Jiunge na mfuko wa afya ya jamii!

Jiunge na mfuko wa afya ya jamii!

meningitis

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
8,464
Reaction score
4,828
Wasalaamu wana JF!

Baada ya kutafakari sana nimeona nije na mada hii hapa jamvini ili tujisaidie wenyewe kama watanzania na wanajamii,namaanisha tusisubiri serikali,wanasiasa au wahisani watusaidie!

UTANGULIZI

Nadhani tumesikia mara kwa mara kuhusu vilio vya wananchi kuhusu utoaji wa huduma katika vituo vya afya hususani vile vya serikali.Tumesikia kuhusu uhaba wa dawa na vifaa muhimu vya tiba bila ya kupata suluhisho la kudumu.

Pia tumesikia juu ya ukosefu wa fedha unaopelekea kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.Ukosefu huu umeelezwa na kuhusishwa na bajeti ndogo inayotengwa katika wizara ya afya mfano mzuri ni mwaka huu tumejionea bajeti ya wizara hii ikishuka kwa takribani 1/4 kulinganisha na mwaka jana kinyume kabisa na makubaliano ya Abuja ambayo yanapendekeza karibu asilimia 15 ya bajeti ya nchi ilenge afya.

Pia tumesikia kuhusu ucheleweshaji au usitishwaji wa bajeti za wahisani katika sekta hii.

Vile vile ni mara chache kusikia halmashauri imetenga au kutoa pesa zitokanazo na makusanyo ya ndani kwa ajili ya idara ya afya.

Serikali both local na central zinaamini fedha kutoka kwa wahisani zinatosha kuhudumia sekta ya afya!

KUHUSU UCHANGIAJI WA WANANCHI KATIKA HUDUMA ZA AFYA

Kuna mfumo uliowekwa kwa wananchi kuchangia huduma za afya;

1.Uchangiaji wa fedha wakati wa kupata huduma yaani papo kwa papo.hapa ni kama vile unavyohudhuria hospitali na kutakiwa kulipa fedha kwa ajili ya faili,vipimo au kulazwa wadini.
Mfumo huu ni mzuri lakini una changamoto nyingi hasa hasa rushwa.

2.Mfumo wa pili ni ule wa kutimia bima za afya,hapa naongelea wale waajiriwa.
NHIF yaweza kuwa ndio bima ya afya iliyofanikiwa au kutimiwa kwa wingi hapa nchini.

3.Mfumo wa tatu na muhimu kwa mada hii ni ule wa mfuko wa afa ya jamii (CHF aka community health fund).

Nitelezea zaidi kuhusu CHF hapo chini.

Kwa ufupi mfumo hii mitatu ndiyo mifumo muhimu ya jinsi gani mwananchi anaweza kuchangia huduma za afya nchini.Yawezekana kuna mingine lakini kwa ufupi na umuhimu hiyo hapo juu ndio mifumo ya kuchangia huduma za afya nchni.

KUHUSU CHF

Kama nilivyosema hapo juu huu ni mfuko wa uchangiaji huduma za afya kwa ngazi ya jamii.

Kila kaya hutakiwa kuchangia kiasi flani cha fedha kwa mwaka mara nyingi ni 5000 au 10000 kwa mwaka na hivyo mwanakaya atakapoumwa atatakiwa kutibiwa matibabu ya kawaida kwa mwaka mzima bila kutoa chochote katika kituo chake cha karibu.Tukumbuke kuwa wastani wa kaya nchini ni 4-6 hivyo mfuko utawajibika kwa watu wanne mpaka sita kwa kutegemea ukubwa wa kaya katika maeneo mbalimbali.

Mfuko huu ni mzuri kwa familia masikini zisizo na ajira rasmi.kuna maeneo kama singida wanasema 'kuku mmoja tiba mwaka mzima'

pia halmashauri yaweza kupewa fedha kulingana na idadi ya kaya zilizojiunga kwa mfano zimejiunga kaya 100 na kulipa shilingi 10000*100 ambayo ni shilingi 1000000 basi halmashauri itapewa nyongeza ya sh. 1000000.

Matumizi ya fedha zinazotokana na mfuko huu ni manunuzi ya dawa na vifaa tiba,posho na ukarabati katika kituo kilichoandikisha wanachama.

Kwa ufupi tu haya ndio yanayohusu mfuko huu wa afya ya jamii.

