Jk kukutana na chadema

Jk kukutana na chadema

SOKON 1

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2010
Posts
1,134
Reaction score
331
Katika vugu vugu la chadema kuendelea na maandamano nchi zima ambayo yameleta hofu kubwa kwa ccm na serikali yake, na pia kusababisha vyama vya siasa jana kukutana kwa dharura kutatua mzozo huo ila wamependekeza rais Jakaya Mrisho Kikwete kukutana na chadema na kuzungumza ili pawe na maelewano na chadema.
My take:
Sidhani kama Chadema na JK kutakuwa na maelewano kwani JK ameshindwa kujibu hoja za chadema na maisha yanaendelea kuwa magumu na uchumi unaendelea kudorora. Kama jana vyama vya siasa vilipokutana vilishindwa kuelewana je JK ATAWEZA?
 
hakuna haja ya rais kukutana na chadema... JK pekee sio solution ya matatizo yaliyopo, kwani inaonekana hata ndani ya chama hana hizo nguvu tunazotegemea awe nazo:hand:
 
hakuna haja ya rais kukutana na chadema... JK pekee sio solution ya matatizo yaliyopo, kwani inaonekana hata ndani ya chama hana hizo nguvu tunazotegemea awe nazo:hand:
Ila ndivyo walivyopendekeza ili kuwe na maelewano na chadema . Ila John Tendwa uwezo wake wa kufikiri umefika tamati kwa kuendeshwa kama gurudumu bovu kwani anafikiria ndio litakuwa sululisho badala ya Raisi kusikiliza hoja za chadema na kutatua matatizo yanayowakuta watazania na hali ngumu ya maisha.
 
Kwenye kikao cha baraza hilo je kulikuwa na mjumbe toka CDM NA CCM
 
JK ndio sehemu ya tatizo sasa hata akikutana na chadema hakuna jipya atakalotupa kama anaipenda Tanzania na anapenda Demokrasia na AMANI basi awajibike kisiasa kwa kujiuzulu ili apishe uchaguzi huru na wa haki ufanyike kwani ameshakosa uhalali wa kisiasa kwa wananchi.
 
Kwenye kikao cha baraza hilo je kulikuwa na mjumbe toka CDM NA CCM
walikuwepo tyena CDM wamekaza uzi na kuwaambia maandamano zaidi yatafuata sasa ni zamu ya kanda ya kusini baada ya bunge la april na moja ya maazimio ya kikao hicho wameishauri serikali kuangalia uwezekano wa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa katika URT.
 
Katika vugu vugu la chadema kuendelea na maandamano nchi zima ambayo yameleta hofu kubwa kwa ccm na serikali yake, na pia kusababisha vyama vya siasa jana kukutana kwa dharura kutatua mzozo huo ila wamependekeza rais Jakaya Mrisho Kikwete kukutana na chadema na kuzungumza ili pawe na maelewano na chadema.
My take:
Sidhani kama Chadema na JK kutakuwa na maelewano kwani JK ameshindwa kujibu hoja za chadema na maisha yanaendelea kuwa magumu na uchumi unaendelea kudorora. Kama jana vyama vya siasa vilipokutana vilishindwa kuelewana je JK ATAWEZA?

Tatizo kubwa si CDM na Kikwete bali ni jinsi Spika Anna Makinda alivyopora haki ya CDM kuisimamia Serikali kama chama kikuu cha upinzani bungeni na jinsi anavyoshughulikia hoja zinazowasilishwa na CDM Bungeni. Badala ya CDM kukutana na Raisi J K ingefaa spika wa zamani Mh Samweli Sitta, Spika wa sasa Mh Anna Makinda na Mwenyekiti wa CCM Raisi Kikwete wao ndio wakutanishwe ili wamwelimishe spika Anna Makinda namna ya kuendesha Bunge kama mhimili ulio huru tofauti na sasa anavyoliendesha Bunge kama kamati ya CCM na idara ya Serikali.
 
CHADEMA kukutana na JK ili iweje?...hoja hapa ni maisha magumu kwa mtanzania, ufisadi, uzembe &kutowajibika n.k; so wanachokifanya CHADEMA mikoani ni kuzidi kuwariji wananchi na kuwaelezea sababu ya umaskini wao na maisha magumu, hakuna haja ya kukutana na JK....kwani wakikutana wataamua maisha kuwa matamu?ufisadi kuisha n.k?
 
Ndoto ya madaraka. JK hana sababu ya kukutana na cdm. Kwa kipi hasa,wachochee watu kufanya uasi halafu watake mazungumzo na Rais.Hawana jipya waendelee na maandamano mazungumzo ya nini. Na wao wanataka kuingia serikalini kama cuf.Waendelee kupost thread humu JF
 
Ila ndivyo walivyopendekeza ili kuwe na maelewano na chadema . Ila John Tendwa uwezo wake wa kufikiri umefika tamati kwa kuendeshwa kama gurudumu bovu kwani anafikiria ndio litakuwa sululisho badala ya Raisi kusikiliza hoja za chadema na kutatua matatizo yanayowakuta watazania na hali ngumu ya maisha.

