Jiunge na mfuko wa afya ya jamii!

Jiunge na mfuko wa afya ya jamii!

Mfumo huu ni mzuri sana, shida ni jinsi unavyotekelezwa. Umewekewa madaraja ambayo mimi naona ni dhambl na ubaguzi. Vitambulisho vya wengine vinaruhusu kutibiwa hospitali zote kwa walioajiriwa na kwa wengine wenye vyeti vyenye rangi fulani hapana.
Kwani ugonjwa wa watu una madaraja ? Bima isibague. Kwa maana wako watu wanachangia na hawaugui hata miaka mitano.
Hii bima wote tuwe na vitambulisho vinavyofanana (kwa watumishi wa serikali ) Na hata hao wa CHF uwepo utaratibu wa usawa.
 
Mfuko huu ni muhimu sana hasa kwa watu wenye matatizo ya ya kudumu / magonjwa sugu ambayo tiba zake ni aghali mno kwa mwezi unakuta m2 anatakiwa dose ya 50000 na zaidi ukiwa na bima hata kama hspt hazipo dawa unapewa form ya kuchukulia dawa hizo katika maduka binafsi, ni kweli hujazipatia hospitali lakini bado hukatoa cash kuzipata.
 
Ni ushauri mzuri sana, ila kuna watu wanaona hakuna mpango wa kujiandaa na matibabu kwa maana wengine sio kipaumbele, eith kwa mjini au vijijini...
kama ulivyoshauri matibabu ni muhimu nia kiasi cha kuangalia unajimudu wapi na kujiunga....[/

Hiyo inawafaa wale wanaoumwa maradhi ya mara kwa mara au ya muda mrefu.
 
Hizi huduma za afya jaman,sio tu kana kwamba wananchi hawazipendi bali wananch wengi hawana uelewa hata kidogo juu ya haya maswala ya bina,ningependa watu humu mfafanue vizuri,manufaa yake,maana NHIF wana nyodo kweli.eti wanataka mwanacha private atoe laki9 hyo kujiunga.na kuchangaia ni 70elfu kila mwezi,je wangapi wangependa ila wanakwama kwasabab ya aina hii ya vikwazo
 
Utaratibu wenu siyo mzuri hasa kwa wategemezi wangu kuniwekea limit kuwa ni mke wangu,watoto wangu,baba na mama wakati mm mpaka sasa sina mke wala watoto na mama kashafariki yupo baba tu.kwa nini msinipe furusa ya kuunganisha ndg zangu wasio na uwezo ili nitumie nao bima yangu ambayo nakatwa kila mwisho wa mwezi????
Bora mngerudisha ule utaratibu wa zamani ili Sisi tusio na wategemezi wa damu pia tuweze kunufaika na NHIF

Kero nyingine ukienda hospitali na hicho kikadi unatazamwa kama mavi na hata dawa ukipata basi ni panadol na kuambiwa zingine ukanunue madukani kwani hapo dawa hakuna.je kwa bali hiyo kuna haja ya kuwa na bima????@acheni kutunyanyasa watumishi kumbukeni kuwa hata Sisi tunakatwa hela siyo makARATASI.
 
Hii inaonyesha hasa ni ubinafsi na kama unajiunga na bima baxi ni vema na ndugu zetu wasio jiweza nao wa ngaliwe na si mpka mfanyazi toka serikalini mjitahidi kuboresha
 
Hiyo kidogo itasaidia na pia somo linatakiwa kwa maana kuna watu wagumu wa kuelewa
 
Hawa jamaa ni wadhaifu kifikra najuuta kuwa mwanachama wao. Wanajua vizur mazingira ya watanzania kuwa wateja wao wengi wako vjjn alafu usajili unafanyka wilayan. Unalipia nauli kuwafuata na bado unatozwa elfu 20000 kwa kumsajili hata mke wako ilhali wanakata fedha zetu kila mwez. Hapa kuna ufisad mkubwa kuliko Escrow
 
Wasalaamu wana JF!

Baada ya kutafakari sana nimeona nije na mada hii hapa jamvini ili tujisaidie wenyewe kama watanzania na wanajamii,namaanisha tusisubiri serikali,wanasiasa au wahisani watusaidie!

UTANGULIZI

Nadhani tumesikia mara kwa mara kuhusu vilio vya wananchi kuhusu utoaji wa huduma katika vituo vya afya hususani vile vya serikali.Tumesikia kuhusu uhaba wa dawa na vifaa muhimu vya tiba bila ya kupata suluhisho la kudumu.

Pia tumesikia juu ya ukosefu wa fedha unaopelekea kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.Ukosefu huu umeelezwa na kuhusishwa na bajeti ndogo inayotengwa katika wizara ya afya mfano mzuri ni mwaka huu tumejionea bajeti ya wizara hii ikishuka kwa takribani 1/4 kulinganisha na mwaka jana kinyume kabisa na makubaliano ya Abuja ambayo yanapendekeza karibu asilimia 15 ya bajeti ya nchi ilenge afya.

Pia tumesikia kuhusu ucheleweshaji au usitishwaji wa bajeti za wahisani katika sekta hii.

