JK: Sina mpango kuvunja Baraza

Makamap,
Tatizo ni kwamba wengine wameingia kwa nguvu za vibuyu!! kwahiyo hayao maandiko matakatifu is not applicable
soma hapa!
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8263

Kibuyu hata farao alikitumia enzi za Musa lakini kwa mkono mtakatifu kilishindwa.
Ukitumia KIKUBUYu ukafamikiwa jambo lako si kwamba kibuyu hicho kimekusaidia ila ndivyo ilivyokuwa iwe kumbe umejitia tu kwenye Gadhabu la BWana bure.
 
Nimesoma maneno ya Rais Kikwete, maoni yangu ya haraka kwake…..


Sijafurahishwa na maneno ya ijumaa ya leo katika siku ya kutimiza miaka miwili ya utawala wako, nilidhani ungetangaza hatua thabiti za kurejesha matumaini ya wananchi na serikali yako katika mstari kwenye ministerial issues- lakini major national questions are yet to be answered! Nadhani washauri wako wanakushauri vibaya; kama matokeo ya REDET ni sahihi kabisa kwamba umaarufu wako ni mara mbili ya Baraza lako basi hatua zozote za kujaribu kulisaficha baraza hilo kwa PR Gimmicks zitakushushia umaarufu zaidi na wewe mwenyewe. Mr President, you can’t swim with them, you will stink and sink with them.

Naona washauri wako wamekushauri ufanya smooth operation! Someni vizuri public opionion na alama za nyakati, hicho sicho umma unatarajia. Sababu za umma kutoridhishwa na Kikwete- Mosi, Ahadi ya Maisha Bora kutotimia(naoana washauri wako wamekushauri ianze PR Gimmick ya kwamba ni mapema sana, na kwamba Maisha Bora hayaji kama Manna toka Mbinguni). Pili; kutotimiza ahadi(naona washauri wako wamekushauri kwamba ifanyike PR Gimmick kwamba wewe ni Muungwana Mtu wa Vitendo hivyo utatekeleza ahadi zako zote); Sababu ya Tatu ni Kuchagua Viongozi dhaifu/wabovu( hapa ndipo mzizi wa mambo ulipo!). Suluhisho lake si hii njia unayopitia hivi sasa; toka Julai kulikuwa na muda wa kutosha sana wa kuwafanyia tathmini, sasa ilikuwa ni wakati wa hatua, kadiri unavyochelewa kuchukua hatua Matumaini ya wananchi yanazidi kupungua na Imani inaanza kujengeka kwamba wewe u mmoja wao).

Opinion polls zinaonyesha kwamba Matumaini ya wananchi juu yako yako inverse proportional na elimu ya wananchi; wale waliofika chuo kikuu ndio hawana imani zaidi na wewe kuliko wale ambao hawakwenda shule kabisa(ambao ndio walio wengi). Hii ina maana kwamba watu wengi wa kawaida wahajui uhusiano wako wewe na Baraza lako la Mawaziri pamoja na kuwekwa kwenye list of shame. Wanapeleka kila lawama kwa viongozi wengine na kukupa benefit of doubt. Sasa kadiri unavyochelewa, utaendelea kuwaamsha walio lala…

Sasa ingia ndani zaidi kwa nini wananchi hawana imani na serikali yako? Sababu ni tofauti kidogo na kwa nini hawana imani na wewe- serikali yako inaonyesha kushindwa kufuatilia utekelezaji, serikali yako inalaumiwa kwa kuwa na ufisadi na kushindwa kutumia vizuri rasilimali za nchi; serikali yako inalaumiwa kwa kushindwa kutoa huduma bora za msingi za kijamii.

Haya ni mambo ambayo yote yanahitaji vitendo na si defense through PR Gimmicks. Uamuzi wa kuunda Kamati ya Madini, Uamuzi wa Kuunda Kamati ya Richmond; Uchunguzi wa BOT; Uamuzi wa kupeleka Kesi ya Rada Mahakamani; Uamuzi wa kumtoa Severe na Wenzake; Uamuzi wa Balali Kujiuzulu; yote haya- yamepunguza mjadala mkali wa umma lakini hayajabadili public opinion- in fact yanatengeneza sustained opinion kwamba serikali inalindana na wewe Mheshimiwa Rais unashindwa kuchukua hatua! Maoni haya yakigeuka kuwa msimamo wa umma mtizamo hautabadilika hata siku utakapoamua kuchukua hatua! It will be too late. The only way is to break this spiral of effect!

