Jinsi nilivyookoa ndoa ya watu

Jinsi nilivyookoa ndoa ya watu

SOCIOLOGISTTZ

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
2,615
Reaction score
929
Jumapili iliyopita nikiwa nimejipumzisha nyumbani kwangu mara akatokea rafiki yangu ambaye ni jirani yangu, akaniomba niende kwake nikamsaidie kusuluhisha kwani kuna kasheshe limetokea kati yake na mke wake.

Pia huyu mkewe ana undugu na mimi kwa mbali hivyo tunaheshimiana kama kaka na dada. Sikukataa wito nikaondoka naye, nilipofika nyumbani kutaka kujua kulikoni..yule dada akaanza kunisimulia kuwa mumewe ana tabia ya kumchungulia housegirl kila anapokwenda kuoga, mara nyingi eti housegirl anapoingia bafuni kuoga mume naye atatafuta mbinu yoyote ya kutoka nje ili aweze kumchungulia.

Bafu lenyewe lipo kwenye nyumba yao kubwa lakini unaweza kumchungulia kwa nje kama utapanda kwenye ngazi au stuli.

Huyu dada akaendelea kusema kuwa alikuwa hajui kitu anachokifanya mumewe kwa muda mrefu kidogo kama miezi miwili iliyopita, lakini siku hiyo ya Jumapili alisikia kishindo kwa nje akatoka haraka kwenda kuangalia nini kimetokea..akamkuta mumewe akiugulia maumivu chini na ndoo aliyokuwa ameitumia kusimamia ili amchungulie housegirl ikiwa imepasuka.

Hivyo akaunganisha tukio la ndoo na kinachofanyika bafuni na akakumbuka mumewe huwa anatoka nje karibu kila siku kwa wakati ambaye h/girl anaoga basi akajua kuwa moja kwa moja alikuwa na tabia ya kumchungulia housegirl.

Dada alikuja juu kama simba aliyenyang'anywa watoto wake anataka talaka yake aanze zake kuliko kuendelea kuaibika namana hiyo. Huyu mume alikana kuwa alikuwa afanyi hivyo bali ndoo ilimtega wakati akizunguka nyuma ya nyumba kuangalia usalama wa nyumba yao. Wakagombana sana..mwisho wa siku wakakubaliana waniite mimi kama rafiki yao wa karibu na walijua nitatoa maamuzi ya busara yatakayowasaidia wote wawili. (kumbuka mimi siyo mshenga wao wala msimamizi wao).

Basi niliposikiliza maelezo ya pande zote mbili nikawaomba tuende eneo la tukio, kweli nikakuta ndoo imetoboka katikati, haiitaji kuwa na degree kujua chanzo cha kutoboka kwa hiyo ndoo, kwani ilitoboka kwa sababu ya kitu kizito kilichowekwa juu yake au mtu kusimama juu yake.

Nikatumia akili yangu ya kuzaliwa nikawaambia kwanza mmefanya vizuri kuja kuniambia ili msijiaibishe kwa watu. Pili nikamwambia mwanamke mumeo anakupenda sana kwani kama kweli unamfikiria kitendo alichokifanya kuwa ni kweli basi angeweza si tu kumchungulia bali kumfanya mke kabisa au nyumba ndogo iliyoko kwenye nyumba kubwa.

Huyu jamaa ana uwezo wote angeweza hata kumwachisha kazi akampangia sehemu nyingine ili aendeleze uharamia wake huo ambao unaufikiria.

Sasa kwa muda huo aliokaa dada (miezi 6) na ajafanya hivyo basi unayodhania siyo kweli kama hayana kithibitisho.

Ni kamwambia mume wako anakupenda ndiyo maana anawahi kuja nyumbani kama siyo hivyo angekuwa anakuja saa nane za usiku kama wanaume wengine, niliongea mengi mwisho wa siku mke akamuomba mumewe msamaha wakapeana mikono yakaisha.

