JK si alisema zilizorudishwa ni 69 billioni?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
...sasa 16 billioni zimeenda wapi!!!? :confused:
Usanii mtupu!!!!


Money recouped from EPA:

Govt tables 53bn/-mini-budget
JAPHET SANGA in Dodoma
Daily News; Wednesday,February 04, 2009 @07:59​

FINANCE and EconomicAffairs Minister Mustafa Mkulo yesterday tabled the Supplementary Appropriation Act, 2009, asking the House to endorse a53bn/- recurrent expenditure for two ministries.

The Bill is aimed at bolstering the Ministry of Agriculture, Food Security and Cooperatives and the Ministry of Livestock Development and Fisheries in the current fiscal year. Deputy Minister for Finance and Economic Affairs, Mr Jeremiah Sumari, said the money has been recouped from the controversial Bank of Tanzania External Payment Arrears (EPA) account.


“There is a new impetus on boosting agricultural and livestock sectors and according to directives by President Jakaya Kikwete when he addressed the House last year,” he said. The Ministry of Agriculture, Food Security and Cooperatives has been allocated 40bn/- for recurrent expenditure while the Ministry of Livestock Development and Fisheries will get 10bn/-. The remainder 3bn/- goes to the Tanzania Investment Bank (TIB) to open up a lending window for farmers.

Agriculture, Food Security and Cooperatives Minister Stephen Wassira said his priority would be to give subsidized fertilizer to about one million farmers under the warehouse receipt system. He said farmers to benefit under the system would be those in Rukwa, Ruvuma, Mbeya, Iringa, Morogoro, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mara, Tabora and Kigoma regions.

Mr Wassira said his ministry would spend 30bn/- to support paddy and maize farmers in the cited regions while the remaining 10bn/- would be used to buy pesticides for cotton, cashew, coffee and tea saplings. Earlier, the government had allocated 31bn/- for the Agricultural Farm Inputs Fund but since prices of fertilizers has shot up, the 40bn/- is expected to cushion the effects of inflation.
 
Mkulu Bubu, kunahaja ya Rais kuwajibishwa bungeni kwa kauli zake feki na ikibadi kucast vote of no confident juu yake. Almost everyday we hear blunders of Tanzanian Top leaders and no explanations made behind the same.. shit!
 
Katika bunge la "upande mmoja" kama bongo unadhani suala la vote of no confidence linaweza kuwa effective kweli.Tatizo nao wapinzani wamestress sana kwenye urais tu.Kama wakiweza kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni pia na wale "walioamka" wa chama tawala wakiongezeka then tunaweza tukajionea significant changes huko tuendako.Vinginevyo huu mduara utaendelea til....
 
Hivi tukiwaambia kuwa fedha hizo siyo za EPA mtaweza vipi kuthibitisha kuwa ni za EPA? Je kama serikali inaamua kuchapa fedha nyingine nyingi mtajuaje?
 
Hivi tukiwaambia kuwa fedha hizo siyo za EPA mtaweza vipi kuthibitisha kuwa ni za EPA? Je kama serikali inaamua kuchapa fedha nyingine nyingi mtajuaje?

Mkjj, kinachofanyika hapa ni ufisadi mtupu!! haiwezekani mafisadi wa EPA warudishe pesa nyingi kiasi hicho na hadi hii leo kushindwa kutoa list ya majina ya wote waliorudisha peza hizo na kiasi walichorudisha na pia zimewekwa katika bank ipi. Hapa naona kuna usanii wa hali ya juu. Kwenye hotuba (nimeitafuta hotuba hiyo mtandaoni na hapa JF bila mafanikio yoyote) aliyoitoa JK (kama sikosei November 2008) alitwambia kiasi kilichorudishwa ni shilingi 69 bilioni, sasa tunaambiwa kumbe ziko 53 billioni tu!!! Hapa kuna mazingaombwe ya hali ya juu. Bila kutoa hiyo list ya majina ya waliorudisha na kiasi kilichorudishwa na kila mmoja wao mimi sitaamini kabisa kwamba hata senti tano ya EPA ilirudishwa na mafisadi hao wa EPA. Serikali inaogopa nini kutoa hayo majina!!? :confused:
 
Hivi tukiwaambia kuwa fedha hizo siyo za EPA mtaweza vipi kuthibitisha kuwa ni za EPA? Je kama serikali inaamua kuchapa fedha nyingine nyingi mtajuaje?

Mwanakijiji, Kimsingi mimi siamini kama hizo pesa zilirudishwa na mafisadi kwa sababu report ya urudishaji inamaswali lukuki hata sitaki kuyataja. Hivyo yawezekana kabisa unachosema kikawa sahihi. Niswala la muda tu tutapata ukweli tuu. Swala la vote of no confident linawezekana tuu hasa pale taratibu za kupiga kura bungeni zikibadilishwa. Mfumo wa kura ya Ndioooooooooooooo na Siyooooooooooooooooo ndio unaosababisha CCm kushika hatamu. Ninahakika wakitumia ballot paper atang'oka mtu bila utata.
 
Mnakumbuka rais aliwahi kutuambia Richmond haijachukua hata senti moja ya Watanzania? Baadaye ikabainika walishachota millioni 23. Ninyi bado mnamwamini huyu?
 
Mnakumbuka rais aliwahi kutuambia Richmond haijachukua hata senti moja ya Watanzania? Baadaye ikabainika walishachota millioni 23. Ninyi bado mnamwamini huyu?

