Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,495
- 113,591
Wanabodi,
Naomba nianze na nilichokisema kuhusu wabunge wapya wa CCM niliobahatika kukutana nao pale bungeni Dodoma November, 2010, ile siku wanaapishwa.
Leo nilikuwa nafanya mapitio ya nilichokisema miaka miwili iliyopita kuhusu wabunge wa CCM. Nilisema baadhi ya wabunge wapya wa CCM wengi ni makapi tuu, hawana substance!. Hili limethibitishwa na JK, katika kulisuka upya baraza lake, kwenye hao wabunge waliopo, amesaka sana akakuta patupu!, yaani hamna kitu mle!, ndipo akajaribu kuvikombeleza vile vichwa vichache vilivyobakia na kulazimika kujaza nakisi kwa kufanya uteuzi mpya wa wabunge wa kumsaidia.
Jee kuna uwezekano wabunge wa CCM waliopo mjengoni kweli ni makapi, vilaza, ni bure kabisa na hana kitu na hawana jipya lolote la kudeliver hadi kumlazimisha mkuu wa nchi kutafuta vichwa vya maana nje ya wabunge waliopo kwa kukopa (bila kuapishwa) ili ajenge timu yake?!.
Nauliza jee ni kweli JK amekosa kabisa watu wa kumsaidia miongoni mwa wabunge wa CCM kwa sababu waliobakia wote ni vilaza tuu au mule bungeni kuna watu wazuri tuu miongoni mwa wabunge wa CCM bali JK ana lake jambo na hao aliowateua?!.
Pasco.
Naomba nianze na nilichokisema kuhusu wabunge wapya wa CCM niliobahatika kukutana nao pale bungeni Dodoma November, 2010, ile siku wanaapishwa.
Wanabodi,
Nikiwa hapa Dom, nimebahatika kukutana baadhi ya wabunge wapya wa CCM na wa kambi ya upinzani, kujaribu kufahamiana, sio siri, baadhi yao hawana hata substance ya ni nini kilichowafanya washinde, na viti maalum ndio usiseme kabisa, wengi ni makapi tuu, kama sio vidumu, basi ni kwa ajili ya kutoa huduma na kibinaadamu, na hili litathibitishwa na michango yao kikao cha Januari.!
Leo nilikuwa nafanya mapitio ya nilichokisema miaka miwili iliyopita kuhusu wabunge wa CCM. Nilisema baadhi ya wabunge wapya wa CCM wengi ni makapi tuu, hawana substance!. Hili limethibitishwa na JK, katika kulisuka upya baraza lake, kwenye hao wabunge waliopo, amesaka sana akakuta patupu!, yaani hamna kitu mle!, ndipo akajaribu kuvikombeleza vile vichwa vichache vilivyobakia na kulazimika kujaza nakisi kwa kufanya uteuzi mpya wa wabunge wa kumsaidia.
Jee kuna uwezekano wabunge wa CCM waliopo mjengoni kweli ni makapi, vilaza, ni bure kabisa na hana kitu na hawana jipya lolote la kudeliver hadi kumlazimisha mkuu wa nchi kutafuta vichwa vya maana nje ya wabunge waliopo kwa kukopa (bila kuapishwa) ili ajenge timu yake?!.
Nauliza jee ni kweli JK amekosa kabisa watu wa kumsaidia miongoni mwa wabunge wa CCM kwa sababu waliobakia wote ni vilaza tuu au mule bungeni kuna watu wazuri tuu miongoni mwa wabunge wa CCM bali JK ana lake jambo na hao aliowateua?!.
Pasco.