JK hujawatendea haki wabunge wa CCM

JK hujawatendea haki wabunge wa CCM

Pasco

Sekta ya fedha -uchumi na nishati hapa nchini zina changamoto kubwa sana. Alichokifanya JK ni kulinganisha wataalam mbalimbali katika sekta hizo na kuona wabunge aliowateua na kuwa mawaziri wana sifa kubwa kuliko ambao anao katika bunge lake. CVs zao tumezisoma hapa JF. Hatuwezi kusema wabunge wa CCM ni vilaza bali hawajafikia sifa za hawa wawili katika sekta hizi mbili. Ingawa wapo wengine ni mzigo kweli.
 
Kama wewe ni mpiga kura na ulichagua mbunge wa CCm stuka! hata kama uliruhusu kura kuibiwa stuka pia! hichi ndicho nilichojifunza kwenye baraza jipya la JK... wabunge wengi JK anawaona useless waganga njaa na wachumia tumbo na posho mjengoni..

Kati ya wabunge zaidi ya 200 JK kakosa mtu wa kumpa Wizara ya nishati na madini!!? Na amini nawaambieni hata waliorudishwa wamerudishwa basi tu kwa kua hakuna jinsi
 

Nauliza jee ni kweli JK amekosa kabisa watu wa kumsaidia miongoni mwa wabunge wa CCM kwa sababu waliobakia wote ni vilaza tuu au mule bungeni kuna watu wazuri tuu miongoni mwa wabunge wa CCM bali JK ana lake jambo na hao aliowateua?!.

Pasco.

Mkuu unao waona kawateua jana wengine kaamua kuwabeba kutokana na tuhuma zao kuwa sio kubwa kivile ile ndo cream ya wabunge wa CCM alishindwa amtoe Maghembe au Mkuchika atamweka nani kuchukua nafasi zao basi akaamua kuwachanga kama karata na kuwatupia kule na huku lakini kiukweli mle bungeni kwa hao walio baki wabunge hakuna anae faa kuwa waziri.
 
  • Thanks
Reactions: ral
Raisi anahaki ya kuchagua yeyeto! Pia sio sisi tunaosema, mbunge asiwe waziri!
 
Hivi Professa Maji Marefu angepewa unaibu wizara ya utamaduni na michezo angeshindwa vipi?
Kumbuka kipindi alipokuwa mganga maarufu....!
Michezo: Alikuwa anadhamini ngumi, bendi, mpira n.k

Utamaduni:Akiitwa mtaani kwenu kuja kutoa wachawi, ngoma zinapigwa mwanzo mwisho
Kabla ajaja manyaunyau huyu jamaa alikuwa kiboko.
Nashangaa JK kutompa wizara ya utamaduni na michezo.
 
jana rais ametangaza baraza jipya la mawaziri,cha kushangaza kuna watu hawakua wabunge lakini wameteuliwa kuwa wabunge na kupewa wizara.swali langu je,katika wabunge wote wa ccm hakuna msafi au mtu mwenye uwezo wa kua mawaziri ni akina wasira pekeyao? Mpaka atoe mawaziri nje? Filipnjombe, malole,baduel,lusinde,mama malecela

Wakuu mbona tunachanganya sana mambo au media ndiyo zinatu-drive, hivi jana Rais Kikwete katangaza Baraza la Mawaziri jipya kweli? Tunajua maana ya baraza jipya na ili lipatikane nini kinafanyika kwanza. Aliambiwa asuke na kweli KASUKA UPYA. Yaani kabadili msuko lakini nywele na kichwa ni vile vile.
 
hakika duniani chama ambacho kila mbunge anaweza kuwa waziri na akaparfome ni chadema peke yake.
ccm makapi ya kumwaga,pamoja na kumwaga povu
KIGWA.
KILANGO.
KAFUMU.
bado wameonekana hamna kitu mpaka wamemlazimisha mwenyekiti wao kuvunja katiba na kuteua raia kuwa mawaziri,na hilo ni fundisho kwa ccm kuwa mbunge mmoja wa chadema sawa na 30 wa kwao,hiyo ina maana kuwa kikwete angekuwa na kazi rahisi sana kuteua kutoka chadema kuliko ccm.
 
Pasco

Sekta ya fedha -uchumi na nishati hapa nchini zina changamoto kubwa sana. Alichokifanya JK ni kulinganisha wataalam mbalimbali katika sekta hizo na kuona wabunge aliowateua na kuwa mawaziri wana sifa kubwa kuliko ambao anao katika bunge lake. CVs zao tumezisoma hapa JF. Hatuwezi kusema wabunge wa CCM ni vilaza bali hawajafikia sifa za hawa wawili katika sekta hizi mbili. Ingawa wapo wengine ni mzigo kweli.
Pamoja na haya tunayosema Uongozi ni kipaji, hivi mtu kama Kigangwala pamoja na usomi wake...! unategemea anaweza kukuongoza kweli???

 
hata huyu Dalali Kafumu aliyekuwa katibu mkuu wizara ya Madini naye sijui ni nini hasa tatizo?
Naona umepoteza umakini wako sasa, huyu Kafumu alikuwa ni Kamishna wa wa madini na sio katibu, je nini tija yake alipokuwa kamishna wa Wizara ya madini ndio atushawishi kumpa Uwaziri?
 