Hatumwamini, ila tunamsikiliza!
 
Mnakumbuka rais aliwahi kutuambia Richmond haijachukua hata senti moja ya Watanzania? Baadaye ikabainika walishachota millioni 23. Ninyi bado mnamwamini huyu?

Na ni huyo huyo aliyetwambia kwamba ili Mtera ijae itabidi zinyeshe elnino 3, lakini in just a moon tena mvua za vuli, Mtera mpaka ikatapika. Huyo jamaa inaonyesha ni careless sana au wasaidizi wake ni vilaza kupita kiasi.
 
Na ni huyo huyo aliyetwambia kwamba ili Mtera ijae itabidi zinyeshe elnino 3, lakini in just a moon tena mvua za vuli, Mtera mpaka ikatapika. Huyo jamaa inaonyesha ni careless sana au wasaidizi wake ni vilaza kupita kiasi.

........Ha ha ha ha mkubwa umenifurahisha sana hapa, wala sio swqala la wasaidizi wake mi nawatetea wasaidizi wake. Niuvivu wake wa kufikiri tuu. Naamini average education inatosha kabisa kuchuja hoja za msingi kama hiyo ya mtela bila hata kuwa na utaalamu mkubwa. Hiyo kauli itakuwa ni yake mwenyewe wala hakushauriwa na mtu yeyote.
 
KUSEMA KWELI TUNA BUNGE KILAZA. SIJUI BUNGE LILIKUBALI VIPI KUPITISHA BILL.53 WAKATI MHE. RAIS KATIKA HOTUBA YAKE KWA TAIFA YA MWEZI OKTOBA 2008 ALISEMA ZILIKUWA ZIMEKUSANYA BILL. 69 NA USHEE. HIVI NDIVYO ALIVYOSEMA "Nilielezea pia kwamba baada ya tarehe 31 Oktoba, 2008, kwa wale ambao watakuwa hawakuteleza, hatua za kisheria zichukuliwe. Leo ndiyo siku ya mwisho. Napenda kuwajulisha kuwa, taarifa nilizoletewa majira ya mchana leo, ni kuwa kiasi cha shilingi 69,326,437,650 kati ya shilingi 90,359,078,804 zilikuwa zimerejeshwa. Hii ni sawa na asilimia 76.7"
 
Serikali na usanii wake

Shilingi bilioni 17 za EPA zatengwa kuwalipa wenyewe

2009-02-13 14:49:23
Na Muhibu Said

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yussuf Mzee, amesema Sh. bilioni 17 zilizobaki katika marejesho ya fedha zilizoibwa na makampuni 22 kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimetengwa kwa ajili ya kuwalipa watakaojitokeza kuzidai hadi ifikapo Juni, mwaka huu.

Kauli hiyo ilitolewa na Mzee alipozungumza na Nipashe juzi ikiwa ni siku chache tangu Bunge liidhinishe Sh. bilioni 53 zilizochukuliwa na serikali katika Sh. bilioni 70 za marejesho ya fedha hizo, zitumike kununulia pembejeo za kilimo, kuwakopesha wakulima na kununulia dawa za mifugo.

Muswada wa serikali wa kuomba idhini hiyo kwa Bunge, uliwasilishwa bungeni Alhamisi ya wiki iliyopita na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.

Mzee alisema serikali imefikia uamuzi huo kwa vile fedha hizo ni za wafanyabiashara hususan makampuni ya nje, na kwamba, endapo hatajitokeza yeyote kuzidai katika kipindi hicho, watazitenga kwenye Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha wa 2009/2010, Julai, mwaka huu.

``Hizo Sh. bilioni 17 zimetengwa kuwalipa watakaojitoekeza hadi mwezi Juni. Akitokea mtu tutamlipa asipotokea tutazitenga kwenye Bajeti mwezi Julai,`` alisema Mzee.

Hata hivyo, Naibu Waziri huyo alisema suala la mahali na namba ya akaunti zilikohifadhiwa fedha hizo, hajui na kwamba anayejua ni waziri.

Fedha hizo ziliidhinishwa na Bunge kwa ajili ya matumizi ya serikali nje ya bajeti ya mwaka 2008/09.

SOURCE: Nipashe
 
Bil 16 hiyo ni processing charge, kuzihamisha kutoka kwenye a/c za mafisadi kwenda a/c ya sirikali... :D :D

Hahaha! brother sio processing charge ila si unajua kuna uchaguzi wa kununua mwaka kesho? sasa hicho ni kianzio kwakua mabalozi wa nchi wafadhili wanachunguza sana misaada yao siku hizi.
 
Hakika serikali yetu inatudharau sana,,nao pia ni ufisadi.Ila yote yana mwisho na mwisho wake ni mbaya kuliko mwanzo.Siamini kama kweli pesa zimerudishwa,pia nashindwa kuelewa jinsi gani bunge limekubali kudanganyika,,,ila ikombozi wetu upo karibu ni jukumu la kila mzalendo kuwajibika kwa ajili ya kizazi kijacho,,,,,,,,,,timiza wajibu wako tanzania yenye neema yawezekana,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
 
JF ya wakati huo ilikuwa ya moto wa kuotea mabali! Hatuna tiktok wakati huo.
===
Uzi huu nimekumbana nao katika kutimiza hoja ya Ndugu Pascal Mayalla ya kurejea Maandishi ya MwanaJF mwenzetu aliyetutoka, FMEs-W. Malecela (R.I.P)
 
Back
Top Bottom