Chinga na mmasai wa inverstment centre wali wakatisha tamaa wawekezaji kutoka Denmark waliotaka kujenga kiwanda cha kusindika matunda pale Lushoto. Chinga aliingia ubia na rafiki zake ambao baadaye aliingia mitini bila kuanzisha hicho kiwanda chao.... Jamaa wa denmark walikwenda Kenya wakaanzisha kiwanda huko na matunda wananunua Tanga. Wakisindika wanaturudisha matunda kwenye chupa na kwa bei mbaya pale shoprite na supermarket zingine.....sio wazo jipya mzee wa bwaga moyo hilo!!!!!!!
na ssafi, bongo, - 20.07.08 @ 21:50 | #23210
NANI AVUMILIE NA WEWE NDIE MZEMBE NAMBA MOJA MAFUTA YAKAPANDA YASIPANDE HALI YA TANZANIA NI UMASKINI, MARADHI ,MADAWA HAKUNA MATATIZO YALIOKUWA HAYANA MSAADA MPAKA ATOKE MZUNGU HUKO AJE ASEIDIE KWANI NYINYI HAMUWAONI TUTASAIDIWA NA WAGENI MPAKA LINI AU TUVUMILIE WEWE NA FAMILIA YAKO MUSTAREHE.
na BONGO FLAVA, BARA, - 21.07.08 @ 01:30 | #23213
HII HALI MBAYA YA MAISHA SIO TUU KWA WATANZANIA NILA DUNIA NZIMA. hUKU MAREKANI TUNANUNUA MAFUTA GALLON $ WAKATI ZAMANI ILIKUWA $2.99! VITA VYA IRAQI NA MAPIGANO YA MUISRAEL NA MPALESTINA VINAZUA BALAA KUBWA LA MAISHA DUNIANI. WAARABU HUPANDISHA BEI YA MAFUTA KILA MPALESTINA MMOJA AKIUWAWA NA HUKO IRAQI SUPPLY YA MAFUTA NDIO KWANZA IMENYONDA SASA KIKAAANGONI TUPO MIMI NA WEWE TUNAIPATA. RAISI WETU KASEMA KWELI KABISAA NA WALA TUSICHUKULIE HASIRA WABONGO WENZANGU. HUYU NDIYE RAISI MUWAZI KULIKO WOTE WALIOPITA . TUYFANYIE KAZI HAYA MAISHA MAGUMU KWA KUOMBA VIWANDA VINGI VIJENGWE NA KUKATAA KABISAA KABISAA KUWATUKANA WAHISANI MANENO MABAYA YA KISIASA. HAYA NI MADHALA YAMETOKEA TOKA ENZI ZA TANU 1978 MPAKA LEO HII YANAPOPOOZWA NA RAISI WETU KIKWETE.
na FERDINANDO SANCHO, MEXICO, - 21.07.08 @ 01:52 | #23214
SANCHO umefananisha vitu viwili tofauti kwani taratibu za uuzaji mafuta TZ na USA ni vitu viwili tofauti umetoa mfano wa bei ya mafuta ya marekani lakini umesahau kutoa bei za majirani zake ambazo ni za chini kabisa kwa mfano VENEZUELA bei ya mafuta huko ni senti 45 kwa galoon na pia huko Mexico uliko bei ya mafuta ni dola 2.50 kwa galooni. kupanda kwa bei ya mafuta marekani kunatokana na sera za mafuta ambazo hazimlindi mteja isipokuwa kampuni za mafuta ambazo George Bush NA **** CHENEY wako karibu nazo kimaslai na ndio maana chama cha demokrasia kimekuwa kikitaka uchunguzi wa kina kwenye kampuni za mafuta kwani zinawahujumu wananchi. tukirudi Tanzania ni kwamba anayewaumiza wananchi kwa ugumu wa maisha ni Kikwete na marafiki zake mafisadi kwani mabilioni yaliyoibiwa ndani ya nchi hii yangeweza kusaidia nchi kwa kiasi kikubwa ikiwemo ku subsidise bei ya mafuta ambayo ingesaidia sana kupunguza bei ya mafuta kwa kiwango kikubwa.
na nick, Tanzania, - 21.07.08 @ 02:58 | #23219
Jamani si afazali ya JK kawambia hali alisi kuliko yule aliekwenda Rufiji kipindi kile cha mafuliko na kuwambia wajomba zangu wafanye bidii kwenye kilimo hali kuna mafuliko.isitoshe na ile kauli ya wafunge mikanda lakini lada na ile ndege ya rais lazima vinunuliwe.....
kaja mkweli na jitihada zake zinaanza tunalalamika naomba tumpe mda
na Miembe saba, Boston USA, - 21.07.08 @ 04:24 | #23223
Nick # 23219
Umetoa uchambuzi mzuri kwa kifupi. Wakulaumiwa ni Mkapa (mlalamikiwa No 1), Kikwete nae anafuatia, hasa kuhusu mikataba ya kutunyonya ambayo serikali yake imeingia.
Hali ya maisha ni ngumu kwa wastani Dunia nzima, Venezuela bei ya mafuta ni rahisi kwakuwa wao wanayo na wanayachimba kwa manufaaa ya wananchi wa Venezuela.
Maisha magumu kwa watanzani hayasababishwi na kupanda kwa bei ya mafuta duniani pekee, haya maisha magumu yalianza kabla hata ya kupanda kwa bei ya mafuta, bei ya mafuta imeongeza ugumu wa maisha na wala sio kisababishi kikuu. Utawala mbovu, kutojali maslahi ya taifa na kutofuata miiko ya kazi kwa watendaji wa serikali ni baadhi ya vyanzo vya maisha magumu kwa watanzania na waafrika kwa ujumla.
Hii safari ni ndefu, lakini tutafika.
na Avisenia Marina, Wellington, - 21.07.08 @ 05:06 | #23226
Huyu JK anachekesha sana la mafuta anaongelea,hajui kwamba kabla bei haijapanda Chinga na washirika wake waliingia mikataba michafu,JK katajiwa wahusika anaunda tume na ***** ni mjumbe kuchunguza wezi.
milioni 150/siku kwa miaka 2[365 days] na 133 bilioni haoni kuwa ni tatizo la maisha magumu.
