Jitahidi mwanao asisome masomo ya Sanaa

Hapo umeongea kuongeza % which I agree but hoja kwamba let us get rid of arts haina mashiko kabisa you must concur ndio maana NKorea haina uhusiano mzuri diplomatically na mataifa ya dunia. Huoni hapo tatizo

Inaonekana umesoma arts, hasara ninayoiona kwako hujui definite na indefinite sentences, imenikera hiyo "but" kwenye sentence yako inayo agree proposal ya argument, then unajipinga mwenyewe.

Ili tuwe na maendeleo endelevu wanasayansi wanapaswa kuwa wengi zaidi nchini, wingi wao utachochea utundu wa kisayansi ndipo itakapokuwa rahisi kufanya tafiti za kiugunduzi, tutapata wataalam wa kuanzisha viwanda from the scratch, tutapata wataalamu si tu wa kusimamia maliasili zetu bali pia kuziongezea thamani kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.

Ningependa siku moja kuwepo maeneo nchini mwetu yameandikwa "SILENCE PLEASE GENIUS AT WORK"

Naipongeza sayansi.
 

Una fikra mgando sana wewe.Hivi kama hayo masomo yako ya Sayansi hayamudu vizuri unataka nimlazimishe tu ayasome hata kama hayapendi wala hayawezi.
Acha kuwa mshamba wewe mtoto lazima apewe Uhuru wa kusoma anachokiweza na anachokipenda na sio kung'ang'ania asome unachotaka wewe asome.
Umejiona mjanja mwenyewe kuandika huo utumbo hapo juu.
Mimi nilifaulu vizuri sana masomo ya sayansi lakini sikuyasoma A-level kwani nilipenda biashara zaidi ya hayo masomo ya sayansi na yamenisaidia na maisha yangu mazuri kuliko hao waliosoma Sayansi.
Mzazi akiwa na mawazo mgando kama ya kwako basi ni hasara kubwa sana kwa watoto wako.
 
Mimi nasoma PGM form 6,ila sijawahi kufikiria kumshauri mtu asome kisa ya ajira,Elimu si kukariri bali Elimu ni kukuza fikra kwa lengo la kutatua changamoto zetu katika maisha,Amini nakwambia kama umesoma kwa ajili ya fedha bado utaendelea kuwa muhanga wa tatizo la kuwa nyuma kimaendeleo japo una vyeti vina A na B+ kwa kuwa kichwani hukufikia dhima ya Elimu. Katika watu wenye mafanikio makubwa duniani kifedha hawakusoma au waliacha shule baada ya kupata walichapata wengine walifeli mfano
1,Bill Gates Founder of Microsoft Corp
2.Steve Jobs Founder of Apple Inc
3. Mark Elliot Zuckerberg Founder of Facebook Inc
4. Henry Ford(Ford Motor Company)
5.Albert Einsten (Father of Modern Physics)
6. Walt Disney (Disney Studios)
7. Charles Darwin
8. Isaac Newton
9.and list goes on
kwa upande wangu tusifikirie karibu kiasi cha kuamini wanaosoma Art ni wavivu au kuwa na fikra mgando masomo ya sanaa ni dhaifu lahasha kila binadamu ana aina ya akili yake "Unaweza ukaenda kwa wana saikolojia wakuelezee kuhusu aina za ulewa wa binadamu mfano kwa nini fulani anweza hesabu na fulani anaweza mashahiri na mwingine ni choraji,nk?" pia tufikirie na kutambua kuwa ajira si maana halisi ya maisha mazuri badala yake tuwe na ndoto zaidi ya hapo
 
siyo umlazimishe bali jitahidi kumjengea mazingira mazuri ya kusoma sayansi. mnunulie vitabu na mpeleke masomo ya ziada. eti hayamudu!, nyie ndiyo mnalisha watoto uzembe. geography na biology au chemistry za olevel zinatofauti gani kubwa kwamba kimoja aweze kingine ashindwe?. mentality ya kwamba it is okay to fail ni mbaya sana kumjengea mtoto. kama we unayo tafadhalli usiipeleke kwa mwanao.
 

Hivi unafahamu kuna wanafunzi wanaojua wanachokifanya na wanajua wanachokitaka kwenye elimu.Mzazi wangu hata kama angetengeneza mazingira mazuri kiasi gani yasingeni-convince nichukue science subjects a-level na chuo ingawa nilikuwa na A kwenye masomo kadhaa ya science O-level.Nilisoma science subjects for fun tu na kufuata utaratibu lakini sikuwa na malengo na hayo masomo ingawa nilikuwa nayamudu vizuri sana tena yamkini kuliko hata wewe.

