Kaka
mshana jr , ni kweli hilo jiwe ni Mfupa wa mnyama na jinsi ya kulitengeneza huwa hivi
JINSI YA KUTENGENEZA "BLACK STONE"
1. Chukua mfupa mrefu wa Nyati au Ngombe, mfupa mzuri ni ule wa zamani ulio mkavu kwa sababu utakuwa hauna mafuta tena
2. Uoshe mfupa wako ikiwezekana na sabuni kabisa, kisha ukaushe, osha tena na tena mpaka uhakikishe mfupa wako hauna utelezi wa aina yoyote au mafuta
3. Kata vipande vidogovidogo vya 2cm mpaka 4cm
4. Chukua msasa au tupa na sugua vipande vyako vya mfupa kuhakikisha kuwa vitobo vidogo vidogo (pores) vilivyopo kwenye mfupa vinakuwa wazi
4. Washa jiko lako la Mkaa au kuni juu ya kipande cha BATI na subiri mpaka mkaa/kuni zikolee kabisa na kipande hicho cha BATI kiwe cha moto sana
5. Fungua mkaa/kuni zako mpaka ulione BATI, weka vipande vyako juu ya hilo BATI la moto kisha vifunike hivyo vipande vya Mifupa na Mkaa/kuni za moto kwa dakika 15
6. Baada ya dakika hizo 15, fungua mkaa wako na anagalia vipande vyako vya mifupa kama ni vyeusi na vyenye kungaa, kama sio vyeusi labda tuseme ni vya Brown basi vurudishe tena kwenye moto
7. Kama ukitoa na kuviona ni vyeusi na vyenye kungaa, basi vichukue na uvitumbukishe kwenye maji ya Kisima, Chemchem au mto kwa dakika chache, kwa kufanya hivyo jiwe litakuwa gumu lililokomaa
Ufafanuzi: inashauriwa kutumika maji ya Kisima, Chemchem au Mto kwa sababu ni maji ambayo hayajapita kwenye madawa ya viwandani, hivyo maji ya Bomba, Chupa au maji Yaliyochemshwa hayafai
JINSI YA KULIJARIBU JIWE KAMA LINAFANYA KAZI VIZURI
Chukua jiwe lako na liweke juu ya ulimi wako na litaganda kwenye ulimi wako kama gundi, na likiwa hivyo basi jiwe lako liko sawa na tayari kwa kutumiwa, lioshe vizuri na litunze kwa dharura
JINSI YA KUTUMIA
Jiwe litumiwe haraka sana baada ya kugongwa na Nyoka au kuumwa na kitu chenye sumu
Fanya hivi
- Osha vizuri jeraha la Nyoka, Nge au chcochote chenye sumu
- Chanja kwa wembe hilo eneo mpaka uhakikishe damu inadondoka
- Weka jiwe lako hapo kwenye Jeraha na hakikisha linaganda hapo
- Hakikisha majeruhi amelala/Kaa kwa utulivu bila kuzungukazunguka
- Jiwe likishiba/likimaliza Sumu lenyewe litadondoka chini
- Tibu jeraha lako kwa dawa za kutibia vidonda, na mgonjwa anaweza pewa dawa za kutuliza maumivu
Jiwe lililotumika linaweza kutumika tena, cha kufanya ni kuliweka jiwe kwenye bilauri (glass) ya Maziwa kwa usiku kucha, na hayo maziwa yasinywewe na mtu yoyote au hata mnyama kwa sababu yatakuwa na sumu kutoka kwenye hilo jiwe.
SO UNAWEZA KUTENGENEZA MWENYEWE NA PIA UTAKUWA UMEPATA MATUMIZI SAHIHI YA HILO JIWE