Vile vile ni mara chache kusikia halmashauri imetenga au kutoa pesa zitokanazo na makusanyo ya ndani kwa ajili ya idara ya afya.

Serikali both local na central zinaamini fedha kutoka kwa wahisani zinatosha kuhudumia sekta ya afya!

KUHUSU UCHANGIAJI WA WANANCHI KATIKA HUDUMA ZA AFYA

Kuna mfumo uliowekwa kwa wananchi kuchangia huduma za afya;

1.Uchangiaji wa fedha wakati wa kupata huduma yaani papo kwa papo.hapa ni kama vile unavyohudhuria hospitali na kutakiwa kulipa fedha kwa ajili ya faili,vipimo au kulazwa wadini.
Mfumo huu ni mzuri lakini una changamoto nyingi hasa hasa rushwa.

2.Mfumo wa pili ni ule wa kutimia bima za afya,hapa naongelea wale waajiriwa.
NHIF yaweza kuwa ndio bima ya afya iliyofanikiwa au kutimiwa kwa wingi hapa nchini.

3.Mfumo wa tatu na muhimu kwa mada hii ni ule wa mfuko wa afa ya jamii (CHF aka community health fund).

Nitelezea zaidi kuhusu CHF hapo chini.

Kwa ufupi mfumo hii mitatu ndiyo mifumo muhimu ya jinsi gani mwananchi anaweza kuchangia huduma za afya nchini.Yawezekana kuna mingine lakini kwa ufupi na umuhimu hiyo hapo juu ndio mifumo ya kuchangia huduma za afya nchni.

KUHUSU CHF

Kama nilivyosema hapo juu huu ni mfuko wa uchangiaji huduma za afya kwa ngazi ya jamii.

Kila kaya hutakiwa kuchangia kiasi flani cha fedha kwa mwaka mara nyingi ni 5000 au 10000 kwa mwaka na hivyo mwanakaya atakapoumwa atatakiwa kutibiwa matibabu ya kawaida kwa mwaka mzima bila kutoa chochote katika kituo chake cha karibu.Tukumbuke kuwa wastani wa kaya nchini ni 4-6 hivyo mfuko utawajibika kwa watu wanne mpaka sita kwa kutegemea ukubwa wa kaya katika maeneo mbalimbali.

Mfuko huu ni mzuri kwa familia masikini zisizo na ajira rasmi.kuna maeneo kama singida wanasema 'kuku mmoja tiba mwaka mzima'

pia halmashauri yaweza kupewa fedha kulingana na idadi ya kaya zilizojiunga kwa mfano zimejiunga kaya 100 na kulipa shilingi 10000*100 ambayo ni shilingi 1000000 basi halmashauri itapewa nyongeza ya sh. 1000000.

Matumizi ya fedha zinazotokana na mfuko huu ni manunuzi ya dawa na vifaa tiba,posho na ukarabati katika kituo kilichoandikisha wanachama.

Kwa ufupi tu haya ndio yanayohusu mfuko huu wa afya ya jamii.

MAONI YANGU

Kwa kuwa jamii kubwa ya watanzania ni masikini lakini sio masikini wa kukosa 5000 au 10000 kwa mwaka ni vyema tukahamasishana kujiunga na mfuko huu.

Tatizo la dawa na vifaa tiba linaweza kumalizwa kwa kuwezesha kila kaya kuwa insured na mfuko huu.

Tujenge utamaduni wa kuchangia huduma za afya na tuondokane na kasumba ya kutegemea hisani za watu wa marekani!

Nipo tayari kwa ufafanuzi zaidi...!

Kumbuka:Sijatokea NHIF/MOHSW bali ni mdau katika sekta ya afya nimejitolea kuhamasisha kwa manufaa ya jamii yetu masikini.

KARIBUNI KWA MJADALA

Nyongeza ya mdau IronLady

Inawezekana wewe nimmoja wafanilia zile ambazo ukitamkaka jina la ukoo unajilikana lakini akina sisi ambao hata nafasi yakitongoji haijawahi shikwa na member waukoo ukifika kupata matibabu dawa unaambia zimeisha kanunue duka la madawa kunahaja gani kuchangia?
 
Last edited by a moderator:
Nipo Mwanza kata ya nyakato. Wilaya ilemela. Naomba kujuzwa ni wapi naweza pata huduma ya kujiunga na CHF. . nishakwenda buzuluga hata wao hawaijui. Pale nyerere road karibu na star times wao wanaijua nhif tu. Wananiambia nilipe laki Tisa+. Mliopo Mwanza nisaidien wapi naweza pata huduma hii. Au contact zao
 
Mkuu hii huduma hapa Dar es Salaam ipo na inapatikana wapi kwa mfano wilaya ya Ilala?
Kwa hapa Dar pia imegawanyika kwa wilaya zote tatu? Naomba unisaidie majibu yake.

Kwa maeneo ya miji inajulikana kama TIKA.
Nenda kwa mganga mkuu wa manispaa utapata ufafanuzi zaidi.
 
Bima hii ikiboreshwa tunaweza kufika mbali katika afya
 
Back
Top Bottom