Jinsi ya kutayarisha chumba cha mtoto (Nursery)

mpya9

Member
Aug 29, 2016
31
18
Kujiandaa kwa ujio wa mtoto ni kuna changamoto zake. Mtoto ni vema akawa na chumba chake ili kumjengea hali ya kujitegemea akiwa angali mdogo na pia kurahisisha uhifadhi wa vitu vyake bila kuchanganyika na vya wengine. Chumba cha mtoto 'Nursery' inatakiwa iwe comfortable na pia ya kisasa na yenye kuvutia.

Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia katika kuandaa chumba cha mtoto anayetarajia kuzaliwa

Tengeneza mpango au design ya chumba

Chagua rangi kwa umakini. Rangi ziwe zenye utulivu na zinazoshabihiana na kuta nyingine za nyumba. Baada ya rangi ni muda wa kuchagua michoro utakayoiweka kwenye kuta. Ingawa michoro ukutani inapendeza, ni ngumu kubadilisha pale hitaji linapotokea. Unaweza kuweka midoli na michoro iliyo kwenye vibao vinavyohamishika au fremu za kuning'iniza.

Usijaze samani kwenye chumba cha mtoto

Sidhani kama ungependa kuingia kwenye chumba cha mtoto asubuhi ukiwa na usingizi tele ukajikwaa kwenye kiti au meza. Weka samani chache zenye ubora. Kitanda cha mtoto, kiti cha kumbembelezea mtoto, meza ya kumbadilishia mtoto na kabati dogo vinatosha. Kitanda kilichounganishwa na kabati ni bora zaidi.

Usisahau vitu vyote vya muhimu

Siku za kwanza baada ya kujifungua huwa ngumu. Kuwa na vitu muhimu vyote itakusaidia pale unapohama kutoka hospitali kwenda nyumbani ili uwe umetulia.

Hivi ni vitu muhimu ambavyo utavihitaji:-

Nepi/Pampers
Mafuta (Ya nazi ni mazuri)
Tishu za kujifutia (Baby Wipes)
Poda
Hand Sanitizer
Dawa ya vidonda (ya kusafishia kitovu)
Nguo za mtoto ( Hasa soksi, kofia na gloves)

Kuwa makini na vitu vya kuchezea mtoto (toys)

Kuwa makini unaponunua vitu vya kuchezea mwanao. Kwanza angalia material yake, size na pia maana ya toy husika( mtoto asikue anachezea bunduki)


Muhimu Zaidi:
Anza sasa. Mimba inachosha hasa katika siku za mwishoni. Usiahirishe kisha ukashindwa kufanya.

========

Leo nakuangazia namna ya kupamba chumba cha mtoto.

Ubunifu kwa namna moja ama nyingine unaokoa gharama za muda na fedha. Ni Ubunifu huu huu wenye nguvu kubwa ya kuwasilisha ujumbe kwa jamii. Wengi wetu naamini tumewahi kusikia njia zilizotumika kuwasiliana miaka ya nyuma kidogo si tu kwenye mapango ya Amboni bali hata Misri ambapo mpaka leo hii wanaakeolojia na wanasayansi wanajaribu kufichua(to decipher) kusoma zile jumbe zilizoandikwa kwenye kuta za mafaraoh kwa kutumia Ubunifu wa hali ya juu.

 
Chumba cha mtoto?, hujui mtoto mchanga kulala na mama yake yaani wawe na direct contact ndio huongeza upendo kati ya mtoto na mama? Endapo ikatokea mabadiliko yoyote kwa mtoto umemlaza chumban kwake utayagundua vp kwa haraka? Sometimes sio kila kitu tuige ili tiomekane eti kama wazungu
 
Chumba cha mtoto?, hujui mtoto mchanga kulala na mama yake yaani wawe na direct contact ndio huongeza upendo kati ya mtoto na mama? Endapo ikatokea mabadiliko yoyote kwa mtoto umemlaza chumban kwake utayagundua vp kwa haraka? Sometimes sio kila kitu tuige ili tiomekane eti kama wazungu


Watu mna hatari!, mama akipitiwa na usingizi akamlalia mtoto kwa bahati mbaya na mtoto aka suffocate? Watoto wanatakiwa kulala wenyewe, tena kuwa safe zaidi hutakiwi kuweka any toys or cushions, especially wanapokuwa wachanga sana.
 
Watu mna hatari!, mama akipitiwa na usingizi akamlalia mtoto kwa bahati mbaya na mtoto aka suffocate? Watoto wanatakiwa kulala wenyewe, tena kuwa safe zaidi hutakiwi kuweka any toys or cushions, especially wanapokuwa wachanga sana.
Mkuu toka umekua umewahi kusikia mama kalalia mwanae akafa Lin?, teke la kuku halimuui mwanae. Anyway mambo ya chumba cha mtoto ni option ya mtu kama una interest hiyo fanya tu but for my opinion naona haina ulazima kama sio maana kabisa
 
Sijawahi sikia hizi kesi,nursery ni kuiga tu kwa wazungu. Watu tumelelewa na kukuzwa karibu na mama zetu bila ajali ya kulaliwa wala kupigwa teke.
Watu mna hatari!, mama akipitiwa na usingizi akamlalia mtoto kwa bahati mbaya na mtoto aka suffocate? Watoto wanatakiwa kulala wenyewe, tena kuwa safe zaidi hutakiwi kuweka any toys or cushions, especially wanapokuwa wachanga sana.
 