MAONI YANGU

Kwa kuwa jamii kubwa ya watanzania ni masikini lakini sio masikini wa kukosa 5000 au 10000 kwa mwaka ni vyema tukahamasishana kujiunga na mfuko huu.

Tatizo la dawa na vifaa tiba linaweza kumalizwa kwa kuwezesha kila kaya kuwa insured na mfuko huu.

Tujenge utamaduni wa kuchangia huduma za afya na tuondokane na kasumba ya kutegemea hisani za watu wa marekani!

Nipo tayari kwa ufafanuzi zaidi...!

Kumbuka:Sijatokea NHIF/MOHSW bali ni mdau katika sekta ya afya nimejitolea kuhamasisha kwa manufaa ya jamii yetu masikini.

KARIBUNI KWA MJADALA

Nyongeza ya mdau IronLady


Vizuri sana.kwa kuongezea, mtu anapata huduma zote zinazotolewa na level ya kituo husika. Mfn huduma zinazoruhusiwa kutolewa na zahanati kwa miongozo ya wizara basi mwanachama wa mfuko wa afya ya jamii anaruhusiwa pia kupata zote zinazotolewa ktk kituo cha afya basi naye mwanachama wa chf anastahili kupata na hospitali ya wilaya hali kadhalika. Na laiti kama kungekuwa na vifaa na wataalamu wa vipimo vikubwa kwa ngazi hizo nao pia wangestahili.
Havitolewi sababu kwa namna utaratibu ulivyo vipimo hivi hupatikana ktk hospitali za mikoa na taifa na Fbo's yani faith base organztn.

Mfuko wa afya ya jamii unaratibiwa na wilaya husika hivyo matibabu yake huishia vituo vilivyo ndani ya wilaya.isipokuwa tu pale wilaya hiyo itakapoingia mkataba wa watu wake kutibiwa ktk hospitali nje ya wilaya.

Habari njema ni kuwa kile kiwango kilichochangwa mfn ml 15 na watu ndani ya wilaya husika serikali kupitia Nhif hutoa fedha kama hiyo yani ml 15 huitwa teke kwa tele kusupport nguvu za wananchi.

Maana yake ni kuwa ikiwa wananchi watachanga sana basi watapata pesa nyingi kutoka nhif na zikisimamiwa vzr basi tatizo la dawa litakuwa ndoto na huduma zitaboreshwa

7 dawa 15 vifaa tiba 5 posho kwa wakusanyaji fedha za michango 3 mislenious.

Mgawanyiko huu wa matumizi ukizingatiwa vyema na kamati za afya za zahanati na vituo vya afya na wilaya ambapo wananchi wana ushiriki wa uwakilishwaji (ni jukumu lao kujua matumizi na kuhoji inapobidi) pesa zilizochangwa huleta mabadiliko makubwa sana ktk vituo vyetu vya kutolea huduma za afya.
Nawahamasisha mjiunge na mfuko huu wa afya ya jamii

Mfuko wa afya ya jamii kwa wote ndio mambo yote.
 
Last edited by a moderator:
Ni ushauri mzuri sana, ila kuna watu wanaona hakuna mpango wa kujiandaa na matibabu kwa maana wengine sio kipaumbele, eith kwa mjini au vijijini...
kama ulivyoshauri matibabu ni muhimu nia kiasi cha kuangalia unajimudu wapi na kujiunga....
 
Wasalaamu wana JF!

Baada ya kutafakari sana nimeona nije na mada hii hapa jamvini ili tujisaidie wenyewe kama watanzania na wanajamii,namaanisha tusisubiri serikali,wanasiasa au wahisani watusaidie!

UTANGULIZI

Nadhani tumesikia mara kwa mara kuhusu vilio vya wananchi kuhusu utoaji wa huduma katika vituo vya afya hususani vile vya serikali.Tumesikia kuhusu uhaba wa dawa na vifaa muhimu vya tiba bila ya kupata suluhisho la kudumu.

Pia tumesikia juu ya ukosefu wa fedha unaopelekea kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.Ukosefu huu umeelezwa na kuhusishwa na bajeti ndogo inayotengwa katika wizara ya afya mfano mzuri ni mwaka huu tumejionea bajeti ya wizara hii ikishuka kwa takribani 1/4 kulinganisha na mwaka jana kinyume kabisa na makubaliano ya Abuja ambayo yanapendekeza karibu asilimia 15 ya bajeti ya nchi ilenge afya.