Anzia na Baraza la Mawaziri- ukianza kwa Ari, Nguvu na Kasi mpya hapo Taasisi nyingine za umma zitafuata maana kila moja ina ‘ka-skeleton kake kwenye kabati’. PCCB imeathiriwa na ile ripoti kanyaboya ya Richmond-wananchi wamepunguza imani nao; mahakama imeathiriwa na mchakato Kesi ya Ditopile wananchi wakaanza kuihoji; Bunge limeathiriwa na kupitisha bajeti iliyongeza gharama za maisha na kumfukuza Zitto Kabwe-wananchi wamepoteza imani na uwingi wa wabunge wa CCM; orodha ya Taasisi inaendelea. Na katika kipindi cha miaka miwili ilijitokeza pia mijadala mingine ambayo pamoja na kuizima kinamna bado inafukuta: Mpasukuko wa kisiasa Zanzibar, Suala la Mahakama ya Kadhi, Suala la Katiba Mpya- orodha ni ndefu kwa kweli. Lakini ni jinsi gani kila mmoja atajirekebisha inatemea ni jinsi gani wewe utarekebebisha mhimili wa serikali(hususani baraza lako la mawaziri).

Tendo la kuunda Kamati ya Madini ama ya Richmond pekee hayajaweza kuwasafisha wakina Lowasa na Karamagi! Huu ni wakati wako wa kuchukua hatua kama Amiri Jeshi Mkuu- ni wakati wa kumwondoa Lowassa na Kuvunja Baraza la Mawaziri. The Karamagi’s are too many and they are tainted beyond painting. The more you be with them the more people confirm that you deserve to be in the “list of shame”; the more you will take a spade for a spade not a big spoon; the more people will take you in the “list of fame”! Nchi inahitaji dira na vitendo.


JJ

Niliandika ujumbe huu hapo juu baada ya kusoma mahojiano na Rais kwa ujumla wake. Jana usiku nimepata wasaa wa kutazama mazungumzo naye kwa kina Channel Ten na baadaye TVT. Mambo kadhaa nimeyaona ambayo ni vyema yakafanyiwa kazi.

1. Inaelekea Rais alifanya mahojiano na makundi mawili tofauti ya waandishi. Lakini kinachozua mjadala ni kuwa kwa makundi yote mawili muktadha wa uulizaji maswali na pengine hata staili ya maneno vilikuwa vinafanana fanana. Je, ni kwamba waandishi wetu wote wanafirikiria sawa sawa? Au masuala yanayohitaji majibu yako mahususi kiasi kwamba kila mtu akiweka kwenye chumba chake tofauti anauliza swali lile lile? Au ni kwamba waandishi walipewa maswali kabla ama maeneo ambayo Rais angependa kuulizwa? This is just food for thought.

2. Nadhani ni vyema Rais akapunguza vicheko katikati ya kujibu maswali ambayo watanzania wanategemea majibu mazito. Rais anapozungumzia kwamba tumewauzia wawekezaji wapya Shirika la Reli likiwa limekufa kabisa; ama Net Group ndio wakaharibu zaidi Tanesco, Ama Alliance na baadaye Patnership vikashindwa kuiamsha ATCL na kwamba tumetoka ndege 9 mpaka 1 kutokana na utawala mbovu huo nyuma- Rais anapozungumzia hali hizi huku akiangua kicheko; kwa kweli si nzuri. Inakatisha tamaa zaidi! Inawafanya wananchi waanze kujiuliza, hivi ni nani alipitisha yote haya huko nyuma? Kwa nini Rais wetu anacheka? Je, anafurahia? Najua pengine nia ya Rais ni kuonyesha kuwa mambo ni mazuri wananchi wasiwe na wasiwasi, everything is under control. Lakini si kwa staili hii ya kuangua vicheko. Inaharibu zaidi ya kujenga haiba ya Rais.

3. Majibu ya Rais yametoa ahadi tu kuhusu ATCL na TRC, hayajatoa dira kuonyesha mwelekeo. Walau kwenye TANESCO kidogo amegusia sheria ya kuleta ushindani kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme. Swali la kujiuliza, ni kwa nini Rais hataki kutazama nyuma na kuchukua hatua? Lazima tutatue tatizo la mazingira ya utiwaji saini wa mikataba ama sivyo mambo ya Netgroup, Richmond nk yatajirudia tena? Ni lazima baadhi wa wahusika wachukuliwe hatua ili iwe fundisho.

