Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Kwema Wakuu!
Mbinu bora ya wakati wote ambayo hata mimi Taikon ninatumia kwenye mahusiano yangu ambayo nimefanikiwa na nitafanikiwa. Yaani kwenye jino kwa jino kufanikiwa sio hiyari bali lazima.
Nipende nikuonyeshe upendo maradufu.
Nijali nikujali.
Niheshimu nikuheshimu.
Niletee upuuzi alafu uone vile shetani akiuvaa mwili wa binadamu. Ukinicheat naku-cheat maradufu.
Ukiniletea uduwanzi utaelewa Watibeli ni Watu wa aina gani.
Sisi ni waaminifu kikamilifu. Ni waaminifu kwa asilimia 90% kwa mazuri na kwa mabaya. Yaani kama nilikuwa mzuri kwako kwa asilimia 90% basi elewa kiwango hichohicho ndicho ambacho nitakuwa mbaya kwako. Huo ndio uaminifu. Hatuwezi kudanganya.
Wanaotumia kanuni ya jino kwa jino wengi wamefanikiwa kwenye mahusiano.
Hakuna msamaha hapa. Ni lazima ulipe.
Na mimi lazima nilipe nikikufanyia upuuzi.
Kuachana ni dakika tuu. Ukinisaliti lazima uachwe lakini kabla hujaachwa lazima nawe uonje utamu wa kusalitiwa kwa kiwango mara mbili ya ulichokitenda.
Hivyo ndivyo namna ambavyo ukitaka mahusiano yenu yaende kwa haki na yasiwe yakitapeli na kuumizana kijingajinga.
Mwambie kabisa mwenza wako kuwa siku ukini-cheat kabla hatujaachana lazima niku-cheat pale panapouma. Tena kwa mtu ambaye atakûumiza.
Mwambie wewe ni mwaminifu na unachokisema ndicho unachokitekeleza, na akujue hivyo hata kwa mambo mengine.
Sio mtu akuletee mambo ya sijui msameheane, sijui Kanisani au misikitini, mwambie hapa Haki bin Haki. Kabla hatuachana.
Hivyo ndivyo Watibeli tunavyoishi. Na hakuna Ngedere yoyote atakayejaribu kukuchezea ikiwa anajua kile ambacho atafanya nawe utamlipa vilevile na kumjazia kabla haujamuacha.
Usaliti hauna Excuse. Msaliti ni msaliti tuu. Na dawa ya msaliti ni Kumpa Haki yake ambayo sio Msamaha.
Mambo yote hayo yasemwe kabla hamjaingia kwenye mahusiano. Mpe muongozo kabisa kama sisi Watibeli tufanyavyo. Ili baadaye asijesema hukumwambia.
Mlale unono
Mbinu bora ya wakati wote ambayo hata mimi Taikon ninatumia kwenye mahusiano yangu ambayo nimefanikiwa na nitafanikiwa. Yaani kwenye jino kwa jino kufanikiwa sio hiyari bali lazima.
Nipende nikuonyeshe upendo maradufu.
Nijali nikujali.
Niheshimu nikuheshimu.
Niletee upuuzi alafu uone vile shetani akiuvaa mwili wa binadamu. Ukinicheat naku-cheat maradufu.
Ukiniletea uduwanzi utaelewa Watibeli ni Watu wa aina gani.
Sisi ni waaminifu kikamilifu. Ni waaminifu kwa asilimia 90% kwa mazuri na kwa mabaya. Yaani kama nilikuwa mzuri kwako kwa asilimia 90% basi elewa kiwango hichohicho ndicho ambacho nitakuwa mbaya kwako. Huo ndio uaminifu. Hatuwezi kudanganya.
Wanaotumia kanuni ya jino kwa jino wengi wamefanikiwa kwenye mahusiano.
Hakuna msamaha hapa. Ni lazima ulipe.
Na mimi lazima nilipe nikikufanyia upuuzi.
Kuachana ni dakika tuu. Ukinisaliti lazima uachwe lakini kabla hujaachwa lazima nawe uonje utamu wa kusalitiwa kwa kiwango mara mbili ya ulichokitenda.
Hivyo ndivyo namna ambavyo ukitaka mahusiano yenu yaende kwa haki na yasiwe yakitapeli na kuumizana kijingajinga.
Mwambie kabisa mwenza wako kuwa siku ukini-cheat kabla hatujaachana lazima niku-cheat pale panapouma. Tena kwa mtu ambaye atakûumiza.
Mwambie wewe ni mwaminifu na unachokisema ndicho unachokitekeleza, na akujue hivyo hata kwa mambo mengine.
Sio mtu akuletee mambo ya sijui msameheane, sijui Kanisani au misikitini, mwambie hapa Haki bin Haki. Kabla hatuachana.
Hivyo ndivyo Watibeli tunavyoishi. Na hakuna Ngedere yoyote atakayejaribu kukuchezea ikiwa anajua kile ambacho atafanya nawe utamlipa vilevile na kumjazia kabla haujamuacha.
Usaliti hauna Excuse. Msaliti ni msaliti tuu. Na dawa ya msaliti ni Kumpa Haki yake ambayo sio Msamaha.
Mambo yote hayo yasemwe kabla hamjaingia kwenye mahusiano. Mpe muongozo kabisa kama sisi Watibeli tufanyavyo. Ili baadaye asijesema hukumwambia.
Mlale unono