JKT yafafanua kuhusu vijana 147 waliokutwa na VVU

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1675707364536.png
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limesikitishwa na taarifa iliyosambaa mitandaoni kwamba vijana wake 147 wana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na kuambatanishwa na picha za vijana wengine wanaohudhuria mafunzo ya JKT makambini.

Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi kwa kipindi cha Februari 2022 hadi Februari 2023 iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma Ijumaa Februari 3, 2023 ilieleza kuwa vijana 147 kati ya 67,299 waliojiunga JKT kwa mujibu wa sheria walikutwa na maambukizi ya VVU.

Takwimu hizo ni sawa na asilimia 0.22 ya vijana waliomaliza kidato cha sita nchini na ambao waliitwa kujiunga na JKT katika kipindi cha miaka ya 2019, 2020 na 2021.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 6, 2023, mkuu wa tawi la utawala wa JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema taarifa zilizotolewa na kamati ni sahihi lakini wamesikitishwa kutumika picha ambazo sio za wahusika.

Amesema picha hizo zimeleta taharuki kwa familia za vijana wanaopatiwa mafunzo kwamba wameathirika na maambukizi ya VVU.

“Vijana ambao hukutwa na changamoto ya kiafya hufanya mafunzo yao chini ya uangalizi wa wakufunzi ili kuhakikisha wanamaliza mafunzo yao salama,” amesema.

Amesema JKT inaamini kitendo hicho ni cha udhalilishaji wa utu wa binadamu kwa kutumia picha za vijana wasiohusika.

“Huo ni ukosefu wa maadili ya uandishi wa habari na uhuru wa vyombo haukutumika ipasavyo. JKT inavitaka vyombo vyote vya habari na mitandao ya kijamii kuomba radhi na kuondoa picha hiyo mara moja,” amesema mkuu huyo wa tawi la utawala JKT.

MWANANCHI
 
Ufafanuzi wa nini? Kwani waliotoa hizo taarifa ni wajinga? Toeni elimu ya VVU ili vijana wasiambukizane hovyo.
 
Bunge ndo watunga sheria , udhalilishaji ni pamoja nakutokusema ukwel. nadhan walijaribu kutumia lugha ya picha inayowakilishwa na mavazi ya jeshi hilo.
 
Hoja sio VVU, hoja ni matumizi ya Picha za Vijana wasohusika Kwa habari kama hiyo .


Pongezi Kwa JKT .... Waombe Radhi Mara Moja !!!
 
Kuna watu hawajui kuhusianisha picha na habari. Hawa itakuwa hawajui kitu kinaitwa pictorial interprentation. Hiyo picha mbona haioneshi waathirika hao inaokubali wapo ila picha sio? Mleta habari ameweka picha ya vijana wa jkt kwa ujumla isiyomaanisha ndio waathirika. Ni picha ya kawaida kuonesha hao ndio vijana wa jkt ila sio ya waathirika. Huyo kiongozi amehamaki bure
 
Back
Top Bottom