4. Kuhusu EPA, Rais amekwepa badala yake amesimulia historia tu- na si mwelekeo na msimamo wa Tanzania katika majadiliano hayo. Pamoja na kuwa ameahidi Mramba atazungumza kwa kina, lakini Rais kama mtu ambaye amekuwa kwenye kada ya diplomasia kwa muda mrefu alipaswa kudokeza terms zetu ni zipi. Na kwa jinsi Rais alivyoirudia rudia tarehe 31 kwamba ni tarehe ya makubaliano inaelekea maamuzi yameshafanyika! Hizo terms za agreement kwa nini haziwekwi open? Napata hisia kwamba tunaburutwa- kwa sababu Rais amerudia rudia sana "wakubwa wakisema" "Hatuna cha kufanya" "Take it or leave it"; na ukishakwenda kwenye majadiliano ukiwa na inferiority complex basi chochote kitakuwa hewala!

5. Nimependa jinsi Rais anavyotumia muda mrefu wa maswali kuzunguka kwenye kufafanua mafanikio ya serikali katika huduma za kijamii na miundo mbinu na mipango iliyopo katika eneo hilo. Mathalani ujenzi wa sekondari kata, ujenzi wa baadhi ya barabara. Mpango wa Afya nnchini utakaohusisha Zahanati, vituo vya Afya nk. Na orodha ya barabara zitakazojengwa hususani kupitia MCC/MCA. Lakini wakati wote nimeendelea kujiuliza- hivi mpaka lini nchi yetu inataendeshwa kwa mfumo wa miradi? Kwa kweli maelezo ya Rais yamedhihirisha hofu yangu kwamba hatuongozwi kwa dira thabiti, tunatekeleza miradi. Katika maelezo ya Rais sijaona dira thabiti ya nini mwelekeo wa msingi wa serikali na malengo kwa mwaka unaofuata na kipindi kilichobaki. Kinachoonekana ni vipande vipande vya shughuli. Na karibu miradi yote iliyokuwa inatajwa ni ile ambayo tumefadhaliwa na washirika wa kimaendeleo. MCA, Japan nk.

6. Mahojiano na Rais yamenidhihirishia kwamba pamoja na kwamba kwa kauli Rais amesisitiza hali ni nzuri na anaridhishwa na mwelekeo nao ni PR Gimmick tu yakuonyesha kwamba things are in control, lakini ukimtazama Rais machoni utajua kabisa kwamba haridhishwi na mambo fulani fulani. Hata ile hamasa ya kusema tutafanya hiki na kile au tumefanya hiki na kile kwa ari, nguvu na kasi mpya imepungua sana. Our president appears to be down! If that is the case, is still call upon him to dissolve the cabinet, and not recycling most of the same Ministers. Mr. President should not let himself be drowned with the likes of Lowassa, Karamagi and Kingunge's!

Mambo ni mengi kwa kweli, ningependa kuyasema lakini wakati ukuta..

JJ
 
Niliandika ujumbe huu hapo juu baada ya kusoma mahojiano na Rais kwa ujumla wake. Jana usiku nimepata wasaa wa kutazama mazungumzo naye kwa kina Channel Ten na baadaye TVT. Mambo kadhaa nimeyaona ambayo ni vyema yakafanyiwa kazi.

1. Inaelekea Rais alifanya mahojiano na makundi mawili tofauti ya waandishi. Lakini kinachozua mjadala ni kuwa kwa makundi yote mawili muktadha wa uulizaji maswali na pengine hata staili ya maneno vilikuwa vinafanana fanana. Je, ni kwamba waandishi wetu wote wanafirikiria sawa sawa? Au masuala yanayohitaji majibu yako mahususi kiasi kwamba kila mtu akiweka kwenye chumba chake tofauti anauliza swali lile lile? Au ni kwamba waandishi walipewa maswali kabla ama maeneo ambayo Rais angependa kuulizwa? This is just food for thought.