Ni lazima umsikilize mwanao anapenda kusoma nini na ana malengo gani yeye kama yeye na umpe uhuru wa kuchagua anachotaka asome.Wewe mzazi unatakiwa utoe ushauri na kumtengenezea mazingira ya kufikia malengo yake na sio kufikia malengo yako.

Unatakiwa pia umuandalie mazingira mwanao pia ya kuwa mbunifu na jinsi gani ya kutumia fursa zilizopo maishani na sio tu kuwaza ajira tu mpe na ujuzi juu ya mbadala mwingine wa kuajiriwa ambao ni kujiajiri.
Watoto hawatakiwi wasome kile unachotaka wewe mzazi.Unatakiwa uwape uhuru wa kuchagua cha kusoma kwani wao ndo wasomaji na sio wewe.
Unawaza ajira tu yaani hapo ndo mwisho wa akili zako zilipofikia.Nenda mbali zaidi ya hapo.
Eti masomo ya sayansi ha ha ha ukikutana na watu wenye akili timamu watakudharau mpaka ujichukie.Usiongee tena huu utumbo mbele za watu.
 
hapa hatushindanishi sayansi na sanaa. kwanza mi o-level sayansi sikufanya vema. somo nililofaulu vizuri ni B ya hesabu na fizikia nilipata D hivyo lengo hapa siyo kujikweza kusoma sayansi. pili unamini kwamba mtoto under 18 anatakiwa kuelekezwa na kuongozwa? watoto wengi huchagua combinations kwa kufuata mkumbo na uchache wa masomo, ni wachache wanaoangalia future.

vipi mwanao akisema hataki shule kwasababu imempendeza , utamuacha bila jitihada zozote? future kwanza mapendezi baadaye.
 

Naona unaenda nje ya point. Hatuongelei kuacha shule hapa tunaongelea uchaguzi wa nini cha kusoma.Mtoto akikuambia baba mi nataka arts/biashara anapaswa kusikilizwa na sio kuendelea kumwambia mi nataka usome Sayansi na ninakutengenezea mazingira yq kusoma sayansi.Hapo ndo wazazi wengi wanapochemka.
Kuna mwanafunzi mmoja alikuwa anachukua PCM na alikuwa akifeli sana mpaka mwalimu wa hesabu akamuuliza hii combination ulichagua mwenyewe?Akasema baba ndo amenilazimisha.Mwanafunzi ana haki yake ya kusikilizwa na kuchagua nini cha kusoma.Mzazi kazi yake ni kushauri lakini uamuzi wa mwisho wa nini cha kusoma upo kwa mwanafunzi na sio mzazi.
 

Duh!! Ndugu kujiajiri haijalishi umesoma nini. Kila mtu anaweza kujiariki kutokana na alichokisomea. Acha kuwa na akili mgando.
 
Soma uelimike ili uwe flexible kwa mazingira yeyote, aliekwambia kuwa shule zilizopo, hospital, mabenki, taasisi, ofisi za mijini hapo, wizara na vingine vingi VINAKUNGOJA WEW NANI?
 
ngoja nikuache maana naona una uelewa mgumu sana. unashindwa kujua kama huo ni mfano. pia unashindwa kutofautisha kulazimisha na kujenga mazingira/kujitahidi.
 
Duh!! Ndugu kujiajiri haijalishi umesoma nini. Kila mtu anaweza kujiariki kutokana na alichokisomea. Acha kuwa na akili mgando.
soma vizuri na jitahidi uelewe hiyo post uliyoniquote
 

Inaonekana umepaniki na uenda we ndo mbumbu....mtoa mada alisema mtoto anakua na #uwanjampana mfano aliyesoma PCB anaweza kuwa lawyer lakn ww wa H*** uwez kuwa docter at all!
 

Nimeelewa ....na nimekuelewa
 
kabanga, pole naona umeguswa- it seems you are a graduate of arts subjects- lakini zinalipa, wabunge, wahasibu, lawyers!
mimi ni mwalimu wa commercail subjects na pia ni Proffesiaonal Accountant, kwa muda ambao nimekaa kufundisha na maisha yalivyo kwa arts kwa sasa ni ngumu sana....
 