Kaambiwa kakaa kimya eti leo anaongela mafuta,si unafiki ni nini. Kama ni karata wa tz tuna garasha.
na leader - 21.07.08 @ 05:35 | #23230
Heeee!
jamani tusidanganyane kwa kuleta data za kila mtu anapoishi , ni kweli maisha magumu kila pahala hapa duniani hakuna hata sehemu moja iliyo kuwa rahisi , ispokuwa muhimu ni juhudi yako mwenyewe kukabiliana na hiyo hali, mimi hapa ninakazi kibao ninafanuya kazi kuanzi saa12 hadi saa nne usiku kutosheleza mahitaji yangu , saa kumbi na mbili nachinja kuku islamic butchery, saa sita naenda kazini kwangu kiwanda cha magodoro, saa 12 naenda airport kwenye kazi ya kutuma vifaranga. hebu leo tuangale kule nyumbani wanaojituma ni akina mama zetu kuanzia asubuhi hadi anaingia kitandani yeye ni kazi tu , wengi wao wapo vibarazani, na kwenye mabaaa, ni kweli tatizo la sera na uongozi lipo lakini la msingi kwanza je? watz wangapi wanaojituma kwa manufaa ya taifa au tunataka raha bila ya kupata shida?
ile nch inamambo mengi ya kuangalia tusidanganyaene kwa miaka miwil au mitano kuwa kuna mtu ataleta unafuu wa maisha, unafuu wa maisha unaletwa kwa watu wote kwa kujibana na kuwajibika kwa taifa , tuache ndoto za mchana, lazima kwanza tufe ndio tupate pepo!!!!
pale kwetu kariakoo, yupo mjomba wangu anaingi shimoni karikoo , akitoka saa tisa , utamkuta maazese kaweka pamba zake anatangaza huduma kwa marafiki zake walio kuwa mitaani , sasa hiyo nchi kweli itajengwa na nani ikiwa wengi wao ni wasanii wa maisha.
na kongera, Australia, - 21.07.08 @ 05:59 | #23234
Kiwete Kwa kweli huna jipya kwani nakukumbuka pale Paris uliulizwa kwa nini wananchi wako na nchi yako ni Maskini Ukasema Hujui!! president wa nchi hujui kwa nini nchi yako ni Maskini na wananchi ni Maskini!!! My God!!! Ila huo wimbo wa kupanda kwa bei ya mafuta naona sasa umezoeleka mno labda tafuta Gear nyingine Mzee!! Hakuna siku nyingi wadanganyika wataanza kukuzomea!!! Hillooo fisadi utapenda? Hivyo tia akili tafuta wimbo mwingine!!
Pia suala la mafuta ni suala nyeti sana ila ikumbukwe kwenye nchi yetu kodi inayotozwa kwenye mafuta ni Tsh 650 kwa kila lita moja!! ina maana kama mafuta yangetolewa uarabuni Bure Kabisa, gharama ya usafiri tu ni Tsh 200 kwa lita hivyo jumla ingekuwa Tsh 850 kwa lita!! Kwa hiyo tatizo si kupanda kwa bei uarabuni ila ni kodi zetu!! Kama kweli unaipenda Tanzania punguzeni kodi Hiyo iwe Hata angalau Tsh 200 kwa lita is reasonable!!!
na TY, Tanzania, - 21.07.08 @ 07:12 | #23237
Ni jambo la kushangaza na aibu kuwa hadi leo wastaafu wa Jumuia ya Afrika Mashariki upande wa TZ hawalipwa pesa zao. Wengine wako huko huko Tanga na wanaambiwa wavumilie shiada!!! Wazee wetu walizunguushwa sana wakati wa Mkapa na sasa naona JK anafanya yale yale...Kama zipo pesa zakupeleka kila mkoa kwa wajasirimali basi uwezo wa kuwalipa wazee wetu upo.. Naomba serikali hii ya sasa imalize kabisa kilio cha wazee wetu
na Zawadi, UK, - 21.07.08 @ 07:51 | #23239
DUH, SIJUI SISI WATZ TUNA MATATIZO GANI?
HIVI HATA UKWELI BADO PIA TUNAUKATAA?
KILA PEMBE YA DUNIA HII MALALAMIKO YA KUPANDA KWA BEI YA MAFUTA KUNAMGUSA KILA MTU, KIKWETE ANASEMA UKWELI, LAKINI BADO KUNA WENGINE WANATAFUTA MTAJI WA KISIASA, AHH, SASA NYIE MNATUANGUSHA KWANI SI WA KWELI.
MIMI NIPO HAPO USA KWA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA BEI YA MAFUTA IMEPANDA MARA DUFU NA INAENDELEA KUPANDA KULA KUKICHA.
KANA KWAMBA HAITOSHI BEI YA VYAKULA NAYO IMEPANDA VILEVILE, KWA MFANO MCHELE BEI YAKE IMEPANDA SANA KWA KIPINDI HIKI CHA MWAKA MMOJA.
KWAHIYO ANAYETUAMBIA KUWA KIKWETE ANASEMA UONGO, BASI HUYO NI WAKUOGOPA KAMA UKOMA.
TUJIFUNZE KUSEMA UKWELI
TUJIFUNZE KUELEKEZA BADALA YA LAWAMA
na Mkweli, USA, - 21.07.08 @ 08:31 | #23241
KAKA YETU USIPATE TABU WEWE SEMA TU. SISI TUMEZOEA SHIDA , HUNA TOFAUTI NA KARUME ANAEWAMBIA WA ZNZ WATAZOEA TU. SASA SISI TUMEZOEA NA WEWE ENDELEA KULA NCHI MANA MAFUTA SI KAZI YAKO. WEWE LINDA MTANDAO WAKO USISAMBARATIKE MANA INABIDI UUTUMIE KURUDI MADARAKANI MWAKA 2010.
na mahsi, dsm, - 21.07.08 @ 09:07 | #23246
Huu anaotufanyia kikwete ni usanii wa maisha yetu, amesahau maneno yake wake wakati anaomba kura kuwa atahakikisha kila mtanzania anapata milo mitatu kwa siku leo anatuambia tuvumilie dhiki tuliyonayo wakati wao akina kiketwe na mafisadi wenzake ndio mnao changia hali hii. ole wenu siku ikifika ya watanzania kusema no.
na Kojak - 21.07.08 @ 09:08 | #23248
HII pesa yetu ya JUMUIYA YA AFRIKA sasa ni zaidi ya miaka 30 hivi kweli tuna Kiongozi(RAIS) anayejali watu wake ?wengi wetu wameishaaga dunia na ambao bado tupo tupo taabu tupu KWELI UFISADI HAUISHI...mara pesa zipo ngojeeni malipo..tunakaa hapo ikulu tunawaona wanapita wako saafi sisi hata mkojo wa kukojoa hakuna mwilini KIKWETE TULIPE VIJISENTI VYETU TUKANUNUE HATA NGUO ZA KUZIKIWA.
na E T LUKUBA, TANZANIA, - 21.07.08 @ 09:22 | #23251
Kula tano Mahsi dsm. Kikwete suala la mafuta na maisha magumu havimuhusu kabisaa. Ndio si anatuonyesha hivyo kwa kuwalinda mafisadi!! Na sasa kapata kisingizio cha bei ya mafuta basi ndo itakuwa hadithi. Hivi wadanganyika wenzangu mnafikiri bei ya mafuta ikishuka (lets say) hadi nusu, ndo maisha yatakuwa bora kwa kila mdanganyika?
Dhahabu imepanda sana bei katika soko la dunia. Kwa nini vitu kama hivi vimeshindwa kufidia pengo la mafuta yaliyopanda?