2. Nadhani ni vyema Rais akapunguza vicheko katikati ya kujibu maswali ambayo watanzania wanategemea majibu mazito. Rais anapozungumzia kwamba tumewauzia wawekezaji wapya Shirika la Reli likiwa limekufa kabisa; ama Net Group ndio wakaharibu zaidi Tanesco, Ama Alliance na baadaye Patnership vikashindwa kuiamsha ATCL na kwamba tumetoka ndege 9 mpaka 1 kutokana na utawala mbovu huo nyuma- Rais anapozungumzia hali hizi huku akiangua kicheko; kwa kweli si nzuri. Inakatisha tamaa zaidi! Inawafanya wananchi waanze kujiuliza, hivi ni nani alipitisha yote haya huko nyuma? Kwa nini Rais wetu anacheka? Je, anafurahia? Najua pengine nia ya Rais ni kuonyesha kuwa mambo ni mazuri wananchi wasiwe na wasiwasi, everything is under control. Lakini si kwa staili hii ya kuangua vicheko. Inaharibu zaidi ya kujenga haiba ya Rais.

3. Majibu ya Rais yametoa ahadi tu kuhusu ATCL na TRC, hayajatoa dira kuonyesha mwelekeo. Walau kwenye TANESCO kidogo amegusia sheria ya kuleta ushindani kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme. Swali la kujiuliza, ni kwa nini Rais hataki kutazama nyuma na kuchukua hatua? Lazima tutatue tatizo la mazingira ya utiwaji saini wa mikataba ama sivyo mambo ya Netgroup, Richmond nk yatajirudia tena? Ni lazima baadhi wa wahusika wachukuliwe hatua ili iwe fundisho.

4. Kuhusu EPA, Rais amekwepa badala yake amesimulia historia tu- na si mwelekeo na msimamo wa Tanzania katika majadiliano hayo. Pamoja na kuwa ameahidi Mramba atazungumza kwa kina, lakini Rais kama mtu ambaye amekuwa kwenye kada ya diplomasia kwa muda mrefu alipaswa kudokeza terms zetu ni zipi. Na kwa jinsi Rais alivyoirudia rudia tarehe 31 kwamba ni tarehe ya makubaliano inaelekea maamuzi yameshafanyika! Hizo terms za agreement kwa nini haziwekwi open? Napata hisia kwamba tunaburutwa- kwa sababu Rais amerudia rudia sana "wakubwa wakisema" "Hatuna cha kufanya" "Take it or leave it"; na ukishakwenda kwenye majadiliano ukiwa na inferiority complex basi chochote kitakuwa hewala!

5. Nimependa jinsi Rais anavyotumia muda mrefu wa maswali kuzunguka kwenye kufafanua mafanikio ya serikali katika huduma za kijamii na miundo mbinu na mipango iliyopo katika eneo hilo. Mathalani ujenzi wa sekondari kata, ujenzi wa baadhi ya barabara. Mpango wa Afya nnchini utakaohusisha Zahanati, vituo vya Afya nk. Na orodha ya barabara zitakazojengwa hususani kupitia MCC/MCA. Lakini wakati wote nimeendelea kujiuliza- hivi mpaka lini nchi yetu inataendeshwa kwa mfumo wa miradi? Kwa kweli maelezo ya Rais yamedhihirisha hofu yangu kwamba hatuongozwi kwa dira thabiti, tunatekeleza miradi. Katika maelezo ya Rais sijaona dira thabiti ya nini mwelekeo wa msingi wa serikali na malengo kwa mwaka unaofuata na kipindi kilichobaki. Kinachoonekana ni vipande vipande vya shughuli. Na karibu miradi yote iliyokuwa inatajwa ni ile ambayo tumefadhaliwa na washirika wa kimaendeleo. MCA, Japan nk.

6. Mahojiano na Rais yamenidhihirishia kwamba pamoja na kwamba kwa kauli Rais amesisitiza hali ni nzuri na anaridhishwa na mwelekeo nao ni PR Gimmick tu yakuonyesha kwamba things are in control, lakini ukimtazama Rais machoni utajua kabisa kwamba haridhishwi na mambo fulani fulani. Hata ile hamasa ya kusema tutafanya hiki na kile au tumefanya hiki na kile kwa ari, nguvu na kasi mpya imepungua sana. Our president appears to be down! If that is the case, is still call upon him to dissolve the cabinet, and not recycling most of the same Ministers. Mr. President should not let himself be drowned with the likes of Lowassa, Karamagi and Kingunge's!

Mambo ni mengi kwa kweli, ningependa kuyasema lakini wakati ukuta..