Yaani mtoto wangu mdogo alale chumba kingine mie nilale chumba kingine! du! wazungu hawa! watoto wanaozaliwa miaka hii wanakosa mapenzi ya mama, ashinde na dada wa kazi, mama hanyonyeshi eti nyonyo zitasinyaa, siku akitoka na mama yake anasukumwa kwenye kigari wala habebwi mgongoni, halafu tena na usiku alale chumba chake, hivi mtoto huyu ni lini atapata harufu ya mama! mweeeeeeeeeeeee! bora nibakie na upare wangu mwanzo mwisho uzungu nooooo!
 
Sijawahi sikia hizi kesi,nursery ni kuiga tu kwa wazungu. Watu tumelelewa na kukuzwa karibu na mama zetu bila ajali ya kulaliwa wala kupigwa teke.

Mkuu toka umekua umewahi kusikia mama kalalia mwanae akafa Lin?, teke la kuku halimuui mwanae. Anyway mambo ya chumba cha mtoto ni option ya mtu kama una interest hiyo fanya tu but for my opinion naona haina ulazima kama sio maana kabisa

1 wafalme 3:16-28
 
Yaani mtoto wangu mdogo alale chumba kingine mie nilale chumba kingine! du! wazungu hawa! watoto wanaozaliwa miaka hii wanakosa mapenzi ya mama, ashinde na dada wa kazi, mama hanyonyeshi eti nyonyo zitasinyaa, siku akitoka na mama yake anasukumwa kwenye kigari wala habebwi mgongoni, halafu tena na usiku alale chumba chake, hivi mtoto huyu ni lini atapata harufu ya mama! mweeeeeeeeeeeee! bora nibakie na upare wangu mwanzo mwisho uzungu nooooo!

Hahahahaaa wee muathu au hethina matunduu? Kule kiurio mwana agera madioo na kweme na atonga mboa mboa tuu.

Namshukuru Mrungu nimelala na mama hadi na miaka 4 ndo nikahamia chumba kingine.

Ila kwenye kichumbi niliendelea kukaa na mama hadi naanza la kwanza.

Namnani heheheheheheh pole kwa kukuchokoza.
 
Ney aliwahi kuimba "Umarekani Mwingi mpaka mnakula unga".. Mtoto awapo mchanga ndio mda anaomuhitaji mama kuliko kitu chochote, mama anahtaji kuwa karibu nae mithili ya ngozi yake. Hiyo nursery labda iwe specific kwa kuanzia umri flani.
 
Hahahahaaa wee muathu au hethina matunduu? Kule kiurio mwana agera madioo na kweme na atonga mboa mboa tuu.

Namshukuru Mrungu nimelala na mama hadi na miaka 4 ndo nikahamia chumba kingine.

Ila kwenye kichumbi niliendelea kukaa na mama hadi naanza la kwanza.

Namnani heheheheheheh pole kwa kukuchokoza.
hhahaah hetu ni Mwanga Tambarare karibu sana hahahahhhah
 
Haya mambo ya copy and paste ...ndio yanayotufanya hatupigi hatua ...tuna copy tuuuu bila kufikiria mazingira yetu!
 
Ndugu sio kila kitu lazima uweke udini. Sasa unapotoa mstari wa biblia unamaanisha nn kwa wenye dini tofauti na ukristo?ni kujitafutia malumbano yasiyo na kichwa wala miguu.

Haya tukiangalia huo mstari huyo aliyemlalia mtoto wake akili zake anazijua mwenyewe maana alikua tayari mtoto wa mwenzie auliwe ili wakose wote,mama mwenye uchungu hawezi ona mtoto wa mwenzie akiumia.
1 wafalme 3:16-28
 
Siku hizi wanakamua maziwa yanawekwa kwenye friji hadi wiki mbili mtoto anakunywa hayobhayo yakiisha ndo anakamua mengine kisa ubusy.
Mtoto anakula viporo tangu akiwa mchanga akifikisha mwaka na nusu keshaanza shule, aaah mzungu atuhurumie tu jaman bora apige marufuku kuigwa igwa.
Yaani mtoto wangu mdogo alale chumba kingine mie nilale chumba kingine! du! wazungu hawa! watoto wanaozaliwa miaka hii wanakosa mapenzi ya mama, ashinde na dada wa kazi, mama hanyonyeshi eti nyonyo zitasinyaa, siku akitoka na mama yake anasukumwa kwenye kigari wala habebwi mgongoni, halafu tena na usiku alale chumba chake, hivi mtoto huyu ni lini atapata harufu ya mama! mweeeeeeeeeeeee! bora nibakie na upare wangu mwanzo mwisho uzungu nooooo!
 
Back
Top Bottom