Watu wengine wanafananisha bongo na marekani eti na marekani maisha yamepanda. Nie ndugu zangu hebu acheni mzaha! Wewe unakula humburg na pizza Macdonald halafu unatuambia maisha yamepanda?? Chonde chonde jamani. Natamani mngerudi huku mkapigika mkashindia kauzu ndo mngejua watu wanaongea nini
Wengine wanatuita wavivu kwa kuwa wako Australia wanachinja kuku. Mbona hutuelezi unalipwa kiasi gani kwa kuchinja hizo kuku? Malipo yako kwa siku ni mshahara wa miezi miwili wa mtanzania. Halafu afadhali hizo kazi zenyewe za kuchinja kuku zingekuwepo. Ndugu yangu kama unavijikazi hebu nisaidie kamoja mwenzio niko kijiweni nimepigika. Ajira milioni tulizoahidiwa bado hazijatufikia wenzio.
na mlugaluga, danganyika, - 21.07.08 @ 09:27 | #23252
Mzee JK mbona unaanza kupingana na ahadi zako? ulisema maisha bora, sasa unasema uvumilivu, next time utasema tufe polepole.
Wakati unaahidi maisha bora ulikuwa unaropoka au kuwahadaa watanzania waliozoea kulaghaiwa kila kukicha?
Lakini hili ni fundisho kwa wapiga kura walio kama vifaranga vya kuku wanaoahidiwa kunyonya kesho hali ya kuwa wajua kabisa mama kuku hana hata chuchu moja ya kutolea maziwa.
Ha ha ha habari ndiyo hiyo.
na Cosmas Gabriel - 21.07.08 @ 09:51 | #23255
MIMI NANSHANGAA JK KILA SIKU KULALAMIKIA BEI ZA MAFUTA.TUSICHOAMBIWA NI KUWA WAKATI BEI YA MAFUTA IMEPANDA HATA BEI YA DHAHABU,TANZANITE NAMAMDINI MENGINE NAYO IMEKUWA IKIPANDA KILA KUKICHA. WAARABU WANAFAIDIKA NA MAFUTA JE SISI TUNAFAIDIKAJE NA BEI YA DHAHABU????????? HALAFU CHA KUCHEKESHA ETI NA SISI TUNALALAMIKIA KUPANDA KWA GHARAMA ZA VYAKULA BADALA YA KUSHANGILIA MAANA SISI NI NCHI YA KILIMO. ZAIDI YA WA-TZ 70% NI WAKULIMA. KAMA SERIKALI INGEKUWA NA SERA NZURI ZA KILIMO TUNGEWEZA KUFAIDI BOOM HII YA GHARAMA ZA CHAKULA LAKINI KINYUME CHAKE TUNAKAA NA KULIA. TATIZO KUBWA LA TZ NI SERA MUFILISI.
na Roman, Tanzania, - 21.07.08 @ 08:14 | #23273
Bila kutafuna maneno hali ya maisha imepanda sana[inflation] hasa baada ya bei za mafuta kupanda katika soko la dunia.
Upandaji wa mafuta unaenda sambamba na upandaji wa kila kitu [bidhaa],lakini kwa upande wa Tanzania kama rasilimali zetu zingetumika kikamilifu hali isingekuwa kama ilivyo sasa.Tanzania ina mbuga za wanyama,ardhi nzuri, maziwa, bahari na madini [dhahabu,Tanzanite,Almasi na nk].Nianze kueleza jinsi rasilimali zetu zisivyotumika kwa manufaa ya taifa.
[1] Mbuga za wanyama,Taifa limekuwa likipoteza mapoto makubwa kupitia sekta ya utali kwasababu TANAPA imeshindwa kukusanya mapato yote yanayostahili.Matumizi mabaya ya fedha kidogo inayokusanywa na TANAPA badala ya kuchangia pato la taifa inatumika au inaishia kuhudumia mafisadi.Mambo ni hivyo hivyo kwa Ngorongoro conservetion.Mahoteli yote yanayojengwa kwenye mbuga za wanyama yanamilikiwa na wageni ambao hawalipi kodi inayostahili.Kila baada ya miaka mitano wanabadilisha majina ili kukwepa kulipa corporate tax na kuendelea kupata tax holiday ya bidhaa watakazo nunua.
[2] Ardhi nzuri,Uwekezaji katika sekta ya kilimo mpaka leo ni mdogo sana,Tanzania ina nafasi kubwa sana kupiga hatua kama ingewekeza kwenye kilimo ambacho kimewaajiri asilimia kubwa ya watanzania.Serekali imekuwa hodari kuhubiri kilimo ni utii wa mgongo lakini hakipewi umuhimu hata kidogo.Ununuzi wa radar, ndege ya rais vinapewa umuhimu mkubwa lakini inapofika sekta ya kilimo tunaambiwa hakuna fedha!,kama hizi fedha za EPA, Import support,Richmond na semina elekezi Ngurdoto na nk zingepelekwa kuhudumia sekta ya kilimo tungekuwa wapi?.Wakenya leo hii wanapiga magoti wanaomba tuwauzie mahindi kama tungewekeza ipasavyo Tanzania ingeweza kuzilisha nchi zote za Afrika mashariki.
[3]Madini,dhahabu Tanzanite na nk mikataba yote tuliyoingia imejaa rushwa.
Dhahabu yetu ingeweza kutumika kupunguza makali ya bei kubwa ya mafuta.Wawekezaji hawalipi kodi,wananyanyasa wafanyakazi wa kitanzania.Kila baada ya miaka mitano wanabadilisha majina ya kampuni zao ili wasilipe kodi,mfano hapa Arusha tuna kampuni moja inayochimba Tanzanite imekuwa ikibadilisha majina kila baada ya miaka mitano,waliaza kujiita SAMAAX baada ya miaka mitano kumalizika wakajiita Tanzania one, halafu sasa wanajiita Half Gem.Ukienda kwenye machimbo ya dhahabu hadithi ni hiyo hiyo.
[4]Bahari mambo ya huko yanatisha,kwanza kuna mkataba wa TICS ambao WATZ tunaujua sina haja ya kuuelezea.Madhara yake ni makubwa sana kwa uchumi wetu,wafanyabiashara wengi siku hizi wanapitisha mizigo yao bandari ya Mombasa kwasababu ya urasimu ulioko bandari ya Dar es salaam.TICS wameongezewa mkataba na serekali ya mzee Mkapa pamoja na kuboronga kwa kiasi kikubwa.
Watanzania kama mambo yote hayo niliyojaribu kuyaeleza kwa ufupi yangefanyiwa kazi na serekali ya JK wala asingetuambia tuvumilie shida,hatukumchagua ili tuvumilie shida ambazo angeweza kuziondoa kama sio kuzipunguza.
na G KABONDE, ARUSHA,TANZANIA, - 21.07.08 @ 08:21 | #23274
'Kama Mwenyeketi wa Umoja wa Africa tunashughulikía tatizo hilo' Watanzania wanakujua kama Rais wao na si vinginevyo. Kama umeshindwa nyumbani utaweza kweli ngazi ya kimataifa. Ningekuelewa kama ungesema 'Kama member wa G8 tunashughulikia tatizo hilo' Ila umoja wa wala mihogo wapi na wapi
na TICO, Mwanza, - 21.07.08 @ 09:29 | #23294
Inaumiza sana. Sasa watanzania tujiandae kwa hali yeyote itakayotokea maana karibu robo ya waliotoa maoni mpaka sasa wanaonyesha kukata tamaa na Rais wetu Jakaya Kikwete aliyebaki yeye na makamu wake kama injini zinazojikongoja kutufikisha salama mwaka 2010.
