Kenya 2022 Jinsi laana ya kuunga mkono Udikteta wa Magufuli ilivyomwangusha Raila Odinga

Kenya 2022 General Election

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,808
218,457
Binadamu tunatakiwa kujifunza na kukumbuka kwamba HAKUNA MAHALI POPOTE KATIKA DUNIA HII AMBAPO SHETANI ALIWAHI KUMSHINDA MUNGU

Kilichomkuta Raila Odinga kiwe fundisho kwa Wanadamu wengine waliosalia hapa Duniani , hata kama hawagombei madaraka , haijawahi kutokea binadamu yeyote mwenye hofu ya Mungu kuunga mkono matendo maovu , kwa vile tu yanafanywa na Kiongozi fulani , ni wafuasi wa Shetani pekee wanaoweza kuunga mkono unyama huo.

Raila akijua anayoyafanya Magufuli nchini mwake , ya kuruhusu utekaji na kupotea kwa watu , ikiwemo uporaji ulioitwa PLEA BARGAIN (ambao hela zake hazijulikani zilipo , hii ni kwa mujibu wa CAG ) , Wanasiasa kusingiziwa kesi za uongo za Uhujumu uchumi na utakatishaji hela , huku uporaji wa mifugo ya nchi jirani zikiwemo Rwanda na Kenya UKIASISIWA RASMI NCHINI TANZANIA , kukiwa pia na Ukatili ambao haujawahi kuonekana kabla ya HITLER kuzaliwa wa KUCHOMA MOTO VIFARANGA VYA KUKU KUTOKA KENYA VISIVYO NA UGONJWA WOWOTE, Lakini Raila Odinga akatia pamba masikioni akaamua kumuunga mkono Magufuli bila hata aibu hadharani, huku akiahidi kuiongoza Kenya kama Magufuli alivyoongoza Tanzania , Hatimaye Mungu amekataa Wakenya kuteswa kinyama kama Watanzania .

ASANTE MUNGU NA SHUKRANI SANA WAKENYA KWA KUKATAA UDIKTETA NCHI MWENU.

FUNZO : HATA KAMA WATAWALA WATASIMIKA MTU WAO BADO WANANCHI MKISHIKAMANA MNAWEZA KUMKATAA NA AKASHINDWA.

Mungu Ibariki Jamhuri ya watu wa Kenya.
 
Asingeweza kuwaongezea mishahara watumishi wa umma hadi angemaliza muda wake.
 
Unaposema Raila alimuunga mkono Magufuli. how? utekaji, plea bargain etc haviwezi kuwa vithibitisho vya kukubaliana na ulichoandika, statement ya Odinga akimuunga mkono Magufuli kuhusu yale matendo yake inahitajika zaidi.

Pia unapofurahia Odinga kushindwa, una uhakika ameshindwa kihalali? mbona kuna malalamiko kila upande kwamba mpaka wajumbe wanne wa IEBC kati ya saba hawakubaliani na hayo matokeo?

Bado naona kuna sarakasi zinaenda kutokea kuhusu huu uchaguzi wa Kenya, hao jamaa wataenda mahakamani kama kweli matokeo ya mwisho hayakuhakikiwa kabla ya kutangazwa, na sitashangaa huko yakitolewa maamuzi mengine yatakayowashangaza watu.
 
download (1).jpeg
download.jpeg


Mtu mwenye Kipara, halafu akawa mnyakyusa msukule hanaga tofauti na kichwa mbege
 
RUTO ni kiongozi kutoka chama kilichopo madarakani, Raila Odinga ni mgombea kutoka chama pinzani.

Mashangilio yako ni kama kushangilia CCM ikishinda uchaguzi hapa Tanzania
 
RUTO ni kiongozi kutoka chama kilichopo madarakani, Raila Odinga ni mgombea kutoka chama pinzani.

Mashangilio yako ni kama kushangilia CCM ikishinda uchaguzi hapa Tanzania
Nyoosha maelezo
 
Back
Top Bottom