Jina la Lowassa kurudishwa tena?

Jina la Lowassa kurudishwa tena?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
12,151
Reaction score
44,072
Huwezi kuamini hicho ndicho kinachoendelea sasa ndani ya CCM, Kambi ya Lowassa iko kwenye mikakati mingi mizito na vikao vizito kuhakikisha jina la Lowassa linarudishwa katika kinyang'anyiro tena.

Tayari Majina matano ya makada wa CCM wanaopambana kugombea urais kwa tiketi ya CCM yameshapitishwa na Kamati kuu lakini mpaka sasa CCM imekataa kata kata kuyatangaza rasmi majina hayo na yatatolewa ndani ya kikao cha Halmashauri kuu leo saa nne asubuhi ili kupigiwa kura na wajumbe ili yabaki majina matatu.

Wadadisi wa siasa za CCM wanasema Rais Kikwete ni mwoga sana, na anapima upepo unakwendaje, hivyo akiona mambo shwari orodha itabaki vile vile na kama akihisi mambo huenda yakamwendea Kombo tusishangae jina la Lowassa likirudishwa tena.
 
Majina matano hayakawahi kutangazwa miaka nend rudi
 
Ndio hivyo tena amekatwa na Nape alisbasema hakuna nafasi ya kukata rufaa hata kama hukubali yaliyotendeka.
 
Soma twitter ya Rais wako Hapo unataka yatangazwe wapi?
 

Attachments

  • 1436590099284.jpg
    1436590099284.jpg
    46.3 KB · Views: 2,891
Sona tweet page ya CCM

Kama ya raisi na chama zote fake basi haya majanga

Bora tu watu wa Lowassa mkubali ukweli
 
Mbona taratibu za siku zote zimekiukwa? Naona ya KANU yatajirudia Tanzania. MTU hawazi kuleta wagombea kwa gunia ndiyo tutapiga kura za moyoni mwaka huu na siyo kwa mapenzi ya Chama!
 
Mbona taratibu za siku zote zimekiukwa? Naona ya KANU yatajirudia Tanzania. MTU hawazi kuleta wagombea kwa gunia ndiyo tutapiga kura za moyoni mwaka huu na siyo kwa mapenzi ya Chama!

Tangu mwanzo ukiukaji wa taratibu ulikuwapo. Matumizi ya fedha yaliokithiri kwenye kutangaza nia tu. Kuanza kampeni kabla ya muda. Wajumbe wa halmashauri kuu kuwa wapiga debe wa mtia nia
Watia nia kuchochea wananchi. Maadam mlinyamazia ukiukwaji wa taratibu uliofanywa na mnaempenda, msilalamike tena
 
Mbona taratibu za siku zote zimekiukwa? Naona ya KANU yatajirudia Tanzania. MTU hawazi kuleta wagombea kwa gunia ndiyo tutapiga kura za moyoni mwaka huu na siyo kwa mapenzi ya Chama!

Ni kweli sasa watu watapiga kura za Ukweli toka moyoni na Ukawa wajiandae kutawala Nchi .
 
Kamari kuu ilifanya mchujo wa kienyeji tu wengi wakekatwa kiaajabu ajabu tu , kikaa kilikaa kikiwa na majina machache badala ya majina 38 ina maana Matokeo yamepangwa nje ya Uwanja lile Goli la mkono la Nape hilo sasa linakuja .
 
Back
Top Bottom