Basi nikaendelea kukaa pale kupima upepo ni kweli yaliisha. mwisho wa siku wakanisindikiza wote wawili nyumbani. Kesho yake yule jamaa akanifuata mapema akanipa 50,000 eti nikanye wine kwani nimeokoa ndoa yake, nikajaribu kumuuliza madai ya mkewe yalikuwa ya ukweli? akasema ni kweli kabisa.

Huyu dada anafanya kazi serikalini na mumewe anafanya kazi kwenye NGO.

Hivyo ndivyo nilivyo okoa ndoa ya watu.
 
Inaonyesha house girl ni mkali kuliko mother house.
 
^^
Pongezi sana.. Japo wanawake ni wepesi wa kuchukulia mambo 'easy' lakini tatizo la msingi la tamaa za mwanaume halijatatuliwa.
^^
 
Jamaa mchunguliaji hajielewi. Nahisi kuna anachokitaka zaidi ya kuchungulia. Mwambie ajiangalie, ndoa yake iko mashakani maana ataendelea kumchungulia h/girl huyo na yeyote atakayekuja hapo home kwake. Iko siku utashindwa kumtetea maana kwenye ukweli ......... KAZI KWAKO MSULUHISHI.
 
Jumapili iliyopita nikiwa nimejipumzisha nyumbani kwangu mara akatokea rafiki yangu ambaye ni jirani yangu, akaniomba niende kwake nikamsaidie kusuluhisha kwani kuna kasheshe limetokea kati yake na mke wake. Pia huyu mkewe ana undugu na mimi kwa mbali hivyo tunaheshimiana kama kaka na dada. Sikukataa wito nikaondoka naye, nilipofika nyumbani kutaka kujua kulikoni..yule dada akaanza kunisimulia kuwa mumewe ana tabia ya kumchungulia housegirl kila anapokwenda kuoga, mara nyingi eti housegirl anapoingia bafuni kuoga mume naye atatafuta mbinu yoyote ya kutoka nje ili aweze kumchungulia. Bafu lenyewe lipo kwenye nyumba yao kubwa lakini unaweza kumchungulia kwa nje kama utapanda kwenye ngazi au stuli. Huyu dada akaendelea kusema kuwa alikuwa hajui kitu anachokifanya mumewe kwa muda mrefu kidogo kama miezi miwili iliyopita, lakini siku hiyo ya Jumapili alisikia kishindo kwa nje akatoka haraka kwenda kuangalia nini kimetokea..akamkuta mumewe akiugulia maumivu chini na ndoo aliyokuwa ameitumia kusimamia ili amchungulie housegirl ikiwa imepasuka. Hivyo akaunganisha tukio la ndoo na kinachofanyika bafuni na akakukbuka mumewe huwa anatoka nje karibu kila siku kwa wakati ambaye h/girl anaoga basi akajua kuwa moja kwa moja alikuwa na tabia ya kumchungulia housegirl. Dada alikuja juu kama simba aliyenyang'anywa watoto wake anataka talaka yake aanze zake kuliko kuendelea kuaibika namana hiyo. Huyu mume alikana kuwa alikuwa afanyi hivyo bali ndoo ilimtega wakati akizunguka nyuma ya nyumba kuangalia usalama wa nyumba yao. Wakagombana sana..mwisho wa siku wakakubaliana waniite mimi kama rafiki yao wa karibu na walijua nitatoa maamuzi ya busara yatakayowasaidia wote wawili. (kumbuka mimi siyo mshenga wao wala msimamizi wao). Basi niliposikiliza maelezo ya pande zote mbili nikawaomba tuende eneo la tukio, kweli nikakuta ndoo imetoboka katikati, haiitaji kuwa na degree kujua chanzo cha kutoboka kwa hiyo ndoo, kwani ilitoboka kwa sababu ya kitu kizito kilichowekwa juu yake au mtu kusimama juu yake. Nikatumia akili yangu ya kuzaliwa nikawaambia kwanza mmefanya vizuri kuja kuniambia ili msijiaibishe kwa watu. Pili nikamwambia mwanamke mumeo anakupenda sana kwani kama kweli unamfikiria kitendo alichokifanya kuwa ni kweli basi angeweza si tu kumchungulia bali kumfanya mke kabisa au nyumba ndogo iliyoko kwenye nyumba kubwa. Huyu jamaa ana uwezo wote angeweza hata kumwachisha kazi akampangia sehemu nyingine ili aendeleze uharamia wake huo ambao unaufikiria. Sasa kwa muda huo aliokaa dada (miezi 6) na ajafanya hivyo basi unayodhania siyo kweli kama hayana kithibitisho. Ni kamwambia mume wako anakupenda ndiyo maana anawahi kuja nyumbani kama siyo hivyo angekuwa anakuja saa nane za usiku kama wanaume wengine.... niliongea mengi mwisho wa siku mke akamuomba mumewe msamaha wakapeana mikono yakaisha. Basi nikaendelea kukaa pale kupima upepo ni kweli yaliisha. mwisho wa siku wakanisindikiza wote wawili nyumbani. Kesho yake yule jamaa akanifuata mapema akanipa 50,000 eti nikanye wine kwani nimeokoa ndoa yake, nikajaribu kumuuliza madai ya mkewe yalikuwa ya ukweli? akasema ni kweli kabisa. Huyu dada anafanya kazi serikalini na mumewe anafanya kazi kwenye NGO. Hivyo ndivyo nilivyo okoa ndoa ya watu.

