Wakuu zangu kuna maswala mawili hapa na lazima tuwe makini sana na jinsi tunavyotazama picha nzima ya mgogoro huu wa Mafisadi.
Kwanza kabisa kwa MASLAHI ya TAIFA hawa mafisadi ni lazima wapoteze mamlaka waliyonayo iwe ndani ya chama au nje kwa sababu ya kinga ya chama tawala chini ya mfumo dume, hivyo kuondoka kwao ni muhimu kwetu sote ili wananchi wapate uwezo wa hata kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zilizopo juu ya hawa mafisadi..Pasipo wao kutolewa hatutakuwa tumefanikisha lolote ndani ya ushabiki huu ya kuitaka CCM isambaratike..
Pili, pamoja na kwamba JK amechelewa kuchukua hatua dhidi ya hawa mafisadi maswahiba wake bado anastahili kupewa motisha ya kumwezesha kuondoa uvivu wa akili ulomkumba baada ya kuchukua madaraka na tukumbuke tu kwamba JK analindwa na katiba dhidi ya machafu yote aloyafanya akiwa rais wa nchi, hivyo hao RACHEL hawawezi kumweka hatiani hata kama wakitafuta njia za kulipa kisasi kwa sababu ni hadi wapate nafasi ya kufanya hivyo..
Nguvu ya dola ni zaidi ya RACHEL, na mamlaka alokabidhiwa JK yanazidi uwezo wa chombo chochote nchini kudhibiti mtu au kundi la watu wanaotaka kuhatarisha usalama wa nchi yetu. In the name of National security, hao kina RACHEL wanaweza kupotezwa ama kulindwa na hakuna chombo wala chma cha kisiasa kinachoweza kupindua..kwa hiyo tunapowapa nguvu hawa mafisadi kwa saabu ya kuipinga CCM na utawala wa JK inanishinda sana kuelewa haswa sisi Wadanganyika tunataka nini?..
Na laukama tunachotaka ni hawa mafisadi kufikishwa mahakamani, nadhani CDM na vyama vinginevyo vijaribu kukusanya mashtaka ambayo kisheria yatatuwezesha kuwafikisha mahakamani kwa ushahidi ambao CCM wanaukalia au hawana kweli..sidhani kama ni jukumu la JK na CCM kuwafikisha RACHEL mahakamani lakini ni jukumu la chama kufanya mageuzi haya ikiwa hawa watu ni mwiba kwa maendeleo ya chama.
Wakuu zangu tumeona madudu mengi yakifanywa na tawala zilizopita, Ufisadi umekuwa ni desturi na maisha ya Mtanzania kiasi kwamba ni lazima tuwe na sehemu ya kuanzia na jitihada hizo zipongezwe. Binafsi sioni sababu ya JK kujivua gamba ikiwa yeye mwenyewe anakubali kutumiwa na kundi hilo lakini maadam leo hii amefikia maamuzi ya kuwatema basi tumpe nguvu ya kufanya haya ili tupate kusonga mbele badala ya kulalamika na kuhoji dhumuni la JK na CCM kuchukua hatua hii hali tunajua wazi CCM wanahitaji kuchukua maamuzi magumu kama haya kukiwezesha chama kushindana..
CDM wana muda na nafasi kubwa ya kuendeleza vagi hili hasa baada ya hawa Mafisadi kuondolewa ndani ya uongozi wa chama. CDM na vyama vinginevyo wanaweza kuwavua ubunge na hata kuwafikisha mahakamani maadam kinga hii itaondolewa. Again, navyofahamu mimi ushahidi wa kujitetea wa hawa Mafisadi hauwezi kukubalika mahakamani ikiwa utamhusisha rais kwa sababu JK analindwa na katiba..For the national security, hawa watu wanatakiwa kuondolewa haraka iwezekanavyo na sintoshangaa wakiwa Kolimbared!
Kwanza kabisa kwa MASLAHI ya TAIFA hawa mafisadi ni lazima wapoteze mamlaka waliyonayo iwe ndani ya chama au nje kwa sababu ya kinga ya chama tawala chini ya mfumo dume, hivyo kuondoka kwao ni muhimu kwetu sote ili wananchi wapate uwezo wa hata kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zilizopo juu ya hawa mafisadi..Pasipo wao kutolewa hatutakuwa tumefanikisha lolote ndani ya ushabiki huu ya kuitaka CCM isambaratike..
Pili, pamoja na kwamba JK amechelewa kuchukua hatua dhidi ya hawa mafisadi maswahiba wake bado anastahili kupewa motisha ya kumwezesha kuondoa uvivu wa akili ulomkumba baada ya kuchukua madaraka na tukumbuke tu kwamba JK analindwa na katiba dhidi ya machafu yote aloyafanya akiwa rais wa nchi, hivyo hao RACHEL hawawezi kumweka hatiani hata kama wakitafuta njia za kulipa kisasi kwa sababu ni hadi wapate nafasi ya kufanya hivyo..
Nguvu ya dola ni zaidi ya RACHEL, na mamlaka alokabidhiwa JK yanazidi uwezo wa chombo chochote nchini kudhibiti mtu au kundi la watu wanaotaka kuhatarisha usalama wa nchi yetu. In the name of National security, hao kina RACHEL wanaweza kupotezwa ama kulindwa na hakuna chombo wala chma cha kisiasa kinachoweza kupindua..kwa hiyo tunapowapa nguvu hawa mafisadi kwa saabu ya kuipinga CCM na utawala wa JK inanishinda sana kuelewa haswa sisi Wadanganyika tunataka nini?..
Na laukama tunachotaka ni hawa mafisadi kufikishwa mahakamani, nadhani CDM na vyama vinginevyo vijaribu kukusanya mashtaka ambayo kisheria yatatuwezesha kuwafikisha mahakamani kwa ushahidi ambao CCM wanaukalia au hawana kweli..sidhani kama ni jukumu la JK na CCM kuwafikisha RACHEL mahakamani lakini ni jukumu la chama kufanya mageuzi haya ikiwa hawa watu ni mwiba kwa maendeleo ya chama.
Wakuu zangu tumeona madudu mengi yakifanywa na tawala zilizopita, Ufisadi umekuwa ni desturi na maisha ya Mtanzania kiasi kwamba ni lazima tuwe na sehemu ya kuanzia na jitihada hizo zipongezwe. Binafsi sioni sababu ya JK kujivua gamba ikiwa yeye mwenyewe anakubali kutumiwa na kundi hilo lakini maadam leo hii amefikia maamuzi ya kuwatema basi tumpe nguvu ya kufanya haya ili tupate kusonga mbele badala ya kulalamika na kuhoji dhumuni la JK na CCM kuchukua hatua hii hali tunajua wazi CCM wanahitaji kuchukua maamuzi magumu kama haya kukiwezesha chama kushindana..
CDM wana muda na nafasi kubwa ya kuendeleza vagi hili hasa baada ya hawa Mafisadi kuondolewa ndani ya uongozi wa chama. CDM na vyama vinginevyo wanaweza kuwavua ubunge na hata kuwafikisha mahakamani maadam kinga hii itaondolewa. Again, navyofahamu mimi ushahidi wa kujitetea wa hawa Mafisadi hauwezi kukubalika mahakamani ikiwa utamhusisha rais kwa sababu JK analindwa na katiba..For the national security, hawa watu wanatakiwa kuondolewa haraka iwezekanavyo na sintoshangaa wakiwa Kolimbared!