Wanabodi,

Naomba nianze na nilichokisema kuhusu wabunge wapya wa CCM niliobahatika kukutana nao pale bungeni Dodoma November, 2010, ile siku wanaapishwa.


Leo nilikuwa nafanya mapitio ya nilichokisema miaka miwili iliyopita kuhusu wabunge wa CCM. Nilisema baadhi ya wabunge wapya wa CCM wengi ni makapi tuu, hawana substance!. Hili limethibitishwa na JK, katika kulisuka upya baraza lake, kwenye hao wabunge waliopo, amesaka sana akakuta patupu!, yaani hamna kitu mle!, ndipo akajaribu kuvikombeleza vile vichwa vichache vilivyobakia na kulazimika kujaza nakisi kwa kufanya uteuzi mpya wa wabunge wa kumsaidia.

Jee kuna uwezekano wabunge wa CCM waliopo mjengoni kweli ni makapi, vilaza, ni bure kabisa na hana kitu na hawana jipya lolote la kudeliver hadi kumlazimisha mkuu wa nchi kutafuta vichwa vya maana nje ya wabunge waliopo kwa kukopa (bila kuapishwa) ili ajenge timu yake?!.

Nauliza jee ni kweli JK amekosa kabisa watu wa kumsaidia miongoni mwa wabunge wa CCM kwa sababu waliobakia wote ni vilaza tuu au mule bungeni kuna watu wazuri tuu miongoni mwa wabunge wa CCM bali JK ana lake jambo na hao aliowateua?!.

Pasco.


Pasco brother hakuna mtu mfuatiliaji, mdadisi wa mwenendo wa mambo nchini, kisiasa, kiuchumi na kijamii na zaidi Great Thinker anaweza kutafuta second thought kujua kuwa wabunge wengi wa CCM ni vilaza, hawajui kwa nini walichaguliwa. Wengine hawajui hata ilikuwaje wakashinda. Nazungumza hili with experience. Nimekuwa bungeni kikazi mara kadhaa. Nimekutana nao kikazi mara nyingi. Hamna kitu. Tunapoteza rasilimali fedha kuhudumia watu ambao output yao ni almost to zero. They have nothing to add.

Lakini hata hao wanaoteuliwa kutoka wabunge wa sasa bado ni kwenye pool ile ile kaka. Samaki wasiofanana (different species) hawawezi kukaa bwawa moja. Hao wako bwawa moja kwa sababu wanafanana.

Mathalani kuna mtu alikuwa ananielezea sifa za Janeth Mbene. Anakiri kuwa kama ni kwa CV, aah mother CV nayo ya kutosha...lakini sasa, kwa mtendo yake kikazi, kanipatia mifano dhahiri kuwa she is not principled at all.

Lakini hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kushangaa. CCM hii...huu mti unaokufa huwezi kutegemea utoe matunda mazuri. In really working sense hata kama kuna kitu kizuri kwa sasa within CCM hakiwezi ku-flourish...with suc corrupted and rotten system.

No wonder bado watu hawana imani na MSUKO MPYA wa Baraza la Mawaziri kwa sababu nywele na kichwa bado ni vile vile. Walisuka twende kilioni sasa wamesuka Sangita au za Kimasai. Haya.
 
Hivi Professa Maji Marefu angepewa unaibu wizara ya utamaduni na michezo angeshindwa vipi? Kumbuka kipindi alipokuwa mganga maarufu....! Michezo: Alikuwa anadhamini ngumi, bendi, mpira n.k Utamaduni:Akiitwa mtaani kwenu kuja kutoa wachawi, ngoma zinapigwa mwanzo mwisho Kabla ajaja manyaunyau huyu jamaa alikuwa kiboko. Nashangaa JK kutompa wizara ya utamaduni na michezo.
hata mi naweza kudhamini pambano la Simba na Yanga lakini sina sifa ya kuwa Waziri/Kiongozi wa michezo
 
Wanabodi,

Naomba nianze na nilichokisema kuhusu wabunge wapya wa CCM niliobahatika kukutana nao pale bungeni Dodoma November, 2010, ile siku wanaapishwa.


