Jina unalompa mwanao lina maana gani?

Jina unalompa mwanao lina maana gani?

Huyo mama yako mkubwa amewapa wanawe majina ya Kireno. Nadhani alikuwa ana ndoto za kuzamia meli enzi za ujana wake
Nawashukuru wazazi wangu mungu awaondolee abadhabu ya dunia na akhera, katika watoto 10 hakuna hata mwenye jina la ajabu,mamangu mkubwa watoto wake laa mpaka nashanga sijui majina anayatoa wapi, Oktoble,sijui Taudundo,yani mpaka nashangaa .. ahh mungu aninusuru sitowapa wanangu majina mpaka yakawa vituko...
 
Mtoto unamwita Zitto kweli mzito. Hata mkitaka kumfanyia ubaya awezekaniki kabisa.
 
sasa na majina ya wanajf humu ndani ya maana gani? hebu nieleweshe hapa, maana mengine hata kuyatamka mpaka ujipange kisawasawa na uwe umeshiba vinginevyo yatakuotea juani. Bujibuji
 
Last edited by a moderator:
sasa na majina ya wanajf humu ndani ya maana gani? hebu nieleweshe hapa, maana mengine hata kuyatamka mpaka ujipange kisawasawa na uwe umeshiba vinginevyo yatakuotea juani. Bujibuji
Sasa ladyfurahia unafurahia nini?
attachment.php
 
Last edited by a moderator:
wengine majina ya watoto wao wanachaguliwa na waganga wa kienyeji.Mtoto akizaliwa anakuwa na mapepo ya kutosha
 
Sisi wasukuma uwapa majina watoto kutokana na matukio na kipindi wanazaliwa, na muonekano na muundo wa mtoto.

Kwa mfano:

Mabula kwa wa kiume na Kabula kwa wa kike. Hawa uwa mara nyingi uwa wamezaliwa kipindi cha mvua kubwa au ndogo.

Igobeko, ili upewa mtoto wa kiume ambaye aidha alipindua uchifu fulani, nikimaanisha alirithi uchifu kinyume na mrithi aliyetarajiwa. Hivyo alijigobeka, kama alijiingiza au alijipachika kiujanjaujanja.

Shimba, mara nyingi upewa mtoto wa kiume, ambaye uonekana kuwa na nguvu kama za simba. Au wazazi utamani mtoto awe na nguvu na uwezo kama wa simba katika maisha yake.

Makune, uwa mara nyingi upewa mtoto wa kiume, ambaye muonekano pengine na uimara wake upo kama vitoto vya ndege.

N.k.
 
Ntigulunde gombeho hupewa wakati gani?
Sisi wasukuma uwapa majina watoto kutokana na matukio na kipindi wanazaliwa, na muonekano na muundo wa mtoto.

Kwa mfano:

Mabula kwa wa kiume na Kabula kwa wa kike. Hawa uwa mara nyingi uwa wamezaliwa kipindi cha mvua kubwa au ndogo.

Igobeko, ili upewa mtoto wa kiume ambaye aidha alipindua uchifu fulani, nikimaanisha alirithi uchifu kinyume na mrithi aliyetarajiwa. Hivyo alijigobeka, kama alijiingiza au alijipachika kiujanjaujanja.

Shimba, mara nyingi upewa mtoto wa kiume, ambaye uonekana kuwa na nguvu kama za simba. Au wazazi utamani mtoto awe na nguvu na uwezo kama wa simba katika maisha yake.

Makune, uwa mara nyingi upewa mtoto wa kiume, ambaye muonekano pengine na uimara wake upo kama vitoto vya ndege.

N.k.
 
Ni Kweli kabisa Bujibuji, unamwita mwanao Nackivona, huyo kwenye maisha yake yote atakiona cha mtema kuni, Au nakijwa, huyo kila atakapoenda atakuwa anafukuzwa tu, Nanzia, huyo yeye na njia tu, Nambombe, huyo yeye na maji tuuu. mwite mwanao jina kama Lisa, Sweet,Furaha, Faith, Upendo, Fortune, Fahami,Love, Bahati, Iqra, Usra, Isra. majina yapo mengi na mazuri ambayo yanakuwa pia ni zawadi kwao na maisha yao.
 