Pia tumesikia kuhusu ucheleweshaji au usitishwaji wa bajeti za wahisani katika sekta hii.

Vile vile ni mara chache kusikia halmashauri imetenga au kutoa pesa zitokanazo na makusanyo ya ndani kwa ajili ya idara ya afya.

Serikali both local na central zinaamini fedha kutoka kwa wahisani zinatosha kuhudumia sekta ya afya!

KUHUSU UCHANGIAJI WA WANANCHI KATIKA HUDUMA ZA AFYA

Kuna mfumo uliowekwa kwa wananchi kuchangia huduma za afya;

1.Uchangiaji wa fedha wakati wa kupata huduma yaani papo kwa papo.hapa ni kama vile unavyohudhuria hospitali na kutakiwa kulipa fedha kwa ajili ya faili,vipimo au kulazwa wadini.
Mfumo huu ni mzuri lakini una changamoto nyingi hasa hasa rushwa.

2.Mfumo wa pili ni ule wa kutimia bima za afya,hapa naongelea wale waajiriwa.
NHIF yaweza kuwa ndio bima ya afya iliyofanikiwa au kutimiwa kwa wingi hapa nchini.

3.Mfumo wa tatu na muhimu kwa mada hii ni ule wa mfuko wa afa ya jamii (CHF aka community health fund).

Nitelezea zaidi kuhusu CHF hapo chini.

Kwa ufupi mfumo hii mitatu ndiyo mifumo muhimu ya jinsi gani mwananchi anaweza kuchangia huduma za afya nchini.Yawezekana kuna mingine lakini kwa ufupi na umuhimu hiyo hapo juu ndio mifumo ya kuchangia huduma za afya nchni.

KUHUSU CHF

Kama nilivyosema hapo juu huu ni mfuko wa uchangiaji huduma za afya kwa ngazi ya jamii.

Kila kaya hutakiwa kuchangia kiasi flani cha fedha kwa mwaka mara nyingi ni 5000 au 10000 kwa mwaka na hivyo mwanakaya atakapoumwa atatakiwa kutibiwa matibabu ya kawaida kwa mwaka mzima bila kutoa chochote katika kituo chake cha karibu.Tukumbuke kuwa wastani wa kaya nchini ni 4-6 hivyo mfuko utawajibika kwa watu wanne mpaka sita kwa kutegemea ukubwa wa kaya katika maeneo mbalimbali.

Mfuko huu ni mzuri kwa familia masikini zisizo na ajira rasmi.kuna maeneo kama singida wanasema 'kuku mmoja tiba mwaka mzima'

pia halmashauri yaweza kupewa fedha kulingana na idadi ya kaya zilizojiunga kwa mfano zimejiunga kaya 100 na kulipa shilingi 10000*100 ambayo ni shilingi 1000000 basi halmashauri itapewa nyongeza ya sh. 1000000.

Matumizi ya fedha zinazotokana na mfuko huu ni manunuzi ya dawa na vifaa tiba,posho na ukarabati katika kituo kilichoandikisha wanachama.

Kwa ufupi tu haya ndio yanayohusu mfuko huu wa afya ya jamii.

MAONI YANGU

Kwa kuwa jamii kubwa ya watanzania ni masikini lakini sio masikini wa kukosa 5000 au 10000 kwa mwaka ni vyema tukahamasishana kujiunga na mfuko huu.

Tatizo la dawa na vifaa tiba linaweza kumalizwa kwa kuwezesha kila kaya kuwa insured na mfuko huu.

Tujenge utamaduni wa kuchangia huduma za afya na tuondokane na kasumba ya kutegemea hisani za watu wa marekani!

Nipo tayari kwa ufafanuzi zaidi...!

KARIBUNI KWA MJADALA
Ni wapi au ofisi gani mwananchi anayetaka kujiunga aende,kwa ajili ya kujiunga,na ni matibabu mpaka ya gharama gani anaweza kutibuwa?
 
Tunashukuru kwa taarifa. Ila ni matibabu yapi hayo ya kawaida?
Mfano iwapo patatokea mgonjwa na akalazwa hspt isiyokuwa ya serikali na anaugua let say figo, je hiyo account inaacomodate hayo matibabu?
 
Huo mfuko unahusisha hosp za serikali pekee au mwanachama ataweza kuhudumiwa katika hosp binafsi pia?
 
una covermatibabu ya meningitis?