Jamani tatizo limeanzia Bungeni. CDM wanatambua kazi ya Bunge ni kuisimamia Serikali na wanataka kufanya kazi hiyo lakini Wabunge wa CCM wakiongozwa na spika hawataki Serikali ikosolewe na ndio maana walikataa hoja ya kujadili Mabomu ya Gongo la Mboto, Hoja ya kujadili tatizo la umeme. Kama hii mijadala ingeruhusiwa Bunge kwa ujumla wake lingekuja na maazimio ya kuelekeza Serikali nini cha kufanya na CDM wasingekuwa na mashtaka ya kupeleka kwa wananchi.
 
walikuwepo tyena CDM wamekaza uzi na kuwaambia maandamano zaidi yatafuata sasa ni zamu ya kanda ya kusini baada ya bunge la april na moja ya maazimio ya kikao hicho wameishauri serikali kuangalia uwezekano wa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa katika URT.

Hakuna cha serikali ya umoja wa kitaifa, huwezi kushirikiana na akina Sophia Simba kuunda serikali
 
JK kukutana na CHADEMA sio solution ya matatizo, pia ndani ya chama chake mwenyewe anaonekana hayuko that stable.
 
Wakuu,
Nisichoelewa ni kwamba kwani kuna tatizo gani kati ya Rais na CDM?...labda mimi sijawa uptodate na hilo...sijaona situation inayofanya cdm kukutana na JK!..Kwani DAMU ishamwagika mahali?...CDM wako mtaani wanafanya siasa za kawaida, tatizo limetokea wapi?...wakikutana na JK itaonekana wanakiri kwamba kweli wamefanya uchochezi, na hivyo namna fulani ya arbitration inatakiwa!...Hell Noooo tto this!!...Iwould suggest(ikilazimu sana kukutana), huyo mtu anayetakiwa kuongea na cdm awe ni mwinginewe, apart fromJK(MAANA AMEPROVE FAILURE KWENYE KILA KITU KWA SASA)!
 
Ndoto ya madaraka. JK hana sababu ya kukutana na cdm. Kwa kipi hasa,wachochee watu kufanya uasi halafu watake mazungumzo na Rais.Hawana jipya waendelee na maandamano mazungumzo ya nini. Na wao wanataka kuingia serikalini kama cuf.Waendelee kupost thread humu JF

Chadema mnafanya vizuri sana,maana kama hawataki kuwasikiliza bungeni na wakati tuliwatuma wakatusemee badala yake wanatetea maslahi ya chama na maisha yao njoni mtueleze sisi tunawaunga mkono na ndiyo dawa itapatikana.Dos santos usioneshe uwezo wako mdogo wa kufikili swala sio uongozi bali hatima ya maisha yetu,hatuna interest na uongozi maana wote hatuwezi kuwa viongozi tunataka ajila,ufisadi uishe,umeme,bei nzuri nk. nyie ndiyo mnaomdanganya Rais wetu na kumchanyanya na maneno ya uongo.
 
Wakuu,
Nisichoelewa ni kwamba kwani kuna tatizo gani kati ya Rais na CDM?...labda mimi sijawa uptodate na hilo...sijaona situation inayofanya cdm kukutana na JK!..Kwani DAMU ishamwagika mahali?...CDM wako mtaani wanafanya siasa za kawaida, tatizo limetokea wapi?...wakikutana na JK itaonekana wanakiri kwamba kweli wamefanya uchochezi, na hivyo namna fulani ya arbitration inatakiwa!...Hell Noooo tto this!!...Iwould suggest(ikilazimu sana kukutana), huyo mtu anayetakiwa kuongea na cdm awe ni mwinginewe, apart fromJK(MAANA AMEPROVE FAILURE KWENYE KILA KITU KWA SASA)!

Mkuu naunga mkono hoja!
hakuna kukutana na JK wala yeyote toka huko Chechemea!
kwani sera na ilani zao na CDM hazilingani.hiyo ni sawa na kumpatia mwanafunzi desa la kufanyia mtihani ilihali mtihani anaujua fika hata akiafanya kasinzia.
CDM keep your trend and go for it, let them murmuring na uzushi wao.
 
Tatizo siyo CDM ni peoples power inafanya kazi, waliidharau kwa miaka Hamsini iliyopita. sasa wameiona kumbe wananchi walikuwa wanawapa nafasi.

Wasitake kuifanya CDM watoto, wameyataka hayo wenyewe sasa wanalalamika nini?, Walikuwa wanafanya mipasho na vitisho kwenye media sasa nadhani wameiona sasa hawana jeuri tena mbele ya wananchi wamebaki kulalama tu.

People Power. Hatudanganyiki tena
 
Chadema mnafanya vizuri sana,maana kama hawataki kuwasikiliza bungeni na wakati tuliwatuma wakatusemee badala yake wanatetea maslahi ya chama na maisha yao njoni mtueleze sisi tunawaunga mkono na ndiyo dawa itapatikana.Dos santos usioneshe uwezo wako mdogo wa kufikili swala sio uongozi bali hatima ya maisha yetu,hatuna interest na uongozi maana wote hatuwezi kuwa viongozi tunataka ajila,ufisadi uishe,umeme,bei nzuri nk. nyie ndiyo mnaomdanganya Rais wetu na kumchanyanya na maneno ya uongo.

maisha magumu mpaka watu waambiwe ni magumu? Kwani watu hawayaoni? Mbona Rais JK ktk hotuba yake amekiri kwamba maisha ni magumu.CDM wakiwahutubia watu maisha ni magumu ndo yanabadilika au kuwapotezea watu muda wa kuhangaikia maisha yao yawe mepesi. Maandamano hayana tija kwa mtz,ila ipo ajenda ambayo wewe huijui unafuata mkumbo. Kama hamkueleweka ktk kampeni ndo mtaeleweka sasa
 
Back
Top Bottom