Alituahidi watanzania mambo tuliyoamini anauwezo wa kuyashughulikia na bila hiyana tukampokea zaidi ya alivyotarajia.
Rais wetu hakuwa amejipanga kuiongoza nchi. Hii naithibitisha kwa kauli yake aliyoitoa mwishoni mwa mwaka 2004 wakati anahojiwa na kituo cha TVT wakati huo kama mgeni rasmi wa kipindi, yeye akiwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa.
Kwa shauku ya watanzania waliokuwa na hamu ya kujua nini mustakabali wake kisiasa hasa kugombea uongozi wa juu wa nchi, yeye alijibu tena kirahisi wakati wa kulizungumzia hilo bado haujafika. Tunaamini alikuwa analinda heshima ya chama, ila nahisi katika mtandao wao waliouratubu kwa muda mrefu huenda hakukua na mtu waliyekuwa wamempata kwa ajili ya kuliwakilisha kundi lao hivyo kumuwia vigumu kuweka wazi hata kama alikuwa na dhamira ya kugombea.
Pindi walipofikia muafaka wa kuwa anafaa kuliwakilisha kundi lao tayari muda ulishapita wa kujaribu kuyatambua matatizo ya watanzania kwa undani zaidi alilazimika kuyajua kupitia kwa wanamtandao wenzake.
Hii ndiyo iliyosukuma kuwa mgombea aliyetembea sehemu nyingi wakati wa kampeni kwa sababu kila alikopita alikuwa haamini anachokiona kama watanzania ni maskini wa kutupwa namna ile hali iliyomshawishi kutamani kufikia kila sehemu.
Alilazimika kuahidi na ambayo hayakuwemo katika ilani ya chama chake kwa kulingana na sehemu aliyopita. Hakufanya hivyo kwa kuwahadaa watanzania ila ni msukumo wa kweli aliokuwa nao na hapo alijisemea nimefanya sahihi kugombea kumbe watnzania wanahitaji ukombozi wa haraka.
Haikushangaza pale alipoituliza inchi na dunia kwa hotuba yake nzuri aliyoitoa bungeni siku ya kwanza iliyogusa kila sehemu kwa uwazi na uchungu. Yalikuwa ni maono yake baada ya kuyashuhudia maisha ya mtanzania kwa wakati mfupi wa kampeni aliofanya.
Ndio maana ukiangalia kwa makini hata mabilioni aliyoyatoa yalikuwa hayana tathmini aliyo ya wazi zaidi ya kukurupuka. yote hiyo ilikuwa ni haraka yake ya kuona wale aliowashuhudia wakati wa kampeni baadhi yao wajaribu kuondokana na hali waliyokuwa nayo kwa kuwezeshwa mitaji. Kwa bahati mbaya jambo lolote kubwa linapofanywa kwa kubahatisha matokeo yake yanaweza kuleta balaa kubwa kijamii. Tumeshuhudia karibuni akilalama ameibiwa pesa japokuwa hakuwataja wajanja wanaoongozwa na vinara wa mtandao.
Kutokana na hotuba yake, aliwakuna wazungu na walimdaka juu juu ili apeleke mipango ya jinsi anavyotaka kuwakomboa watanzania. Ndio maana hatukumuona akitulia inchini muda mchache baada ya kuikamata Ikulu ya Tanzania. Hakuwa na wakati wa kufuatilia kwa karibu yale aliyoyaeleza katika hotuba au aliyoyaagiza yafanywe chini ya wizara.
Mtu pekee aliyemuamini alishindwa ( Waziri mkuu aliyepita ) kufuata maelekezo yake labda kwa kuwa na nguvu katika mtandao pasipo kuangalia anayekwenda kinyume naye sasa ni Rais. Taratibu Rais wetu akaanza kutupa hofu ya utekelezaji wa aliyoyaahidi. Kwa kutumia karata ya upendo wa watanzania kwake bado aliendelea kuwa imara ndani ya mioyo ya watanzania.
Kilichotokea ni kupishana kwa utekelezaji wa masuala nyeti kati yake namtandao. Yeye alishabadilika na kujitolea kwa ajili ya wanzania, wakati mtandao bado unamalengo yake ambayo ni lazima yatimizwe kabla ya kuwahudumia wantanzania.
Wamekamatwa wakisaini KIMBUNGA CHA KWANZA KATIKA SERIKALI YAKE (BUZWAGI) nje ya maelekezo yake aliyoyatoa bungeni. kushindwa kwake kulichukulia hatua suala lile kwa kuwa lipo ndani ya mabosi wake wa mtandao ndio iliyokuwa chachu ya hata wauguzi kurejea tena kwa kasi yenye nguvu mpya kujitafutia maisha bora kwa njia za rushwa zilizokuwa zimepungua kabla.
Alikuwa nje kutafuta misaada mtandao ukabaki ndani unaitafuna inchi. Misaada aliyokuwa anaifukuzia sasa imesitishwa kwa kutokuwa na ujasili wa kuyashughulikia aliyoyasema na yametokea mengi yakiuhusisha mtandao.
Leo anarudi kwa watanzania akiwa hana aliloagiza wala aliloomba kusaidiwa la maana alilofanikiwa. Ni mpweke asiyejitambua baada ya kulihujumu kundi la mtandao waliowekeana mipaka kabla ya kumsimamisha kuwa muwakilishi wao.
Watanzania tuna kazi ya kupata mtu anayesema na hapo hapo anatekeleza kwa vitendo pasipokuangalia mke au mwanagu ataumia kwa sababu umeshaomba kuvikwa uwezo wa kuwamiliki watu wote na ukapewa.
Angeandaa utaratibu mzuri wa kuwasaidia wakulima kama alivyoongea leo tusingekuwa katika shinikizo la kupatwa na njaa. Watanzania walikuwa tayari kumsaidia Rais wao kipindi anaingia Ikulu hata kwa kujitolea kufanya kazi za harambee kuokoa nchi tofauti na aombavyo sasa. Aige marais wa Uganda na Rwanda wanaojitolea kwa hali na mali kwa ajili ya wananchi wao.
Tujipe moyo zaidi kwa watanzania kama hatutafanya kazi ya ziada, harubu azipatazo mtu wa kipato cha chini wakati njia za marekebisho ni nyingi zitageuka kuwa chachu ya machafuko ichini.
Rais wetu wafanyakazi wa viwandani wananyanyasika kwa malipo na hiana wanazofanyiwa na wahindi mliowatulia nchi.
Rais wetu waangalieni wachina wanaouangamiza uchumi wa mtanzania kwa vitu visivyo bora.
Rais wetu kama hausomi shule za Binafsi jua utaelewa zaidi somo kwa kuhudhulia masomo ya ziada.
Rais wetu ukiwa huna mtu hospitali wa kukushika mkono hata hiyo hela uliyoandaa kumpatia dr kama rushwa ili mgonjwa wako ashughulikiwe hutaipata.