CHF ni moja ya social health insurence zinazoweza wakomboa wananchi kupitia risk pooling. Yaani wazima kuwachangia wagonjwa. Tatizo kubwa lililopo kwa sasa kwenye mfuko huu ni utaratibu mbaya wa matumizi ya fedha hizi. Zinalipiwa per diem badala ya kununulia dawa, maeneo mengi hazitumiki kabisa kutokana na ukiritimba wa sheria zake/za manunuzi. Watu walichanga na baadae kuona mfuko huu hauwasaidii kitu kwa kuwa fedha yake haiwarudii walengwa. Nyingi hubaki kama bakaa kwenye accounts za halmashauri.

Ili kuboresha mfuko huu, ni lazima halmashauri zitunge sheria na taratibu za mfuko huu zitakazosimamia ukusanyaji wake na matumizi yake. Vinginevyo hakuna mwananchi atakae changa na asione fedha yake imefanya nini.
 
sheria za kuboresha mfuko huu ni mhim lakini pia kuna mwamko mdogo wa wanajamii kuhusu suala la afya,ukiangalia hata hizi bima ya NHIF kuna watumishi wa serikari hawana vitambulisho sababu kubwa ni uzembe wao na kukosa mwamko, serikari na wanajamii tuelimishane
 
Kujiunga na Chf si tatizo.tatizo lipo pale utakapo ugua na kwenda kituo cha afya au hospitali na kuandikiwa KIPIMO AU DAWA NA KUSHAURIWA AU KUTAKIWA UKANUNUE DUKA JIRANI TENA KWA BEI GHALI!
 
Mifuko hii ni mizuri ila tatizo lipo kwenye usimamizi wake maana wakati mwingine unaweza pata ugonjwa mdogo unaenda hospitali wanaandika hata na magonjwa usiyoumwa kuwa umetibiwa hii maana yake ni nini kama sio wizi
 
malengo ya mifuko ya aina hii mazuri tatizo ni usimamizi na kugeuka kuwa ni mitaji ya kuchotwa kwenye uchaguzi na maslahi binafsi!
 
Hii ni habari njema kwetu sisi tunaoishi huku vijijini. Naomba kufahamishwa endapo nitajiunga na mfuko huu wa CHF ni kituo gani cha afya nitakwenda kupata tiba katika hiki kijiji chetu cha Kibara wilaya ya Bunda
 
Wasalaamu wana JF!

Baada ya kutafakari sana nimeona nije na mada hii hapa jamvini ili tujisaidie wenyewe kama watanzania na wanajamii,namaanisha tusisubiri serikali,wanasiasa au wahisani watusaidie!

UTANGULIZI

Nadhani tumesikia mara kwa mara kuhusu vilio vya wananchi kuhusu utoaji wa huduma katika vituo vya afya hususani vile vya serikali.Tumesikia kuhusu uhaba wa dawa na vifaa muhimu vya tiba bila ya kupata suluhisho la kudumu.

Pia tumesikia juu ya ukosefu wa fedha unaopelekea kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.Ukosefu huu umeelezwa na kuhusishwa na bajeti ndogo inayotengwa katika wizara ya afya mfano mzuri ni mwaka huu tumejionea bajeti ya wizara hii ikishuka kwa takribani 1/4 kulinganisha na mwaka jana kinyume kabisa na makubaliano ya Abuja ambayo yanapendekeza karibu asilimia 15 ya bajeti ya nchi ilenge afya.

Pia tumesikia kuhusu ucheleweshaji au usitishwaji wa bajeti za wahisani katika sekta hii.

Vile vile ni mara chache kusikia halmashauri imetenga au kutoa pesa zitokanazo na makusanyo ya ndani kwa ajili ya idara ya afya.

Serikali both local na central zinaamini fedha kutoka kwa wahisani zinatosha kuhudumia sekta ya afya!

KUHUSU UCHANGIAJI WA WANANCHI KATIKA HUDUMA ZA AFYA

Kuna mfumo uliowekwa kwa wananchi kuchangia huduma za afya;

1.Uchangiaji wa fedha wakati wa kupata huduma yaani papo kwa papo.hapa ni kama vile unavyohudhuria hospitali na kutakiwa kulipa fedha kwa ajili ya faili,vipimo au kulazwa wadini.
Mfumo huu ni mzuri lakini una changamoto nyingi hasa hasa rushwa.

