Mwanza ni mji uliotulia, hauna vurugu za kijinga na wahuni wasio na kazi, pamoja na hali ya hewa maridhawa, upepo mzuri wa ziwa, rangi ya kijani, msongamano mdogo kusema kweli ni mji ideal kwa watu watulivu! Hakuna mji unaokosa "uswahilini", hata mwanza ukienda igogo huko milimani, mabatini, baadhi ya maeneo ya butimba kuna mitaa ambayo inaudhi, watu wanatofautiana vipato hivyo ni kawaida kuwa na maisha ya utofauti katika mji. Muda mrefu kidogo sijafika Mwanza lakini kule sehemu za starehe si nyingi sana, hakuna mitaa yenye mabar kila kona, night clubs sidhani kama zinazidi mbili, i really miss mwanza; asubuhi supu ya samaki, mchana ugali samaki choma, jioni wali samaki...daaah..samaki samaki! Mwanza, mji ambao napenda kutulia nitakaporetire na michakato ya dunia, mishe zangu zikiwa zinajiendesha zenyewe na mifereji ya pesa ikimwagika pomoni, hapo nitarudi mwanza, nitanunua kisiwa na kusubiri kifo kwa amani zote...lol!
View attachment 143117
View attachment 143118