Chuki imeanza wasiotupenda watatuchonganisha tumalizane. Tulia ili ujue wananchi wako wanautajiri wa kiwango gani na mpange jinsi ya kuutumia.
na Elian Gz, Tanzania, - 21.07.08 @ 10:46 | #23321
Naanza na MARINA WA vocha#23226 hivi unajua kuwa TZ kuna gas ya songosongo lakini Tanesco wananunua kwa bei mbaya mpaka wame admitt ni bora wangechimba wenye ingekuwa rahisi
Tatizo JK anawalinda sana mafisadi wake kwani most of them ni marafiki zake,watu wake wa karibu BEI ya mafuta kweli imepanda lakini kuna alternative nyingine za kuchangia ili kupunguza gharama za maisha kwa sisi masikini wa tanzania
Tuna rasili mali nyingi tulizo barikiwa na mungu lakini hazitunufaishi sisi watanzania ambazo zingeweza kutusaidia kupunguza ukali wa maisha
Zaidi ya mali zetu zetu kuwanufaisha watu wachache kwa manufaa yao nawazungu na hicho kidogo tukipatacho mafisadi wakichukua chote je kwa nn tusiumie sisi watanzania wenye kipato cha chini
JK Tusitafute mchawi bali wachawi ni sisi wenyewe na kwa mwelekeo huu maisha yatazidi kuwa magumu zaidi na zaidi wakati sisi ni matajiri wa mali za asili lakini wananufaika nazo wachache
JK Tutangazie tu kama TUFUNGE MIKANDA TUMESHAZOEA
na yakhe, pemba, - 21.07.08 @ 11:00 | #23327
hatukatai ukweli. JKN alsiema tufunge mikanda kwa miezi 18, ikawa miaka 18. Ikaendelea, AHM kukawa na nafuu ya nguvu ya soda, baadae BWM tukapata ukapa bab kubwa na kwa mbwebwe boys2men wakasema ndege inapaa kwenye MAISHA bora kwa kasi nguvu na ari mpya. Na mwenye kipaza sauti "6" kwa standard na speed, tutakuwa hatuna shida. Sasa kwa nini tunarudi kule kwa JKN kwenye yanga kwa kadi, mgao wa mafuta, foleni za sukari wakati kuna mavuno ya almasi, dhahabu, tanzanite, sangara, tumbaku, kahawa, korosho???
na plplp, lplplp, - 21.07.08 @ 11:02 | #23330
NYIE watoto wa mafisadi mlio ughaibuni acheni kushabikia msiyoyajua.kama mnafikiri sisi ni mambumbumbu basi sawa.Saa yenu itafika tutapowasimamisha vizimbani wazee wenu na kuwafilisi ndiyo na nyie mjue tunachopigia kelele kina maana gani
na DAFFA, MUHEZA /TANZANIA, - 21.07.08 @ 11:04 | #23332
IK anashangaza sana masuala anayoyaweza anayafumbia macho anarukia mambo ya mafuta,simelewi.jk shughulikia orodha ya mafisadi,orodha ya wauza madawa ya kulevya.orodha ya orodha ya watendaji wako wabovu baada ya hapo ongelea kupanda kwa bei mafuta na sio utuambie tuvumilie shida bali tuambie tuongeze bidii,ww umeanza kuongeza bidii kweny huo uvumilivu au unakaa tz wiki moja na majuu siku mbili?TUSIDANGANYANE
na jimmy, tz, - 21.07.08 @ 11:09 | #23333
navutiwa zaidi na mjadala unavyoendelea. ingawa bahati maya baadhi yetu tuaacha kuchangia mada husika.
navutiwa zaidi na watanznaia walioko tanzania, wengi wao wanauelewa mkubwa kuliko walioko nje ya nchi.
mchangiaji mmoja anayedai kuwa marekani anajitahidi kufafamua ongezeko la bei ya mafuta katika kipindi cha mwaka mmoja limesababisa maisha kuwa magumu!
nimevutiwa na maelezo ya mtanzania, aliyeko tanzania aliyejaribu kumfafanulizi kwamba bei ya mafuta kwa Mexico na Venezuela iko chini zaidi ya marekani kutokana na sera mbovu za utawala wa bush
labda niongeze kidogo kuwa, licha ya ongezeko la bei ya mafuta, ukiwa marekani unapaswa kutambua athari vita vita vinavyoendelea Iraq, Afghanistan n.k katika uchumi wa marekani
mwaka jana aliyekuwa akiitwa Iron Lady wa Tanznaia alidai kuongeza kodi ya mafuta kwa kisingizio la kujenga barabara!, lakini hakuna hata kilomita moja ( nje ya zilizoachwa na magufuli zilizojengwa), unaweza kuangalia kwmaba sera mbovu za serikali zinasababisha kupanda kwa gharama za maisha bila kusingizia ongezeko la bei ya mafuta duniani
kingine kinachofurahisha ni kuwa ukiwa marekani unafanya kazi kuanzia saa 12 jioni hadi saa nne usiku!.
watanzaia wa aina yenu wanafurahisha, mkiwa kwenu hamwezi kufanya kazi kwa kujituma kwa kiwango hicho na pia mkiwa huku mnabagua kazi kama nini.
suala la msingi hapa ni kuwa sera mbovu za serikali ni sababu kubwa za kuathirika kwa maisha ya wananchi
wachangiaji wengine wameongelea kuhusu madini kwa ufasaha mkubwa na kwaba serikali hii ya kisanii imekuwa ikiwachanganywa wananchi kwa kuunda tume na tume bila kuchukua hatua.
na tunafahamu kuwa hawawezi kuchukua hatua kwani Jakaya Kikwete huyu anahusika na mchakato wa kuundwa kwa sheria ya madini na kutoa raslimali za watanznaia kwa wageni kwa bei za kutupwa, Bulyanhulu, IPTL
ukiacha hayo hivi sasa tunasikia habari za kuwepo kwa mafuta karibu kila pembe hadi kiwira, subir utaona madudu badala ya kuyatumia kutusaida sisi tunaongeza juhudi kutoa ardhi yetu ili kuzalisha nafasi za kutengeneza mafuta!
badala ya kuzalisha chakula ambacho kwa hakika sasa kina soko kubwa duniani na kuboresha kaisha ya wananchi, serikali inaagiza mashangangingi kila kukicha huku wilaya nzima hakuna trekta hata moja, Rais akifika katika wilaya hiyo akiwa na msururu wa mashangingi pengine zaidi ya 40, anawaambia mvute subira, mafuta yamepanda na kuharibu uchumi.Hii ni akili kweli!
kikwete hawezi kuboresha uchumi na hali za watanzania kwani angekuwa na nia hiyo angepunguza safari za nje ya nchi ni gharam sana
watanznaia wenzangu mliko nje kama huko USA tusaidieni kufahamu gharama za misafara ya wakubwa hawa nje ya nchi, zinaakisi kweli uchumi wa watu wanaoambiwa kuwa mafuta yamepanda, waendelea kuwa wavumilivu?