JJ

Naamini washauri wa Rais watayafanyia kazi haya maelezo na mengine ambayo nimeyatoa toka awali.

Lingine ni la kusahau maswali. Katika mahojiano yale ilikuwa mwandishi mmoja anauliza, Rais anajibu na baadaye ndio anauliza mwingine. Lakini kila aliyepewa wasaa alikuwa akiuliza maswali 2 mpaka 4. Sasa Rais akianza kuyajibu hayo 2 au 4; akifika la pili- tayari anakuwa ameshasahau maswali mengine 2 au 1 yaliyobaki. Hili ni suala ambalo linahitaji kurekebishwa. Haya ni baadhi ya mambo ambayo bila kujua yanapunguza imani za baadhi ya watu. Sababu zinaweza kuwa nyingi, na najua wataalamu wa ikulu wa mawasiliano wanazijua. Lakini la muhimu tu, kama Rais ameamua kutoa maelezo marefu kwa swali moja(kama alivyokuwa akifanya) basi ni muhimu yale mengine akayaweka katika maandishi(hints kidogo) ili akimaliza ayarudia. Niliona katika mahojiano alikuwa na note pad na kalamu, lakini alikuwa akiandika mara chache sana wakati maswali yanaulizwa; na kiasi kikubwa alikuwa haandiki! Sasa ikija wakati wa kujibu maswali yanakuwa yameshasahaulika. Ingetokea kwa muulizaji mmoja ningesema ni bahati mbaya. lakini imetokea mara kadhaa. Na suala hili nimeliona katika mikutano yote miwili niliyoitazama! Leo tuko ndani ya nchi watanzania wenyewe, lakini mambo haya yanaweza kutokea vile vile kwenye press conference za ugenini. Hivyo watu wa mawasiliano ikulu nawaombeni mzingatie hili. Communicators are born, but they are also made. Msitake kumfanya Rais wetu aonekane kuwa ni msahaulifu, ni wajibu wenu kwa kuwa taswira ya mawasiliano ya Rais mwisho wa siku ndicho ambacho mnalipwa kwa kodi za wananchi mkijenge na mnawajibu wa kufanya hivyo kwa Rais yoyote atakayekuwa hapo ikulu.

JJ
 
2. Nadhani ni vyema Rais akapunguza vicheko katikati ya kujibu maswali ambayo watanzania wanategemea majibu mazito. Rais anapozungumzia kwamba tumewauzia wawekezaji wapya Shirika la Reli likiwa limekufa kabisa; ama Net Group ndio wakaharibu zaidi Tanesco, Ama Alliance na baadaye Patnership vikashindwa kuiamsha ATCL na kwamba tumetoka ndege 9 mpaka 1 kutokana na utawala mbovu huo nyuma- Rais anapozungumzia hali hizi huku akiangua kicheko; kwa kweli si nzuri. Inakatisha tamaa zaidi! Inawafanya wananchi waanze kujiuliza, hivi ni nani alipitisha yote haya huko nyuma? Kwa nini Rais wetu anacheka? Je, anafurahia? Najua pengine nia ya Rais ni kuonyesha kuwa mambo ni mazuri wananchi wasiwe na wasiwasi, everything is under control. Lakini si kwa staili hii ya kuangua vicheko. Inaharibu zaidi ya kujenga haiba ya Rais.

JJ

This boy is naive, he does not know that Rais kucheka is part of the art of speeching. Au yeye akiwa kiongozi atakuwa ananuna tu! Shame on him

PM
 
Yaani unataka acheke then alete historia badala ya kujibu maswali ? Now who is naive here wewe ama yeye ?

JK kuongea na wahariri alitumia mbinu anazo pewa na Salva . Hii ndiyo kazi ambayo Salva imempa kula pale Ikulu .JK aliwatafuta wanao kubaliana naye akaongea nao kwa siri . Mikanda ikawa edited kwenye makali ya hoja ndipo wakatoa hizo mlizo sikiliza . I was there japokuwa sikuwa mwana habari ila msikilizaji .Maswali ni ya kupangwa kabisa na ndiyo maana haya yana jitokeza .
 
Alicheka sana walipokuwa wanamwuliza kuhusu Balali, huku wakitumia maneno "amekimbia nchi", alicheka mno kisha akawa anasema "mniwie radhi". Inaelekea hii habari ilikuwa inamchekesha sana, kuna kituko ndani yake!
 
Back
Top Bottom