Kamanda
Senior Member
- Dec 5, 2007
- 150
- 176
Rais Jakaya Kikwete jana wakati 'anakamata' Fanta yake wakati wa kuwapongeza wabunge waliopitisha hoja aliyoiita muhimu kwa uchaguzi wa demokrasia, aliwaponda na kuwaruka watu wanaojipitisha kwenye majimbo kuomba kupendwa ili waweze kuwa wabunge kwenye Bunge lijalo.
JK akiwa mjini Dodoma alisema wapo 'wabunge' wanaoeleza kuwa wametumwa naye kutangaza nia na kujipitisha kwa wapiga kura ili baada ya ushindi wachaguliwe kuwa mawaziri.
"Hao wanaojipitisha wakitumia jina langu kuwa nimewatuma ni waongo, siwezi kutuma mtu kuwania ubunge, siko hivyo."
"Mimi nina nafasi zangu 10 kuwachagua watu ambao naamini watanisaidia kuwaletea maendeleo Watanzania wenzangu, sasa niwatume hao wanini, wakati hizo 10 zinanitosha sana," aliongeza JK kwa tabasamu kama kawaida na kufuatiwa na kicheko cha kiaina.
-------
Kazi kweli kweli, ingawa kwenye nafasi zake najua anateua wabnge wake wakati wa lala salama, sina uhakika na hatua hiyo. Tuchangie mawazo
JK akiwa mjini Dodoma alisema wapo 'wabunge' wanaoeleza kuwa wametumwa naye kutangaza nia na kujipitisha kwa wapiga kura ili baada ya ushindi wachaguliwe kuwa mawaziri.
"Hao wanaojipitisha wakitumia jina langu kuwa nimewatuma ni waongo, siwezi kutuma mtu kuwania ubunge, siko hivyo."
"Mimi nina nafasi zangu 10 kuwachagua watu ambao naamini watanisaidia kuwaletea maendeleo Watanzania wenzangu, sasa niwatume hao wanini, wakati hizo 10 zinanitosha sana," aliongeza JK kwa tabasamu kama kawaida na kufuatiwa na kicheko cha kiaina.
-------
Kazi kweli kweli, ingawa kwenye nafasi zake najua anateua wabnge wake wakati wa lala salama, sina uhakika na hatua hiyo. Tuchangie mawazo