na mashilatu, ngara, - 21.07.08 @ 11:32 | #23341
haya mambo hayo !!!! tuendelee kuvumilia duu!!!! kasahau kusema tukaze mikanda? hakuna asiyejua kwamba uchumi wa nchi umeharibiwa na uongozi mbovu, tamaa na ulafi wa viongozi wa CCM. vIONGOZI HAWAJIPIMI KWA KUANGALIA WAMEWAFANYIA WATANZANIA KITU GANI BALI HUJIPIMA WENYEWE KWAMBA WAMEFAULU KUJIJENGEA MAJUMBA MANGAPI, WANAHISA KIASI GANI KWENYE MAKAMPUNI MAKUBWA, WATOTO WAO KAMA WAMEFANIKIWA KUPATA ELIMU YA JUU HUKO NG'AMBO, STAREHE ZAO BINAFSI NJE YA NCHI NAKADHALIKA.HIVYO NDIVYO VIPIMO VYA MAFANIKIO KWA VIONGOZI WETU. IKO SIKU WATATUJIBU NA SASA KAZI IMEAZA. Tumechoka kuvumilia na kuambiwa tuvumilie. Bei ya mafuta siyo sababu pekee kwa ugumu wa maisha kwa watanzania. Serikali imeweka kima chachini cha mshahara kidogo sana na kuwapa advantage hata wawekezaji wenye uwezo kulipa hivyo hivyo wakiamini MTZ Anaweza kuishi kwa kiwango hicho kisichotosha hata nauli ya mwezi kwenda kazi.
na ba - 21.07.08 @ 12:27 | #23350
JK usifikiri ni sifa kila mtu kukutaja mahala alipo kuwa we ni bomu kwa utawala bora. Angalia umeanza kutugawa wadanganyika kwa kuwatumia mafisadi na pia wana mtandao wako. Umeendeleza kutugawa wadanganyika kwa kuendeleza mfumo mbovu wa fisadi Mkapa aliyetugawa watumishi wa umma ktk viwango vya mishahara, tofauti kati ya mtumishi wa chini na wa juu imekuwa kubwa mno. Haiyumkiniki huelewi matatizo ya wanyonge kwa kuwa unakula na kulala bure. Hivi mshahara anaopewa Rais ni kwa minajili gani ilhali mtu anatunzwa na kulelewa? Au huu ndiyo chanzo cha ugonjwa wa mfumuko wa bei??
na Bodaboda, TBR-TZ, - 21.07.08 @ 12:42 | #23353
Du, jamaa kashindwa kuongoza sasa anasubiri miujiza! Ni bora aanze kutangaza kuwa kwenye uchaguzi ujao hatagombea kwakuwa hana uwezo wa kuwasaidia watanzania.Yani hali ni tete na wale waliokulwa wanakula mlo mmoja kwa siku sasa wanakula mlo nusu kwa siku. yani afadhali ya Zimbabwe kuna sababu ya hali ngumu! Yapaswa atueleze vizuri, kwanini Tanzania tuna hali hii? Aache ziara zinazozidi kuwatia machungu watanzania. Atulie ofisini aangalie ni namna gani ya kupunguza dhahama hii kwa wabongo. Ni bora basi tungegawana haya machungu kuliko kuumia watu wengi na wachache ambao wametajirika kwa dhuluma wakiendelea kufaidi matunda ya nchi hii. Yana mwisho haya!!!!
na Major, Tanzania, - 21.07.08 @ 13:12 | #23362
Maisha magumu hayajaletwa na kupanda bei ya mafuta, yanameletwa na UZEMBE wa viongozi.
Hospitali zilikuwa hazina dawa KABLA ya kupanda bei za mafuta.
Shule zilikwa hazina walimu, vitabu, majengo etc kabla ya kupanda bei ya mafuta.
Ninanaweza kuendela hapa mpaka kesho asubuhi.
Point hela zilizo ibiwa na zinazo endelea kuibiwa na viongozi - zingetumika kisahihi, shida ya mtanzania ingekuwa tofauti.
Huyo Raisi angelikuwa anashughulikia wafisadi kisahihi, speech yake ingepokelewa kitofauti.
BADO HAJAFANYA KITU!!!!
na Fimbo Kali - 21.07.08 @ 13:39 | #23365
Yaani haya ndiyo maisha bora kwa kila mtanzania yanawezekana? Kuvumilia shida badala ya kula manna na asali ni ****** ya nguoni. Kama umeshindwa si uishie ndugu yangu. Tunataka maziwa na asali. Uliahidi kutupeleka Kanani siyo kwenye nchi ya kufunga mikanda bwana rais.
na Mpayukaji Msemahovyo, Siri, - 21.07.08 @ 14:08 | #23372
Mheshimiwa Rais,pamoja na kuvumilia,tilia mkazo uchmbaji mdogo mdogo wa madini,kama STAMICO itapewa nguvu ijiendeshe kama Tanesco,kisha ilete vifaa vya uchimbaji mdogomdogo wa madini,mathalani= Compressors,wet ball mill capacities 1t,2t/hr] Jaw crushers,winchi na mitarimbo na bits zake,kisha kila kanda kuwe na workshop iliyosheheni vyombo hivyo,hata kama kwa kuazia wachimbaji wtashindwa kumudu kununua,lakini kuna makota[local brokers]wanaweza kununua baadhi ya viaa kama compressor na kuwakodisha wachimbaji.Niko hapa Nyarugusu,fani yangu ni uhandisi wa migodi, najitahidi kushauri wachimbaji namna bora ya kuchimba lakini maneno matupu yanawakera maana wangependa waone vifaa,tena wengine wangeweza kupata mikopo kwenye bank iliyopo hapa hapa Nyarugusu,lakini vyombo hivyo havipo!!.Kwa hiyo STAMICO ikilielewa hili,tutaweza kuwawezesha wachimbaji wachimbe kitaalamu na vilevile ni njia bora ya kudhibiti dhahabu isiuzwe kupitia njia za panya.
Sekta hii inaweza kutoa ajira lukuki,kwa mfano:mchimbaji mwenye hati ya kuchimba,akipata vifaa ambavyo havizidi US$150,000,ANWEZA KUAJIRI WAFANYAKAZI SITINI [60],FIKIRIA KUNA HATI MILIKI ZA UCHIMBAJI ZILIZO HAI NGAPI NCHI NZIMA[KWA MADINI YA DHAHABU ZINZKADIRIW KUFIKIA 6000],INA MAANA KATIKA MIGODI YA DHAHABU PEKE YAKE KUNGEPATIKANA AJIRA 360,000[DIRECT EMPLOYMENTS]SASA JE ZILE ZITAKAZOJITOKEZA [INDIRECT],NA JE DHAHABU KIASI GANI KIGEPATIKANA?HUU UMASIKINI TUNAULEA TU KWA KUTOKUTHUBUTU,LAZIMA TUONDOKANE NA ILE DHANA YA KIZAMANI,TUFANYE YALE TULIYO NAYO,MATOKEO YAKE BEI ZA BDHAA ZA
WENGINE ZITAPAMBANISHWA NA DHAHABU YETU.Kwa mchimbaji wa kawaida aliye na mgodi unaozalisha kwa wastani ni wakia[ounce[oz]6.4/siku,lakini kuna wanaozalisha mara dufu.ina maana kwa mwezi anaweza kuzalisha wakia 160 kwa mwezi.hii ni sawa na US$ 122,880,KWA ASILIMIA 80 YA UBORA.
kAMA HUU NI WASTANI WA VIWANJA VYOTE 6000,INA MAANA KWA MWEZI DHAHABU ITAKAYOZALISHWA KWA MWEZI NI 160 X 25
4000 oz. au US$ 491,520,000.KWA MWEZI,AU
US$ 5,898,240,000 KWA MWAKA.Ikumbukwe tumechukulia wastani wa chini tu.Ukibadilisha katika shiling za kitanzania ni sawa na Sh.trilioni 6.8.Je bajeti yetu ikoje?au chukulia imepatikana asilimia 40 tu,sawa na trilioni2.72,si haba.NASISITIZA STAMICO NA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO NA VYOMBO VYA KUCHIMBIA MADHUBUTI INAWEZEKANA.
na Andrew Gadi Mrinji, Geita/Tanzania, - 21.07.08 @ 14:19 | #23378
kila siku JK ANATELEZA ULAYA HALAFU SIE TUVUMILIE TAABU NA SHIDA NA MSHAHATRA KIMA CHA CHINI KILA MWAKA WA FEDHA WANAONGEZA BUKU MBILI MBILI.
