JK aagiza Kagasheki, Meya wa Bukoba wamalize mgogoro

bulama

JF-Expert Member
Dec 13, 2012
561
135
Bukoba. Rais Jakaya Kikwete amewaagiza Mbunge wa Bukoba Mjini (CCM), Balozi Khamis Kagasheki na Meya wa Manispaa hiyo, Anatory Aman kumaliza mara moja mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu kwenye manispaa hiyo ukiwahusisha.

Rais Kikwete alitoa agizo hilo alipokuwa akihitimisha ziara yake ya siku sita mkoani Kagera kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Akihutubia mkutano huo, Rais Kikwete alimtaka Balozi Kagasheki ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii kuzungumza mgogoro huo na alipopanda jukwaani alisema miradi iliyopangwa kutekelezwa na Manispaa ya Bukoba chini ya meya huyo haiko wazi, inawaumiza wananchi na ina harufu ya ufisadi.

Alisema kulikuwa na mgawo wa viwanja vilivyokuwa vitolewe kwa wananchi na walikuwa wamelipia fedha kwa ajili hiyo, lakini havikuwahi kutolewa. Alisema kuna viwanja 5,000 lakini havijatolewa mpaka sasa.
Hata hivyo, Rais Kikwete alisema haoni sababu ya wawili hao kuendelea kulumbana na kusema kinachotakiwa ni kukaa pamoja kupima viwanja vilivyopo na utaratibu wa kugawa uendelee.


“Ugawaji viwanja uendelee, kila mwenye kustahili apewe na ambaye hakuridhika ana nafasi ya kukata rufani... hakuna sababu ya kuendelea kulumbana,” alisema Rais.


Mgogoro kati ya Meya Amani na Balozi Kagasheki, ulianza baada ya Manispaa ya Bukoba kuanza kutekeleza miradi mbalimbali ikiwamo ya ujenzi wa soko la kisasa, kituo cha mabasi na upimaji wa viwanja 5,000.


Mapema Machi mwaka huu, CCM, kupitia kwa Katibu wake wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kilitolea tamko mgogoro huo na kusema hauna tija na badala yake, unarudisha nyuma jitihada za kuimarisha chama.


Nnauye, aliwataka wakazi wa Manispaa ya Bukoba kuendelea na shughuli zao zikiwamo za miradi ya maendeleo.'Mwananchi' Kwa jinsi tulivyoteseka na upuuzi wa hawa akina kagasheki alitakiwa kutoka na suluhu. Kwani alichisema hakina tofauti na aliyosema nape sasa yupi ni bisi na ninani anachukua amri?CCM ni majanga.
 
Nae anaagiza? nani wa kuumaliza? Rais anashindwa? only in Tanzania, baba mwenye familia analia lia...
 
It is a lost opportunity and public resources, Sasa kama Baba amekwenda amewakuta watoto wanamgogoro halafu anashindwa kuongea nap kwa kuwasikiliza na kutoa msimamo ni nani tena ataweza kuwasuluhisha?

Du safari yetu ni ndefu sasa, Sasa ushauri wake kwa Kagame kwa skills za aina hiyo kutatua migogoro si ni hatari tupu?
 
Jamani, wanamme wawili viongozi wa nchi wanasuluhishwa kama wake wenza.

Kazi tunayo.
 
aliagiza waliochukuwa pesa za epa warudishe

wakati mwingine Mh Raisi anajitakia mwenyewe kuchambuliwa vibaya. Huu mgogoro mpaka unamfikia maana yake umewashinda Kagasheki na Meya wake, sasa anawaagiza wautatue wenyewe, watawezaje?
 
wakati mwingine Mh Raisi anajitakia mwenyewe kuchambuliwa vibaya. Huu mgogoro mpaka unamfikia maana yake umewashinda Kagasheki na Meya wake, sasa anawaagiza wautatue wenyewe, watawezaje?

Hizo ndio symptoms za ugonjwa uitwao Dhaifu!
 
Rais wetu ana mzaa mwingi, meya na mbunge hawaelewani kabisa, yaani mgogoro walionao ni zaid ya maji na mafuta hata wananch wengine wameenda mbali zaid wakauhusisha na udini, bas kama majib ya rais yako hivyo itatokea vita zaid ya ile ya idd Amin
 
ivi kagasheki si ndie kwenye uchaguz aliforce kujitangaza mshindi hadi wananchi wakamwambia asikanyage na anaishi dar tu au ndio jitiada za kujikosha maana kwa fact alishindwa ubunge!!!
 
nilitegemea aseme "naagiza" sio watu kuanza kukaaa kuongea wakati hilo limefanyika na mpaka sasa ni yale yale.
 
aliagiza waliochukuwa pesa za epa warudishe

Aliagiza viongozi wakristu na wale wa kiislamu wakutane wayamalize.....

Liagiza Kagame na waasi wakutane wayamalize ............

Aliagiza wauza unga anwafahamu kwa hiyo waache mara moja.....

Aliagiza majambazi waache mara moja ..........

Aliagiza haramu waondoke mara moja ...............


Aliagiza -------------------------------------

etc .....................

etc .........................

Kiongozi wa maagizo, siyo maamuzi!!!
 
Back
Top Bottom