JK: Sikuidhalilisha Tume ya Warioba

JK: Sikuidhalilisha Tume ya Warioba

Limeshamwagika ,lililobakia umalizie hii ngweyako au majeshi watakuondoa.
 
Hapo ndio kachanganya za kuambiwa na zake.. aibu Presida.
 
Wananchi wanaotaka serikali tatu ni 49 elfu tu wakati nchi inawatu zaidi ya milioni 45.

Ikiwa wananchi tuko milioni 49 waliopiga kura uchaguzi mkuu 2010 hawafiki hata robo, basi tuamini Watanzania 75% hawamkubali Mh. Rais?
 
Maon ni ya watanzania si ya warioba,na Ba'mkwe pamoja na watanzania wengine wamebak kumshambulia warioba,,,
 
Kitendo cha kumtaja Warioba na si tume, kitendo cha kuwadhalilisha akina Salim, Butiku, maprofesa na wasomi mbele ya TV, umma ukiangalia ni laana ambayo JK ataishi nayo milele.

Tulimweleza mapema awaombe radhi siku ile ile kwani ndio uungwana akakataa sasa anakimbia Uingereza baada ya kuwafedhehesha, kuwanyannyasa na kuwatia madole ya macho wazee wetu.

JK umeidhalilisha tume kuliko alivywahi kufanya kiongozi mwingine aliyetangulia.

Huwezi kumwita Jaji Warioba na Augustino Ramadhani wake meza ya juu halafu uanze kuwavua nguo kwa kuzusha.
Si umesema tume imependekeza majeshi 3, wapi hilo lipo.

Baada ya kuawatukana na kuwadhalilisha akina Salim Ahmed Salim, Butiku na wengine ukarudi Ikulu siku hiyo na kuvunja tume ili wasipate nafasi ya kujitetea. Ukawafunga midomo ili wabaki na aibu ya kuvuliwa nguo.

JK hili utaishi nalo miaka yako yote nasisi tunalaani sana dhalili uliyowafanyia hawa wazee

tupe nukuu ya hotuba ya Rais alipofunguwa bunge maalum inayomdhalilisha yeyote kati ya ho unaosema.
.
Ufataani unauweza,
 
Wananchi wanaotaka serikali tatu ni 49 elfu tu wakati nchi inawatu zaidi ya milioni 45.
Elfu 49 nafikiri ni namba kubwa sana kuliko Wajumbe 621 ambao wamejitwisha jukumu la kutuamulia aina ya serikali tunayoitaka!
 
tupe nukuu ya hotuba ya Rais alipofunguwa bunge maalum inayomdhalilisha yeyote kati ya ho unaosema.
.
Ufataani unauweza,
kuzalilishwa cio lazima utukanwe matus ya nguon, ukiambiwa wewe mpumbav tayar umedhalilishwa
 
"Usanii" wa JK umegonga ukuta. Mungu ibariki Zanzibar mungu ibariki Tanganyika.
 
Dar es Salaam.
"Nilitoa maoni yangu ya rasimu kwa sababu ninayo dhamana hiyo… Wao walitaka niseme; wajumbe nimelizindua Bunge. Hiyo haiwezekani," aliongeza Rais Kikwete akiashiria kuwa ilimpasa pia kutoa nasaha zake.
Chanzo: Mwananchi
Hapo ndipo penye shida, kwani kipindi cha maoni si kilishapita? Inamaana kabla hukupata kabisa muda wa kuyatoa maoni yako au uliyatoa yakakataliwa kwa maana pengine hayakuishawishi kamati hadi iyatupe kapuni then uyaokote na kuyapeleka upya katika bunge???? Napata shida tafsiri ya hili!
 
Kwani mkuu alichaguliwa kwa kura ngapi kati ya watanzania .je hapk hakuona haja ya kuangalia sampling
.....!tuwe fair kwa mambo ya muhimu
 
Kosa kubwa lilifanyika pale uongozi wa bunge la Katiba chini ya Sitta ulipokiuka kanuni na kumtanguliza mwenyekiti wa Tume kabla rais hajafungua bunge. Taasis ya urais ilitegemewa kuwa na utashi wa kuona kosa hili la kihistoria lakini haikuwa hivyo!

Kwa sasa hakuna kitu kinaweza kuondoa makovi yaliyo moyoni kwa Jaji Warioba na wazee wenzake pamoja na wanakamati. Na kama kuna mtu historia itamhukumu vibaya kwenye hili ni Samweli Sitta. Jaji Warioba amezomewa hadharani kwa sababu yake! Unforgivable.
 
Wananchi wanaotaka serikali tatu ni 49 elfu tu wakati nchi inawatu zaidi ya milioni 45.

Hao waliosalia walisema wanataka muundo gani?

Vipi kuhusu kiongozi kuchaguliwa na watu m5 katika nchi ya watu zaidi ya m45. Ina maana hao waliosalia hawamtaki?
 
Back
Top Bottom