JK: Anachosema Nape ndio msimamo wa chama

Kabla ya kutoa kauli hiyo katika Tamasha hilo la Pasaka, lililofanyika mjini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Assemblies of God Tanzania (TAG) Onesmo Ndegi, alisema hatua ya kujivua gamba inayochukuliwa na CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Kikwete ina mkono wa Mungu.

Askofu Ndegi alisema sherehe za Pasaka mwaka huu ni maalumu kwa kuwa ni mwaka ambao Tanzania itaadhimisha miaka 50 tangu Uhuru ambayo katika Ukristo inaitwa Jubilee na maana yake ni kuweka kitu huru ama kukiondoa katika mateso.

Alisema kutokana na hali hiyo, Mungu amempa ujasiri Rais Kikwete wa kujivua gamba, kitendo ambacho CCM ilikianza hivi karibuni kwa kuwaondoa madarakani baadhi ya viongozi wake wa juu.



Source: Gazeti la Habari Leo, April 25, 2011

BRAVO JK!!!

Onesmo Ndegi sio askofu wa TAG, yeye ni mchungaji wa kanisa la Living Waters Ministry....
 
Thanks Mkuu kwa kutuletea hii post.
It will go a long way kuwanyamazisha wale doubting Thomases juu ya muelekeo wa chama.
Kimsingi itawafanya wale wapinzani-waandamanaji wakose mada ya kuongea hadharani-maana hawana sera wala mikakati ya kuwaendeleaza waTz, zaidi ya kukodolea macho kiti cha Urais.

Ndugu,
Tunapozungumzia mageuzi na mabadiliko hata siku moja hatuongelei watu.ccm inadandia treni likiwa limeshaondoka.kinachotakiwa kuzungumza na chama kilichoshika hatamu ni jinsi gani ya kuweka mfumo madhubuti ili mafisadi wanaotajwa wasilazishwe tena kwenye serikali.ukiangalia kwa undani fedha zimechotwa kwenye serikali na si chama.kama ccm haitaweza kuiadhibu serikali juu ya kushindwa kwake kusimamia hilo basi wajue bado wana kibarua kikubwa cha kuwafanya watanzzania waamini hii falsafa ya kujivua gamba.wakia nape wanatwanga maji tu na nafikiri upeo wao kiasa ni mdogo mno.
 
Thanks Mkuu kwa kutuletea hii post.
It will go a long way kuwanyamazisha wale doubting Thomases juu ya muelekeo wa chama.
Kimsingi itawafanya wale wapinzani-waandamanaji wakose mada ya kuongea hadharani-maana hawana sera wala mikakati ya kuwaendeleaza waTz, zaidi ya kukodolea macho kiti cha Urais.
Cheaply bought!...Can u tell us how much u costed them?
 
Nae sasa anatuchanganya. Ni juzi tu (Oktoba) alipowanadi kwenye kampeni kwamba ni wachapakazi hodari na hajaona kama wao. Sasa ndo wamekua magamba? Tusubiri siku 90 alizotoa tuone kama atapata ujasiri.
 
Hivi Tanzania iliwahi kuwa koloni la nchi gani hata isherehekee miaka 50 ya uhuru wake? Ninachojua mimi ni Tanganyika ndio inasherehekea miaka 50 ya uhuru, Lakini , huyu Tanganyika yuko wapi? Kuna maana kusherehekea uhuru wa nchi ambayo kimsingi hai-exist?

Let me think!!! I think you have a point. We are actually commemorating the birthday of the deceased Tanganyika who died at a tender age of three.

Nadhani kuna haja ya kuwekeza zaidi kwenye maadhimisho ya siku kifo cha Tanganyika ambayo ni tarehe 26/04/64 kama sijakosea.
 
Back
Top Bottom