Inaonesha hujaisoma vizuri thread.
Tumepatana ofisini na tumelipa ofisini, ni wao waliopiga simu tukaichukulie mtaani tukakataa.
Ulitaka taratibu za hapo atueleze nani kama si hao wahusika? Ambao ukinisoma vizuri utaona kuwa hao hao ni matapeli na wabadhirifu waliotengeneza hizo mashine kwa kutumia vifaa vya chuo, muda wa chuo, na mpaka wametoa Invoice za chuo (BICO) ambazo kwa jinsi inavyoonekana wanazo zao ambazo hazifiki kwenye uongozi wa chuo (BICO) na wameweza kuzitoa mashine nje ya chuo na kutaka kutupachika nazo kama vile sisi tumeshirikiana nao kuiba.
Kuchukua namba Sinza au kwengine popote si shida, hiyo ilikuwa ni kujulishwa tu, au wewe ulizaliwa unajua kila kitu?