Kitu cha kwanza huwa simpi mwanangu jina wakati sijui maana yake......
kama nampa John nahakikisha hiyo John ina maana gani, siangalii kama kuna Pope aliitwa John wala nini.
maana ya jina naona ndo muhimu sana kuliko hata huyo mtu alikuwa nani hapa duniani
 
Mi nina Jamaa yangu kampa jina baby boy wake "MAJANGA" kwa hiyo yeye anaitwa baba MAJANGA!
 
angalia mwezi uliozaliwa ujue tabia zako;
Jan;jasiri na mkorofi
Feb:mwenye bahati na mkweli
Mar:msumbufu lakini mzuri
Apr:anajali na ni mpiganaji
May:anaupendo na ulio halisi
Jun:mwenye mvuto wa mapenzi na kiu ya kujua mambo
Jul;amebarikiwa vipaji na ana busara
Aug;makini na mchapa kazi
Sep;anaelewa haraka na ni mzuri wa sura
Oct;anakwenda na wakati na ni rafiki mwema
Nov;anakipaji na ni mbunifu
Dec; mtu wa starehe tuu!!!!!!!!!!
Vipi je wewe ni mzaliwa wa mwezi gani?? tafadhali usibadili kulingana na tabia za mwezi wako na jee unaonaje matokeo vp yana ukweli???
By KILITIME JF Member

Ni vizuri kuelewa maana ya Jina na uhusiano wake na mafanikio.
Hebu fikira Vijijini wanavyosafa bila kujali majina waliyonayo.
Vile vile Jina linaweza kuwa na maana nyingine mbaya sana katika lugha nyingine. Je hapo jina litamaathiri mhusika? Mfano Mboopesa
Palipotawaliwa na umasikini na uzembe wa hali ya juu, watu hufikiria superstitions zaidi kuliko kufanya kazi. Wataaza jina ndo linaleta shida na kulilamikia jina. Hivi kweli wazazi wa mtu watampati jina kwa ajili ya kuletea shida dunia? Kama ni hivyo basi kila mtu na amwite mwanaye Tajiri ili aje awe tajiri duniani.

Jibu la mafanikio ni kufanya kazi mengine haya yote hayana maana sana zaidi ya kuwa physiological effects kwenye maisha yetu.



 
angalia mwezi uliozaliwa ujue tabia zako;
Jan;jasiri na mkorofi
Feb:mwenye bahati na mkweli
Mar:msumbufu lakini mzuri
Apr:anajali na ni mpiganaji
May:anaupendo na ulio halisi
Jun:mwenye mvuto wa mapenzi na kiu ya kujua mambo
Jul;amebarikiwa vipaji na ana busara
Aug;makini na mchapa kazi
Sep;anaelewa haraka na ni mzuri wa sura
Oct;anakwenda na wakati na ni rafiki mwema
Nov;anakipaji na ni mbunifu
Dec; mtu wa starehe tuu!!!!!!!!!!
Vipi je wewe ni mzaliwa wa mwezi gani?? tafadhali usibadili kulingana na tabia za mwezi wako na jee unaonaje matokeo vp yana ukweli???
By KILITIME JF Member

Mboopesa







Mboopesa ni watu wa mkoa gani?
 
Majina yana maana kubwa sana kwenye maisha yetu.
Tabia na muonekano wetu umejengwa kwa kiasi kikubwa na majina tuliyopewa.
Mtoto akiitwa siwema, kamwe hawezi kuwa mwema.
Ukimuita mwanao Majuto, daima atakuwa anajuta.
Haya sasa oneni maajabu haya yaliyotokea Sinza.

535610_10151536096921660_1951249359_n.jpg

Mboopesa ni watu wa mkoa gani?

Wajapani hao giLESI. Mchezaji wa soka wa timu ya taifa ya Japani.
 
Kitu cha kwanza huwa simpi mwanangu jina wakati sijui maana yake......
kama nampa John nahakikisha hiyo John ina maana gani, siangalii kama kuna Pope aliitwa John wala nini.
maana ya jina naona ndo muhimu sana kuliko hata huyo mtu alikuwa nani hapa duniani

Life and death are in the power of the tongue
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom