Habari wadau, Leo asubuhi nimepatwa na mshangao baada ya kuona jiko langu la gesi likiwaka moto na kupelekea kioo cha juu kuvunjika vipande vipande, ikumbukwe kuwa hili jiko lina kama miezi miwili tu toka nimelinunua dukani. Nimejaribu kuwaita mafundi nao wameshindwa kuelewa tatizo ni nini! Nimeamua kuleta uzi kwenu nikiamini JF ni kisima cha maarifa na pia kupata angalizo juu ya vitu vya kuwanavyo makini pindi nitakaponunua jiko jingine. Unaweza angalia picha hapo chini ili angalau nipate msaada wa mawazo.