Leo nilikuwa nafanya mapitio ya nilichokisema miaka miwili iliyopita kuhusu wabunge wa CCM. Nilisema baadhi ya wabunge wapya wa CCM wengi ni makapi tuu, hawana substance!. Hili limethibitishwa na JK, katika kulisuka upya baraza lake, kwenye hao wabunge waliopo, amesaka sana akakuta patupu!, yaani hamna kitu mle
 
Huo ni mtazamo pia lakini tusubiri tuone kama hata hawa wa kukopa sio vilaza kutoka reserve bench!!
 
hakika duniani chama ambacho kila mbunge anaweza kuwa waziri na akaparfome ni chadema peke yake.
ccm makapi ya kumwaga,pamoja na kumwaga povu
KIGWA.
KILANGO.
KAFUMU.
bado wameonekana hamna kitu mpaka wamemlazimisha mwenyekiti wao kuvunja katiba na kuteua raia kuwa mawaziri,na hilo ni fundisho kwa ccm kuwa mbunge mmoja wa chadema sawa na 30 wa kwao,hiyo ina maana kuwa kikwete angekuwa na kazi rahisi sana kuteua kutoka chadema kuliko ccm.

Dr. Kafumu atadondokea pua kwenye kesi yake ndo maana kaachwa
 
Nchi inaendeshwa kihuni sana,MWL aliwahi kusema ktk Uchaguzi wa kura za maoni ya Urais 1995 Dodoma.BILA CCM MADHUBUTI NCHI YETU ITAYUMBA,yametimia maneno Kambarage.RAIS WK 2 AMEKOSA KABISA M2 WA KUMPA UWAZIRI KT WABUNGE 200 WA CCM.Wtz wenzangu inatosha sasa.Tusirudie tena kutupa kura zetu 2015 jalalani, km ilivyotokea 2010.Nchi inazama jama.TUSIMAME IMARA KUTETEA NCHI YETU.
 
Pasco,
Natamani watu kama Kigwa wangekujibu hii hoja yako, but najua hapa watapita kama wanakimbia, si tunajua ni juzi tu walitamba hapa kuwa hawawezi kukata mti walioupanda bila kujua kuwa wanatakiwa kupunguza matawi yale yaliyochoka ili mti ustawi. Wabunge wa ccm ni mzigo mzito kwa taifa letu na ndio wanaotuangusha zaidi. Ndio JK ni dhaifu sana uwezo wake wa utawala ni mdogo sana but he is just one person ambaye angeweza kubanwa na kuelekezwa mambo ya kufanya ila amekosa msaada, Wabunge wa ccm ni mzigo kwa Taifa letu
 
hata huyu Dalali Kafumu aliyekuwa katibu mkuu wizara ya Madini naye sijui ni nini hasa tatizo?

Huyo Dalali Kafumu hana lolote,amechangia uwepo wa mikataba mibovu ambayo nchi tunapata mrahaba wa asilimia 3 kutoka kwenye migodi yetu.Pia huyo ushindi wake wa jimbo la Igunga umepingwa mahakamani na CHADEMA na juzi kesi ilianza.
 
Huwezi kufanya zaidi ya uwezo wako bila nyenzo,mkuu alipofanya ni kulingana na uwezo wake wa juu kabisa,zaidi ya hapo ilihitajika nyenzo
 
Wanabodi,

Naomba nianze na nilichokisema kuhusu wabunge wapya wa CCM niliobahatika kukutana nao pale bungeni Dodoma November, 2010, ile siku wanaapishwa.


Leo nilikuwa nafanya mapitio ya nilichokisema miaka miwili iliyopita kuhusu wabunge wa CCM. Nilisema baadhi ya wabunge wapya wa CCM wengi ni makapi tuu, hawana substance!. Hili limethibitishwa na JK, katika kulisuka upya baraza lake, kwenye hao wabunge waliopo, amesaka sana akakuta patupu!, yaani hamna kitu mle!, ndipo akajaribu kuvikombeleza vile vichwa vichache vilivyobakia na kulazimika kujaza nakisi kwa kufanya uteuzi mpya wa wabunge wa kumsaidia.

Jee kuna uwezekano wabunge wa CCM waliopo mjengoni kweli ni makapi, vilaza, ni bure kabisa na hana kitu na hawana jipya lolote la kudeliver hadi kumlazimisha mkuu wa nchi kutafuta vichwa vya maana nje ya wabunge waliopo kwa kukopa (bila kuapishwa) ili ajenge timu yake?!.

Nauliza jee ni kweli JK amekosa kabisa watu wa kumsaidia miongoni mwa wabunge wa CCM kwa sababu waliobakia wote ni vilaza tuu au mule bungeni kuna watu wazuri tuu miongoni mwa wabunge wa CCM bali JK ana lake jambo na hao aliowateua?!.

Pasco.

Pasco,

..Raisi ameteua wabunge 2 wapya na kuwateua kuwa mawaziri.

..Now, why do u believe kwamba kumetokea mabadiliko makubwa mno kiasi cha kuhalalisha wewe kuleta posting kama hii?

..mimi nakushauri upumzike kwanza, ili kurudisha fahamu zako. hicho unachokiamini, kwamba Raisi amefanya mabadiliko makubwa ktk baraza lake la mawaziri, sicho kilichotokea.
 
Back
Top Bottom