2.Mfumo wa pili ni ule wa kutimia bima za afya,hapa naongelea wale waajiriwa.
NHIF yaweza kuwa ndio bima ya afya iliyofanikiwa au kutimiwa kwa wingi hapa nchini.

3.Mfumo wa tatu na muhimu kwa mada hii ni ule wa mfuko wa afa ya jamii (CHF aka community health fund).

Nitelezea zaidi kuhusu CHF hapo chini.

Kwa ufupi mfumo hii mitatu ndiyo mifumo muhimu ya jinsi gani mwananchi anaweza kuchangia huduma za afya nchini.Yawezekana kuna mingine lakini kwa ufupi na umuhimu hiyo hapo juu ndio mifumo ya kuchangia huduma za afya nchni.

KUHUSU CHF

Kama nilivyosema hapo juu huu ni mfuko wa uchangiaji huduma za afya kwa ngazi ya jamii.

Kila kaya hutakiwa kuchangia kiasi flani cha fedha kwa mwaka mara nyingi ni 5000 au 10000 kwa mwaka na hivyo mwanakaya atakapoumwa atatakiwa kutibiwa matibabu ya kawaida kwa mwaka mzima bila kutoa chochote katika kituo chake cha karibu.Tukumbuke kuwa wastani wa kaya nchini ni 4-6 hivyo mfuko utawajibika kwa watu wanne mpaka sita kwa kutegemea ukubwa wa kaya katika maeneo mbalimbali.

Mfuko huu ni mzuri kwa familia masikini zisizo na ajira rasmi.kuna maeneo kama singida wanasema 'kuku mmoja tiba mwaka mzima'

pia halmashauri yaweza kupewa fedha kulingana na idadi ya kaya zilizojiunga kwa mfano zimejiunga kaya 100 na kulipa shilingi 10000*100 ambayo ni shilingi 1000000 basi halmashauri itapewa nyongeza ya sh. 1000000.

Matumizi ya fedha zinazotokana na mfuko huu ni manunuzi ya dawa na vifaa tiba,posho na ukarabati katika kituo kilichoandikisha wanachama.

Kwa ufupi tu haya ndio yanayohusu mfuko huu wa afya ya jamii.

MAONI YANGU

Kwa kuwa jamii kubwa ya watanzania ni masikini lakini sio masikini wa kukosa 5000 au 10000 kwa mwaka ni vyema tukahamasishana kujiunga na mfuko huu.

Tatizo la dawa na vifaa tiba linaweza kumalizwa kwa kuwezesha kila kaya kuwa insured na mfuko huu.

Tujenge utamaduni wa kuchangia huduma za afya na tuondokane na kasumba ya kutegemea hisani za watu wa marekani!

Nipo tayari kwa ufafanuzi zaidi...!

KARIBUNI KWA MJADALA

Hapa Kibara hospital tunaruhusiwa kupata matibabu kwa CHF?
 
Ni ushauri mzuri sana, ila kuna watu wanaona hakuna mpango wa kujiandaa na matibabu kwa maana wengine sio kipaumbele, eith kwa mjini au vijijini...
kama ulivyoshauri matibabu ni muhimu nia kiasi cha kuangalia unajimudu wapi na kujiunga....

Sielewi kwa nini afya haijewi kipaumbele cha bajeti hata katika level ya familia,yaani familia inaweza kupanga bajeti ya chakula mwaka mzima,ada,ujenzi,mavazi n.k lakini sio afya!
 
Ni wapi au ofisi gani mwananchi anayetaka kujiunga aende,kwa ajili ya kujiunga,na ni matibabu mpaka ya gharama gani anaweza kutibuwa?
Waweza kujiunga katika kituo cha kutoa huduma za afya kilichopo karibu na wewe.hapa namaanisha zahanati,kituo cha afya na kwa sasa hata hospitali za wilaya na baadhi ya hospitali za mikoa.

Kuhusu matibabu ya gharama gani?
Hapa unaweza kujionea kuwa kutokana na mchango ulivyo..CHF ililenga matibabu katika ngazi za msingi hasa hasa zahanati na vituo vya afya.pia miongozo ilielekeza mgonjwa apewe huduma za kawaida kwa lugha rahisi na ngumu kidogo 'general OPD services'
ambapo kwa maeneo mengi ni kati ya shilingi 500-5000.Kwa uzowefu wangu kwa sasa kuna wilaya nyingi zimeamua kutoa huduma zote kwa ngazi zote za huduma yaani kama umejiunga na CHF basi utatibiwa bila kuingia mfukoni katika kituo cha huduma ''cha serikali au chenye mkataba na serikali'' kwenye wilaya husika.