Hahahahaha.... Nimecheka sana. Hahaha nacheka sana.baba yangu angepata shida sana nadhani. Kumbe kusoma nikuajiriwa? Sasa si bora niende veta nikimaliza nakuwa fundi umeme au gereji.

Elimu sio yakulazimisha bwana kila mtu anakile apendacho. Walazimishe watoto wako kwenda pcm pcb ili ukishalewa kilabuni ujisifu mwanangu daktari mtarajiwa uone anavyopiga ziro na kuwa amepoteza miaka yake miwili shule.

Huo wigo mpana wa ajira ni upi kwanza? Uinjinia? Sisi tunataka wakichina hapa bongo. Waliosoma arts ndo wanaamua yupi tunampa tenda ya kujenga daraja la mkapa. Sasa Acha watoto wako wawe madaktari wanaopewa mshahara kiduchu wakigoma aliyesoma arts ataagiza akanyofolewe kucha mabwepandeee. Then akipona atapelekwa mahakamani kwa kosa lakuchochea vurugu na uvunjifu wa amani, sijui atamwita daktari mwenzie amtetee? Aaaaah kumbe na hakimu atakuwa pcb sawa.ila itakuwa afadhali kwakuwa hakutakuwa na mbea wakuandika limakala reeeefu kuhusu kufinywa kwa dokta mwanao.


Hahahahaha nacheka sana
 
Samahani Wanajamvi, wala msiumizane kwa ukali wa hoja dakika za kuishi ni ndefu kuliko joto la ugumu wa maisha. Ni hv wote mko sahihi kulingana na mtazamo wa kila mtu binafs. Hebu chek hii ktk Arts mtu anaweza kuwa Mwanasheria, mwanamzik, mwandish wa vitabu, Mfasiri wa lugha, mwanadiplosia, na hata mwl. Fani hzo pia mtu wa sayansi anaweza kuzisoma ila si kwa kiwango cha ubobeaji kama wa Arts, ila kama atapitia (post-graduate kwa baadhi ya koz elekezi) bas anaweza kufiti. Ktk maisha ya leo kila kitu ni SAYANSI ni kila Arts inaihitaji sayansi, Mtazamo wa nchi yetu ya Tz hasa kwa viongoz wasio na maono ya mbele ndyo unaojenga hii nadhari ya kusema upande mmoja wa shilingi ni bora na mwingine hauna umuhimu. Kama lugha ni sanaa basi sayans inaihitaj lugha ili ijipambanue. Kufeli kwa sayans kunatokana na mtu kushndwa kuelewa fumbu/swali la lugha iliyotumika. Haya n mawazo tu kwasababu watu wako tofaut kmtazamo, rangi, na hata uchaguz.
 
Samahani Wanajamvi, wala msiumizane kwa ukali wa hoja dakika za kuishi ni ndefu kuliko joto la ugumu wa maisha. Ni hv wote mko sahihi kulingana na mtazamo wa kila mtu binafs. Hebu chek hii ktk Arts mtu anaweza kuwa Mwanasheria, mwanamzik, mwandish wa vitabu, Mfasiri wa lugha, mwanadiplosia, na hata mwl. Fani hzo pia mtu wa sayansi anaweza kuzisoma ila si kwa kiwango cha ubobeaji kama wa Arts, ila kama atapitia (post-graduate kwa baadhi ya koz elekezi) bas anaweza kufiti. Ktk maisha ya leo kila kitu ni SAYANSI ni kila Arts inaihitaji sayansi, Mtazamo wa nchi yetu ya Tz hasa kwa viongoz wasio na maono ya mbele ndyo unaojenga hii nadharia ya kusema upande mmoja wa shilingi ni bora na mwingine hauna umuhimu. Kama lugha ni sanaa basi sayans inaihitaj lugha ili ijipambanue. Kufeli kwa sayans kunatokana na mtu kushndwa kuelewa fumbo/swali la lugha iliyotumika. Haya n mawazo tu kwasababu watu wako tofaut kmtazamo, rangi, na hata uchaguz.
 
mimi ni mwalimu wa commercail subjects na pia ni Proffesiaonal Accountant, kwa muda ambao nimekaa kufundisha na maisha yalivyo kwa arts kwa sasa ni ngumu sana....

Mbona unanitisha sasa watoto niwabadilishe? Tatizo ni kuwa wanataka masomo ya arts!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…