kidE Meshack
Member
- Jan 8, 2013
- 92
- 7
Mungu saidia tupate hizi nafasi
SIKILIZEN
Usikilize moyo wako na utayari wako nafasi hii ya jkt ni ya kujitolea lkn ajira zitakukuta humo cha msingi uwe mvumilivu na utayari ukijua kwamba unaenda kupigania taifa lako ...nimepitia comments zote humu lakini sijashangaa kukutana na maswali km hayo sababu bdo hamjaingia kufundishwa uzalendo watakaobaatika watakuja kukubaliana na mimi
NAMNA YA KUJIUNGA
Fuatilia kwa makini wilayani au mikoani kama tayar wameshaanza kupokea maombi suala la form ni baada ya jina lako juchaguliwa cha kufanya sasaiv andaa barua. kutoka serikali ya mitaa ya kukutambulisha, passport size, barua ya maombi pamoja na vyeti vyako vyote hivi ndivyo utakavyo wasilisha hukoo alafu baadae sasa litakuja suala la fom ikiwa tayar jna lako limepita
ONYO
Epuka kutapeliwa kwa form zinazouzwa mtaani
MWISHO
Anza kuiweka akili yako fiti kwa ajili ya kuingia katika mazingi mapya..mazingira ya kiaskari sio tna kiraia
JIONI NJEMA NA KILA LA KHERI MA COMRADE WENZANGU
Mkuu nakubari sana harakati zako tupo pamoja.... naomba tujulishe wilaya ya ilala wanapokea maombi mwisho lini? na form zinatolewa kwa utaratibu upi?Andika barua ipitie serikali ya mtaa na kata. Then ipeleke wilayani. Hii ni sample ya kinondoni.
View attachment 237690
Mkuu nakubari sana harakati zako tupo pamoja.... naomba tujulishe wilaya ya ilala wanapokea maombi mwisho lini? na form zinatolewa kwa utaratibu upi?
Unaweza kwenda moja kwa moja kadetI bila kupitia mafunzo ya tpdf nikimaanisha kuruta?
Kwanza unaingia jkt then tpdf the kadeti ...kama ukipata mafunzo ya jkt ya awali ukafanikiwa kuchukuliwa jwtz ni rahisi kwako kwenda kadeti ..lakini yote haya yatategemea Kiwango chako cha elimu I mean kuanzia diploma
Nashukuru mkuu kwa ufafanuzi mzuri
Alikuambia nini mkuu ?????? maana nami nataka nikachukue fomu hizo kesho zinakopatikana, nijuze nisijeingia mkenge.... hata kwa PM nitashukuru mkuu.Mkuu nimekuelewa kote kote ulikoongea.
Watu wameshaanza kupiga madili hapa mjini.
Jana usiku nimeongea na jamaa yangu mmoja hivi, mambo aliyoiambia yani hata sijaamini...
All in all bongo kuna tatizo kubwa sana la ajira...
mkuu kuna ukweli kuwa watu wenye kigugumizi hawahitajiki jeshini?Ilala japo cna uhakika sana ila kwa za chini ya kapet wameanza kupokea barua nao wiki hii na mwisho nadhani ni wiki hii. Usahili kwa habari nilizozipata utaanza kufanyika week ijayo ngazi ya wilaya. Utaratibu wa barua nadhani ni ule ule ila unaweza kwenda pale ofc za mshauri wa mgambo wilaya ukapata maelezo zaidi. Ila kwa kinondoni wanapokea barua mpk tar 30. Ova