake ndio ikoh hivyo. Hana akili timamu ndio maana anafanya haya.
Kwa wajinga wachache wanaweza kufikiri kama anakisaidia chama cha ccm lakini ukweli ni kwamba anakiharibia tu. Sura ya ccm mbele ya jamii inazidi kuchafuliwa na watu kama hawa.

Nilitaka kucomment ila nikaona majibu yangu na yako yanashabihiana.
Kwa hiyo napotezea.
 
Vetting ya kutosha inahitajika hasa kwa watu wanaokwenda kushika madaraka ya uongozi wa nchi hii - tusipokuwa makini tutakuwa kama somalia, maana nao walianza hivi hivi - kudharauriana.
 
Back
Top Bottom