Kama ni kweli kuwa JK na IGP walikuwa Arusha siku ya tukio la mbunge wa Arusha kupigwa maana yake ni nini? Haina maana kuwa alikuwepo katika kupanga hayo yaliyotokea? Tunaweza kutafsiri vipi matukio haya ya vurugu katika chaguzi za wenyeviti na Mameya katika maeneo ambayo wapinzani wana nguvu? Je, hii inaweza kutafsiriwa kuwa serikali inaingilia kwa makusudi na kuvuruga chaguzi hizi?
Humo JF kuna mtu alikuja na tetesi kuwa Dr. Batilda Buriani ameteuliwa kuwa mkuu wa Mkoa wa Arusha. Tafsiri ya kitendo kama hicho ina maana ya kuendeleza vurugu ambayo ilianza wakati wa kampeni kati ya aliyeshindwa katika harakati za ubunge na aliyeshinda ubunge. Kama ilivyokuwa kwa mwaka 2005 kati ya Mwakyembe na Mwakipesile, baada ya Mwakipesile kushindwa kwenye ubunge alikwenda Mbeya kama mkuu wa mkoa wakati mpinzani wake katika kinyang'anyiro cha ubunge akiwa mbunge katika mkoa huo huo. Matokeo yake uhasama wao wa kuwania ubunge uliendelea. Kitendo kama hicho kilikuwa cha makusudi hasa kwa yule aliyemteua.Jk unataka kuipeleka nchi wapi? nchi hii ni ya watanzania, usidhani ni ya CCM.
Humo JF kuna mtu alikuja na tetesi kuwa Dr. Batilda Buriani ameteuliwa kuwa mkuu wa Mkoa wa Arusha. Tafsiri ya kitendo kama hicho ina maana ya kuendeleza vurugu ambayo ilianza wakati wa kampeni kati ya aliyeshindwa katika harakati za ubunge na aliyeshinda ubunge. Kama ilivyokuwa kwa mwaka 2005 kati ya Mwakyembe na Mwakipesile, baada ya Mwakipesile kushindwa kwenye ubunge alikwenda Mbeya kama mkuu wa mkoa wakati mpinzani wake katika kinyang'anyiro cha ubunge akiwa mbunge katika mkoa huo huo. Matokeo yake uhasama wao wa kuwania ubunge uliendelea. Kitendo kama hicho kilikuwa cha makusudi hasa kwa yule aliyemteua.Jk unataka kuipeleka nchi wapi? nchi hii ni ya watanzania, usidhani ni ya CCM.