Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
maeneo matano ambayo jk na ccm yake wanalipotosha taifa ni pamoja na:-
1) kulinganisha utaratibu wa kupata katiba mpya na marekebisho ya katiba iliyopo. jukumu la kurekebisha katiba iliyopo ni la bunge wakati jukumu la kuandika katiba mpya ni la watanzania wote.
2) kudai yapo maeneo ambayo hayajadiliwi.....................ni nani aliyetuamulia kuwa yawepo maeneo ambayo yapo nje ya mjadala wa kuandika katiba mpya..........................kama nafasi ya muungano, mihimili ya serikali n.k
3) kusahau ya kuwa Jk na wabunge wake wa ccm waliapa kuilinda katiba iliyopo sasa wanatoka wapi kuwa waasisi wa kuinyambulisha hiyo katiba kama siyo kuvunja katiba iliyopo ambayo hata wao wanakiri kwa vinywa vyao kuwa wanaipenda hii iliyopo?
4) Kutupotosha ya kuwa katiba ya Kenya ilifuata mchakato wa kwetu hapa.....................huu ni uongo usio na kifani Kenya tume yao ilitangazwa kwenye magazeti na wenye sifa waliomba na kuchujwa na kamati maalumu ya bunge kabla ya bunge lote kuwapigia kura...............raisi Kibaki kazi yake ilikuwa kuthibitisha uteuzi huo baada ya mchakato wa wazi kutumika na ambao ulitoa fursa sawa kwa wote....................kwetu Jk ana majina ya wajumbe wa tume kibindoni kwake..................tukihoji sisi tunaonekana tunaleta chokochoko!!!!!!!1
5) Jk anatetea michakato ya zamani ya kufanyia marekebisho katiba iliyopo..................anachoshindwa kujifunza ni kuwa kama utaratibu ule ulikuwa sahihi mbona bado tunahitaji katiba mpya? ukweli ni kuwa michakato ile haikuwa shirikishi na ndiyo maana tulikwama................
hitimisho:-
mchakato huu utazaa katiba ya viongozi na wala siyo ya wataliwa na matokeo yake vuguvugu la kudai katiba mpya litaendelea hadi hapo mwafaka wa kitaifa utakapopatikana..........
1) kulinganisha utaratibu wa kupata katiba mpya na marekebisho ya katiba iliyopo. jukumu la kurekebisha katiba iliyopo ni la bunge wakati jukumu la kuandika katiba mpya ni la watanzania wote.
2) kudai yapo maeneo ambayo hayajadiliwi.....................ni nani aliyetuamulia kuwa yawepo maeneo ambayo yapo nje ya mjadala wa kuandika katiba mpya..........................kama nafasi ya muungano, mihimili ya serikali n.k
3) kusahau ya kuwa Jk na wabunge wake wa ccm waliapa kuilinda katiba iliyopo sasa wanatoka wapi kuwa waasisi wa kuinyambulisha hiyo katiba kama siyo kuvunja katiba iliyopo ambayo hata wao wanakiri kwa vinywa vyao kuwa wanaipenda hii iliyopo?
4) Kutupotosha ya kuwa katiba ya Kenya ilifuata mchakato wa kwetu hapa.....................huu ni uongo usio na kifani Kenya tume yao ilitangazwa kwenye magazeti na wenye sifa waliomba na kuchujwa na kamati maalumu ya bunge kabla ya bunge lote kuwapigia kura...............raisi Kibaki kazi yake ilikuwa kuthibitisha uteuzi huo baada ya mchakato wa wazi kutumika na ambao ulitoa fursa sawa kwa wote....................kwetu Jk ana majina ya wajumbe wa tume kibindoni kwake..................tukihoji sisi tunaonekana tunaleta chokochoko!!!!!!!1
5) Jk anatetea michakato ya zamani ya kufanyia marekebisho katiba iliyopo..................anachoshindwa kujifunza ni kuwa kama utaratibu ule ulikuwa sahihi mbona bado tunahitaji katiba mpya? ukweli ni kuwa michakato ile haikuwa shirikishi na ndiyo maana tulikwama................
hitimisho:-
mchakato huu utazaa katiba ya viongozi na wala siyo ya wataliwa na matokeo yake vuguvugu la kudai katiba mpya litaendelea hadi hapo mwafaka wa kitaifa utakapopatikana..........