UNAWAPELEKEA UZURI WAZUNGU WE SUBIRI MATOKEO...
na wily, mby, - 21.07.08 @ 14:22 | #23379
Wazungu ndo wanaotufilisi hii nchi. Mna habari kuwa Alhamisi wiki iliyopita balozi wa Canada alienda na ujumbe Dodoma kuonana na baadhi y wabuge eti ku-loby mswada mpya na mapendekezo ya kamati ya madini usikubaliwe. Barrick ni kampuni toka Kanada wanachukua matrilioni yetu halafu wanatulete msaada wa mamilioni. Kweli wajinga ndo waliwao. Siju na hawa wabunge wanaokubali kujadili suala kama hili wanaitakia mema kweli nchi hii?
na Robert, DSM, - 21.07.08 @ 14:50 | #23385
Mheshimiwa rais nasikitika kauli yako uliyo itoa kwa wanyonge watavumilia mpaka lini?kwenye ilani ya chama chako ulisema utatoa maisha bara kwa kila mtanzania yako wapi?mfumko wa bei haujaanza leo ulianza pale tangu uliposhika madaraka. Mwaka 2006 nauli zilipanda,2007 naulizikapanda tena na 2008 nauli zimepanda pia,mbona waliokutangulia waliweza kudhibiti mfumko wa bei?.Tatizo lako mheshimiwa umekalia kuchekacheka na kuweka watu madarakani kiurafiki kwa kuangalia masilahi yako naya rafiki zako tu,kwakuwa walikusaidia kuingia ikulu kwa fedha zao hivyo hata wakianza kupandisha vitu bei huwezi kuwakemea maana wanarudisha fedha zao walizokusaidia wakati wa kampaini.Angalia richmond ilivyokula pesa za wanyonge ulipopata taarifa hukuchukua hatua zozote eti unaunda tume nayo tumeimekupa ripoti unasema eti katibu mkuu wa serikali ataangalia hatua za kuchukua sasa wewe unakazigani hapo?ni msaada gani unautoa kwa wanyonge kama rais?. Ulichaguliwa kwa kishindo lakini hakuna lolote unalofanya kazi kukumbatia mafisadi ila mungu ataipigania nchi ya tanzania.
na Joe Das, china, - 21.07.08 @ 16:00 | #23406
Hi! shida haivumiliki wakati mwenzako unamuona anamega pale patamu.Ingekuwa wote tunapata shida hapo shida ingevumilika. Je kwanini wengine wavumilie shida wakati wengine wanaishi kama peponi tena kwa wizi wa hela za walalafofo?
na MR.JOO, PWANI-KIBAHA, - 21.07.08 @ 16:38 | #23414
Kama ni ushauri basi Rais ana matatizo makubwa!! Hawa washauri wameonyesha kuwa na uwezo mdogo wa kumshauri mkuu wa nchi. Kama ni yeye mwenyewe, basi taifa lina tatizo kubwa!!
Katika hali tuliyo nayo sasa watanzania ni mtu gani mwenye akili timamu anaweza kusimama na kuwataka watu waendelee kuwa na uvumilivu? Uvumilivu maana yake ni nini? Kwa nini Rais asitamke tu kwamba wanaotaka kufa na wafe kwani serikali haijali wala haitishiki.
Waendelee kuvumilia nini? Kuvumilia kuna maana kwamba wasubiri hatua zinazochukuliwa zifanikiwe. Sasa ni hatua gani zinazochukuliwa na serikali? Kuwakingia kifua mafisadi kutatusaidia nini sii akina "kafie mbali"?
Kana kwamba hiyo haitoshi, Rais anabainisha kupanda kwa bei ya mafuta duniani kama sababu ya matatizo yetu!! Tafadhali Mheshimiwa Rais, mswalie mtume jamani!! Bei ya mafuta imepanda lini na maisha ya Watanzania yameanza kuwa magumu lini? Mwogope Mungu jamani!! Kumbuka baadhi ya viongozi wa dini wanafiki walikuita chaguo la Mungu; angalia usimkasirishe huyo Mungu maana adhabu zake ni kali kupita kiasi mnachofikiri mafisadi.
Mbona Mheshimiwa hutaji sababu yenyewe ya hali hii: ufisadi uliokithiri wa viongozi wa nchi hii? Kweli ni halali katika nchi ambayo Kiongozi Mkuu ni mmojawapo wa "the best JK eleven", kuendelea kulaumu kupanda kwa bei ya mafuta? Hata hiyo bei ingeshuka leo tutapata faida gani?
Ni jana tu TANESCO imetwambia kwamba kusitishwa kwa mkataba wa Dowans hakusaidii chochote kwani malipo yale hayakuwa na athari kwenye mapato ya shirika!! Sasa kama milioni 154 kwa siku ni vijisenti, mnataka mafuta yashuke kwa kiasi gani ili tufaidike nayo?
Acheni kutudanganya, wakati huo umepita.
na Amk, Dar, - 21.07.08 @ 17:29 | #23425
Sasa Kikwete amepata sababu ya kuwadanganya wananchi matarajio ya 'maisha bora kwa kila mtanzania' yanapoota mbawa!
na chavala, UK, - 21.07.08 @ 19:40 | #23455
Je Raisi wetu Kikwete ulidhani utarithi nchi isiyo na matatizo? Kazi ya raisi si kuzunguka nchi kukagua matatizo bali ku-solve matatizo!Ilipoingia madarakani ulilia tatizo la njaa! Ohh jamani kunaukame na tatizo la chakula hivyo msitegemea uchumi utakua kwa kasi ilele! Tukakubali! Mara ukaanza kulia Oooh ukame jamani hatuwezi kufua umeme wa kutosha kasi ya ukuaji wa uchumi itapungua, wahisana wakakukopesha fedha kwa ajili ya kufua umeme wa dharura zikaishia katika ufisadi Richmond na safari zako zisizo na mwisho! Kukaja ugonnjwa unaoathiri mifugo ukalia jamani uchumi hauwezi kukua ipasavyo tatizo la mifugo, watanzania tukala samaki Mungu akatunusuru na wala si juhudi za serikali ugonjwa ukatokomea! Haya sasa umesikia Bei ya mafuta unalia kama kawaida yako! Je Kikwete unadhani uraisi ni kulia shida au kubuni njia za kutatua matatizo. kila nchi ina matatizo: Msumbiji jirani zetu, uchumi wake unakua kwa karibu asilimia 10 licha ya miaka mingi ya vita je wao hawako kwenye dunia hihi yenye shida ya mafuta. mikakati gani sirikali yako inafanya kutumia Gesi asilia tuliyonayo kwa wingi kama nishati? Tatizo lako ni kulia tu! Mawaziri wako wakiuliywa Bungeni kuhusu mikakati ya kujikwamua utegemezi wa nishati! Majibu kila siku wizara yangu inafanya sijui inafanya upembuzi yakinifu juu ya utumia Gesia asili... mapaka lini? Tumechoka nanyi hamna ubunifu ila kulia Tu. Raisi anakwenda Hospital Muhimbili wagonjwa wanalala sakafuni yeye, waziri wake anaficha dola million moja nje! Yeye aogopa kutumia nguvu zake kmweka kiyuizini kurudisha fedha zetu! Kila mhali kucheka tu na kuahidi kutafuta wahisani Mapaka lini?