hahahahaha mbavu zangu..duh kitu juu ya ndoo cha mno haswa p
 
Jamaa mchunguliaji hajielewi. Nahisi kuna anachokitaka zaidi ya kuchungulia. Mwambie ajiangalie, ndoa yake iko mashakani maana ataendelea kumchungulia h/girl huyo na yeyote atakayekuja hapo home kwake. Iko siku utashindwa kumtetea maana kwenye ukweli ......... KAZI KWAKO MSULUHISHI.
Na kweli hili linaweza kutokea, nanilimwambia tukiwa peke yetu mambo anyoyafanya yataatarisha ndoa yao kam ataendelea na mchezo huo, aliniapia kwamba hatarudia tena, Tuwaombee tu waishi vizuri
 
Inaonesha jamaa anamwogopa mother house kuliko kingine chochote. Shida yote nini mpaka mtu uvunjike guu kisa kuchungulia? Tena hapo sio kuchungulia bali kutazama, ukiwa mbali na kumeza mate mpaka akimaliza kuoga na weye umeshashiba mimate?? Jamani, mijitu mingine ni hasara tu.
Mihele yote alokupa si angempa h/g anejilambia kiulainiiii au apewe ruksa ya kumwogesha?? Akili nyingine, tope tupu.
 
ha ha h ha nimependa hiyo kudondoka na ndooo
za mwizi kwel arobaini...anachunglia bila kula mzigo

Tatizo hapo sio kuchungulia bali kuna mzizi.......jamaa anatamani amle mzigo H/girl sema bado hajampatia timing lakini hilo dume linaonyesha ni design za wale madomo zege
 
Duh!!..huyo jamaa nadhan atakuwa mcheza pool ndio tabia za walachabo..hivi mtoto wake ndio amkute eti baba kasimamia kweny ndoo anamchungulia h/g akioga ndio tunawafundisha nin watoto wetu..hivi kuna mijitu kupanuka akili wanapanuka mat.........k...o
 
Tatizo hapo sio kuchungulia bali kuna mzizi.......jamaa anatamani amle mzigo H/girl sema bado hajampatia timing lakini hilo dume linaonyesha ni design za wale madomo zege

yaaa hili domo zege...hakuna cha timing miezi 3 anachungulia tuuu.it seems h/gal ana kijungu.
 
Duh,Ukistaajabu ya Mussa.Huyo jamaa bila shaka hata kazini anawachungulia wafanyakazi wenzie.Huyo House girl anajua kuhusu huo mzozo?.Mwanamke ameamua kupotezea ila ana yake moyoni,siku wakikosana jamaa asishangae kuambiwa ndio maana ulimchungulia House girl.
 
Back
Top Bottom