Threesixteen Himself
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 8,351
- 8,087
tuanze na memory card kubwa
zipo memory card za 1tb na 512gb wanazionyesha san disk na makampuni mengine lakini bado hazijaingia mainstream na upatikanaji wake ni shida. memory card kubwa zinazopatikana kirahisi ni za 128gb na 64gb hizi zipo za kutosha tu.
ukubwa wa memory card na bei zake
hii issue ni ngumu kidogo na inahitaji utaalamu ila nitajitahidi kuielezea kirahisi
-jinsi computer/simu inavyohifadhi vitu.
computer inahifadhi vitu kwa kutumia binary na kila herufi au namba ina namna yake ya kuiandika kwa kutumia binary, chukulia mfano upo shule kabla ya mtihani wewe na mwenzako mkapanga muigiliziane mkafundishana na ishara nikinyoosha kidole kimoja jibu ni A, vidole viwili jibu ni B...... vidole vi 5 jibu ni E nk then mkafanya mtihani na kuigiliziana bila mtu kutamka herufi just ishara tu.
computer nayo ipo hivyo hivyo kila herufi/data wanaigeuza kuwa binary halafu ndio inahifadhiwa, na hizi Binary ni namba 0 na 1 tu. mfano neno MAMA kwa binary linakuwa hivi
M kwa binary ni 01001101
A kwa binary ni 01000001
hivyo unaweza kuta neno mama likawa hivi (01001101 01000001 01001101 01000001)
-kutoka binary kuja bytes
tunaona memory card zetu zinatumia bytes, hapo juu umetaja 2g (2 gigabytes) na 8gb (8 gigabytes) je kuna mahusiano gani kati ya bytes na binary? binary digit inaitwa bit na kila digit 8 ndio byte 1 ukichunguza hizo binary za juu utaona kila herufi ina digit 8 za binary.
kwa lugha rahisi tutasema kila herufi ni byte 1 . byte zikiwa milioni 1 ni MB 1 na zikiwa bilioni 1 ni gb 1
so memory card ya gb 8 ina bytes bilioni 8 au binary digit bilioni 64.
-kwanini sd card zina umbo moja?
hizi ni standard kaka watu wanakaa chini wanakubaliana, vitu kama sd card, tundu la earphone, usb port ya kuchajia, line za simu nk hivi vitu watu wanakaa chini wanaamua viwe na ukubwa fulani.
-wanachofanya watengeneza memory card kama samsung na san disk
wao sasa wanashindana kuweka binary nyingi kadri iwezekanavyo kwenye umbo moja walilokubaliana (standard) ndio hapo sasa tunapata memory card za gb tofauti tofauti
-kitu gani kinafanya binary ziingie nyingi?
hizi memory card zinatumia flash memory na uwezo wa kuhifadhi vitu unaekwa kwa layer jinsi manufacturing process zinavyokuwa duniani basi wanaweza kufit layer nyingi kwenye umbo dogo kama hilo. pengine umeshawahi sikia kitu kinaitwa transistor na manufacturing process kama 28nm, 22nm, 14,nm, 10nm etc jinsi hio process inavyoshuka ndio jinsi wanavyotumia eneo dogo na kuweza kufit transistor na hizo layer kwa wingi.
unakuta memory card ya 64gb ina layer ndogo ndogo za 4gb mara 16
-kujibu swali lako sasa
bei zinatofautiana sababu memory card zina layer tofauti na manufacturing process tofauti. memory card yenye layer chache na inayotumia manufacturing process ya kizamani itauzwa bei rahisi na vice versa is true.
bonus
kuna makundi matatu sasa hivi ya memory card
sd card- za kizamani na uwezo mdogo mfano za 2gb
sdhc card hizi ni kama za 32gb na 64gb
sdxc card hizi ndio za kisasa zaidi zinaanzia 64gb kupanda
!
!
Ankoo daah.... Heshima kwako mkuu. Nimekubali sana. Salute sana