na Zamani wa Kale, Moshi, - 21.07.08 @ 21:24 | #23480
Sikilizeni ndungu zangu, mnamraum Rais bila kufikilia. Ndio nakubali wakati ni mgum! Hali hii iko dunian kote, hata huku Africa kusini mambo ni yale yale vitu vimepanda beyi sana kwa mfururizo. na Rais wetu hawezi kutatua jambo hili kwa siku moja. Hata kama tuta badirisha chama mambo yatakua yeleyale. Na Nchi yetu bado maskini. Ndoo kwanza tunaanza kupiga hatua kiuchumi kuliko huko mwanzo. Tanzania ilikua haijulikani Duniani kama inavyo julikana sasa kiuchumi na kijiografia. Watanzania tulizoea vyakunyonga bila kuangalia ushindani wa kimataifa. Leo hii tuko kwenye mfumo mpya wa kimataifa. Tafadhali tuwe na subira huku tukifanya kazi kwa bidii. Kukosoana ni jambo zuri, lakini sio vizuri kukata tamaa, tutafika tuu. Rais wetu ana mdamchache tangu kupata Urais. Kunamapengo kibao yakuyaziba ambayo viongozi wengine waliacha huko nyuma. Kumbuka Tanzania ilikuawa haina pesa kabisa serekalini banki kuu ilikua tupu na madeni kibao kutoka duniani. Licha yakwamba Nchi kibao zilitusamehe na (IMF) pia. Lakini hali yakiuchumi ilikua inatisha. Sasa hivi uchumi wa Nchi unapand kidogokidogo. Rais JK ana uchungu wa Nchi, kuliko wengine huko nyuma yake. Tuache uswazi hii ni dunia mpya. Ufisadi ni jambo gum kulishugulikia kila Nchi. It will take time not by one night, to bring all perpetrators into justice. Bila JK tusinge jua kua hera zilikua zinaibiwa, pia jambo hili hatulifikilii!!! Msidanganywe na wenye kiu na madaraka. Peace to our country TZ.
na Exodus, South Africa, - 22.07.08 @ 01:00 | #23487
We Exodus mjinga sana, ehe? Tanzania si maskini hata kidogo, bali tuna umaskini wa akili katika viongozi na wataalamu wetu. Ukitaka kujua maana ya haya ninayosema, tembelea dunia uone vinchi maskini vinavyoipatia Tanzania misaada! aibu saaaaana!
na Chengula, Musoma, - 22.07.08 @ 01:55 | #23504
Watanzania wenzangu, kawaida mti uzaao matunda mazuri ni ule wenye maandalizi mazuri tangu unapandwa. Kiwete amekabidhiwa nchi ktk wakati mgumu sana. na kazi anayoifanya kurekebisha uozo anastahili pongezi na kuungwa mkono. kilio cha mafuta na ghalama ya vitu kupanda si la tanzania tu. Sasa wewe Sungura usilete masuala ya siasa na issue muhimu kama hii. Kwani kunachama ani cha siasa kinazalisha mafuta ili tukipe nafasi ya uongozi wananchi tupone. Nilitegemea utaponda serikali na kushauri nini kifanyike ili kutatua tatizo na sio kuomba uongozi. si kwamba namtetea Kikwete na uongozi wake kuwa wako safi, la hasha, ila ponda kitu alafu sema nini kifanyike si kuomba kuongoza serikali. kwa wachambuzi tunagundua huo ni wivu wa madalaka. Fanya kitu tutakukumbuka 2010 badala ya kuponda
na kajungu mturi, Mugumu Tanzania, - 22.07.08 @ 05:39 | #23538
Tatizo kubwa walilonalo viongozi wengi duniani, ni kuelezea matatizo yaliyopo badala ya kuelezea namna ya kuyatatua.
Utakuta kiongozi anasema kwa mfano "Tuna matatizo ya njaa wakati huu, hivyo wananchi mfanye bidii katika kilimo msiwe wazembe, limeni kwa bidii ili kuepusha njaa."
Kiongozi kwa kusema hivyo anadhani kuwa kuna jambo litafanikiwa, na hivyo ndivyo viongozi wengi wanavyofanya. Hawaelezi nani afanye nini na wapi, na ni zana zipi zitatumika katika hicho wanachotaka kifanyike. Wanadhani kwa kusema hivyo tu basi wananchi watakazana kufanya kile walichoagizwa ili kujiepusha na madhara yanayowajia mbele yao. Wataanzia wapi? Kiongozi anatakiwa awe mbunifu na pia awe na uwezo wa kusimamia kile alichokibuni.
Waandishi wa habari na wengineo nao utawasikia "Kiongozi---- amewahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii katika kuepuka madhara yatakayowapata katika maeneo yao". Kwa kufanya hivyo wengi wanadhani kuwa kiongozi kafanya jambo na kutakuwa na matokeo mazuri. Ukweli ni kwamba hakuna litakalofanyika, kila mmoja katika eneo husika atabaki kusema, kiongozi wetu amesema tufanye kazi kwa bidii.Nani afanye, aanzie wapi, hakuna.
Uongozi unaotakiwa, ni kiongozi muhusika kupanga mikakati thabiti. Pamoja na matatizo yanayokuwa yamejitokeza ili kutatua, kiongozi awapange wahusika namna ya kufanya hilo jambo analotaka lifanyike. Apange kuwa wewe utafanya moja mbili tatu, na huyu atafanya nne tano na sita. Siku ya ___ nitakuja kuangalia kilichofanyika katika hili. Hapo kweli unakuwa umefanya uongozi, kwa sababu umeeleza tatizo lililopo na namna ya kulitatua, siyo ulalamishi tu usio na ubunifu namna ya kutatua.
Ukiwaeleza watu wafanye jambo bila kufanya mikakati yoyote yakufanikisha jambo hilo lifanyike, kwamba ni nani atafanya nini na nini na kwa wakati gani, hakuna kitakachofanyika.
Viongozi wakiwa na ubunifu, mikakati na malengo na kusimamia, muda si mrefu Taifa letu litabadilika.
na Bernard Mwenda, Zanzibar, - 22.07.08 @ 10:23 | #23590