Ni obvious kwamba kwa sasa huwezi kutegemea CHF ikufanyie vipimo vikubwa kama CT SCAN AU MRI!

kwa miundo mbinu iliyopo katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini unaweza kupata huduma ya magonjwa kumi yanayosababisha watu kufika hospitalini.

Ni vizuri kutoa 5000 kwa mwaka kuliko kutoa 3000 kwa kila unapohudhuria,Mfano kwa mwaka unaweza kuhudhuria hospitali mara moja,mke wako akahudhuria mara mbili,binti yako akahudhuria mara moja na katika kila hudhurio mlilipa 3000 mtakuwa mmetumia shilingi 12000.
 
Waweza kujiunga katika kituo cha kutoa huduma za afya kilichopo karibu na wewe.hapa namaanisha zahanati,kituo cha afya na kwa sasa hata hospitali za wilaya na baadhi ya hospitali za mikoa.

Kuhusu matibabu ya gharama gani?
Hapa unaweza kujionea kuwa kutokana na mchango ulivyo..CHF ililenga matibabu katika ngazi za msingi hasa hasa zahanati na vituo vya afya.pia miongozo ilielekeza mgonjwa apewe huduma za kawaida kwa lugha rahisi na ngumu kidogo 'general OPD services'
ambapo kwa maeneo mengi ni kati ya shilingi 500-5000.Kwa uzowefu wangu kwa sasa kuna wilaya nyingi zimeamua kutoa huduma zote kwa ngazi zote za huduma yaani kama umejiunga na CHF basi utatibiwa bila kuingia mfukoni katika kituo cha huduma ''cha serikali au chenye mkataba na serikali'' kwenye wilaya husika.

Ni obvious kwamba kwa sasa huwezi kutegemea CHF ikufanyie vipimo vikubwa kama CT SCAN AU MRI!

kwa miundo mbinu iliyopo katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini unaweza kupata huduma ya magonjwa kumi yanayosababisha watu kufika hospitalini.

Ni vizuri kutoa 5000 kwa mwaka kuliko kutoa 3000 kwa kila unapohudhuria,Mfano kwa mwaka unaweza kuhudhuria hospitali mara moja,mke wako akahudhuria mara mbili,binti yako akahudhuria mara moja na katika kila hudhurio mlilipa 3000 mtakuwa mmetumia shilingi 12000.
Asante kwa ufahamisho wako mzuri
 
Tunashukuru kwa taarifa. Ila ni matibabu yapi hayo ya kawaida?
Mfano iwapo patatokea mgonjwa na akalazwa hspt isiyokuwa ya serikali na anaugua let say figo, je hiyo account inaacomodate hayo matibabu?
Mkuu nadhani ukinisoma kwenye post hapo juu niliyofafanua kuhusu gharama utakuwa umepata mwanga juu ya huduma zitolewazo.

Nimeleta mada hii makusudi ili jamii ya kitanzania ijibebee jukumu la kujitibu!
Nionavyo hii ni hatua muhimu sana katika kufikia hilo.leo tukiweza kusustain michango ya CHF na ikatumiwa vizuri sina shaka huduma kama za figo au moyo zitatolewa kihurahisi hapa hapa nchini na pia katika level za hospitali za wilaya.

Nadhani muda si mrefu tutasikia sera hii ya CHF itageuka kuwa 'sheria' au lazima yaani kama vile unavyomiliki boda boda na kutakiwa uliwekee fire extinguisher!
 
Huo mfuko unahusisha hosp za serikali pekee au mwanachama ataweza kuhudumiwa katika hosp binafsi pia?

Swali muhimu kiutendaji!

Kwa asilimia kubwa kwa sasa mfuko huu umehusisha hospitali au vituo vya serikali ingawa yako maeneo ambayo yamekuwa ni mifano ya kuigwa kwani halmashauri zimeingia makubalano na vituo binafsi au mashirika ya dini kuhudumia wateja wa CHF.

Hili suala likieleweka litakuja kuwa kama Bima ya afya(NHIF) kwa mtu masikini asiye na ajira.
 
Back
Top Bottom